< Mika 1 >

1 Hili ni neno la Yahwe ambalo lilikuja kwa Mika Mmorashti katika siku za Yotahamu, Ahazi, na Hezekeia, mfalme wa Yuda, lile neno aliloliona kuhusiana na Samaria na Yerusalemu.
Palabra de Yahvé que vino a Miqueas de Morashet en los días de Jotam, Acaz y Ezequías, reyes de Judá, que vio sobre Samaria y Jerusalén.
2 Sikilizeni, ninyi watu wote. Sikilizeni, dunia, na vyote vilivyomo kwenye dunia. Acheni Yahwe ashuhudiwe dhidi yenu, Bwana kutoka kwenye hekalu lake takatifu.
¡Oíd, pueblos, todos vosotros! Escucha, oh tierra, y todo lo que hay en ella. Que el Señor Yahvé sea testigo contra ti, al Señor de su santo templo.
3 Tazama, Yahwe anakuja kutoka mahali pake; atashuka chini na kupakanyaga mahali pa juu katika dunia.
Porque he aquí que Yahvé sale de su lugar, y bajará y pisará los lugares altos de la tierra.
4 Milima itayeyuka chini yake; mabonde yatapasuka vipande vipande kama mshumaa mbele ya moto, kama maji ambayo yamemwagika chini ya mteremko mkali.
Las montañas se derriten bajo él, y los valles se deshacen como la cera ante el fuego, como las aguas que se vierten por un lugar escarpado.
5 Haya yote ni kwasababu ya uasi wa Yakobo, na kwasababu ya dhambi za nyumba ya Israeli. Je sababu ilikuwa nini kwa uasi wa Yakobo? Je ilikuwa Samaria? Je sababu ilikuwa nini kwa mahali pa juu pa Yuda? Je haiukuwa Yerusalemu?
“Todo esto es por la desobediencia de Jacob, y por los pecados de la casa de Israel. ¿Cuál es la desobediencia de Jacob? ¿No es Samaria? ¿Y cuáles son los lugares altos de Judá? ¿No son Jerusalén?
6 “Nitaifanya Samaria rundo la uharibifu katika shamba, kama eneo la kupandia mizabibu. Nitayavuta mawe ya jengo lake kwenda kwenye bonde; Nitaifunua misingi yake.
Por eso haré que Samaria sea como un montón de escombros del campo, como lugares para plantar viñedos; y derramaré sus piedras en el valle, y yo descubriré sus cimientos.
7 Sanamu zake zote za kuchonga zitapondwa vipande vipande; na zawadi zake zote zitachomwa moto. Kwa kuwa zawadi zake za ukahaba amezikusanya, na kama malipo ya ukahaba yatarudi.”
Todos sus ídolos serán despedazados, todos sus regalos del templo serán quemados con fuego, y destruiré todas sus imágenes; pues del alquiler de una prostituta los ha reunido, y al alquiler de una prostituta volverán”.
8 Kwa sababu hii nitalia na kuomboleza; nitaenda peku peku na uchi; Nitaomboleza kama mbeha na kuomboleza kama bundi.
Por esto me lamentaré y lloraré. Iré despojado y desnudo. Aullaré como los chacales y llorar como los avestruces.
9 Kwa kuwa jeraha lake haliponi, kwa kuwa imefika kwa Yuda. Imefikia lango la watu wangu, hadi Yerusalemu.
Porque sus heridas son incurables; porque ha llegado incluso a Judá. Llega hasta la puerta de mi pueblo, incluso a Jerusalén.
10 Msiache kuwambia kuhusu katika Gathi; msilie tena. Katika Bethi Leafra nabiringisha mwenyewe kwenye mavumbi.
No lo cuentes en Gat. No llores en absoluto. En Beth Ophrah me he revolcado en el polvo.
11 Piteni karibu na, makao ya Shafiri, katika uchi na aibu. Makazi ya Zaanani hayatatoka nje. Maombolezo ya Beth Ezeli, kwa ajili ya ulinzi yamechukuliwa.
Pasa, habitante de Shaphir, en desnudez y vergüenza. El habitante de Zaanan no saldrá. El lamento de Beth Ezel te quitará su protección.
12 Kwa kuwa wakaaji wa Marothi hungoja habari njema, kwa sababu hofu, kwa sababu msiba umetoka kwa Yahwe hadi kwenye malango ya Yerusalemu.
Porque el habitante de Maroth espera ansiosamente el bien, porque el mal ha bajado de Yahvé a la puerta de Jerusalén.
13 Wfuungeni lijamu farasi wakokote gari la farasi, makazi ya Lakishi. Wewe Lakishi, ulikuwa mwanzo wa dhambi kwa binti Sayuni, kwa kuwa makosa ya Israeli yalionekana kwako.
Engancha el carro al veloz corcel, habitante de Laquis. Fue el principio del pecado para la hija de Sión; porque las transgresiones de Israel fueron encontradas en ti.
14 Hivyo utaipa zawadi ya kuagia Moreshethi Gathi; mji wa Akzibu utawavunja moyo wafalme wa Israeli.
Por lo tanto, darás un regalo de despedida a Moresheth Gath. Las casas de Achzib serán un engaño para los reyes de Israel.
15 Tena nitaleta ushindi kwako, makazi ya Maresha; uzuri wa Israeli utakuja Adulamu.
Aún traeré un conquistador a ustedes, habitantes de Mareshah. La gloria de Israel llegará a Adulam.
16 Kata kipara chako na kata nywele zako kwa ajili ya watoto ambao unaowafurahisha. Fanya kipara chako mwenyewe kama tai, kwa ajili ya watoto wako watakao kwenda utumwani kutoka kwako
Aféitate la cabeza, y cortarte el pelo por los hijos de tu deleite. Agranda tu calvicie como el buitre, ¡porque han ido al cautiverio de ti!

< Mika 1 >