< Nehemia 11 >
1 Viongozi wa watu waliishi Yerusalemu, na watu wengine walipiga kura ili kuleta mmoja kati ya watu kumi kuishi Yerusalemu, mji mtakatifu, na wengine tisa walibakia katika miji mingine.
And the rulers of the people dwelt in Jerusalem, —and, the rest of the people, cast lots, to bring in one out of ten to dwell in Jerusalem, the holy city, and nine parts in [other] cities.
2 Na watu wakawabariki wote waliojitoa kwa hiari kuishi Yerusalemu.
And the people bestowed a blessing on all the men, who willingly offered themselves to dwell in Jerusalem.
3 Hawa ndio viongozi wa mkoa ambao waliishi Yerusalemu. Hata hivyo, katika miji ya Yuda kila mtu aliishi katika nchi yake mwenyewe, ikiwa ni pamoja na Waisraeli, makuhani, Walawi, watumishi wa hekalu, na wazao wa watumishi wa Sulemani.
Now, these, are the chiefs of the province, who dwelt in Jerusalem, but, in the cities of Judah, dwelt every man in his possession throughout their cities, Israel, the priests, and the Levites and the Nethinim, and the Sons of the Servants of Solomon.
4 Katika Yerusalemu waliishi baadhi ya wana wa Yuda na baadhi ya wana wa Benyamini. Watu wa Yuda walikuwa pamoja na Athaya, mwana wa Uzia, mwana wa Zekaria, mwana wa Amaria, mwana wa Shefatia, mwana wa Mahalaleli, mwana wa Peresi.
And, in Jerusalem, dwelt certain of the sons of Judah and of the sons of Benjamin, —Of the sons of Judah, Athaiah son of Uzziah, son of Zechariah, son of Amariah, son of Shephatiah, son of Mahalalel, of the sons of Perez;
5 Na Maaseya, mwana wa Baruki, mwana wa Kolhoze, mwana wa Hazaya, mwana wa Adaya, mwana wa Yoyaribu, mwana wa Zakaria, mwana wa Mshelani, alikuwa mwana wa Baruki.
and Maaseiah son of Baruch, son of Col-hozeh, son of Hazaiah, son of Adaiah, son of Joiarib, son of Zechariah, son of the Shilonite.
6 Wana wote wa Peresi waliokaa Yerusalemu walikuwa 468. Walikuwa masujaa.
All the sons of Perez who were dwelling in Jerusalem, four hundred and sixty-eight, men of ability.
7 Hao ndio wana wa Benyamini, Salu, mwana wa Meshulamu, mwana wa Yoedi, mwana wa Pedaya, mwana wa Kolaya, mwana wa Maaseva, mwana wa Ithieli, mwana wa Yehaya.
And, these, are the sons of Benjamin, —Sallu son of Meshullam, son of Joed, son of Pedaiah, son of Kolaiah, son of Maaseiah, son of Ithiel, son of Jeshaiah;
8 Na baada yake, Gabai na Salai, watu 928.
and, after him, Gabbai, Sallai, —nine hundred and twenty-eight.
9 Yoeli mwana wa Zikri alikuwa mwangalizi wao; na Yuda mwana wa Hasenua alikuwa mkuu wa pili juu ya mji.
And, Joel son of Zichri, was in charge over them, —and, Judah son of Hassenuah, was over the city, as second.
10 Kutoka kwa makuhani Yedaya, mwana wa Yoyaribu, Yakini,
Of the priests, Jedaiah son of Joiarib, Jachin;
11 Seraya mwana wa Hilikia, mwana wa Meshulamu, mwana wa Sadoki, mwana wa Merayoti, mwana wa Ahitubu, mkuu wa nyumba ya Mungu,
Seraiah son of Hilkiah, son of Meshullam, son of Zadok, son of Meraioth, son of Ahitub, chief ruler of the house of God;
12 na wenzake waliofanya kazi ya ukoo, watu 822. na Adaya mwana wa Yerohamu, mwana wa Pelalia, mwana wa Amzi, mwana wa Zekaria, mwana wa Pashuri, mwana wa Malkiya.
and their brethren who were doing the work of the house, eight hundred and twenty-two, —and Adaiah son of Jeroham, son of Pelaliah, son of Amzi, son of Zechariah, son of Pashhur, son of Malchijah;
13 Nao walikuwa washirika wake waliokuwa wakuu wa jamaa, wanaume 242, na Maasai mwana wa Azareli, mwana wa Azai, mwana wa Meshilemothi, mwana wa Imeri;
and his brethren, ancestral chiefs, two hundred and forty-two, —and Amashsai son of Azarel, son of Ahzai, son of Meshillemoth, son of Immer;
14 na ndugu zao, 128 wapiganaji wenye ujasiri, wenye ujasiri; Waziri wao aliyeongoza alikuwa Zabdieli, mwana wa Hageoli.
and their brethren, strong men of ability, a hundred and twenty-eight, —and, he who was in charge of them, was Zabdiel, son of Haggedolim.
