< Mika 3 >

1 Nimesema'”Sasa sikilizeni, ninyi viongozi wa Yakobo na kutawala nyumba ya Israeli: Je siyo sahihi kwenu kuielewa haki?
Then I said, “Please listen, leaders of the descendants of Jacob, people of Israel. You are meant to know the difference between right and wrong,
2 Ninyi manaochukia mazuri na kupenda uovu, ninyi mnaoambua ngozi yao, miili yao kutoka kwenye mifupa yao-
you who hate good and love evil! You tear off their skin, and rip the flesh from their bones.
3 ninyi mnaokula pia miili ya watu wangu, na kuambua ngozi yao, kuvunja mifupa yao, na kuwakatakata katika vipande vipande, kama nyama kwenye chungu, kama nyama kwenye sufuria kubwa.
You eat the flesh of my people, you strip off their skin, you break their bones. You chop them up like meat for the saucepan, like flesh for the cooking pot.”
4 Kisha ninyi watawala mtalia kwa Yahwe, lakini hatawajibu. Atauficha uso wake kutoka kwenu kipindi hicho, kwasababu mmefanya matendo maovu.”
Then they'll cry out to the Lord, but he won't answer them. He will turn away from them at that time because of the evil things they have done.
5 Yahwe asema hivi kuhusu manabii ambao wawafanyao watu wangu kushindwa, “Kwa wale wawalishao wanatangaza, 'Kutakuwa na ustawi.' Lakini kwa wale wasioweka kitu kwenye vinywa vyao, wanaanzisha vita dhidi yake.
This is what the Lord says about the prophets who deceive my people. To those who feed them they prophesy peace to them, while to those who do not they prophesy war against them.
6 Kwa hiyo, itakuwa usiku kwenu usiokuwa na maono juu yenu; itakuwa giza ili kwamba msiweze kubashiri. Jua litakwenda chini juu ya manabii, na siku itakuwa giza juu yao.
Therefore it will be like night for you, with no visions; dark, with no predictions. The sun will set on these prophets; their day will end in darkness.
7 Waonaji watawekwa kwenye aibu, waaguzi wa watachanganyikiwa. Wote watafunga midomo yao, kwa kuwa hakuna jibu kutoka kwangu.”
The seers will be disgraced, the fortune-tellers put to shame, and they will cover their faces because none of them receive any answer from God.
8 Lakini kwangu, nimejazwa nguvu kutoka kwa Roho wa Yahwe, na nimejaa haki na uweza, kumwambia Yakobo kosa lake, na Israeli dhambi yake.
But as for me, I am filled with power, with the spirit of the Lord. I am filled with justice and strength to make clear to the descendants of Jacob their rebellion, and to the people of Israel their sin.
9 Sasa sikieni hii, ninyi viongozi wa nyumba ya Yakobo, na watawala wa nyumba ya Israeli, ninyi ambao mnaochukia haki, na kupotosha kila haki.
Listen to me, leaders of the descendants of Jacob and the people of Israel, you who hate justice and distort all that is right.
10 Mnaijenga Sayuni kwa damu na Yerusalemu kwa uovu.
You are building Zion with blood, and Jerusalem with evil.
11 Viongozi wenu huhukumu kwa rushwa, makuhani wenu hufundisha kwa hijara, na manabii wenu hufanya utabiri kwa ajili ya pesa. Hata hivyo bado mtamtegemea Yahwe na kusema, “Je hayupo Yahwe pamoja nasi? Hakuna uovu utakaokuja juu yetu.”
Your leaders judge for a bribe, and your priests teach for a price, and your prophets only prophesy for pay. Yet they all lean on the Lord saying, “Isn't the Lord here with us? Nothing bad can happen to us!”
12 Kwa hiyo, kwasababu yenu, Sayuni italimwa kama shamba, Yerusalemu itakuwa rundo la kifusi, na mwinuko wa hekalu utakuwa kama mwinuko wa msituni.
Therefore because of you Zion will become a ploughed field and Jerusalem a heap of rubble, and the Temple mount will be overgrown.

< Mika 3 >