< Nehemia 11 >
1 Viongozi wa watu waliishi Yerusalemu, na watu wengine walipiga kura ili kuleta mmoja kati ya watu kumi kuishi Yerusalemu, mji mtakatifu, na wengine tisa walibakia katika miji mingine.
And the rulers of the people dwelt in Ierusalem: the other people also cast lottes, to bring one out of ten to dwel in Ierusalem the holy citie, and nine partes to be in the cities.
2 Na watu wakawabariki wote waliojitoa kwa hiari kuishi Yerusalemu.
And the people thanked all the men that were willing to dwell in Ierusalem.
3 Hawa ndio viongozi wa mkoa ambao waliishi Yerusalemu. Hata hivyo, katika miji ya Yuda kila mtu aliishi katika nchi yake mwenyewe, ikiwa ni pamoja na Waisraeli, makuhani, Walawi, watumishi wa hekalu, na wazao wa watumishi wa Sulemani.
These now are the chiefe of the prouince, that dwelt in Ierusalem, but in the cities of Iudah, euery one dwelt in his owne possession in their cities of Israel, the Priestes and the Leuites, and the Nethinims, and the sonnes of Salomons seruants.
4 Katika Yerusalemu waliishi baadhi ya wana wa Yuda na baadhi ya wana wa Benyamini. Watu wa Yuda walikuwa pamoja na Athaya, mwana wa Uzia, mwana wa Zekaria, mwana wa Amaria, mwana wa Shefatia, mwana wa Mahalaleli, mwana wa Peresi.
And in Ierusalem dwelt certaine of the children of Iudah, and of the children of Beniamin. Of the sonnes of Iudah, Athaiah, the sonne of Vziiah, the sonne of Zechariah, the sonne of Amariah, the sonne of Shephatiah, the sonne of Mahaleel, of the sonnes of Perez,
5 Na Maaseya, mwana wa Baruki, mwana wa Kolhoze, mwana wa Hazaya, mwana wa Adaya, mwana wa Yoyaribu, mwana wa Zakaria, mwana wa Mshelani, alikuwa mwana wa Baruki.
And Maaseiah the sonne of Baruch, the sonne of Col Hozeh, the sonne of Hazaiah, the sonne of Adaiah, the sonne of Ioiarib, the sonne of Zechariah, the sonne of Shiloni.
6 Wana wote wa Peresi waliokaa Yerusalemu walikuwa 468. Walikuwa masujaa.
All the sonnes of Perez that dwelt at Ierusalem, were foure hundreth, three score and eight valiant men.
7 Hao ndio wana wa Benyamini, Salu, mwana wa Meshulamu, mwana wa Yoedi, mwana wa Pedaya, mwana wa Kolaya, mwana wa Maaseva, mwana wa Ithieli, mwana wa Yehaya.
These also are the sonnes of Beniamin, Sallu, the sonne of Meshullam, the sonne of Ioed, the sonne of Pedaiah, the sonne of Kolaiah, the sonne of Maaseiah, the sonne of Ithiel, the sonne of Ieshaiah.
8 Na baada yake, Gabai na Salai, watu 928.
And after him Gabai, Sallai, nine hundreth and twentie and eight.
9 Yoeli mwana wa Zikri alikuwa mwangalizi wao; na Yuda mwana wa Hasenua alikuwa mkuu wa pili juu ya mji.
And Ioel the sonne of Zichri was gouernour ouer them: and Iudah, the sonne of Senuah was the second ouer the citie:
10 Kutoka kwa makuhani Yedaya, mwana wa Yoyaribu, Yakini,
Of the Priestes, Iedaiah, the sonne of Ioiarib, Iachin.
11 Seraya mwana wa Hilikia, mwana wa Meshulamu, mwana wa Sadoki, mwana wa Merayoti, mwana wa Ahitubu, mkuu wa nyumba ya Mungu,
Seraiah, the sonne of Hilkiah, the sonne of Meshullam, the sonne of Zadok, the sonne of Meraioth, the sonne of Ahitub was chiefe of the house of God.
12 na wenzake waliofanya kazi ya ukoo, watu 822. na Adaya mwana wa Yerohamu, mwana wa Pelalia, mwana wa Amzi, mwana wa Zekaria, mwana wa Pashuri, mwana wa Malkiya.
And their brethren that did the worke in the Temple, were eight hundreth, twenty and two: and Adaiah, the sonne of Ieroham, the sonne of Pelaliah, the sonne of Amzi, the sonne of Zechariah, the sonne of Pashur, the sonne of Malchiah:
13 Nao walikuwa washirika wake waliokuwa wakuu wa jamaa, wanaume 242, na Maasai mwana wa Azareli, mwana wa Azai, mwana wa Meshilemothi, mwana wa Imeri;
And his brethren, chiefe of the fathers, two hundreth and two and fourtie: and Amashsai the sonne of Azareel, the sonne of Ahazai, the sonne of Meshilemoth, the sonne of Immer:
14 na ndugu zao, 128 wapiganaji wenye ujasiri, wenye ujasiri; Waziri wao aliyeongoza alikuwa Zabdieli, mwana wa Hageoli.
And their brethren valiant men, an hundreth and eight and twentie: and their ouerseer was Zabdiel the sonne of Hagedolim.
