< Nahumu 3 >
1 Ole kwa mji uliojaa damu! Wote umejaa uongo na mali za wizi; wahanga wapo kwake daima.
Woe to the city of blood! it is all full of lies and robbery; never ceaseth the preying;
2 Lakini sasa kunasauti ya mijeledi na sauti za kugongesha matairi, farasi wakicheza, na magari ya vita yanaruka ruka.
The noise of a whip, and the noise of the rattling of wheels, and of prancing horses, and of the skipping chariots.
3 Kuna wapanda farasi wanashambulia, Upanga unang'ara, mikuki inametameta, marundo ya maiti, mafungu makubwa ya miili; hakuna ukomo wa miili, washambuliaji wanajikwaa juu yake.
Horsemen mount, and there are the flaming sword and the glittering spear: and there is a multitude of slain, and heaps of carcasses; and without end are the corpses; they stumble on their corpses;
4 Hii inatokea kwa sababu ya matendo ya tamaa ya kahaba mzuri, mzoefu wa uchawi, mwenye kuuza taifa kwa umalaya wake, na watu kwa njia ya matendo yake ya kichawi.
Because of the multitude of the lewd deeds of the harlot, that is rich in gracefulness, the mistress of witchcrafts, that selleth nations through her lewd deeds, and families through her witchcrafts.
5 “Tazama, mimi nipo kinyume na wewe- hili ni neno la Yehova wa majeshi- sketi yako nitaiinua juu ya uso wako na kuzionyesha sehemu zako za siri kwa mataifa, aibu yako kwa falme.
Behold, I will be against thee, saith the Lord of hosts; and I will lay thy skirts open over thy face, and I will let nations see thy nakedness, and kingdoms thy shame.
6 Nitarusha uchafu wa kuchukiza na kukufanya uwe mbaya sana; nitakufanya uwe mtu wa kutazamwa na kila mmoja.
And I will cast abominable filth upon thee, and defile thee, and will render thee a dirt-heap.
7 Itakuwa kwamba kila mmoja anayekutazama atakukimbia na kusema, “Ninawi ameharibika; ni nani ataomboleza kwa ajili yake?' Ni wapi nitampata mtu anayeweza kukufariji?”
And it shall come to pass, that all they that see thee shall flee from thee, and say, Laid waste is Nineveh: who will condole with her? whence shall I seek comforters for thee?
8 Ninawi, je wewe ni bora kuliko Noamoni, uliojengwa juu ya Mto Naili, uliokuwa umezungukwa na maji, ambao ulinzi wake ilikuwa bahari, ambao ukuta wake ilikuwa bahari yenyewe?
Art thou better than No-amon, that was situated on the rivers, that had water round about her, the rampart of which was the sea, and the walls of which rose out of the sea?
9 Ethiopia na Misri zilikuwa nguvu zake, na mwisho wake haukuwepo; Putu na Libya walikuwa rafiki zake.
Ethiopia the numerous, and Egypt that was without end, Put and Lubim were thy helpers.
10 Lakini Noamoni alichukuliwa; alikwenda kwenye mateka; watoto wake wadogo walivunjwa vipande vipande katika kila makao makuu ya mtaa; adui zake walipiga kura kwa watu wake wenye heshima na wakuu wake wote walifungwa minyororo.
Yet also she was exiled, was carried away into captivity; also her young children were dashed in pieces at the corners of all streets: and for her honorable men they cast lots, and all her great ones were bound with chains.
11 Wewe pia utalewa; utajaribu kujificha, na utatafuta makimbilio kutoka kwa adui yako.
Thou also shalt be made drunken, thou shalt be hidden from view: thou also shalt seek refuge because of the enemy.
12 Ngome zako zote zitakuwa kama mitini yenye tini zilizoiva mapema: kama zikitikiswa, zitaangukia kwenye kimywa cha mlaji.
All thy strong-holds shall be like fig-trees with the first ripe figs, which, if they be shaken, will fall into the mouth of the eater.
13 Tazama, watu miongoni mwenu ni wanawake; malango ya nchi yako yamefunguliwa sana kwa ajili ya adui zako; moto umeharibu bawaba zake.
Behold, thy people are become women in the midst of thee: unto thy enemies are the gates of thy land set wide open; the fire hath devoured thy bars.
14 Nenda ukachote maji kwenye boma iliyozingirwa; ziimarishe ngome zako; nenda kwenye udongo na kandamiza matope; finyanga kwa ajili ya matofali.
Water for the siege draw for thyself, fortify thy strongholds: go into the clay, and tread the mortar, make strong the brick-kiln.
15 Moto utakuteketeza pale, na upanga utakuangamiza. Utateketezwa kama nzige wachanga wanavyoteketeza kila kitu. Ninyi wenyewe mjitengeneze kuwa wengi kama nzige wachanga, na wengi kama nzinge waliopevuka.
There shall the fire devour thee; the sword shall cut thee off, it shall devour thee up like the cankerworm: [though] thou make thyself many as the cankerworm; make thyself many as the locusts.
16 Umezidisha wafanyabiashara wako zaidi kuliko nyota mbinguni; lakini wapo kama tunutu: wanapora nchi na kisha kuruka kwenda mbali.
[Though] thou hadst multiplied thy merchants more than the stars of heaven: the cankerworm spreadeth itself out, and flieth away.
17 Wafalme wenu wapo wengi kama zinge, na wakuu wenu wa majeshi ni kama kundi la wadudu wenye kuweka kambi katika ukuta wakati wa baridi. Lakini jua linapowaka wanaruka kwenda mbali ambako hakuna anayepajua.
Thy crowned ones are like the locusts, and thy leaders like the swarms of locusts, which camp in the hedges on a cold day, but when the sun ariseth they flee away, and their place is not known where they are.
18 Mfalme wa Ashuru, wachungaji wako wamelala; watawala wako wamejilaza chini kupumzika. Watu wako wametawanyika juu ya milima, na hakuna hata mmoja wa kuwakusanya.
Thy shepherds slumber, O king of Assyria; thy valiant men are at rest: scattered are thy people upon the mountains, and there is none that gathereth them.
19 Hakuna uponyaji unaowezekana kwa ajili ya vidonda vyako. Vidonda vyako ni vikubwa. Wanaosikia habari juu yako watapiga makofi kwa furaha juu yako. Ni nani aliyejiepusha kwa uovu wako wa daima?
There is no healing for thy breach; fatal is thy wound: all that hear the report of thee will clap their hands over thee; for over whom did not thy wickedness pass continually?