< Mathayo 6 >
1 Zingatia kutotenda matendo ya haki mbele ya watu ili kujionyesha, vinginevyo hutapata thawabu kutoka kwa Baba aliye mbinguni.
“不要将善事做在人的面前,叫别人看见,否则就得不到天父的赏赐。
2 Hivyo basi unapotoa usipige tarumbeta na kujisifu mwenyewe kama wanafiki wanavyofanya katika masinagogi na katika mitaa, ili kwamba watu wawasifu. Kweli nawaambia, wamekwisha kupokea thawabu yao.
所以若你施舍穷人,不要像那些伪君子一样,在会堂和街头到处张扬,博取众人的称赞。实话告诉你们,他们已经得到了他们的赏赐。
3 Lakini wewe unapotoa, mkono wako wa kushoto usijue kinachofanywa na mkono wa kulia,
你施舍的时候,不要叫你的左手知道右手所做的。
4 ili kwamba zawadi yako itolewe kwa siri. Ndipo Baba yako aonaye sirini atakupatia thawabu yako.
你的施舍应隐秘进行。因圣父在隐秘中观察,必将赏赐于你。
5 Na unapokuwa ukiomba, usiwe kama wanafiki, kwa kuwa wanapenda kusimama na kuomba kwenye masinagogi na kwenye kona za mitaani, ili kwamba watu wawatazame. Kweli nawaambia, wamekwishapokea thawabu yao.
当你们祈祷,不可如伪君子一般:他们只喜欢站在会堂和路口祈祷,只为让人看见。说实话,他们已经得到了他们的赏赐。
6 Lakini wewe, unapo omba, ingia chumbani. Funga mlango, na uombe kwa kwa Baba yako aliye sirini. Ndipo Baba yako aonaye sirini atakupatia thawabu yako.
至于你们,你们的祈祷应在密室中进行,关上门,向隐密中的圣父祈祷。因圣父在隐密中观察,必将赏赐于你。
7 Na unapokuwa ukiomba, usirudie rudie maneno yasiyo na maana kama mataifa wanavyofanya, kwa kuwa wanafikiri kwamba watasikiwa kwa sababu ya maneno mengi wanayosema.
当你祈祷,不可如异教徒般反复念叨毫无意义的词语。他们误以为只要重复,上帝就可以听到。
8 Kwa hiyo, usiwe kama wao, kwa kuwa Baba yako anatambua mahitaji yako hata kabla hujaomba kwake.
不可像他们那样,因为早在你们开口祈祷之前,圣父便已洞悉你们需要什么。
9 Hivyo basi omba hivi: Baba yetu uliye mbinguni, ulitukuze jina lako.
所以要这样祈祷: 我们的天父,赞颂你的圣名。
10 Ufalme wako uje, mapenzi yako yafanyike hapa duniani kama huko mbinguni.
愿你的国度降临!愿你的意志在世间成真,一如在天国一般。
11 Utupatiye leo mkate wetu wa kila siku.
今天请赐予我们需要的食物;
12 utusamehe deni zetu, kama nasi tunavyowasamehe wadeni wetu.
赦免我们的罪恶,一如我们饶恕了那些曾对我们犯下罪行之人;
13 Na usitulete katika majaribu, lakini utuepushe kutoka kwa yule mwovu.'
请阻止我们深陷诱惑,拯救我们脱离恶人。
14 Ikiwa mtawasemehe watu makosa yao, Baba yako aliye mbinguni pia atawasamehe ninyi.
如果你们饶恕他人对你犯下的罪,天父自会饶恕你们的罪。
15 Lakini ikiwa hamtawasamehe makosa yao, wala Baba yenu hatawasamehe makosa yenu.
如果你们不饶恕他人对你犯下的罪,天父也不会饶恕你们。
16 Zaidi ya yote, unapokuwa umefunga, usioneshe sura ya huzuni kama wanafiki wanavyofanya, kwa kuwa wanakunja sura zao ili kwamba watu wawatambue wamefunga. Kweli ninakuambia, wamekwisha kupokea thawabu yao.
