< Mika 2 >
1 Ole wao wale wanao wanaokusudia mabaya, kwa wale wanaokusudia kwenye vitanda vyao kufanya maovu. Katika asubuhi wanayafanya kwa sababu wana nguvu.
Woe to those that devise wickedness, and resolve on evil upon their couches! by the first light of the morning they execute it, if they have it in the power of their hand.
2 Wanatamani mashamba na kuyapunguza; wanazitamani nyumba na kuzichukua. Wanadhulumu mtu na nyumba yake, mtu na urithi wake.
And they covet fields, and rob them; and houses, and take them away: so they defraud the master and his house, and the man and his heritage.
3 Kwa hiyo Yahwe asema hivi, “Tazama, nakaribia kuleta janga dhidi ya huu ukoo, ambalo hamtazitoa shingo zenu. Hamtatembea kwa kiburi, kwa kuwa itakuwa wakati wa uovu.
Therefore thus hath said the Lord, Behold, I will devise against this family an evil, from which ye shall not remove your necks; nor shall ye go erect; for it is an evil time.
4 Katika siku hiyo maadui zako wataimba wimbo kuhusu wewe, na kuomboleza kwa maombolezo ya huzuni. Wataimba, 'Sisi Waisraeli tumeangamizwa kabisa; Yahwe hubadilisha eneo la watu wangu. Je ataliondoaje kutoka kwangu? Huwagawia mshamba yetu kusaliti.”'
On that day shall one take up a parable against you, and lament with a mournful lamentation, and say, “We are utterly wasted: the portion of my people hath he exchanged; how hath he removed it from me! instead of restoring [them to us] he divideth our fields.”
5 Kwa hiyo, ninyi watu matajiri hamtakuwa uzao kugawanya eneo kwa kupiga kura katika mkutano wa Yahwe.
Therefore shalt thou have none that shall draw the [measuring] cord in [his] lot in the congregation of the Lord.
6 “Msitabiri,” wanasema. “Hawatayatabiri haya mambo; lawama hazitakuja.”
“Preach not;” [but] they shall preach: they shall not preach [indeed] to these, that reproach may not overtake them.
7 Je litasemwa kweli, nyumba ya Yakobo, “je Roho ya Yahwe? Je haya ni matendo yake kweli?” Maneno yangu hayafai kwa kila mmoja atembeaye kwa unyoofu?
Shall it be said [in] the house of Jacob, Is the spirit of the Lord straightened? are these his doings? Do not my words do good to him that walketh uprightly?
8 Hivi karibuni watu wangu wameinuka kama adui. Mmelivua joho, nguo, kutoka wale wapitao wasioshutumiwa, kama maaskari kurudi kutoka kwenye vita kwa kile wakifikiriacho ni salama.
But long since is my people risen up as an enemy: from the garment do you pull off the ornament; of those that pass by securely [ye make] men returned from war.
9 Mnawaendesha wanawake wangu kwa watu wangu kutoka kwenye nyumba nzuri; mnachukua baraka kutoka kwa watoto wao wadogo daima.
The wives of my people do you drive out of their delightful houses; from their children do ye take away my ornament for ever.
10 Inukeni na muondoke, kwa kuwa hii sio sehemu ambayo mnaweza kuishi, kwa sababu ya unajisi wake; imeangamizwa kwa maangamizo kabisa.
Arise ye, and depart; for this is not your resting-place; because it is polluted, it shall destroy [you], even with a grievous destruction.
11 Kama mtu akija kwenu katika roho ya uongo na kudanganya na kusema, “Nitatabiri kwenu kuhusu mvinyo na kilevi kikali,” angeweza kufikiriwa kuwa nabii kwa ajili ya hawa watu.
If a man that goeth after wind and lieth with falsehood [should say], “I will preach unto thee of wine and of strong drink:” he would be a preacher for this people.
12 Nitawaleta pamoja wote hakika, Yakobo. Hakika nitawakusanya mabaki ya Israeli. Nitawaleta pamoja kama kondoo katika zizi, kama kundi la wanyama katika malisho. Kutakuwa na kelele kwasababu ya wingi wa watu.
I will [once] surely assemble, O Jacob, all of thee; I will surely gather up the remnant of Israel; I will place them together as flocks in the fold, as droves in the midst of their pen: they shall be crowded with men.
13 Mtu avunjaye hufungua njia zao kwa ajili yao kwenda mbele yao. Wamebomoa kupitia lango na kutoka nje; mfalme wao atapita mbele yao. Yahwe atakuwa mbele yao.
The wall-breaker cometh up before them; they break in and pass through the gate, and go out by it: and their king passeth on before them, and the Lord at their head.