< Nahumu 3 >

1 Ole kwa mji uliojaa damu! Wote umejaa uongo na mali za wizi; wahanga wapo kwake daima.
Malheur à la ville sanglante! Elle n'est que mensonges et rapines, et la proie est sans fin.
2 Lakini sasa kunasauti ya mijeledi na sauti za kugongesha matairi, farasi wakicheza, na magari ya vita yanaruka ruka.
Le bruit du fouet, le bruit des roues, des chevaux cabrés, des chars bondissants,
3 Kuna wapanda farasi wanashambulia, Upanga unang'ara, mikuki inametameta, marundo ya maiti, mafungu makubwa ya miili; hakuna ukomo wa miili, washambuliaji wanajikwaa juu yake.
des cavaliers qui chargent, l'épée étincelante, la lance étincelante, une multitude de morts, un grand monceau de cadavres, et les cadavres n'en finissent pas. Ils trébuchent sur leurs corps
4 Hii inatokea kwa sababu ya matendo ya tamaa ya kahaba mzuri, mzoefu wa uchawi, mwenye kuuza taifa kwa umalaya wake, na watu kwa njia ya matendo yake ya kichawi.
à cause de la multitude de la prostitution de la séduisante prostituée, la maîtresse de la sorcellerie, qui vend des nations par sa prostitution, et des familles par sa sorcellerie.
5 “Tazama, mimi nipo kinyume na wewe- hili ni neno la Yehova wa majeshi- sketi yako nitaiinua juu ya uso wako na kuzionyesha sehemu zako za siri kwa mataifa, aibu yako kwa falme.
« Voici, je suis contre toi, dit Yahvé des armées, et je lèverai tes jupes au-dessus de ton visage. Je montrerai aux nations ta nudité, Et aux royaumes ta honte.
6 Nitarusha uchafu wa kuchukiza na kukufanya uwe mbaya sana; nitakufanya uwe mtu wa kutazamwa na kila mmoja.
Je jetterai sur toi des souillures abominables, je te rendrai infâme, et je ferai de toi un spectacle.
7 Itakuwa kwamba kila mmoja anayekutazama atakukimbia na kusema, “Ninawi ameharibika; ni nani ataomboleza kwa ajili yake?' Ni wapi nitampata mtu anayeweza kukufariji?”
Tous ceux qui te regarderont s'enfuiront loin de toi, et diront: « Ninive est dévastée! Qui la pleurera? Où chercherai-je pour vous des consolateurs? »
8 Ninawi, je wewe ni bora kuliko Noamoni, uliojengwa juu ya Mto Naili, uliokuwa umezungukwa na maji, ambao ulinzi wake ilikuwa bahari, ambao ukuta wake ilikuwa bahari yenyewe?
Vaux-tu mieux que No-Amon, qui était située parmi les fleuves, qui était entourée par les eaux, dont le rempart était la mer, et dont la muraille était la mer?
9 Ethiopia na Misri zilikuwa nguvu zake, na mwisho wake haukuwepo; Putu na Libya walikuwa rafiki zake.
Cush et l'Égypte étaient sa force illimitée. Put et la Libye étaient ses soutiens.
10 Lakini Noamoni alichukuliwa; alikwenda kwenye mateka; watoto wake wadogo walivunjwa vipande vipande katika kila makao makuu ya mtaa; adui zake walipiga kura kwa watu wake wenye heshima na wakuu wake wote walifungwa minyororo.
Mais elle a été emportée. Elle est allée en captivité. On a écrasé ses petits enfants à la tête de toutes les rues, On a tiré au sort ses grands, Et tous ses grands ont été enchaînés.
11 Wewe pia utalewa; utajaribu kujificha, na utatafuta makimbilio kutoka kwa adui yako.
Vous aussi, vous serez ivres. Vous vous cacherez. Toi aussi, tu chercheras une forteresse à cause de l'ennemi.
12 Ngome zako zote zitakuwa kama mitini yenye tini zilizoiva mapema: kama zikitikiswa, zitaangukia kwenye kimywa cha mlaji.
Toutes vos forteresses seront comme des figuiers avec les premières figues mûres. Si on les secoue, elles tombent dans la bouche de celui qui les mange.
13 Tazama, watu miongoni mwenu ni wanawake; malango ya nchi yako yamefunguliwa sana kwa ajili ya adui zako; moto umeharibu bawaba zake.
Voici, tes troupes au milieu de toi sont des femmes. Les portes de ton pays sont grandes ouvertes à tes ennemis. Le feu a dévoré tes barres.
14 Nenda ukachote maji kwenye boma iliyozingirwa; ziimarishe ngome zako; nenda kwenye udongo na kandamiza matope; finyanga kwa ajili ya matofali.
Tirez de l'eau pour le siège. Renforcez vos forteresses. Entrez dans l'argile, et foulez le mortier. Fortifiez le four à briques.
15 Moto utakuteketeza pale, na upanga utakuangamiza. Utateketezwa kama nzige wachanga wanavyoteketeza kila kitu. Ninyi wenyewe mjitengeneze kuwa wengi kama nzige wachanga, na wengi kama nzinge waliopevuka.
Là, le feu vous dévorera, l'épée vous tranchera. L'épée te tranchera. Elle vous dévorera comme la sauterelle. Multipliez comme les sauterelles. Multipliez comme les sauterelles, Multipliez comme les criquets.
16 Umezidisha wafanyabiashara wako zaidi kuliko nyota mbinguni; lakini wapo kama tunutu: wanapora nchi na kisha kuruka kwenda mbali.
Vous avez multiplié vos marchands plus que les étoiles des cieux. La sauterelle se dépouille et s'enfuit.
17 Wafalme wenu wapo wengi kama zinge, na wakuu wenu wa majeshi ni kama kundi la wadudu wenye kuweka kambi katika ukuta wakati wa baridi. Lakini jua linapowaka wanaruka kwenda mbali ambako hakuna anayepajua.
Tes gardes sont comme les sauterelles, et tes fonctionnaires comme les essaims de sauterelles, qui se posent sur les murs par un jour froid, mais dès que le soleil paraît, ils s'enfuient, et on ne sait pas où ils sont.
18 Mfalme wa Ashuru, wachungaji wako wamelala; watawala wako wamejilaza chini kupumzika. Watu wako wametawanyika juu ya milima, na hakuna hata mmoja wa kuwakusanya.
Tes bergers sommeillent, roi d'Assyrie. Tes nobles se couchent. Ton peuple est dispersé sur les montagnes, et il n'y a personne pour le rassembler.
19 Hakuna uponyaji unaowezekana kwa ajili ya vidonda vyako. Vidonda vyako ni vikubwa. Wanaosikia habari juu yako watapiga makofi kwa furaha juu yako. Ni nani aliyejiepusha kwa uovu wako wa daima?
On ne peut pas guérir ta blessure, car ta blessure est mortelle. Tous ceux qui entendent parler de toi battent des mains sur toi, car qui n'a pas ressenti ta cruauté sans fin?

< Nahumu 3 >