< Mika 6 >
1 Sasa sikilizeni kile ambacho Yahwe asemacho, “Inuka na ueleze kesi yako mbele ya milima; acha milima isikie sauti yako.
Now hear that which YHWH is saying: “Rise—strive with the mountains, And cause the hills to hear your voice.
2 Sikilizeni madai ya Yahwe, enyi milima, na ninyi misingi mivumilivu ya dunia. Kwa kuwa Yahwe anavumilia pamoja na watu wake, na atapigana katika mahakama juu ya Israeli.”
Hear, O mountains, the strife of YHWH, You strong ones—foundations of earth! For a strife [is] to YHWH, with His people, And with Israel He reasons.
3 Watu wangu, nimefanya nini kwenu? nimewachosha mara ngapi? shuhudieni dhidi yangu!
O My people, what have I done to you? And how have I wearied you? Testify against Me.
4 Kwa kuwa niliwaleta kutoka nchi ya Msiri na kuwaokoa kutoka kwenye nyumba ya utumwa. Nawatuma Musa, Aruni, na Mariamu kwako.
For I brought you up from the land of Egypt, And I have ransomed you from the house of servants, And I send Moses, Aaron, and Miriam before you.
5 Watu wangu, kumbukeni ambavyo Balaki mfalme wa Moabu alivyotunga, na vile ambavyo Balamu mwana wa Beori alivyomjibu kama ulipokuwa ukienda kutoka kwa Gilgali, hivyo mnaweza kujua matendo ya haki ya Yahwe.”
O My people, please remember What Balak king of Moab counseled, What Balaam son of Beor answered him (From Shittim to Gilgal), In order to know the righteous acts of YHWH.”
6 Je nilete nini kwa Yahwe, ninapoenda kumwinamia Mungu aliye juu? Je ninaweza kuja kwake na sadaka za kuteketeza, pamoja na ndama wenye mwaka mmoja?
With what do I come before YHWH? Do I bow to God Most High? Do I come before Him with burnt-offerings? With calves—sons of a year?
7 Je Yahwe atapendezwa na maelfu ya kondoo waume, au na elfu kumi za mito ya mafuta? Je nimtoe mzaliwa wangu wa kwanza kwa ajili ya kosa langu, tunda la mwili wangu kwa ajili ya dhambi yangu mwenyewe?
Is YHWH pleased with thousands of rams? With myriads of streams of oil? Do I give my firstborn [for] my transgression? The fruit of my body [for] the sin of my soul?
8 Amekwambia, mtu, kile kilicho bora, na kile ambacho Yahwe atakacho kutoka kwako: Kutenda haki, kupenda ukarimu, na kutembea kwa unyenyekevu pamoja na Mungu wako.
He has declared to you, O man, what [is] good; Indeed, what is YHWH requiring of you, Except—to do judgment, and love kindness, And to walk lowly with your God?
9 Sauti ya Yahwe inatangaza kwenye mji-hata sasa hekima hukukiri jina lako: “Kaa tayari kwa ajili ya fimbo, na kwa yule aliyeiweka.
A voice of YHWH calls to the city, And wisdom fears Your Name, “Hear the rod, and Him who appointed it.
10 Kuna utajiri katika nyumba za waovu, na kipimo cha uongo hilo ni chukizo mno.
Are there yet [in] the house of the wicked Treasures of wickedness, And the abhorred meager ephah?
11 Ningeweza kumfikira mtu kuwa hana hatia kama anatumia kipimo cha ulaghai, pamoja na mfuko wa kipimo wa udanganyifu?
Do I reckon [it] pure with balances of wickedness? And with a bag of deceitful stones?
12 Matajiri wamejaa uharibifu, makazi yao yamesema uongo, na ulimi wao katika midomo yao unaudanganyifu.
Whose rich ones have been full of violence, And its inhabitants have spoken falsehood, And their tongue [is] deceitful in their mouth.
13 Kwa hiyo nimekupiga kwa pigo linaloumiza, nimekufanya gofu kwa sababu ya dhambi zako.
And I also, I have begun to strike you, To make desolate, because of your sins.
14 Utakula lakini hutatosheka; utupu wako utabakia ndani yako. Utatunza mizigo mbali lakini hutahifadhi, na kile unachokihifadhi nitakitoa kwa upanga.
You eat, and you are not satisfied, And your pit [is] in your midst, And you remove, and do not deliver, And that which you deliver, I give to a sword.
15 Utapanda lakini huatavuna; utazikusanya zaituni lakini hutajipaka mafuta; utasindika zabibu lakini hutakunywa divai.
You sow, and you do not reap, You tread the olive, And you do not pour out oil, And new wine—and you do not drink wine.
16 Kanuni zilizotengenezwa na Omri zimetunzwa, na matendo yote ya nyumba ya Ahabu. Mnatembea kwa ushauri wao. Hivyo nitakufanya wewe, mji, gofu, na makazi yako jambo la zomeo, na matabeba dharau kama watu wangu.”
And the statutes of Omri are kept habitually, And all the work of the house of Ahab, And you walk in their counsels, For My giving you for a desolation, And its inhabitants for a hissing, And you bear the reproach of My people!”