< Mika 2 >

1 Ole wao wale wanao wanaokusudia mabaya, kwa wale wanaokusudia kwenye vitanda vyao kufanya maovu. Katika asubuhi wanayafanya kwa sababu wana nguvu.
Woe to those who plan iniquity, to those who plan on their beds to do evil. In the morning light they do it because they have power.
2 Wanatamani mashamba na kuyapunguza; wanazitamani nyumba na kuzichukua. Wanadhulumu mtu na nyumba yake, mtu na urithi wake.
They desire fields and seize them; they desire houses and take them. They oppress a man and his house, a man and his inheritance.
3 Kwa hiyo Yahwe asema hivi, “Tazama, nakaribia kuleta janga dhidi ya huu ukoo, ambalo hamtazitoa shingo zenu. Hamtatembea kwa kiburi, kwa kuwa itakuwa wakati wa uovu.
Therefore Yahweh says this, “Look, I am about to bring disaster against this clan, from which you will not remove your necks. You will not walk arrogantly, for it will be an evil time.
4 Katika siku hiyo maadui zako wataimba wimbo kuhusu wewe, na kuomboleza kwa maombolezo ya huzuni. Wataimba, 'Sisi Waisraeli tumeangamizwa kabisa; Yahwe hubadilisha eneo la watu wangu. Je ataliondoaje kutoka kwangu? Huwagawia mshamba yetu kusaliti.”'
In that day men will sing a song about you, and lament with a wailing lamentation. They will sing, 'We Israelites are completely ruined; Yahweh changes the territory of my people. How can he remove it from me? He portions out our fields to traitors!'”
5 Kwa hiyo, ninyi watu matajiri hamtakuwa uzao kugawanya eneo kwa kupiga kura katika mkutano wa Yahwe.
Therefore, you rich people will have no descendants to divide up the territory by lot in the assembly of Yahweh.
6 “Msitabiri,” wanasema. “Hawatayatabiri haya mambo; lawama hazitakuja.”
“Do not prophesy,” they say. “They must not prophesy these things; reproaches must not come.”
7 Je litasemwa kweli, nyumba ya Yakobo, “je Roho ya Yahwe? Je haya ni matendo yake kweli?” Maneno yangu hayafai kwa kila mmoja atembeaye kwa unyoofu?
Should it really be said, house of Jacob, “Is the Spirit of Yahweh angry? Are these really his deeds?” Do not my words do good to anyone who walks uprightly?
8 Hivi karibuni watu wangu wameinuka kama adui. Mmelivua joho, nguo, kutoka wale wapitao wasioshutumiwa, kama maaskari kurudi kutoka kwenye vita kwa kile wakifikiriacho ni salama.
Lately my people have risen up like an enemy. You strip the robe, the garment, from those who pass by unsuspectingly, as soldiers return from war to what they think is safety.
9 Mnawaendesha wanawake wangu kwa watu wangu kutoka kwenye nyumba nzuri; mnachukua baraka kutoka kwa watoto wao wadogo daima.
You drive the women belonging to my people from their pleasant houses; you take my blessing from their young children forever.
10 Inukeni na muondoke, kwa kuwa hii sio sehemu ambayo mnaweza kuishi, kwa sababu ya unajisi wake; imeangamizwa kwa maangamizo kabisa.
Get up and leave, for this is not a place where you can stay, because of its uncleanness; it is destroyed with complete destruction.
11 Kama mtu akija kwenu katika roho ya uongo na kudanganya na kusema, “Nitatabiri kwenu kuhusu mvinyo na kilevi kikali,” angeweza kufikiriwa kuwa nabii kwa ajili ya hawa watu.
If someone comes to you in a spirit of falsehood and lies and says, “I will prophesy to you about wine and strong drink,” he would be considered to be a prophet for this people.
12 Nitawaleta pamoja wote hakika, Yakobo. Hakika nitawakusanya mabaki ya Israeli. Nitawaleta pamoja kama kondoo katika zizi, kama kundi la wanyama katika malisho. Kutakuwa na kelele kwasababu ya wingi wa watu.
I will surely assemble all of you, Jacob. I will surely gather the remnant of Israel. I will bring them together like sheep in a fold, like a flock in the midst of their pasture. There will be a loud noise because of the multitude of people.
13 Mtu avunjaye hufungua njia zao kwa ajili yao kwenda mbele yao. Wamebomoa kupitia lango na kutoka nje; mfalme wao atapita mbele yao. Yahwe atakuwa mbele yao.
Someone who breaks open their way for them will go ahead of them. They break through the gate and go out; their king will pass on before them. Yahweh will be at their head.

< Mika 2 >