< Mathayo 1 >

1 Kitabu cha ukoo wa Yesu Kristo mwana wa Daudi, mwana wa Ibrahimu.
Abraham le David i suan ahi, Jesus Christ i khang thu sia hibang a hihi.
2 Ibrahimu alikuwa baba wa Isaka, na Isaka baba wa Yakobo, na Yakobo baba wa Yuda na ndugu zake.
Abraham tapa Isaac; Isaac tapa Jacob; Jacob tapa Judah le a suapuite;
3 Yuda alikuwa baba wa Peresi na Sera kwa Tamari, Peresi baba wa Hezeroni, na Hezeroni baba wa Ramu.
Judah le Tamar tapa te Perez le Zerah, Perez ta Hezron; Hezron tapa Aram,
4 Ramu alikuwa baba wa Aminadabu, Aminadabu baba wa Nashoni, na Nashoni baba wa Salimoni.
Aram tapa Amminadab; Amminadab tapa Nahshon; Nahshon tapa Salmon;
5 Salimoni alikuwa baba wa Boazi kwa Rahabu, Boazi baba wa Obedi kwa Ruth, Obedi baba wa Yese,
Salmon tapa Boaz hi; Boaz i nu Rahab; Boaz tapa Obed; Obed nu Ruth; Obed tapa Jesse;
6 Yese alikuwa baba wa mfalme Daudi. Daudi alikuwa baba wa Sulemani kwa mke wa Uria.
Jesse tapa David Kumpipa; David kumpipa tapa Solomon; a nu sia Uriah i zi hi ngei hi.
7 Sulemani alikuwa baba wa Rehoboamu, Rehoboamu baba wa Abiya, Abiya baba wa Asa.
Solomon tapa Roboam; Roboam tapa Abijah; Abijah tapa Asa;
8 Asa alikuwa baba wa Yehoshafati, Yehoshafati baba wa Yoramu, na Yoramu baba wa Uzia.
Asa tapa Jehoshaphat; Jehoshaphat tapa Jehoram; Jehoram ta Uzziah;
9 Uzia alikuwa baba wa Yothamu, Yothamu baba wa Ahazi, Ahazi baba wa Hezekia.
Uzziah ta Jotham; Jotham ta Ahaz; Ahaz ta Hezekiah;
10 Hezekia alikuwa baba wa Manase, Manase baba wa Amoni na Amoni baba wa Yosia.
Hezekiah ta Manasseh; Manasseh ta Amon; Amon tapa Josiah;
11 Yosia alikuwa baba wa Yekonia na kaka zake wakati wa kuchukuliwa kwenda Babeli.
Josiah ta Jechoniah, Jechoniah in Babylon khua ah a ki khin ma a nei a suapui te;
12 Na baada ya kuchukuliwa kwenda Babeli, Yekonia alikuwa baba wa Shatieli, Shatieli alikuwa babu yake na Zerubabeli.
Babylon a ki khin zawkciang Jechoniah tapa Shealtiel; Shealtiel tapa Zerubbabel;
13 Zerubabeli alikuwa baba wa Abiudi, Abiudi baba wa Eliakimu, na Eliakimu baba wa Azori.
Zerubbabel ta Abiud; Abiud ta Eliakim; Eliakim ta Azor;
14 Azori alikuwa baba wa Zadoki, Zadoki baba wa Akimu, na Akimu baba wa Eliudi.
Azor ta Zadok; Zadok ta Achim; Achim ta Elihud;
15 Eliudi alikuwa baba wa Elieza, Elieza baba wa Matani na Matani baba wa Yakobo.
Elihud ta Eleazar; Eleazar ta Matthan; Matthan ta Jacob;
16 Yakobo alikuwa baba wa Yusufu mume wa Mariamu, ambaye kwa yeye Yesu alizaliwa, aitwaye Kristo.
Jacob ta Joseph; Joseph sia Mary i pasal hi a, Mary sung pan Christ a kici Jesus hong suak hi.
17 Vizazi vyote tangu Ibrahimu hadi Daudi vilikuwa vizazi kumi na vinne, kutoka Daudi hadi kuchukuliwa kwenda Babeli vizazi kumi na vinne, na kutoka kuchukuliwa kwenda Babeli hadi Kristo vizazi kumi na vinne.
Tua ahikom Abraham pan in David dong khang sawm le khang li hi a; David pan in Babylon ah a ki khin dong khang sawm le khang li; Babylon a ki khin pan in Christ ciang dong khang sawm le khang li a hihi.
18 Kuzaliwa kwa Yesu Kristo kulikuwa kwa namna hii. Mama yake, Mariamu, alichumbiwa na Yusufu, lakini kabla hawajakutana, alionekana kuwa na mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu.
Jesus Christ sua na thu sia hibang a hihi: A nu Mary sia Joseph in dokzu a piak sa hi a, a ki ngawm khop ma in Thaa Thiangtho taw nau ngil om hi.
19 Mume wake Yusufu, alikuwa mtu mwenye haki hakutaka kumwaibisha hadharani. Aliamua kusitisha uchumba wake naye kwa siri.
Joseph sia thutang khat hi a, Mary mindaisak nuam ngawl ahikom, nol ku tu in ngaisun hi.
20 Alipokuwa akifikiri juu ya mambo haya, Malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akisema,'' Yusufu mwana wa Daudi, usiogope kumchukua Mariamu kama mkeo, kwa sababu mimba aliyonayo ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu.
Tabang a ngaisut laitak in, a mang sung ah vantungmi khat hong ki lang a, David suan Joseph awng, Mary na zi tu in teenpui tu lau heak in: banghangziam cile a naungil sia Tha Thiangtho taw a hihi.
21 Atajifungua mtoto wa kiume na utamwita jina lake Yesu, kwa maana atawaokoa watu wake na dhambi zao.''
Tapa nei tu a, tua tapa in a mite mawna pan ngum tu ahi man in, Jesus ci in a min na phuak tu hi: ci in vangtungmi in son hi.
22 Yote haya yalitokea kutimizwa kile kilichonenwa na Bwana kwa njia ya nabii, akisema,
Hi te theampo Pathian in kamsang te tungtawn in a sonkholsa a tangtun na hi, kamsang i sonkhol na ah,
23 “Tazama, bikira atachukua mimba na kuzaa mtoto wa kiume, na watamwita jina lake Imanueli”— maana yake, “Mungu pamoja nasi.”
En vun, ngaknu thiangtho khat naungil om tu a, tapa khat nei tu hi, a min Immanuel kiphuak tu hi, Emmanuel a khiakna sia, Pathian eite taw hong om hi, ci nopna a hihi.
24 Yusufu aliamka kutoka usingizini na kufanya kama malaika wa Bwana alivyomwamuru na alimchukua kama mkewe.
Joseph a khanlaw ciang, Topa vantungmi i sawl bang in, Mary tenpui hi.
25 Hata hivyo, hakulala naye mpaka alipojifungua mtoto wa kiume na alimwita jina lake Yesu.
Ahihang taciil a nei dong luppui ngawl a, a min Jesus ci in phuak hi.

< Mathayo 1 >