15 Na Walawi Shemaya mwana wa Hashubu, mwana wa Azrikamu, mwana wa Hashabia, mwana wa Buni,
And of the Leuites, Shemaiah, the sonne of Hashub, the sonne of Azrikam, the sonne of Hashabiah, the sonne of Bunni.
16 na Shabethai, na Yozabadi, ambao walikuwa ni viongozi wa Walawi, waliosimamia kazi za nje ya nyumba ya Mungu.
And Shabbethai, and Iozabad of the chiefe of the Leuites were ouer the workes of the house of God without.
17 Alikuwepo Matania, mwana wa Mika, mwana wa Zakri, mwana wa Asafu, aliyekuwa mkurugenzi aliyeanza shukrani kwa sala, na Bakbukia, wa pili miongoni mwa ndugu zake, na Abda mwana wa Shemaya, mwana wa Galali, mwana wa Yeduthuni.
And Mattaniah, the sonne of Micha, the sonne of Zabdi, the sonne of Asaph was the chiefe to begin the thankesgiuing and prayer: and Bakbukiah the second of his brethren, and Abda, the sonne of Shammua, the sonne of Galal, the sonne of Ieduthun.
18 Katika mji wote mtakatifu walikuwa Walawi 284.
All the Leuites in the holy citie were two hundreth foure score and foure.
19 Walinzi wa malango Akubu, Talmoni, na washirika wao, ambao waliolinda milango, wanaume 172.
And the porters Akkub, Talmon and their brethren that kept the gates, were an hundreth twentie and two.
20 Na wale waliosalia wa Israeli, na makuhani, na Walawi, walikuwa katika miji yote ya Yuda. Kila mtu aliishi katika milki yake mwenyewe.
And the residue of Israel, of the Priests, and of the Leuites dwelt in al the cities of Iudah, euery one in his inheritance.
21 Wafanyakazi wa hekalu waliishi Ofeli, na Siha na Gishpa walikuwa wakiwaongoza.
And the Nethinims dwelt in the fortresse, and Ziha, and Gispa was ouer the Nethinims.
22 Mtawala mkuu juu ya Walawi waliokuwa wakitumikia Yerusalemu alikuwa Uzi mwana wa Bani, mwana wa Hashabia, mwana wa Matania, mwana wa Mika, wa wana wa Asafu, ambao walikuwa waimbaji wa kazi katika nyumba ya Mungu.
And the ouerseer of the Leuites in Ierusalem was Vzzi the sonne of Bani, the sonne of Ashabiah, the sonne of Mattaniah, the sonne of Micha: of the sonnes of Asaph singers were ouer the worke of the house of God.
23 Walikuwa chini ya maagizo kutoka kwa mfalme na maagizo imara yalitolewa kwa waimbaji kila siku inavyohitajika.
For it was the Kings commandement cocerning them, that faithfull prouision shoulde bee for the singers euery day.
24 Pethahia mwana wa Meshezabeli, mwana wa Zera, mwana wa Yuda, alikuwa upande wa mfalme kwa habari zote za watu.
And Pethahiah the sonne of Meshezabeel, of the sonnes of Zerah, the sonne of Iudah was at the Kings hand in all matters concerning the people.
25 Kuhusu vijiji na mashamba yao, baadhi ya watu wa Yuda wakakaa Kiriath-arba, na vijiji vyake, na Diboni, na vijiji vyake, na Yekabzeeli na vijiji vyake.
And in the villages in their landes, some of the children of Iudah dwelt in Kiriath-arba, and in the villages thereof, and in Dibon, and in the villages thereof, and in Iekabzeel. and in the villages thereof,
26 Wakaishi katika Yeshua, Molada, Beth-Peleti,
And in Ieshua, and in Moladah, and in Beth palet,
27 Hazar-Shuali, Beersheba na vijiji vyake.
And in Hazer-shual, and in Beer-sheba, and in the villages thereof,
28 Nao wakakaa Siklagi, na Mekona, na vijiji vyake,
And in Ziklag, and in Mechonah, and in the villages thereof,
29 Enrimoni, Sora, Yarmuthi,
And in En-rimmon, and in Zareah, and in Iarmuth,
30 Zanoa, Adulamu, na vijiji vyake, na Lakishi, na mashamba yake, na Azeka, na vijiji vyake. Basi wakakaa kutoka Beer-sheba mpaka bonde la Hinomu.
Zanoah, Adullam, and in their villages, in Lachish, and in the fieldes thereof, at Azekah, and in the villages thereof: and they dwelt from Beer-sheba, vnto the valley of Hinnom.
31 Watu wa Benyamini pia walikuwa wakiishi kutoka Geba, kwenda Mikmashi na Aiya, na Beth-eli na vijiji vyake.
And the sonnes of Beniamin from Geba, in Michmash, and Aiia, and Beth-el, and in the villages thereof,
32 Waliishi Anathothi, Nobu, Anania,
Anathoth, Nob, Ananiah,
33 Hazori, Rama, Gitaimu,
Hazor, Ramah, Gittaim,
34 Hadidi, Seboimu, Nebalati,
Hadid, Zeboim, Nebalat,
35 Lodi, na Ono, bonde la wafundi.
Lod and Ono, in the carpenters valley.
36 Walawi wengine waliishi Yuda wengine Benyamini.
And of the Leuites were diuisions in Iudah and in Beniamin.