< Nehemia 11 >

1 Viongozi wa watu waliishi Yerusalemu, na watu wengine walipiga kura ili kuleta mmoja kati ya watu kumi kuishi Yerusalemu, mji mtakatifu, na wengine tisa walibakia katika miji mingine.
The leaders of the people lived in Jerusalem, and the rest of the people cast lots to bring one of ten to live in Jerusalem, the holy city, and the other nine remained in other towns.
2 Na watu wakawabariki wote waliojitoa kwa hiari kuishi Yerusalemu.
Then the people blessed all those who willingly offered to live in Jerusalem.
3 Hawa ndio viongozi wa mkoa ambao waliishi Yerusalemu. Hata hivyo, katika miji ya Yuda kila mtu aliishi katika nchi yake mwenyewe, ikiwa ni pamoja na Waisraeli, makuhani, Walawi, watumishi wa hekalu, na wazao wa watumishi wa Sulemani.
These are the provincial officials who lived in Jerusalem. However, in the towns of Judah everyone lived on his own land, including some Israelites, priests, Levites, temple servants, and descendants of Solomon's servants.
4 Katika Yerusalemu waliishi baadhi ya wana wa Yuda na baadhi ya wana wa Benyamini. Watu wa Yuda walikuwa pamoja na Athaya, mwana wa Uzia, mwana wa Zekaria, mwana wa Amaria, mwana wa Shefatia, mwana wa Mahalaleli, mwana wa Peresi.
In Jerusalem lived some of the descendants of Judah and some of the descendants of Benjamin. The people from Judah included: Athaiah son of Uzziah son of Zechariah son of Amariah son of Shephatiah son of Mahalalel, a descendant of Perez.
5 Na Maaseya, mwana wa Baruki, mwana wa Kolhoze, mwana wa Hazaya, mwana wa Adaya, mwana wa Yoyaribu, mwana wa Zakaria, mwana wa Mshelani, alikuwa mwana wa Baruki.
There was Maaseiah son of Baruch son of Kol-Hozeh son of Hazaiah son of Adaiah son of Joiarib son of Zechariah, the son of the Shilonite.
6 Wana wote wa Peresi waliokaa Yerusalemu walikuwa 468. Walikuwa masujaa.
All the sons of Perez who lived in Jerusalem were 468. They were outstanding men.
7 Hao ndio wana wa Benyamini, Salu, mwana wa Meshulamu, mwana wa Yoedi, mwana wa Pedaya, mwana wa Kolaya, mwana wa Maaseva, mwana wa Ithieli, mwana wa Yehaya.
These are the descendants of Benjamin: Sallu son of Meshullam son of Joed son of Pedaiah son of Kolaiah son of Maaseiah son of Ithiel son of Jeshaiah,
8 Na baada yake, Gabai na Salai, watu 928.
and those following him, Gabbai and Sallai, 928 men.
9 Yoeli mwana wa Zikri alikuwa mwangalizi wao; na Yuda mwana wa Hasenua alikuwa mkuu wa pili juu ya mji.
Joel son of Zichri was their overseer, and Judah son of Hassenuah was second in command over the city.
10 Kutoka kwa makuhani Yedaya, mwana wa Yoyaribu, Yakini,
From the priests: Jedaiah son of Joiarib, Jakin,
11 Seraya mwana wa Hilikia, mwana wa Meshulamu, mwana wa Sadoki, mwana wa Merayoti, mwana wa Ahitubu, mkuu wa nyumba ya Mungu,
Seraiah son of Hilkiah son of Meshullam son of Zadok son of Meraioth son of Ahitub, the chief official of the house of God,
12 na wenzake waliofanya kazi ya ukoo, watu 822. na Adaya mwana wa Yerohamu, mwana wa Pelalia, mwana wa Amzi, ​​mwana wa Zekaria, mwana wa Pashuri, mwana wa Malkiya.
and their associates who did the work for the house, 822 men, along with Adaiah son of Jeroham son of Pelaliah son of Amzi son of Zechariah son of Pashhur son of Malchijah.
13 Nao walikuwa washirika wake waliokuwa wakuu wa jamaa, wanaume 242, na Maasai mwana wa Azareli, mwana wa Azai, mwana wa Meshilemothi, mwana wa Imeri;
His brothers were heads of clans, 242 men; and Amashsai son of Azarel son of Ahzai son of Meshillemoth son of Immer,
14 na ndugu zao, 128 wapiganaji wenye ujasiri, wenye ujasiri; Waziri wao aliyeongoza alikuwa Zabdieli, mwana wa Hageoli.
and their brothers, 128 courageous fighting men; their overseer was Zabdiel son of Haggedolim.
