< Mika 5 >
1 Sasa njoni pamoja katika safu ya kupigana, binti wa maaskari; maaskari wameuzingira mji, kwa ufito watampiga mwamuzi wa Israeli kwenye shavu.
Maintenant assemble-toi par troupes, fille des troupes! On a mis le siège contre nous. De la verge on frappera sur la joue le juge d'Israël.
2 Lakini wewe, Bethlehemu Efrata, hata kama uko mdogo miongoni mwa koo za Yuda, kutoka kweko mmoja atakuja kwangu kutawala Israeli, ambaye mwanzo wake ni kutoka nyakati za kale, toka milele.
Mais toi, Bethléhem Éphrata, qui es petite entre les milliers de Juda, de toi sortira celui qui doit être dominateur en Israël. Ses origines sont d'ancienneté, dès les jours éternels.
3 Kwa hiyo Mungu atawapa, hata mda wa yeye aliye katika uchungu kuzaa mtoto, na mabaki ya ndugu zake yatawarudia wana wa Israeli.
C'est pourquoi il les livrera jusqu'au temps où celle qui doit enfanter enfantera; et le reste de ses frères reviendra auprès des enfants d'Israël.
4 Atasimama na kuchunga kundi lake kwa nguvu za Yahwe, kwa ukuu wa enzi ya jina la Yahwe Mungu wake. Watabaki, kwa kuwa atakuwa mashuhuri hata mwisho wa dunia.
Il se maintiendra, et il gouvernera avec la force de l'Éternel, avec la majesté du nom de l'Éternel son Dieu. Ils habiteront en paix, car alors il sera glorifié jusqu'aux extrémités de la terre. Et c'est lui qui sera la paix.
5 Atakuwa amani yetu. Wakati Waashuru watakapokuja kwenye nchi yetu, wakati wakitembea dhidi ya boma yetu, kisha kisha tutainuka juu yao wachungaji saba na viongozi nane juu ya watu.
Quand l'Assyrien viendra dans notre pays, et qu'il mettra le pied dans nos palais, nous lui opposerons sept pasteurs et huit princes du peuple.
6 Watachunga nchi ya Ashuru kwa upanga, na nchi ya Nimrodi katika malango yake. Atatuokoa kutoka kwa Waashuru, watakapokuja kwenye nchi yetu, watakapoingia kwenye mipaka yetu.
Ils paîtront le pays d'Assyrie avec l'épée, et le pays de Nimrod dans ses portes. Il nous délivrera de l'Assyrien, quand il viendra dans notre pays, et quand il mettra le pied sur notre territoire.
7 Mabaki ya Yakobo yatakuwa katika kabila za watu wengi, kama umande utokao kwa Yahwe, kama manyunyu kwenye majani, ambayo hayamsubiri mtu, na hayawasubiri watoto wa mwanadamu.
Et le reste de Jacob sera, parmi des peuples nombreux, comme une rosée qui vient de l'Éternel, comme les gouttes de pluie sur l'herbe, qui n'attend rien de l'homme, et n'espère rien des enfants des hommes.
8 Mabaki ya Yakobo yatakuwa miongoni mwa mataifa, miongoni mwa watu wengi, kama simba katikati ya kundi la kondoo. wakati akipita katikati yao, atawakanyaga juu yao na kuwachachana kuwa vipande vipande, na hakutakuwa na mtu wa kuwaokoa.
Et le reste de Jacob sera entre les nations, parmi des peuples nombreux, comme un lion parmi les bêtes de la forêt, comme un lionceau parmi les troupeaux de brebis, qui, lorsqu'il passe, foule et déchire, et personne ne délivre.
9 Mkono wako utainuliwa dhidi ya maadui zako, na utawaharibu.
Que ta main se lève contre tes adversaires, et que tous tes ennemis soient exterminés!
10 “Itatokea siku hiyo,” asema Yahwe, “kwamba nitawaharibu farasi wako kutoka miongoni mwenu na nitayavunja magari yako ya farasi.
En ce jour-là, dit l'Éternel, je retrancherai tes chevaux du milieu de toi, et je détruirai tes chars.
11 Nitaiharibu miji katika nchi yako na kuzingusha ngome zako zote.
Je retrancherai les villes de ton pays, et je renverserai toutes tes forteresses.
12 Nitauharibu uchawi kwenye mkono wako, na hakutakuwa na waaguzi tena.
Je retrancherai de ta main les enchantements, et tu n'auras plus de devins.
13 Nitaziaharibu sanamu zako za pango na nguzo za mawe kutoka miongoni mwako. Hautaabudu tena ustadi wa mikono yako.
Je retrancherai du milieu de toi tes images taillées et tes statues, et tu ne te prosterneras plus devant l'ouvrage de tes mains;
14 Nitazin'goa nguzo zako za Ashera kutoka miongoni mwenu, na nitaiharibu miji yenu.
J'arracherai du milieu de toi tes emblèmes d'Ashéra, et je détruirai tes villes.
15 Nitalipiza kisasi kwa hasira na ghadhabu juu ya mataifa ambayo hayakusikiliza.”
Dans ma colère et ma fureur, j'exercerai la vengeance sur les nations qui n'auront point écouté.