< Mika 3 >

1 Nimesema'”Sasa sikilizeni, ninyi viongozi wa Yakobo na kutawala nyumba ya Israeli: Je siyo sahihi kwenu kuielewa haki?
And I said: Listen, leaders of Jacob and chiefs of the house of Israel. Does it not belong to you to know judgment,
2 Ninyi manaochukia mazuri na kupenda uovu, ninyi mnaoambua ngozi yao, miili yao kutoka kwenye mifupa yao-
you who hold hatred for good, and love evil, who violently steal their skins from over them and their flesh from over their bones?
3 ninyi mnaokula pia miili ya watu wangu, na kuambua ngozi yao, kuvunja mifupa yao, na kuwakatakata katika vipande vipande, kama nyama kwenye chungu, kama nyama kwenye sufuria kubwa.
They have devoured the flesh of my people, and have stripped their skin from over them, and they have shattered and chopped their bones, as if for the kettle, and like flesh in the middle of the pot.
4 Kisha ninyi watawala mtalia kwa Yahwe, lakini hatawajibu. Atauficha uso wake kutoka kwenu kipindi hicho, kwasababu mmefanya matendo maovu.”
Then they will cry out to the Lord, and he will not heed them. And he will hide his face from them in that time, just as they have acted wickedly with their inventions.
5 Yahwe asema hivi kuhusu manabii ambao wawafanyao watu wangu kushindwa, “Kwa wale wawalishao wanatangaza, 'Kutakuwa na ustawi.' Lakini kwa wale wasioweka kitu kwenye vinywa vyao, wanaanzisha vita dhidi yake.
Thus says the Lord about the prophets who seduce my people: They bite with their teeth and preach peace, and if anyone does not give something to their mouth, they sanctify a battle against him.
6 Kwa hiyo, itakuwa usiku kwenu usiokuwa na maono juu yenu; itakuwa giza ili kwamba msiweze kubashiri. Jua litakwenda chini juu ya manabii, na siku itakuwa giza juu yao.
Because of this, night will be yours for vision, and darkness yours for divination, and the sun will meet with death over the prophets, and the day will be darkened over them.
7 Waonaji watawekwa kwenye aibu, waaguzi wa watachanganyikiwa. Wote watafunga midomo yao, kwa kuwa hakuna jibu kutoka kwangu.”
And those who see visions will be confounded, and the diviners will be confounded. And they will all cover their faces, because there is no response from God.
8 Lakini kwangu, nimejazwa nguvu kutoka kwa Roho wa Yahwe, na nimejaa haki na uweza, kumwambia Yakobo kosa lake, na Israeli dhambi yake.
Nevertheless, truly I have been filled with the strength of the Spirit of the Lord, with judgment and virtue, in order to announce to Jacob his wickedness and to Israel his sin.
9 Sasa sikieni hii, ninyi viongozi wa nyumba ya Yakobo, na watawala wa nyumba ya Israeli, ninyi ambao mnaochukia haki, na kupotosha kila haki.
Hear this, leaders of the house of Jacob and judges of the house of Israel, you who abominate judgment and who pervert all that is right.
10 Mnaijenga Sayuni kwa damu na Yerusalemu kwa uovu.
You build up Zion with blood, and Jerusalem with iniquity.
11 Viongozi wenu huhukumu kwa rushwa, makuhani wenu hufundisha kwa hijara, na manabii wenu hufanya utabiri kwa ajili ya pesa. Hata hivyo bado mtamtegemea Yahwe na kusema, “Je hayupo Yahwe pamoja nasi? Hakuna uovu utakaokuja juu yetu.”
Her leaders have judged for tributes, and her priests have taught for payment, and her prophets divined for money. And they leaned upon the Lord, saying: “Is not the Lord in our midst? No disaster will overcome us.”
12 Kwa hiyo, kwasababu yenu, Sayuni italimwa kama shamba, Yerusalemu itakuwa rundo la kifusi, na mwinuko wa hekalu utakuwa kama mwinuko wa msituni.
For this reason, because of you, Zion will be plowed under like a field, and Jerusalem will become like a pile of stones, and the mountain of the temple like the high places of the forests.

< Mika 3 >