< Nahumu 1 >
1 Maono kuhusu Ninawi. Kitabu cha maono ya Nahumu, Mwelkoshi.
The prophecy concerning Nineveh. The book of the prophecy of Nahum, the Elkoshite.
2 Yehova ni Mungu mwenye wivu na analipa kisasi; Yehova hulipa kisasi na amejaa ghadhabu; Yohova analipiza kisasi kwa adui zake, na huiendeleza hasira yake kwa adui zake.
Jehovah is a jealous God, and an avenger; Jehovah is an avenger, and full of wrath! Jehovah taketh vengeance on his adversaries, And keepeth indignation for his enemies!
3 Yehova ni mwenye nguvu nyingi na mpole wa hasira; hatakuwa na namna ya kuacha kuwahesabia hatia adui zake. Yehova hufanya njia yake kwenye upepo wa kisulisuli na dhoruba, na mawingu ni mavumbi ya miguu yake.
Jehovah is slow to anger, but great in power; He will by no means clear the guilty; Jehovah cometh in the whirlwind and the storm, And the clouds are the dust of his feet.
4 Huikemea bahari na kuifanya ikauke; hukausha mito yote. Bashani ni dhaifu, na Karmeli pia; maua ya Lebanoni ni dhaifu.
He rebuketh the sea, and maketh it dry, And drieth up all the rivers. Bashan languisheth, and Carmel, And the flower of Lebanon languisheth.
5 Milima hutetema kwenye uwepo wake, na vilima huyeyuka; dunia huanguka mbele zake, kabisa, dunia na watu wote wanaoishi ndani yake.
The mountains tremble before him, And the hills melt; The earth is moved at his presence, Yea, the world and all that dwell therein.
6 Ni nani anaweza kusimama mbele ya ghadhabu yake? Nani anaweza kuzuia ukali wa hasira yake? Ghadhabu yake imemwagwa kama moto, na miamba ameibomoa mbalimbali.
Who can stand before his indignation, And who can abide before the fierceness of his anger? His fury is poured out like fire, And the rocks are cast down by him!
7 Yehova ni mwema, boma katika siku ya taabu; na yeye ni mwaminifu kwa wale wanaomkimbilia.
Jehovah is good, A stronghold in the day of trouble; He careth for them that trust in him;
8 Lakini atafanya mwisho wa adui zake kwa mafuriko ya kutisha; atawawinda kwenye giza.
But with an overwhelming flood will he make a full end of her place, And darkness shall pursue his enemies.
9 Watu wanapanga nini dhidi ya Yehova? Yeye atakomesha; taabu haitainuka mara ya pili.
What do ye meditate against Jehovah? He will make a full end; Not the second time shall the calamity come.
10 Maana watakuwa wamevurugika kama michongoma; wataloweshwa katika kinywaji chao mwenyewe; wataharibiwa kabisa kwa moto kama mashina ya mabua.
For while they are entangled like thorns, And like those that are drunk with wine, They shall be devoured as stubble fully dry.
11 Mtu mmoja aliinuka miongoni mwenu, Ninawi, aliyepanga ubaya dhidi ya Yehova, mtu ambaye aliimarisha uovu.
From thee hath gone forth one that devised evil against Jehovah; That meditated destruction.
12 Hivi ndivyo anavyosema Yehova, “Hata kama wananguvu zao timilifu na idadi timilifu, hata hivyo watanyolewa, watu wao hawatakuwepo tena. Bali wewe, Yuda: Ingawa nimekutesa, sitakutesa tena.
Thus saith Jehovah: Though they be flourishing, and likewise many, Yet shall they be cut down, and pass away; I have afflicted thee, but I will afflict thee no more.
13 Sasa nitaivunja ile nira ya watu kutoka kwako; nitaikata minyororo yako.
For now will I break his yoke from off thee, And will burst thy bonds in sunder.
14 Yehova ametoa amri juu yako, Ninawi: “Hakutakuwa na kizazi tena chenye kubeba jina lako. Nitazizuia sanamu zilizochongwa na kuziondoa sanamu za chuma kutoka kwenye nyumba za miungu yenu. Nitachimba makaburi yenu, kwa kudharauliwa kwenu.”
And concerning thee hath Jehovah given command, That thy name shall no more be sown. From the house of thy god I will cut off the graven image and the molten image; I will make thy grave; for thou hast become vile!
15 Tazama, juu ya milima kuna miguu ya mtu aletaye habari njema, anayetangaza amani! Sherehekeeni sikukuu zenu, Yuda, na tunzeni nadhiri zenu, kwa maana mwovu hatawavamia tena; ameondolewa kabisa.
Behold upon the mountains the feet of him that bringeth good tidings, That publisheth peace! Keep, O Judah, thy feasts, perform thy vows! For no more shall the destroyer pass through thee; He is utterly consumed.