< Mathayo 1 >
1 Kitabu cha ukoo wa Yesu Kristo mwana wa Daudi, mwana wa Ibrahimu.
İbrıhımaaşina, Davudaaşina eyxhena I'sa Masixhna nasıl:
2 Ibrahimu alikuwa baba wa Isaka, na Isaka baba wa Yakobo, na Yakobo baba wa Yuda na ndugu zake.
İbrıhımıke I'saq' g'arı. I'saq'ıke Yaaq'ub g'arı. Yaaq'ubukeb Yahudiy mang'un çocar g'abı.
3 Yuda alikuwa baba wa Peresi na Sera kwa Tamari, Peresi baba wa Hezeroni, na Hezeroni baba wa Ramu.
Yahudukeb Tamaree vuxuyn Peresiy Zarax g'avayle. Peresıker Xetsron g'arayle. Xetsronuker Ram g'arayle.
4 Ramu alikuwa baba wa Aminadabu, Aminadabu baba wa Nashoni, na Nashoni baba wa Salimoni.
Ramıker Amminadav g'arayle. Amminadavıker Naxşon g'arayle. Naxşonıker Salmon g'arayle.
5 Salimoni alikuwa baba wa Boazi kwa Rahabu, Boazi baba wa Obedi kwa Ruth, Obedi baba wa Yese,
Salmonıker Raxavee uxuna Boaz g'arayle. Boazıker Rutee uxuna Oved g'arayle. Ovedıker Yessey g'arayle.
6 Yese alikuwa baba wa mfalme Daudi. Daudi alikuwa baba wa Sulemani kwa mke wa Uria.
Yesseyker paççah Davud g'arayle. Davuduker Uriyeyne xhunaşşee uxuna Sıleyman g'arayle.
7 Sulemani alikuwa baba wa Rehoboamu, Rehoboamu baba wa Abiya, Abiya baba wa Asa.
Sıleymanıke Rexavam g'arayle. Rexavamıke Aviya g'arayle. Aviyadıker Asaf g'arayle.
8 Asa alikuwa baba wa Yehoshafati, Yehoshafati baba wa Yoramu, na Yoramu baba wa Uzia.
Asafıker Yehoşafat g'arayle. Yehoşafatıke Yehoram g'arayle. Yehoramıker Uzziya g'arayle.
9 Uzia alikuwa baba wa Yothamu, Yothamu baba wa Ahazi, Ahazi baba wa Hezekia.
Uzziyeker Yotam g'arayle. Yotamıker Axaz g'arayle. Axazıker Xizqiya g'arayle.
10 Hezekia alikuwa baba wa Manase, Manase baba wa Amoni na Amoni baba wa Yosia.
Xizqiyeker Menaşşe g'arayle. Menaşşeyker Amos g'arayle. Amosuker Yoşiya g'arayle.
11 Yosia alikuwa baba wa Yekonia na kaka zake wakati wa kuchukuliwa kwenda Babeli.
İzrailin millet Baabil eyhene ölkeeqa g'e'eşşemee, Yoşiyayke Yekonyayiy mang'un çocar g'avayle.
12 Na baada ya kuchukuliwa kwenda Babeli, Yekonia alikuwa baba wa Shatieli, Shatieli alikuwa babu yake na Zerubabeli.
Baabileençe qabıyle qiyğa, Yekonyayke Şealtiel g'arayle. Şealtieliker Zorubbabil g'arayle.
13 Zerubabeli alikuwa baba wa Abiudi, Abiudi baba wa Eliakimu, na Eliakimu baba wa Azori.
Zorubbabiliker Avihud g'arayle. Avihuduker Elyaqim g'arayle. Elyaqimıker Azor g'arayle.
14 Azori alikuwa baba wa Zadoki, Zadoki baba wa Akimu, na Akimu baba wa Eliudi.
Azoruker Tsadok g'arayle. Tsadokuker Axim g'arayle. Aximiker Elihud g'arayle.
15 Eliudi alikuwa baba wa Elieza, Elieza baba wa Matani na Matani baba wa Yakobo.
Elihuduker Eleazar g'arayle. Eleazarıker Mattan g'arayle. Mattanıker Yaaq'ub g'arayle.