15 Na Walawi Shemaya mwana wa Hashubu, mwana wa Azrikamu, mwana wa Hashabia, mwana wa Buni,
And, of the Levites, Shemaiah son of Hasshub, son of Azrikam, son of Hashabiah, son of Bunni;
16 na Shabethai, na Yozabadi, ambao walikuwa ni viongozi wa Walawi, waliosimamia kazi za nje ya nyumba ya Mungu.
and Shabbethai and Jozabad, over the outside business of the house of God, of the chiefs of the Levites;
17 Alikuwepo Matania, mwana wa Mika, mwana wa Zakri, mwana wa Asafu, aliyekuwa mkurugenzi aliyeanza shukrani kwa sala, na Bakbukia, wa pili miongoni mwa ndugu zake, na Abda mwana wa Shemaya, mwana wa Galali, mwana wa Yeduthuni.
and Mattaniah son of Mica, son of Zabdi, son of Asaph, leader of the praise who giveth thanks, in prayer, and Bakbukiah the second among his brethren, —and Obadiah son of Shemaiah, son of Galal, son of Jeduthun.
18 Katika mji wote mtakatifu walikuwa Walawi 284.
All the Levites in the holy city, were two hundred and eighty-four.
19 Walinzi wa malango Akubu, Talmoni, na washirika wao, ambao waliolinda milango, wanaume 172.
And, the door-keepers—Akkub, Talmon, and their brethren who were keeping watch in the gates, were a hundred and seventy-two.
20 Na wale waliosalia wa Israeli, na makuhani, na Walawi, walikuwa katika miji yote ya Yuda. Kila mtu aliishi katika milki yake mwenyewe.
But, the residue of Israel, the priests, the Levites, were in all the cities of Judah, every one in his inheritance.
21 Wafanyakazi wa hekalu waliishi Ofeli, na Siha na Gishpa walikuwa wakiwaongoza.
Howbeit, the Nethinim, were dwelling in Ophel, —and, Ziha and Gishpa, were over the Nethinim.
22 Mtawala mkuu juu ya Walawi waliokuwa wakitumikia Yerusalemu alikuwa Uzi mwana wa Bani, mwana wa Hashabia, mwana wa Matania, mwana wa Mika, wa wana wa Asafu, ambao walikuwa waimbaji wa kazi katika nyumba ya Mungu.
And, the overseer of the Levites in Jerusalem, was Uzzi son of Bani, son of Hashabiah, son of Mattaniah, son of Mica, —of the sons of Asaph the singers, to take lead in the business of the house of God.
23 Walikuwa chini ya maagizo kutoka kwa mfalme na maagizo imara yalitolewa kwa waimbaji kila siku inavyohitajika.
For, the commandment of the king, was upon them, —as to a fixed provision for the singers, the need of a day upon its day.
24 Pethahia mwana wa Meshezabeli, mwana wa Zera, mwana wa Yuda, alikuwa upande wa mfalme kwa habari zote za watu.
And, Pethahiah son of Meshezabel, of the sons of Zerah, son of Judah, was at the hand of the king, in every matter pertaining to the people.
25 Kuhusu vijiji na mashamba yao, baadhi ya watu wa Yuda wakakaa Kiriath-arba, na vijiji vyake, na Diboni, na vijiji vyake, na Yekabzeeli na vijiji vyake.
And, as for the villages in their fields, some of the sons of Judah, dwelt in Kiriath-arba, and the hamlets thereof, and in Dibon, and the hamlets thereof, and in Jekabzeel, and the villages thereof;
26 Wakaishi katika Yeshua, Molada, Beth-Peleti,
and in Jeshua, and in Moladah, and in Beth-pelet;
27 Hazar-Shuali, Beersheba na vijiji vyake.
and in Hazar-shual, and in Beer-sheba, and the hamlets thereof;
28 Nao wakakaa Siklagi, na Mekona, na vijiji vyake,
and in Ziklag, and in Meconah, and in the hamlets thereof,
29 Enrimoni, Sora, Yarmuthi,
and in En-rimmmon, and in Zorah, and in Jarmuth;
30 Zanoa, Adulamu, na vijiji vyake, na Lakishi, na mashamba yake, na Azeka, na vijiji vyake. Basi wakakaa kutoka Beer-sheba mpaka bonde la Hinomu.
Zanoah, Adullam and their villages, Lachish, and the fields thereof, Azekah, and the hamlets thereof, —so they encamped from Beer-sheba, unto the valley of Hinnom.
31 Watu wa Benyamini pia walikuwa wakiishi kutoka Geba, kwenda Mikmashi na Aiya, na Beth-eli na vijiji vyake.
And, the sons of Benjamin, [dwelt] from Geba, to Michmas and Aija, and Bethel, and the hamlets thereof:
32 Waliishi Anathothi, Nobu, Anania,
Anathoth, Nob, Ananiah;
33 Hazori, Rama, Gitaimu,
Hazor, Ramah, Gittaim;
34 Hadidi, Seboimu, Nebalati,
Hadid, Zeboim, Neballat;
35 Lodi, na Ono, bonde la wafundi.
Lod and Ono, the valley of craftsmen.
36 Walawi wengine waliishi Yuda wengine Benyamini.
Howbeit, of the Levites, certain courses of Judah, pertained unto Benjamin.