< Mika 1 >

1 Hili ni neno la Yahwe ambalo lilikuja kwa Mika Mmorashti katika siku za Yotahamu, Ahazi, na Hezekeia, mfalme wa Yuda, lile neno aliloliona kuhusiana na Samaria na Yerusalemu.
The word of the Lord, which was maad to `Mychee of Morasti, in the daies of Joathan, Achas, Ezechie, kyngis of Juda; which word he sai on Samarie, and Jerusalem.
2 Sikilizeni, ninyi watu wote. Sikilizeni, dunia, na vyote vilivyomo kwenye dunia. Acheni Yahwe ashuhudiwe dhidi yenu, Bwana kutoka kwenye hekalu lake takatifu.
Here ye, alle puplis, and the erthe perseyue, and plentee therof, and be the Lord God to you in to a witnesse, the Lord fro his hooli temple.
3 Tazama, Yahwe anakuja kutoka mahali pake; atashuka chini na kupakanyaga mahali pa juu katika dunia.
For lo! the Lord schal go out of his place, and schal come doun, and schal trede on hiy thingis of erthe.
4 Milima itayeyuka chini yake; mabonde yatapasuka vipande vipande kama mshumaa mbele ya moto, kama maji ambayo yamemwagika chini ya mteremko mkali.
And mounteyns schulen be waastid vndur hym, and valeis schulen be kit, as wex fro the face of fier, as watirs that rennen in to a pit.
5 Haya yote ni kwasababu ya uasi wa Yakobo, na kwasababu ya dhambi za nyumba ya Israeli. Je sababu ilikuwa nini kwa uasi wa Yakobo? Je ilikuwa Samaria? Je sababu ilikuwa nini kwa mahali pa juu pa Yuda? Je haiukuwa Yerusalemu?
In the grete trespas of Jacob is al this thing, and in the synnes of the hous of Israel. Which is the greet trespas of Jacob? whether not Samarie? and whiche ben the hiy thingis of Juda? whether not Jerusalem?
6 “Nitaifanya Samaria rundo la uharibifu katika shamba, kama eneo la kupandia mizabibu. Nitayavuta mawe ya jengo lake kwenda kwenye bonde; Nitaifunua misingi yake.
And Y schal put Samarie as an heep of stoonys in the feeld, whanne a vynyerd is plauntid; and Y schal drawe awei the stoonys therof in to a valei, and Y schal schewe the foundementis therof.
7 Sanamu zake zote za kuchonga zitapondwa vipande vipande; na zawadi zake zote zitachomwa moto. Kwa kuwa zawadi zake za ukahaba amezikusanya, na kama malipo ya ukahaba yatarudi.”
And alle `grauun ymagis therof schulen be betun togidere, and alle hiris therof schulen be brent in fier; and Y schal putte alle idols therof in to perdicioun; for of hiris of an hoore tho ben gaderid, and `til to hire of an hoore tho schulen turne ayen.
8 Kwa sababu hii nitalia na kuomboleza; nitaenda peku peku na uchi; Nitaomboleza kama mbeha na kuomboleza kama bundi.
On this thing Y schal weile and yelle, Y schal go spuylid and nakid; Y schal make weilyng of dragouns, and mournyng as of ostrigis.
9 Kwa kuwa jeraha lake haliponi, kwa kuwa imefika kwa Yuda. Imefikia lango la watu wangu, hadi Yerusalemu.
For wounde therof is dispeirid; for it cam til to Juda, it touchide the yate of my puple, til to Jerusalem.
10 Msiache kuwambia kuhusu katika Gathi; msilie tena. Katika Bethi Leafra nabiringisha mwenyewe kwenye mavumbi.
In Geth nyle ye telle, bi teeris wepe ye not; in the hous of dust with dust togidere sprynge you.
11 Piteni karibu na, makao ya Shafiri, katika uchi na aibu. Makazi ya Zaanani hayatatoka nje. Maombolezo ya Beth Ezeli, kwa ajili ya ulinzi yamechukuliwa.
And ye a fair dwellyng passe, which is confoundid with yuel fame; it is not goon out, which dwellith in the goyng out; a niy hous schal take of you weilyng, which stood to it silf.
12 Kwa kuwa wakaaji wa Marothi hungoja habari njema, kwa sababu hofu, kwa sababu msiba umetoka kwa Yahwe hadi kwenye malango ya Yerusalemu.
For it is maad sijk to good, which dwellith in bitternessis. For yuel cam doun fro the Lord in to the yate of Jerusalem, noise of foure horsid cart,
13 Wfuungeni lijamu farasi wakokote gari la farasi, makazi ya Lakishi. Wewe Lakishi, ulikuwa mwanzo wa dhambi kwa binti Sayuni, kwa kuwa makosa ya Israeli yalionekana kwako.
of drede to the puple dwellynge at Lachis. It is the bigynnyng of synne of the douyter of Sion, for the grete trespassis of Israel ben foundun in thee.
14 Hivyo utaipa zawadi ya kuagia Moreshethi Gathi; mji wa Akzibu utawavunja moyo wafalme wa Israeli.
Therfor he schal yyue werriours on the eritage of Geth, on housis of leesyng in to deseit to kyngis of Israel.
15 Tena nitaleta ushindi kwako, makazi ya Maresha; uzuri wa Israeli utakuja Adulamu.
Yit Y schal brynge an eir to thee, that dwellist in Maresa; the glorie of Israel schal come til to Odolla.
16 Kata kipara chako na kata nywele zako kwa ajili ya watoto ambao unaowafurahisha. Fanya kipara chako mwenyewe kama tai, kwa ajili ya watoto wako watakao kwenda utumwani kutoka kwako
Be thou maad ballid, and be thou clippid on the sones of thi delices; alarge thi ballidnesse as an egle, for thei ben lad caitif fro thee.

< Mika 1 >