15 Na Walawi Shemaya mwana wa Hashubu, mwana wa Azrikamu, mwana wa Hashabia, mwana wa Buni,
From the Levites: Shemaiah son of Hasshub son of Azrikam son of Hashabiah son of Bunni,
16 na Shabethai, na Yozabadi, ambao walikuwa ni viongozi wa Walawi, waliosimamia kazi za nje ya nyumba ya Mungu.
and Shabbethai and Jozabad, who were from the leaders of the Levites and were in charge of the outside work of the house of God.
17 Alikuwepo Matania, mwana wa Mika, mwana wa Zakri, mwana wa Asafu, aliyekuwa mkurugenzi aliyeanza shukrani kwa sala, na Bakbukia, wa pili miongoni mwa ndugu zake, na Abda mwana wa Shemaya, mwana wa Galali, mwana wa Yeduthuni.
There was Mattaniah son of Mika son of Zabdi, a descendant of Asaph, who was the director who began the thanksgiving in prayer, and Bakbukiah, the second among his brothers, and Abda son of Shammua son of Galal son of Jeduthun.
18 Katika mji wote mtakatifu walikuwa Walawi 284.
All the Levites in the holy city numbered 284.
19 Walinzi wa malango Akubu, Talmoni, na washirika wao, ambao waliolinda milango, wanaume 172.
The gatekeepers: Akkub, Talmon, and their associates, who kept watch at the gates, 172 men.
20 Na wale waliosalia wa Israeli, na makuhani, na Walawi, walikuwa katika miji yote ya Yuda. Kila mtu aliishi katika milki yake mwenyewe.
The remainder of Israel and of the priests and the Levites were in all the towns of Judah. Everyone lived on his own inherited property.
21 Wafanyakazi wa hekalu waliishi Ofeli, na Siha na Gishpa walikuwa wakiwaongoza.
The temple workers lived in Ophel, and Ziha and Gishpa were in charge of them.
22 Mtawala mkuu juu ya Walawi waliokuwa wakitumikia Yerusalemu alikuwa Uzi mwana wa Bani, mwana wa Hashabia, mwana wa Matania, mwana wa Mika, wa wana wa Asafu, ambao walikuwa waimbaji wa kazi katika nyumba ya Mungu.
The chief officer over the Levites in Jerusalem was Uzzi son of Bani son of Hashabiah son of Mattaniah son of Mika, of the descendants of Asaph, singers over the work in the house of God.
23 Walikuwa chini ya maagizo kutoka kwa mfalme na maagizo imara yalitolewa kwa waimbaji kila siku inavyohitajika.
They were under orders from the king, and firm orders were given for the singers as every day required.
24 Pethahia mwana wa Meshezabeli, mwana wa Zera, mwana wa Yuda, alikuwa upande wa mfalme kwa habari zote za watu.
Then Pethahiah son of Meshezabel, a descendant of Zerah son of Judah, was at the king's side in all matters concerning the people.
25 Kuhusu vijiji na mashamba yao, baadhi ya watu wa Yuda wakakaa Kiriath-arba, na vijiji vyake, na Diboni, na vijiji vyake, na Yekabzeeli na vijiji vyake.
As for the villages and their fields, some of the people of Judah lived in Kiriath Arba and its villages, and in Dibon and its villages, and in Jekabzeel and its villages,
26 Wakaishi katika Yeshua, Molada, Beth-Peleti,
and in Jeshua, Moladah, Beth Pelet,
27 Hazar-Shuali, Beersheba na vijiji vyake.
Hazar Shual, and Beersheba and its villages.
28 Nao wakakaa Siklagi, na Mekona, na vijiji vyake,
Some of the people of Judah lived in Ziklag, Mekonah and its villages,
29 Enrimoni, Sora, Yarmuthi,
Enrimmon, Zorah, Jarmuth,
30 Zanoa, Adulamu, na vijiji vyake, na Lakishi, na mashamba yake, na Azeka, na vijiji vyake. Basi wakakaa kutoka Beer-sheba mpaka bonde la Hinomu.
Zanoah, Adullam, and their villages, and in Lachish its fields and Azekah and its villages. So they lived from Beersheba to the Valley of Hinnom.
31 Watu wa Benyamini pia walikuwa wakiishi kutoka Geba, kwenda Mikmashi na Aiya, na Beth-eli na vijiji vyake.
The people of Benjamin also lived from Geba onward, at Mikmash and Aija, at Bethel and its villages,
32 Waliishi Anathothi, Nobu, Anania,
at Anathoth, Nob, Ananiah,
33 Hazori, Rama, Gitaimu,
Hazor, Ramah, Gittaim,
34 Hadidi, Seboimu, Nebalati,
Hadid, Zeboim, Neballat,
35 Lodi, na Ono, bonde la wafundi.
Lod, and Ono, the valley of craftsmen.
36 Walawi wengine waliishi Yuda wengine Benyamini.
Some of the Levites who lived in Judah were assigned to the people of Benjamin.

< Nehemia 11 >