< Nahumu 3 >
1 Ole kwa mji uliojaa damu! Wote umejaa uongo na mali za wizi; wahanga wapo kwake daima.
Woe to thee, O city of blood, all full of lies and violence: rapine shall not depart from thee.
2 Lakini sasa kunasauti ya mijeledi na sauti za kugongesha matairi, farasi wakicheza, na magari ya vita yanaruka ruka.
The noise of the whip, and the noise of the rattling of the wheels, and of the neighing horse, and of the running chariot, and of the horsemen coming up,
3 Kuna wapanda farasi wanashambulia, Upanga unang'ara, mikuki inametameta, marundo ya maiti, mafungu makubwa ya miili; hakuna ukomo wa miili, washambuliaji wanajikwaa juu yake.
And of the shining sword, and of the glittering spear, and of a multitude slain, and of a grievous destruction: and there is no end of carcasses, and they shall fall down on their dead bodies.
4 Hii inatokea kwa sababu ya matendo ya tamaa ya kahaba mzuri, mzoefu wa uchawi, mwenye kuuza taifa kwa umalaya wake, na watu kwa njia ya matendo yake ya kichawi.
Because of the multitude of the fornications of the harlot that was beautiful and agreeable, and that made use of witchcraft, that sold nations through her fornications, and families through her witchcrafts.
5 “Tazama, mimi nipo kinyume na wewe- hili ni neno la Yehova wa majeshi- sketi yako nitaiinua juu ya uso wako na kuzionyesha sehemu zako za siri kwa mataifa, aibu yako kwa falme.
Behold I come against thee, saith the Lord of hosts: and I will discover thy shame to thy face, and will shew thy nakedness to the nations, and thy shame to kingdoms.
6 Nitarusha uchafu wa kuchukiza na kukufanya uwe mbaya sana; nitakufanya uwe mtu wa kutazamwa na kila mmoja.
And I will cast abominations upon thee, and will disgrace thee, and will make an example of thee.
7 Itakuwa kwamba kila mmoja anayekutazama atakukimbia na kusema, “Ninawi ameharibika; ni nani ataomboleza kwa ajili yake?' Ni wapi nitampata mtu anayeweza kukufariji?”
And it shall come to pass that every one that shall see thee, shall flee from thee, and shall say: Ninive is laid waste: who shall bemoan thee? whence shall I seek a comforter for thee?
8 Ninawi, je wewe ni bora kuliko Noamoni, uliojengwa juu ya Mto Naili, uliokuwa umezungukwa na maji, ambao ulinzi wake ilikuwa bahari, ambao ukuta wake ilikuwa bahari yenyewe?
Art thou better than the populous Alexandria, that dwelleth among the rivers? waters are round about it: the sea is its riches, the waters are its walls.
9 Ethiopia na Misri zilikuwa nguvu zake, na mwisho wake haukuwepo; Putu na Libya walikuwa rafiki zake.
Ethiopia and Egypt were the strength thereof, and there is no end: Africa and the Libyans were thy helpers.
10 Lakini Noamoni alichukuliwa; alikwenda kwenye mateka; watoto wake wadogo walivunjwa vipande vipande katika kila makao makuu ya mtaa; adui zake walipiga kura kwa watu wake wenye heshima na wakuu wake wote walifungwa minyororo.
Yet she also was removed and carried into captivity: her young children were dashed in pieces at the top of every street, and they cast lots upon her nobles, and all her great men were bound in fetters.
11 Wewe pia utalewa; utajaribu kujificha, na utatafuta makimbilio kutoka kwa adui yako.
Therefore thou also shalt be made drunk, and shalt be despised: and thou shalt seek help from the enemy.
12 Ngome zako zote zitakuwa kama mitini yenye tini zilizoiva mapema: kama zikitikiswa, zitaangukia kwenye kimywa cha mlaji.
All thy strong holds shall be like fig trees with their green figs: if they be shaken, they shall fall into the mouth of the eater.
13 Tazama, watu miongoni mwenu ni wanawake; malango ya nchi yako yamefunguliwa sana kwa ajili ya adui zako; moto umeharibu bawaba zake.
Behold thy people in the midst of thee are women: the gates of thy land shall be set wide open to thy enemies, the fire shall devour thy bars.
14 Nenda ukachote maji kwenye boma iliyozingirwa; ziimarishe ngome zako; nenda kwenye udongo na kandamiza matope; finyanga kwa ajili ya matofali.
Draw thee water for the siege, build up thy bulwarks: go into the clay, and tread, work it and make brick.
15 Moto utakuteketeza pale, na upanga utakuangamiza. Utateketezwa kama nzige wachanga wanavyoteketeza kila kitu. Ninyi wenyewe mjitengeneze kuwa wengi kama nzige wachanga, na wengi kama nzinge waliopevuka.
There shall the fire devour thee: thou shalt perish by the sword, it shall devour thee like the bruchus: assemble together like the bruchus, make thyself many like the locust.
16 Umezidisha wafanyabiashara wako zaidi kuliko nyota mbinguni; lakini wapo kama tunutu: wanapora nchi na kisha kuruka kwenda mbali.
Thou hast multiplied thy merchandises above the stars of heaven: the bruchus hath spread himself and flown away.
17 Wafalme wenu wapo wengi kama zinge, na wakuu wenu wa majeshi ni kama kundi la wadudu wenye kuweka kambi katika ukuta wakati wa baridi. Lakini jua linapowaka wanaruka kwenda mbali ambako hakuna anayepajua.
Thy guards are like the locusts: and thy little ones like the locusts of locusts which swarm on the hedges in the day of cold: the sun arose, and they flew away, and their place was not known where they were.
18 Mfalme wa Ashuru, wachungaji wako wamelala; watawala wako wamejilaza chini kupumzika. Watu wako wametawanyika juu ya milima, na hakuna hata mmoja wa kuwakusanya.
Thy shepherds have slumbered, O king of Assyria, thy princes shall be buried: thy people are hid in the mountains, and there is none to gather them together.
19 Hakuna uponyaji unaowezekana kwa ajili ya vidonda vyako. Vidonda vyako ni vikubwa. Wanaosikia habari juu yako watapiga makofi kwa furaha juu yako. Ni nani aliyejiepusha kwa uovu wako wa daima?
Thy destruction is not hidden, thy wound is grievous: all that have heard the fame of thee, have clapped their hands over thee: for upon whom hath not thy wickedness passed continually?