16 Yakobo alikuwa baba wa Yusufu mume wa Mariamu, ambaye kwa yeye Yesu alizaliwa, aitwaye Kristo.
Yaaq'ubuke Mayramna adamiy Yusuf g'arayle. Mayrameeyir I'sa, insanaaşe Masixhva eyhena uxoxa.
17 Vizazi vyote tangu Ibrahimu hadi Daudi vilikuwa vizazi kumi na vinne, kutoka Daudi hadi kuchukuliwa kwenda Babeli vizazi kumi na vinne, na kutoka kuchukuliwa kwenda Babeli hadi Kristo vizazi kumi na vinne.
Gırgıda İbrıhımılee Davudulqameen nasılbı qədəqqəxhee yits'ıyoq'ab vooxhe, Davudulee Baabilqa g'e'epşesmeen nasılbıd qədəqqəxhee yits'ıyoq'ab vooxhe, Baabilqa g'eepşiyled Masixhılqameen nasılbı qədəqqəxheeyid yits'ıyoq'abcab nasıl vooxhe.
18 Kuzaliwa kwa Yesu Kristo kulikuwa kwa namna hii. Mama yake, Mariamu, alichumbiwa na Yusufu, lakini kabla hawajakutana, alionekana kuwa na mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu.
I'sa Masixhın yedike ıxhay inəxüd ıxha: mang'una yed Mayram Yusufne doyulyniy qey'ı. Manbışe davatbı ha'assecad, məng'ı'n vuxhne yixhay aq'valqa qığeç'e. Məng'ee uxasın Uşax Muq'addasne Rı'hı'ke eyxhe.
19 Mume wake Yusufu, alikuwa mtu mwenye haki hakutaka kumwaibisha hadharani. Aliamua kusitisha uchumba wake naye kwa siri.
Yusuf qorkuna insan eyxhe, Mayram insanaaşine k'ane tesser hidee'esva, mang'us mana dyugulenra galerç'es yikkiykan.
20 Alipokuwa akifikiri juu ya mambo haya, Malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akisema,'' Yusufu mwana wa Daudi, usiogope kumchukua Mariamu kama mkeo, kwa sababu mimba aliyonayo ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu.
Mang'vee man kar ək'leeqa k'eççumee, mang'us nik'ek Rəbbin malaaik dyagu eyhen: – Davudaaşda dix Yusuf! Mayram hee'es qıməyq'ən, məng'ı'ne vuxhnedın Uşax Muq'addasne Rı'hı'ken vodun.
21 Atajifungua mtoto wa kiume na utamwita jina lake Yesu, kwa maana atawaokoa watu wake na dhambi zao.''
Mayramee Dix uxas, ğu Mang'un do I'sa (Rəbbee g'attixhan ha'a) gixhxhe, Mang'vee Cun millet manbışde bınahbışike g'attixhan ha'as.
22 Yote haya yalitokea kutimizwa kile kilichonenwa na Bwana kwa njia ya nabii, akisema,
İn gırgın kar, Rəbbine mizele yuşan ha'ane peyğambaree otk'unin xhinne eyxhe:
23 “Tazama, bikira atachukua mimba na kuzaa mtoto wa kiume, na watamwita jina lake Imanueli”— maana yake, “Mungu pamoja nasi.”
«Haane, içiy vuxhne ayxu sa Dix uxas, Doyud İmmanuel gixhxhes». (İmmanuel «Allah şaka vornava» eyhen vodun.)
24 Yusufu aliamka kutoka usingizini na kufanya kama malaika wa Bwana alivyomwamuru na alimchukua kama mkewe.
Yusuf muğur qıxhamee, mang'vee Rəbbine malaaikee uvhuyn xhinne ha'a: Mayramıke cus xhunaşşe hee'e.
25 Hata hivyo, hakulala naye mpaka alipojifungua mtoto wa kiume na alimwita jina lake Yesu.
Mayramee Dix uxasmee, Yusuf məng'ı'ka g'ılexha deş. Məng'ee uxuyne Uşaxın doyud, Yusufee I'sa giyxhe.