< Mika 5 >

1 Sasa njoni pamoja katika safu ya kupigana, binti wa maaskari; maaskari wameuzingira mji, kwa ufito watampiga mwamuzi wa Israeli kwenye shavu.
Maintenant, vous allez vous rassembler en troupes, la fille des troupes. Il a fait le siège contre nous. Ils frapperont le juge d'Israël avec une baguette sur la joue.
2 Lakini wewe, Bethlehemu Efrata, hata kama uko mdogo miongoni mwa koo za Yuda, kutoka kweko mmoja atakuja kwangu kutawala Israeli, ambaye mwanzo wake ni kutoka nyakati za kale, toka milele.
Mais toi, Bethléem Ephrata, étant petit parmi les clans de Juda, de vous sortira quelqu'un qui sera le chef d'Israël; dont les sorties viennent d'autrefois, des temps anciens.
3 Kwa hiyo Mungu atawapa, hata mda wa yeye aliye katika uchungu kuzaa mtoto, na mabaki ya ndugu zake yatawarudia wana wa Israeli.
Il les abandonnera donc jusqu'au moment où la femme en travail accouchera. Puis le reste de ses frères reviendra aux enfants d'Israël.
4 Atasimama na kuchunga kundi lake kwa nguvu za Yahwe, kwa ukuu wa enzi ya jina la Yahwe Mungu wake. Watabaki, kwa kuwa atakuwa mashuhuri hata mwisho wa dunia.
Il se tiendra debout, et il paîtra dans la force de l'Éternel, dans la majesté du nom de Yahvé son Dieu. Ils vivront, car alors il sera grand jusqu'aux extrémités de la terre.
5 Atakuwa amani yetu. Wakati Waashuru watakapokuja kwenye nchi yetu, wakati wakitembea dhidi ya boma yetu, kisha kisha tutainuka juu yao wachungaji saba na viongozi nane juu ya watu.
Il sera notre paix lorsque l'Assyrie envahira notre pays. et quand il marche à travers nos forteresses, alors nous dresserons contre lui sept bergers, et huit chefs d'hommes.
6 Watachunga nchi ya Ashuru kwa upanga, na nchi ya Nimrodi katika malango yake. Atatuokoa kutoka kwa Waashuru, watakapokuja kwenye nchi yetu, watakapoingia kwenye mipaka yetu.
Ils domineront le pays d'Assyrie par l'épée, et le pays de Nimrod dans ses portes. Il nous délivrera de l'Assyrien, quand il envahira notre pays, et quand il défile à l'intérieur de notre frontière.
7 Mabaki ya Yakobo yatakuwa katika kabila za watu wengi, kama umande utokao kwa Yahwe, kama manyunyu kwenye majani, ambayo hayamsubiri mtu, na hayawasubiri watoto wa mwanadamu.
Le reste de Jacob sera parmi de nombreux peuples. comme la rosée de Yahvé, comme des averses sur l'herbe, qui n'attendent pas l'homme ni attendre les fils des hommes.
8 Mabaki ya Yakobo yatakuwa miongoni mwa mataifa, miongoni mwa watu wengi, kama simba katikati ya kundi la kondoo. wakati akipita katikati yao, atawakanyaga juu yao na kuwachachana kuwa vipande vipande, na hakutakuwa na mtu wa kuwaokoa.
Le reste de Jacob sera parmi les nations, parmi de nombreux peuples, comme un lion parmi les animaux de la forêt, comme un jeune lion parmi les troupeaux de moutons; qui, s'il passe, piétine et met en pièces, et il n'y a personne pour le faire.
9 Mkono wako utainuliwa dhidi ya maadui zako, na utawaharibu.
Que ta main s'élève au-dessus de tes adversaires, et que tous vos ennemis soient exterminés.
10 “Itatokea siku hiyo,” asema Yahwe, “kwamba nitawaharibu farasi wako kutoka miongoni mwenu na nitayavunja magari yako ya farasi.
« Cela arrivera en ce jour-là », dit Yahvé, « que je retrancherai vos chevaux du milieu de vous et détruira tes chars.
11 Nitaiharibu miji katika nchi yako na kuzingusha ngome zako zote.
J'exterminerai les villes de ton pays et détruira toutes vos forteresses.
12 Nitauharibu uchawi kwenye mkono wako, na hakutakuwa na waaguzi tena.
Je détruirai la sorcellerie de ta main. Tu n'auras pas de devins.
13 Nitaziaharibu sanamu zako za pango na nguzo za mawe kutoka miongoni mwako. Hautaabudu tena ustadi wa mikono yako.
J'éliminerai du milieu de vous vos images gravées et vos statues; et vous n'adorerez plus l'ouvrage de vos mains.
14 Nitazin'goa nguzo zako za Ashera kutoka miongoni mwenu, na nitaiharibu miji yenu.
Je déracinerai vos mâts d'Ashérah du milieu de vous; et je détruirai vos villes.
15 Nitalipiza kisasi kwa hasira na ghadhabu juu ya mataifa ambayo hayakusikiliza.”
J'exécuterai la vengeance dans la colère et la colère sur les nations qui n'ont pas écouté. »

< Mika 5 >