< Nahumu 2 >

1 Yule ambaye atakuharibu vipande vipande anakuja dhidi yako. Linda kuta za mji, linda barabara, jitieni nguvu ninyi wenyewe, yakusanyeni majeshi yenu.
Un destructeur s'avance contre toi; garde la forteresse, surveille le chemin, affermis tes reins, ramasse toute ta force!
2 Maana Yehova anarejesha fahari ya Yakobo, kama fahari ya Israeli, ingawa wateka nyara waliwaharibu na kuharibu matawi ya zabibu zao.
Car Yahweh rétablit la gloire de Jacob, ainsi que la gloire d'Israël, parce que des pillards les ont pillés, et ont détruit leurs ceps.
3 Ngao za mashujaa wake ni nyekundu, na watu hodari wamevaa nguo nyekundu; magari ya vita yameandaliwa yanang'ara kwenye vyuma vyake wakati wa mchana, na mikuki ya mivinje inarushwa hewani.
Le bouclier de ses guerriers est teint en rouge, ses hommes d'armes sont vêtus d'écarlate; dans le feu des aciers ses chars apparaissent, au jour où il prépare la bataille, et les lances s'agitent.
4 Magari ya vita yapo kasi kwenye mitaa; yanakimbia mbele na nyuma katika mitaa. Yapo kama kurunzi, na yanakimbia kama radi.
Dans les rues les chars s'élancent avec furie; ils se précipitent sur les places. Leur aspect est celui des flammes, des éclairs qui courent.
5 Yule ambaye atakuvunja vipande vipande anawaita maafisa wake; wanajikwaa kila mmoja kwa mwingine katika kutembea kwao; wanaharakisha kuushambulia ukuta wa mji. Ngao kubwa imetayarishwa kujikinga na hawa washambuliaji.
Il se souvient de ses nobles; eux trébuchent dans leur marche. Ils se précipitent vers les murs; on se prépare à la défense.
6 Malango kwenye mito yamelazishwa kufunguka, na jumba la mfalme linaanguka kwenye uharibifu.
Les portes des fleuves s'ouvrent, et le palais s'effondre.
7 Husabu amevuliwa mavazi yake na amachukuliwa; watumishi wake wa kike wanaomboleza kama njiwa, wanavipiga vifua vyao.
C'en est fait, elle est mise à nu, elle est emmenée, et ses servantes poussent des gémissements, pareils aux plaintes des colombes; elles se frappent la poitrine.
8 Ninawi ni kama bwawa la maji linalovuja, watu wake kwa pamoja wanakimbia kama maji yanayotiririka. Wengine wanasema, “Simama, simama,” lakini hakuna anayegeuka nyuma.
Ninive est comme un bassin d'eau depuis son origine... Ils s'enfuient!... Arrêtez! Arrêtez!... Pas un ne se retourne!
9 Chukua nyara ya fedha, kuchua nyara ya dhahabu, maana hakuna mwisho wake, kwa fahari ya vitu vyote vizuri vya Ninawi.
Pillez l'argent, pillez l'or! Car il n'y a pas de fin à ses richesses, à l'amas de tous ses objets précieux.
10 Ninawi ipo tupu na imeharibiwa. Moyo wa kila mtu unayeyuka, magoti ya kila mmoja yanagongana pamoja, na uchungu upo kwa kila mmoja; sura zao wote zimepauka.
Vidée, pillée, mise à sec! Les cœurs défaillent, les genoux tremblent; tous les reins sont dans l'angoisse, tous les visages sont livides.
11 Sasa liko wapi pango la simba, sehemu ambapo simba wadogo hula chakula, sehemu ambapo simba dume na simba jike walitembea, pamoja wana-simba, ambapo hawakuogopa kitu chochote?
Où est-il, le repaire des lions, qui était un lieu de pâture pour les jeunes lions; où se retiraient le lion, la lionne et le lionceau, sans que personne les effrayât?
12 Simba alirarua mawindo yake vipande vipande kwa ajili ya watoto wake; aliwanyonga mawindo wake kwa ajili ya wake zake, na kulijaza pango lake mawindo, makao yake kwa mizoga iliyoraruliwa.
Le lion ravissait ce qu'il fallait à ses petits, il étranglait pour ses lionnes, il remplissait de proie ses cavernes, et ses antres de dépouilles.
13 “Tazama, mimi nipo kinyume na wewe- hili ni neno la Yehova wa majeshi. Nitayachoma magari yenu ya vita katika moshi, na upanga utateketeza simba wenu vijana. Nitazuia nyara zenu kutoka kwenye nchi yangu, na sauti za wajumbe wenu hazitasikika tena.”
Me voici contre toi! — oracle de Yahweh des armées; je vais réduire tes chars en fumée; l'épée dévorera tes jeunes lions; j'arracherai du pays ta proie, et l'on n'entendra plus la voix de tes messagers.

< Nahumu 2 >