< Mathayo 6 >
1 Zingatia kutotenda matendo ya haki mbele ya watu ili kujionyesha, vinginevyo hutapata thawabu kutoka kwa Baba aliye mbinguni.
Take heed that ye do not your alms before men, to be seen by them: otherwise ye have no reward from your Father who is in heaven.
2 Hivyo basi unapotoa usipige tarumbeta na kujisifu mwenyewe kama wanafiki wanavyofanya katika masinagogi na katika mitaa, ili kwamba watu wawasifu. Kweli nawaambia, wamekwisha kupokea thawabu yao.
Therefore, when thou doest [thy] alms, do not sound a trumpet before thee, as the hypocrites do, in the synagogues, and in the streets, that they may have glory from men. Verily, I say to you, they have their reward.
3 Lakini wewe unapotoa, mkono wako wa kushoto usijue kinachofanywa na mkono wa kulia,
But when thou doest alms, let not thy left hand know what thy right hand doeth:
4 ili kwamba zawadi yako itolewe kwa siri. Ndipo Baba yako aonaye sirini atakupatia thawabu yako.
That thy alms may be in secret; and thy Father who seeth in secret, himself will reward thee openly.
5 Na unapokuwa ukiomba, usiwe kama wanafiki, kwa kuwa wanapenda kusimama na kuomba kwenye masinagogi na kwenye kona za mitaani, ili kwamba watu wawatazame. Kweli nawaambia, wamekwishapokea thawabu yao.
And when thou prayest, thou shalt not be as the hypocrites [are]: for they love to pray standing in the synagogues, and in the corners of the streets, that they may be seen by men. Verily, I say to you, they have their reward.
6 Lakini wewe, unapo omba, ingia chumbani. Funga mlango, na uombe kwa kwa Baba yako aliye sirini. Ndipo Baba yako aonaye sirini atakupatia thawabu yako.
But thou, when thou prayest, enter into thy closet, and when thou hast shut thy door, pray to thy Father who is in secret, and thy Father who seeth in secret, will reward thee openly.
7 Na unapokuwa ukiomba, usirudie rudie maneno yasiyo na maana kama mataifa wanavyofanya, kwa kuwa wanafikiri kwamba watasikiwa kwa sababu ya maneno mengi wanayosema.
But when ye pray, use not vain repetitions, as the heathen do: for they think that they shall be heard for their much speaking.
8 Kwa hiyo, usiwe kama wao, kwa kuwa Baba yako anatambua mahitaji yako hata kabla hujaomba kwake.
Therefore be ye not like them: for your Father knoweth what things ye need before ye ask him.
9 Hivyo basi omba hivi: Baba yetu uliye mbinguni, ulitukuze jina lako.
After this manner therefore pray ye: Our Father who art in heaven, Hallowed be thy name.
10 Ufalme wako uje, mapenzi yako yafanyike hapa duniani kama huko mbinguni.
Thy kingdom come. Thy will be done on earth as [it is] in heaven.
11 Utupatiye leo mkate wetu wa kila siku.
Give us this day our daily bread.
12 utusamehe deni zetu, kama nasi tunavyowasamehe wadeni wetu.
And forgive us our debts, as we forgive our debtors.
13 Na usitulete katika majaribu, lakini utuepushe kutoka kwa yule mwovu.'
And lead us not into temptation, but deliver us from evil. For thine is the kingdom, and the power, and the glory, for ever. Amen.
14 Ikiwa mtawasemehe watu makosa yao, Baba yako aliye mbinguni pia atawasamehe ninyi.
For, if ye forgive men their trespasses, your heavenly Father will also forgive you:
15 Lakini ikiwa hamtawasamehe makosa yao, wala Baba yenu hatawasamehe makosa yenu.
But if ye forgive not men their trespasses, neither will your Father forgive your trespasses.
16 Zaidi ya yote, unapokuwa umefunga, usioneshe sura ya huzuni kama wanafiki wanavyofanya, kwa kuwa wanakunja sura zao ili kwamba watu wawatambue wamefunga. Kweli ninakuambia, wamekwisha kupokea thawabu yao.
Moreover, when ye fast, be not as the hypocrites, of a sad countenance: for they disfigure their faces, that they may appear to men to fast. Verily, I say to you, they have their reward.
17 Lakini wewe, unapokuwa umefunga, paka mafuta kichwa chako na uoshe uso wako.
But thou, when thou fastest, anoint thy head, and wash thy face;
18 Hivyo haitakuonesha mbele ya watu kuwa umefunga, lakini tu itakuwa kwa Baba yako aliye sirini. Na Baba yako aonaye sirini, atakupa thawabu yako.
That thou mayest not appear to men to fast, but to thy Father, who is in secret: and thy Father, who seeth in secret, shall reward thee openly.
