< Mika 7 >

1 Ole wangu! Kwangu mimi ni kama msimu wa mavuno ulipokwisha, na pia makombo ya mavuno ya zabibu kwenye shamba la mizabibu: Hakuna tena kishamba cha matunda kinachoonekana, hakuna matini ya malimbuka ambayo ninayoyatamani.
Woe! to me for I have become like gathering of summer fruit like gleanings of [the] grape harvest there not [is] a cluster of grapes to eat early fig[s] it craves appetite my.
2 Watu waaminifu wamepotelea kutoka kwenye nchi, hakuna mtu mwadilifu katika wanadamu wote. Wote hudanganya katika kusubiri kumwaga damu; kila mtu humuwinda ndugu yake mwenyewe kwa wavu.
He has perished [the] faithful from the land and [is] an upright [person] among humankind there not all of them for blood they lie in wait each brother his they hunt a net.
3 Mikono yao ni mizuri mno kwa kufanya madhara. watawala huuliza pesa, hakimu yuko tayari kwa rushwa, na mtu mwenye nguvu anawaambia wengine kile anachokitaka kujipatia. Hivyo ndivyo waundavyo kwa pamoja.
[are] on Evil both hands to do [it] well the official [is] asking and the judge (for bribe *L(abh)*) and the great [person] [is] speaking [the] craving of self his he and they weave it.
4 Mtu bora kwao ni kama mitemba, mwadilifu sana ni kama mche wa miba. Imefika siku iliyosemwa nyuma na walinzi wako, siku ya hukumu. Sasa ni mda wa machafuko.
Good person their [is] like a thorn-bush an upright [person] more than a thorn hedge [the] day of watchmen your punishment your it has come now it will be confusion their.
5 Msimwamini kila jirani; msimuweke kiongozi katika rafiki yeyote. Kuweni makini kuhusiana na kile msemacho hata kwa mwanamke ambaye adanganyaye kwenye mikono yenu.
May not you believe in a neighbor may not you trust in a close friend from [she who] lies of bosom your guard [the] openings of mouth your.
6 Kwa kuwa mwana humfedhehesha baba yake, binti huinuka kushindana na mama yake, na mke wa mwana wa kiume hushindana na mama mkwe wake. Adui wa watu ni watu wa nyumba yake mwenyewe.
For a son [is] treating with contempt a father a daughter [is] arising on mother her a daughter-in-law on mother-in-law her [are the] enemies of a person [the] people of own household his.
7 Lakini kama kwangu mimi, nitamtazama Yahwe. Nitamsubiri Mungu wa wokovu wangu; Mungu wangu ataniskia.
And I for Yahweh I will watch I will wait for [the] God of salvation my he will hear me God my.
8 Usifurahi juu yangu, adui yangu. Niangukapo, nitainuka. Wakati nitakapokuwa nimekaa katika giza, Yahwe atakuwa mwanga kwangu.
May not you rejoice O enemy my to me for I have fallen I will arise for I sit in darkness Yahweh [will be] light of me.
9 Kwasababu nimetenda dhambi dhidi ya Yahwe, nitachukua ghadhabu yake hata aniteteapo kosa langu, na kutekeleza hukumu kwa ajili yangu. Atanileta kwenye nuru, na nitamwona akiniokoa kwenye haki yake.
[the] indignation of Yahweh I will bear for I have sinned to him until that he will conduct case my and he will do justice my he will bring out me to the light I will look on righteousness his.
10 Kisha adui yangu atakapoliona hilo, na aibu itamfunika yule aliyeniambia, “Yahwe Mungu wako yuko wapi?” macho yangu yatamtazama; atakanyagwa chini kama tope kwenye mitaa.
And she will see enemy my and it will cover her shame [she] who says to me where [is]? he Yahweh God your eyes my they will look on her now she will become a trampling place like [the] mud of [the] streets.
11 Siku ya ya kujenga kuta zako zitafika; siku hiyo mipaka itasogezwa mbali sana.
A day to build walls your a day that it will be far a boundary.
12 Siku hiyo watu watakuja kwako, kutoka Ashuru na miji katika Misri, kutoka Misri hata mto mkubwa, kutoka bahari kwenda bahari, na kutoka mlima kwenda mlima.
A day that and to you someone will come from Assyria and [the] cities of Egypt and from Egypt and to [the] River and sea from sea and mountain the mountain.
13 Hizo nchi zitakuwa zimejitenga kwasababu ya watu ambao wanaishi huko sasa, kwasababu ya tunda la matendo yao.
And it will become the earth a desolation on inhabitants its from [the] fruit of deeds their.
14 Chunga watu wako kwa fimbo yako, kundi la urithi wako. Wanaishi wenyewe kwenye msitu, katikati ya msitu. Wachunge katika Bashani na Gileadi kama siku za zamani.
Shepherd people your with rod your [the] flock of inheritance your [who] dwell alone a forest in [the] midst of a garden-land let them graze Bashan and Gilead like [the] days of antiquity.
15 Kama katika siku wakati mlipotoka nje ya nchi ya Misri, nitawaonyesha maajabu.
Like [the] days coming out you from [the] land of Egypt I will show him wonders.
16 Mataifa yataona na kuwa na aibu ya nguvu zao zote. Wataweka mikono yao kwenye midomo yao; masikio yao yatakuwa kiziwi.
They will see nations so they may be ashamed from all strength their they will put a hand on a mouth ears their they will be deaf.
17 Watalamba vumbi kama nyoka, kama viumbe vitaambavyo juu ya nchi. Watatoka nje kwenye maficho kwa hofu; watakuja kwako kwa hofu, Yahwe Mungu wetu, na wataogopa kwa sababu yako.
They will lick up dust like snake like [things which] crawl of [the] earth they will quake from strongholds their to Yahweh God our they will be in dread and they may be afraid from you.
18 Ni nani aliye Mungu kama wewe, wewe uchukuaye dhambi, wewe upitaye juu ya kosa la mabaki ya mrithi wako? Hutunzi hasira yako milele, kwa sababu unapenda kutuonyesha agano lako la aminifu.
Who? [is] a God like you [who] forgives iniquity and [who] passes over transgression to [the] remnant of inheritance his not he keeps hold of for ever anger his for [is one] desirous of covenant loyalty he.
19 Tena utakuwa na huruma juu yetu; utayakanyaga maovu chini ya miguu yako. Utazitupa dhambi zetu zote kwenye vilindi vya bahari.
He will return he will have compassion on us he will subdue iniquities our so you may cast in [the] depths of [the] sea all sins their.
20 Utampatia ukweli Yakobo na agano aminifu kwa Abrahamu, ulipoapa kwa babu zetu katika siku za kale.
You will give faithfulness to Jacob covenant loyalty to Abraham which you swore to fathers our from days of antiquity.

< Mika 7 >