< Mika 5 >

1 Sasa njoni pamoja katika safu ya kupigana, binti wa maaskari; maaskari wameuzingira mji, kwa ufito watampiga mwamuzi wa Israeli kwenye shavu.
Nowe assemble thy garisons, O daughter of garisons: he hath layed siege against vs: they shall smite the iudge of Israel with a rod vpon the cheeke.
2 Lakini wewe, Bethlehemu Efrata, hata kama uko mdogo miongoni mwa koo za Yuda, kutoka kweko mmoja atakuja kwangu kutawala Israeli, ambaye mwanzo wake ni kutoka nyakati za kale, toka milele.
And thou Beth-leem Ephrathah art litle to bee among the thousandes of Iudah, yet out of thee shall he come forth vnto me, that shalbe the ruler in Israel: whose goings forth haue bene from the beginning and from euerlasting.
3 Kwa hiyo Mungu atawapa, hata mda wa yeye aliye katika uchungu kuzaa mtoto, na mabaki ya ndugu zake yatawarudia wana wa Israeli.
Therefore will he giue them vp, vntill the time that shee which shall beare, shall trauaile: then the remnant of their brethren shall returne vnto the children of Israel.
4 Atasimama na kuchunga kundi lake kwa nguvu za Yahwe, kwa ukuu wa enzi ya jina la Yahwe Mungu wake. Watabaki, kwa kuwa atakuwa mashuhuri hata mwisho wa dunia.
And he shall stand, and feed in the strength of the Lord, and in the maiestie of the Name of the Lord his God, and they shall dwel still: for now shall he be magnified vnto the ends of the world.
5 Atakuwa amani yetu. Wakati Waashuru watakapokuja kwenye nchi yetu, wakati wakitembea dhidi ya boma yetu, kisha kisha tutainuka juu yao wachungaji saba na viongozi nane juu ya watu.
And hee shall be our peace when Asshur shall come into our lande: when he shall tread in our palaces, then shall we raise against him seuen shepheardes, and eight principall men.
6 Watachunga nchi ya Ashuru kwa upanga, na nchi ya Nimrodi katika malango yake. Atatuokoa kutoka kwa Waashuru, watakapokuja kwenye nchi yetu, watakapoingia kwenye mipaka yetu.
And they shall destroy Asshur with the sword, and the land of Nimrod with their swordes: thus shall he deliuer vs from Asshur, when hee commeth into our lande, and when he shall tread within our borders.
7 Mabaki ya Yakobo yatakuwa katika kabila za watu wengi, kama umande utokao kwa Yahwe, kama manyunyu kwenye majani, ambayo hayamsubiri mtu, na hayawasubiri watoto wa mwanadamu.
And the remnant of Iaakob shalbe among many people, as a dewe from the Lord, and as the showres vpon the grasse, that waiteth not for man, nor hopeth in the sonnes of Adam.
8 Mabaki ya Yakobo yatakuwa miongoni mwa mataifa, miongoni mwa watu wengi, kama simba katikati ya kundi la kondoo. wakati akipita katikati yao, atawakanyaga juu yao na kuwachachana kuwa vipande vipande, na hakutakuwa na mtu wa kuwaokoa.
And the remnant of Iaakob shalbe among the Gentiles in the middes of many people, as the lyon among the beastes of the forest, and as the lyons whelpe among the flockes of sheepe, who when he goeth thorow, treadeth downe and teareth in pieces, and none can deliuer.
9 Mkono wako utainuliwa dhidi ya maadui zako, na utawaharibu.
Thine hand shall bee lift vp vpon thine aduersaries, and all thine enemies shalbe cut off.
10 “Itatokea siku hiyo,” asema Yahwe, “kwamba nitawaharibu farasi wako kutoka miongoni mwenu na nitayavunja magari yako ya farasi.
And it shall come to passe in that day, sayth the Lord, that I will cut off thine horses out of the middes of thee, and I will destroy thy charets.
11 Nitaiharibu miji katika nchi yako na kuzingusha ngome zako zote.
And I will cut off the cities of thy land, and ouerthrowe all thy strong holdes.
12 Nitauharibu uchawi kwenye mkono wako, na hakutakuwa na waaguzi tena.
And I will cut off thine enchanters out of thine hande: and thou shalt haue no more southsayers.
13 Nitaziaharibu sanamu zako za pango na nguzo za mawe kutoka miongoni mwako. Hautaabudu tena ustadi wa mikono yako.
Thine idoles also will I cut off, and thine images out of the middes of thee: and thou shalt no more worship the woorke of thine hands.
14 Nitazin'goa nguzo zako za Ashera kutoka miongoni mwenu, na nitaiharibu miji yenu.
And I wil plucke vp thy groues out of the middes of thee: so will I destroy thine enemies.
15 Nitalipiza kisasi kwa hasira na ghadhabu juu ya mataifa ambayo hayakusikiliza.”
And I will execute a vegeance in my wrath and indignation vpon the heathen, which they haue not heard.

< Mika 5 >