< Nahumu 1 >

1 Maono kuhusu Ninawi. Kitabu cha maono ya Nahumu, Mwelkoshi.
Ausspruch über Ninive. Das Buch des Gesichtes Nahums, des Elkoschiters.
2 Yehova ni Mungu mwenye wivu na analipa kisasi; Yehova hulipa kisasi na amejaa ghadhabu; Yohova analipiza kisasi kwa adui zake, na huiendeleza hasira yake kwa adui zake.
Ein eifernder und rächender Gott [El] ist Jehova, ein Rächer ist Jehova und voll von Grimm; Jehova übt Rache an seinen Widersachern und trägt seinen Feinden nach.
3 Yehova ni mwenye nguvu nyingi na mpole wa hasira; hatakuwa na namna ya kuacha kuwahesabia hatia adui zake. Yehova hufanya njia yake kwenye upepo wa kisulisuli na dhoruba, na mawingu ni mavumbi ya miguu yake.
Jehova ist langsam zum Zorn und groß an Kraft, und er hält keineswegs für schuldlos [O. läßt keineswegs ungestraft] den Schuldigen. Jehova-im Sturmwind und im Gewitter ist sein Weg, und Gewölk ist der Staub seiner Füße.
4 Huikemea bahari na kuifanya ikauke; hukausha mito yote. Bashani ni dhaifu, na Karmeli pia; maua ya Lebanoni ni dhaifu.
Er schilt das Meer und legt es trocken, und alle Flüsse macht er versiegen; Basan und Karmel verwelken, und es verwelkt die Blüte des Libanon.
5 Milima hutetema kwenye uwepo wake, na vilima huyeyuka; dunia huanguka mbele zake, kabisa, dunia na watu wote wanaoishi ndani yake.
Vor ihm erbeben die Berge und zerfließen die Hügel, und vor seinem Angesicht erhebt sich die Erde [Vergl. Jes. 13,13,] und der Erdkreis und alle, die darauf wohnen.
6 Ni nani anaweza kusimama mbele ya ghadhabu yake? Nani anaweza kuzuia ukali wa hasira yake? Ghadhabu yake imemwagwa kama moto, na miamba ameibomoa mbalimbali.
Wer kann vor seinem Grimme bestehen, und wer standhalten bei der Glut seines Zornes? Sein Grimm ergießt sich wie Feuer, und die Felsen werden von ihm zerrissen.
7 Yehova ni mwema, boma katika siku ya taabu; na yeye ni mwaminifu kwa wale wanaomkimbilia.
Jehova ist gütig, er ist eine Feste [O. ein Schutz, eine Zuflucht] am Tage der Drangsal; und er kennt die, welche auf ihn vertrauen [Eig. die Zuflucht zu ihm nehmen.]
8 Lakini atafanya mwisho wa adui zake kwa mafuriko ya kutisha; atawawinda kwenye giza.
Und mit einer überschwemmenden Flut wird er ihre Stätte [d. i. Ninives] gänzlich zerstören, und Finsternis wird [And. üb.: in [od. mit] Finsternis wird er] seine Feinde verfolgen.
9 Watu wanapanga nini dhidi ya Yehova? Yeye atakomesha; taabu haitainuka mara ya pili.
Was sinnet ihr wider Jehova? [O. [an die Juden gerichtet] Was denket ihr von Jehova?] Er wird gänzlich zerstören; die Drangsal wird nicht zweimal erstehen.
10 Maana watakuwa wamevurugika kama michongoma; wataloweshwa katika kinywaji chao mwenyewe; wataharibiwa kabisa kwa moto kama mashina ya mabua.
Denn wären sie gar wie Dornen verflochten und von ihrem edlen Weine berauscht, sie sollen völlig verzehrt werden wie dürre Stoppeln.
11 Mtu mmoja aliinuka miongoni mwenu, Ninawi, aliyepanga ubaya dhidi ya Yehova, mtu ambaye aliimarisha uovu.
Von dir [d. i. Ninive] ist ausgegangen, der Böses sann wider Jehova, ein nichtswürdiger Ratgeber.
12 Hivi ndivyo anavyosema Yehova, “Hata kama wananguvu zao timilifu na idadi timilifu, hata hivyo watanyolewa, watu wao hawatakuwepo tena. Bali wewe, Yuda: Ingawa nimekutesa, sitakutesa tena.
So spricht Jehova: Wenn sie gleich unversehrt und noch so zahlreich sind, auch so sollen sie weggemäht werden; und er wird dahin sein. -Und habe ich dich [d. i. Juda] auch niedergebeugt, ich werde dich nicht mehr niederbeugen;
13 Sasa nitaivunja ile nira ya watu kutoka kwako; nitaikata minyororo yako.
sondern ich werde nun sein Joch von dir zerbrechen und deine Bande zerreißen. -
14 Yehova ametoa amri juu yako, Ninawi: “Hakutakuwa na kizazi tena chenye kubeba jina lako. Nitazizuia sanamu zilizochongwa na kuziondoa sanamu za chuma kutoka kwenye nyumba za miungu yenu. Nitachimba makaburi yenu, kwa kudharauliwa kwenu.”
Und über dich [d. i. den Assyrer] hat Jehova geboten, daß von deinem Namen nicht mehr gesät werden soll; aus dem Hause deines Gottes werde ich das geschnitzte und das gegossene Bild ausrotten; ich werde dir ein Grab machen, denn verächtlich bist du [O. zu leicht bist du erfunden.]
15 Tazama, juu ya milima kuna miguu ya mtu aletaye habari njema, anayetangaza amani! Sherehekeeni sikukuu zenu, Yuda, na tunzeni nadhiri zenu, kwa maana mwovu hatawavamia tena; ameondolewa kabisa.
Siehe, auf den Bergen die Füße dessen, der gute Botschaft bringt, der Frieden [Zugl.: Heil] verkündigt! Feiere, Juda, deine Feste, bezahle deine Gelübde! denn der Nichtswürdige wird fortan nicht mehr durch dich ziehen; er ist ganz ausgerottet.

< Nahumu 1 >