19 Usijitunzie hazina yako mwenyewe hapa duniani, ambapo nondo na kutu huharibu, ambapo wezi huvunja na kuiba.
Lay not up for yourselves treasures upon earth, where moth and rust doth corrupt, and where thieves break through and steal:
20 Badala yake, jitunzie hazina yako mwenyewe mbinguni, ambapo wala nondo wala kutu hawezi kuharibu, na ambapo wezi hawawezi kuvunja na kuiba.
But lay up for yourselves treasures in heaven, where neither moth nor rust doth corrupt, and where thieves do not break through nor steal.
21 Kwa kuwa hazina yako ilipo, ndipo na moyo wako utakapokuwepo pia.
For where your treasure is, there will your heart be also.
22 Jicho ni taa ya mwili. Kwa hiyo, ikiwa jicho lako ni zima, mwili wote utajazwa na nuru.
The light of the body is the eye: if therefore thy eye be single, thy whole body will be full of light.
23 Lakini ikiwa jicho lako ni bovu, mwili wako wote umejaa giza totoro. Kwahiyo, ikiwa nuru ambayo imo ndani yako ni giza hasa, ni giza kubwa kiasi gani!
But if thy eye be evil, thy whole body will be full of darkness. If therefore the light that is in thee is darkness, how great [is] that darkness!
24 Hakuna hata mmoja anayeweza kuwatumikia mabwana wawili, kwa kuwa atamchukia mmoja na kumpenda mwingine, au la sivyo atajitoa kwa mmoja na kumdharau mwingine. Hamuwezi kumtumikia Mungu na mali.
No man can serve two masters: for either he will hate the one, and love the other; or else he will hold to the one, and despise the other. Ye cannot serve God and mammon.
25 Kwa hiyo nakuambia, usiwe na mashaka kuhusu maisha yako, kuwa utakula nini au utakunywa nini, au kuhusu mwili wako, utavaa nini. Je! Maisha si zaidi ya chakula na mwili zaidi ya mavazi?
Therefore I say to you, Be not anxious for your life, what ye shall eat, or what ye shall drink; nor yet for your body, what ye shall put on. Is not the life more than food, and the body than raiment?
26 Tazama ndege walioko angani. Hawapandi na hawavuni na hawakusanyi na kutunza ghalani, lakini Baba yenu wa mbinguni huwalisha wao. Je ninyi si wa thamani zaidi kuliko wao?
Behold the fowls of the air: for they sow not, neither do they reap, nor gather into barns; yet your heavenly Father feedeth them. Are ye not much better than they?
27 Na ni nani miongoni mwenu kwa kujihangaisha anaweza kuongeza dhiraa moja kwenye uhai wa maisha yake?
Which of you by anxious care can add one cubit to his stature?
28 Na kwa nini mna kuwa na wasiwasi kuhusu mavazi? Fikiria kuhusu maua kwenye mashamba, jinsi yanavyokua. Hayafanyi kazi na hayawezi kujivisha.
And why are ye anxious for raiment? Consider the lilies of the field how they grow? they toil not, neither do they spin?
29 Bado ninawaambia, hata Sulemani katika utukufu wake wote hakuvikwa kama mojawapo ya haya.
And yet I say to you, that even Solomon in all his glory was not arrayed like one of these.
30 Ikiwa Mungu anayavalisha majani katika mashamba, ambayo yadumu siku moja na kesho yanatupwa katika moto, je ni kwa kiasi gani atawavalisha ninyi, ninyi wenye imani ndogo?
Wherefore, if God so clotheth the grass of the field, which to-day is, and to-morrow is cast into the oven, [will he] not much more [clothe] you, O ye of little faith?
31 Kwa hiyo msiwe na wasiwasi nakusema, 'Je tutakula nini?' au “Je tutakunywa nini?” au “Je tutavaa nguo gani?”
Therefore be not anxious, saying, What shall we eat? or what shall we drink? or, with what shall we be clothed?
32 Kwa kuwa mataifa wanatafuta mambo haya, na Baba yenu wa mbinguni anajua kuwa mnahitaji hayo.
(For after all these things do the Gentiles seek) for your heavenly Father knoweth that ye have need of all these things.
33 Lakini kwanza tafuteni ufalme wake na haki yake na haya yote yatakabidhiwa kwako.
But seek ye first the kingdom of God, and his righteousness, and all these things shall be added to you.
34 Kwa hiyo, usione shaka kwa ajili ya kesho, kwa kuwa kesho itajishughulikia yenyewe. Kila siku inatosha kuwa na tatizo lake yenyewe.
Therefore be not anxious for the morrow: for the morrow will be solicitous for the things of itself. Sufficient to the day [is] its own evil.