< Nahumu 3 >

1 Ole kwa mji uliojaa damu! Wote umejaa uongo na mali za wizi; wahanga wapo kwake daima.
Ô ville de sang, toute pleine de mensonges et d'iniquités, tes rapines ne s'amoncelleront plus.
2 Lakini sasa kunasauti ya mijeledi na sauti za kugongesha matairi, farasi wakicheza, na magari ya vita yanaruka ruka.
Voilà le bruit des fouets, le bruit des roues ébranlées, des chevaux lancés, des chars frémissants et des cavaliers en marche;
3 Kuna wapanda farasi wanashambulia, Upanga unang'ara, mikuki inametameta, marundo ya maiti, mafungu makubwa ya miili; hakuna ukomo wa miili, washambuliaji wanajikwaa juu yake.
voilà le glaive étincelant, l'armure brillante de la multitude des blessés, et une ruine profonde. Et ses peuples étaient sans nombre, mais ils ont énervé leurs corps dans la multitude de leurs prostitutions.
4 Hii inatokea kwa sababu ya matendo ya tamaa ya kahaba mzuri, mzoefu wa uchawi, mwenye kuuza taifa kwa umalaya wake, na watu kwa njia ya matendo yake ya kichawi.
Courtisane belle et gracieuse, reine des enchantements, tu vendais les peuples par tes débauches, et les nations par tes sortilèges.
5 “Tazama, mimi nipo kinyume na wewe- hili ni neno la Yehova wa majeshi- sketi yako nitaiinua juu ya uso wako na kuzionyesha sehemu zako za siri kwa mataifa, aibu yako kwa falme.
Et voilà que Je M'attaque à toi, dit le Seigneur Dieu tout-puissant; Je dévoilerai tes nudités à tous les yeux, Je montrerai aux nations ta honte, et aux royaumes ton opprobre.
6 Nitarusha uchafu wa kuchukiza na kukufanya uwe mbaya sana; nitakufanya uwe mtu wa kutazamwa na kila mmoja.
Et Je ferai retomber sur toi l'abomination que méritent tes impuretés, et Je ferai de toi un exemple.
7 Itakuwa kwamba kila mmoja anayekutazama atakukimbia na kusema, “Ninawi ameharibika; ni nani ataomboleza kwa ajili yake?' Ni wapi nitampata mtu anayeweza kukufariji?”
Et il arrivera que tout homme, en te voyant, s'éloignera de toi, disant: Malheureuse Ninive, qui se lamentera sur elle? Où chercher pour elle une consolation?
8 Ninawi, je wewe ni bora kuliko Noamoni, uliojengwa juu ya Mto Naili, uliokuwa umezungukwa na maji, ambao ulinzi wake ilikuwa bahari, ambao ukuta wake ilikuwa bahari yenyewe?
Prépare ta partie, ajuste tes cordes, prépare ta partie pour Ammon, qui demeure au milieu des fleuves; les flots l'entourent; la mer est son empire, et l'eau lui sert de remparts,
9 Ethiopia na Misri zilikuwa nguvu zake, na mwisho wake haukuwepo; Putu na Libya walikuwa rafiki zake.
et l'Éthiopie est sa force, et aussi l'Égypte; et pourtant il n'y aura pas de terme à sa fuite. En vain les Libyens sont ses auxiliaires.
10 Lakini Noamoni alichukuliwa; alikwenda kwenye mateka; watoto wake wadogo walivunjwa vipande vipande katika kila makao makuu ya mtaa; adui zake walipiga kura kwa watu wake wenye heshima na wakuu wake wote walifungwa minyororo.
Elle-même sera transportée captive, et ses enfants seront écrasés à terre, à l'entrée de toutes les rues, et l'on se partagera au sort toutes les richesses qui faisaient sa gloire; et tous ses grands auront les mains chargées de chaînes.
11 Wewe pia utalewa; utajaribu kujificha, na utatafuta makimbilio kutoka kwa adui yako.
Et toi, tu seras enivrée, et tu seras méprisée, et tu solliciteras l'appui de tes propres ennemis.
12 Ngome zako zote zitakuwa kama mitini yenye tini zilizoiva mapema: kama zikitikiswa, zitaangukia kwenye kimywa cha mlaji.
Toutes tes forteresses seront comme des figuiers gardés; si on les secoue, les figues tombent dans la bouche et sont mangées.
13 Tazama, watu miongoni mwenu ni wanawake; malango ya nchi yako yamefunguliwa sana kwa ajili ya adui zako; moto umeharibu bawaba zake.
Voilà que ton peuple sera comme un peuple de femmes; les portes de ton pays seront ouvertes à tes ennemis; le feu consumera tes barrières.
14 Nenda ukachote maji kwenye boma iliyozingirwa; ziimarishe ngome zako; nenda kwenye udongo na kandamiza matope; finyanga kwa ajili ya matofali.
Tire de l'eau pour soutenir un siège; fortifie tes remparts; entre dans l'argile; foule-la aux pieds; mêle-la de lits de paille; sois toi-même plus ferme que la brique.
15 Moto utakuteketeza pale, na upanga utakuangamiza. Utateketezwa kama nzige wachanga wanavyoteketeza kila kitu. Ninyi wenyewe mjitengeneze kuwa wengi kama nzige wachanga, na wengi kama nzinge waliopevuka.
C'est là que la flamme te dévorera, que le glaive te détruira; comme une nuée de sauterelles tu seras engloutie; tu seras appesantie comme de grandes sauterelles.
16 Umezidisha wafanyabiashara wako zaidi kuliko nyota mbinguni; lakini wapo kama tunutu: wanapora nchi na kisha kuruka kwenda mbali.
Tu as multiplié tes marchandises plus que les étoiles du ciel; la nuée de sauterelles les a attaquées et s'est envolée.
17 Wafalme wenu wapo wengi kama zinge, na wakuu wenu wa majeshi ni kama kundi la wadudu wenye kuweka kambi katika ukuta wakati wa baridi. Lakini jua linapowaka wanaruka kwenda mbali ambako hakuna anayepajua.
La multitude étrangère mêlée à toi s'est enfuie comme l'escarbot, ou comme la sauterelle perchée sur la haie un jour de gelée; le soleil s'élève, elle saute dehors, et nul ne sait où elle s'était posée. Malheur à eux!
18 Mfalme wa Ashuru, wachungaji wako wamelala; watawala wako wamejilaza chini kupumzika. Watu wako wametawanyika juu ya milima, na hakuna hata mmoja wa kuwakusanya.
Tes pasteurs se sont assoupis; ton roi assyrien s'est endormi avec tes hommes de guerre; ton peuple s'est enfui sur les montagnes, et nul n'était là pour lui donner asile.
19 Hakuna uponyaji unaowezekana kwa ajili ya vidonda vyako. Vidonda vyako ni vikubwa. Wanaosikia habari juu yako watapiga makofi kwa furaha juu yako. Ni nani aliyejiepusha kwa uovu wako wa daima?
Il n'est point de guérison pour tes blessures, ta plaie s'est enflammée; tous ceux qui entendent parler de tes malheurs battent des mains; car contre qui n'as-tu pas constamment tourné ta scélératesse?

< Nahumu 3 >