< Mika 5 >

1 Sasa njoni pamoja katika safu ya kupigana, binti wa maaskari; maaskari wameuzingira mji, kwa ufito watampiga mwamuzi wa Israeli kwenye shavu.
Now come together in battle ranks, daughter of soldiers; the soldiers have set up a siege around city, with a rod they will strike the judge of Israel on the cheek.
2 Lakini wewe, Bethlehemu Efrata, hata kama uko mdogo miongoni mwa koo za Yuda, kutoka kweko mmoja atakuja kwangu kutawala Israeli, ambaye mwanzo wake ni kutoka nyakati za kale, toka milele.
But you, Bethlehem Ephrathah, even though you are small among the clans of Judah, out of you one will come to me to rule in Israel, whose beginning is from ancient times, from everlasting.
3 Kwa hiyo Mungu atawapa, hata mda wa yeye aliye katika uchungu kuzaa mtoto, na mabaki ya ndugu zake yatawarudia wana wa Israeli.
Therefore God will give them up, until the time when she who is in labor bears a child, and the rest of his brothers return to the people of Israel.
4 Atasimama na kuchunga kundi lake kwa nguvu za Yahwe, kwa ukuu wa enzi ya jina la Yahwe Mungu wake. Watabaki, kwa kuwa atakuwa mashuhuri hata mwisho wa dunia.
He will stand and shepherd his flock in the strength of Yahweh, in the majesty of the name of Yahweh his God. They will remain, for then he will be great to the ends of the earth.
5 Atakuwa amani yetu. Wakati Waashuru watakapokuja kwenye nchi yetu, wakati wakitembea dhidi ya boma yetu, kisha kisha tutainuka juu yao wachungaji saba na viongozi nane juu ya watu.
For this shall be the peace— when the Assyrians come into our land, and when they march against our fortresses, then we will raise against them seven shepherds and eight leaders over men.
6 Watachunga nchi ya Ashuru kwa upanga, na nchi ya Nimrodi katika malango yake. Atatuokoa kutoka kwa Waashuru, watakapokuja kwenye nchi yetu, watakapoingia kwenye mipaka yetu.
They will shepherd the land of Assyria with the sword, and the land of Nimrod in its entrances. He will rescue us from the Assyrians, when they come into our land, when they march inside our borders.
7 Mabaki ya Yakobo yatakuwa katika kabila za watu wengi, kama umande utokao kwa Yahwe, kama manyunyu kwenye majani, ambayo hayamsubiri mtu, na hayawasubiri watoto wa mwanadamu.
The remnant of Jacob will be in the midst of many peoples, like dew from Yahweh, like showers on the grass, that do not wait for a man, and they do not wait for the children of mankind.
8 Mabaki ya Yakobo yatakuwa miongoni mwa mataifa, miongoni mwa watu wengi, kama simba katikati ya kundi la kondoo. wakati akipita katikati yao, atawakanyaga juu yao na kuwachachana kuwa vipande vipande, na hakutakuwa na mtu wa kuwaokoa.
The remnant of Jacob will be among the nations, among many peoples, like a lion among the animals of the forest, like a young lion among the flocks of sheep. When he goes through them, he will trample over them and tear them to pieces, and there will be no one to save them.
9 Mkono wako utainuliwa dhidi ya maadui zako, na utawaharibu.
Your hand will be lifted against your enemies, and it will destroy them.
10 “Itatokea siku hiyo,” asema Yahwe, “kwamba nitawaharibu farasi wako kutoka miongoni mwenu na nitayavunja magari yako ya farasi.
“It will happen in that day”—this is Yahweh's declaration— “that I will destroy your horses from among you and will demolish your chariots.
11 Nitaiharibu miji katika nchi yako na kuzingusha ngome zako zote.
I will destroy the cities in your land and throw down all your strongholds.
12 Nitauharibu uchawi kwenye mkono wako, na hakutakuwa na waaguzi tena.
I will destroy the witchcraft in your hand, and you will no longer have any diviners.
13 Nitaziaharibu sanamu zako za pango na nguzo za mawe kutoka miongoni mwako. Hautaabudu tena ustadi wa mikono yako.
I will destroy your carved figures and your stone pillars from among you. You will no longer worship the workmanship of your hands.
14 Nitazin'goa nguzo zako za Ashera kutoka miongoni mwenu, na nitaiharibu miji yenu.
I will uproot your Asherah poles from among you, and I will destroy your cities.
15 Nitalipiza kisasi kwa hasira na ghadhabu juu ya mataifa ambayo hayakusikiliza.”
I will execute vengeance in anger and wrath on the nations that have not listened.”

< Mika 5 >