< Mathayo 7 >

1 Usihukumu, nawe usije ukahukumiwa.
Judge not, that ye be not judged.
2 Kwa hukumu unayohukumu, nawe utahukumiwa. Na kwa kipimo unachopima na wewe pia utapimiwa hicho hicho.
For with what judgment ye judge, ye will be judged; and with what measure ye mete, it will be measured to you.
3 Na kwa nini unatazama kipande cha mti kilichoko kwenye jicho la ndugu yako, lakini hutambuwi kipande cha gogo ambalo limo katika jicho lako?
And why dost thou look at the mote that is in thy brother's eye, and not perceive the beam in thine own eye?
4 Unawezaje kusema kwa ndugu yako, ngoja nikutolee kipande kilichomo kwenye jicho lako, wakati kipande cha gogo kimo ndani ya jicho lako?
Or how wilt thou say to thy brother, Let me take the mote out of thine eye; when, lo! the beam is in thine own eye?
5 Mnafiki wewe; kwanza toa gogo lililomo kwenye jicho lako, na ndipo utakapoweza kuona vizuri na kukitoa kipande cha mti kilichomo kwenye jicho la ndugu yako.
Hypocrite! first cast the beam out of thine own eye; and then wilt thou see clearly to take the mote out of thy brother's eye.
6 Usiwape mbwa kilicho kitakatifu, na usiwarushie nguruwe lulu mbele yao. Vinginevyo wataviharibu na kuvikanyaga kwa miguu, na tena watakugeukia wewe na kukurarua vipande vipande.
Give not that which is holy to dogs, neither cast ye your pearls before swine; lest they trample them under their feet, and turn upon you and rend you.
7 Omba, nawe utapewa. Tafuta, nawe utapata. Bisha hodi, na wewe utafunguliwa.
Ask, and it will be given you; seek, and ye will find; knock, and the door will be opened to you.
8 Kwa yeyote anayeomba, hupokea. Na kwa yeyote anayetafuta, hupata. Na kwa mtu ambaye anayebisha hodi, atafunguliwa.
For every one that asketh, receiveth; and he that seeketh, findeth; and to him that knocketh, the door will be opened.
9 Au kuna mtu miongoni mwenu ambaye, ikiwa mtoto wake amemwomba kipande cha mkate atampa jiwe?
Or what man is there of you, who, if his son ask for bread, will give him a stone?
10 Au ikiwa atamwomba samaki, na yeye atampa nyoka?
or, if he ask for a fish, will give him a serpent?
11 Kwa hiyo, ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu zawadi nzuri, Je! Ni kiasi gani zaidi Baba aliye mbinguni atawapa vitu vizuri wale wanao muomba yeye?
If ye then, though evil, know how to give good gifts to your children, how much more will your Father who is in heaven give good things to them that ask him!
12 Kwa sababu hiyo, unapotaka kufanyiwa kitu chochote na watu wengine, nawe pia itakupasa kuwafanyia hivyo hivyo wao. Kwa kuwa hiyo ni sheria na manabii.
All things, then, whatever ye would that men should do to you, do ye also so to them; for this is the Law and the Prophets.
13 Ingieni kwa kupitia geti jembamba. Kwa kuwa geti ni pana na njia ni pana inayoongoza kwenye uharibifu, na kuna watu wengi wanaopitia njia hiyo.
Enter in at the strait gate; for wide is the gate, and broad is the way, that leadeth to destruction; and many are they who go in thereat.
14 Geti ni jembamba, Geti jembamba ni njia inayongooza katika uzima na ni wachache wanaoweza kuiona.
For strait is the gate, and narrow the way, that leadeth to life; and few are they who find it.
15 Jihadhari na manabii wa uongo, wanaokuja wamevaa ngozi ya kondoo, lakini kweli ni mbweha wakali.
Beware of the false prophets, who come to you in sheep's clothing, but inwardly are ravening wolves.
16 Kwa matunda yao mtawatambua. Je watu wanaweza kuvuna matunda kwenye miba, au mtini kwenye mbengu ya mbaruti?
Ye may know them by their fruits. Do men gather grapes of thorns, or figs of thistles?
17 Kwa jinsi hiyo, kila mti mzuri huzaa matunda mazuri, lakini mti mbaya huzaa matunda mabaya.
So every good tree beareth good fruit; but a bad tree beareth bad fruit.
18 Mti mzuri hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mbaya hauwezi kuzaa matunda mazuri.
A good tree cannot bear bad fruit, nor call a bad tree bear good fruit.
19 Kila mti ambao hauzai matunda mazuri utakatwa na kutupwa katika moto.
Every tree that beareth not good fruit is cut down, and cast into the fire.
20 Hivyo basi, utawatambua kutokana na matunda yao.
So then ye may know them by their fruits.
21 Si kila mtu aniambiaye mimi, 'Bwana, Bwana,' ataingia katika ufalme wa mbinguni, bali ni yule pekee atendaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.
Not every one that saith to me, Lord, Lord, will enter into the kingdom of heaven; but he that doeth the will of my Father who is in heaven.
22 Watu wengi wataniambia siku hiyo, 'Bwana, Bwana, hatukutoa unabii kwa jina lako, hatukutoa mapepo kwa jina lako, na kwa jina lako tulifanya matendo mengi makuu?'
Many will say to me in that day, Lord, Lord, did we not prophesy in thy name, and in thy name cast out demons, and in thy name work many miracles?
23 Ndipo nitawaambia wazi, 'sikuwatambua ninyi! Ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu!'
And then will I declare to them, I never knew you: depart from me, ye that work iniquity.
24 Kwa hiyo, kila mmoja asikiaye maneno yangu na kutii atafanana na mtu mwenye hekima aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba.
Every one then that heareth these sayings of mine, and doeth them, shall be likened to a wise man, who built his house upon a rock;
25 Mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, na upepo ukaja na ukaipiga nyumba hiyo, lakini haikuweza kuanguka chini, kwa kuwa ilikuwa imejengwa juu ya mwamba.
and the rain descended, and the streams came, and the winds blew, and beat upon that house; and it fell not; for it was founded upon a rock.
26 Lakini kila mtu anayesikia neno langu na asilitii, atafananishwa na mtu mpumbavu aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga.
And every one that heareth these sayings of mine, and doeth them not, shall be likened to a foolish man, who built his house upon the sand;
27 Mvua ikaja, mafuriko yakaja, na upepo ukaja na kuipiga nyumba hiyo. Na ikaanguka, na uharibifu wake ukakamilika.”
and the rain descended, and the streams came, and the winds blew, and beat upon that house; and it fell; and great was its fall.
28 Ulifika wakati ambao Yesu alipomaliza kuongea maneno haya, makutano walishangazwa na mafundisho yake,
And it came to pass, when Jesus had ended these sayings, that the multitudes were astonished at his teaching.
29 kwa kuwa alifundisha kama mtu mwenye mamlaka, na si kama waandishi wao.
For he taught them as having authority, and not as their scribes.

< Mathayo 7 >