当你们禁食,不可如伪君子般愁眉苦脸,他们只是装作难受的模样,向别人显示其正在禁食。实话告诉你们,他们已经得到了他们的赏赐。
17 Lakini wewe, unapokuwa umefunga, paka mafuta kichwa chako na uoshe uso wako.
当你禁食,要梳洗得当,
18 Hivyo haitakuonesha mbele ya watu kuwa umefunga, lakini tu itakuwa kwa Baba yako aliye sirini. Na Baba yako aonaye sirini, atakupa thawabu yako.
不要叫外人看到你在禁食,因圣父在隐秘中正在观察你,必将与你予以赏赐。
19 Usijitunzie hazina yako mwenyewe hapa duniani, ambapo nondo na kutu huharibu, ambapo wezi huvunja na kuiba.
不可在这世界上堆积财富,因地上有虫蛀,有锈蚀,还有贼闯入偷窃。
20 Badala yake, jitunzie hazina yako mwenyewe mbinguni, ambapo wala nondo wala kutu hawezi kuharibu, na ambapo wezi hawawezi kuvunja na kuiba.
你应在天堂积聚财富,那里没有虫蛀锈蚀,没有盗贼偷窃。
21 Kwa kuwa hazina yako ilipo, ndipo na moyo wako utakapokuwepo pia.
因为你最看重什么,就表明你是谁。
22 Jicho ni taa ya mwili. Kwa hiyo, ikiwa jicho lako ni zima, mwili wote utajazwa na nuru.
你的眼,就是点亮身体的灯。若眼睛健康,整个身体就会亮起来。
23 Lakini ikiwa jicho lako ni bovu, mwili wako wote umejaa giza totoro. Kwahiyo, ikiwa nuru ambayo imo ndani yako ni giza hasa, ni giza kubwa kiasi gani!
若眼睛邪恶,你的身体就会身处黑暗。如果你心中的‘光’成为黑暗,那才是真正的黑暗!
24 Hakuna hata mmoja anayeweza kuwatumikia mabwana wawili, kwa kuwa atamchukia mmoja na kumpenda mwingine, au la sivyo atajitoa kwa mmoja na kumdharau mwingine. Hamuwezi kumtumikia Mungu na mali.
一个人不能侍奉两主;你必会爱其中一人,恨另一人,或忠于其中一人,鄙视另一人;你无法同时服务于上帝和金钱。
25 Kwa hiyo nakuambia, usiwe na mashaka kuhusu maisha yako, kuwa utakula nini au utakunywa nini, au kuhusu mwili wako, utavaa nini. Je! Maisha si zaidi ya chakula na mwili zaidi ya mavazi?
所以我要说的是,不必担心生命,忧虑衣食住行。难道生命不比食物重要?身体不比衣服更重要?
26 Tazama ndege walioko angani. Hawapandi na hawavuni na hawakusanyi na kutunza ghalani, lakini Baba yenu wa mbinguni huwalisha wao. Je ninyi si wa thamani zaidi kuliko wao?
看天空中的鸟:它们不播种、不收割、不存粮食,但天父仍喂养它们。难道你们不比它们更宝贵吗?
27 Na ni nani miongoni mwenu kwa kujihangaisha anaweza kuongeza dhiraa moja kwenye uhai wa maisha yake?
你们谁又能通过忧虑,让寿命延长一分钟?
28 Na kwa nini mna kuwa na wasiwasi kuhusu mavazi? Fikiria kuhusu maua kwenye mashamba, jinsi yanavyokua. Hayafanyi kazi na hayawezi kujivisha.
何必为衣着忧虑?看看田野中那些美丽的鲜花,看看它们成长的方式:不必辛苦劳作,不必忙于纺织。
29 Bado ninawaambia, hata Sulemani katika utukufu wake wote hakuvikwa kama mojawapo ya haya.
但我想说的是,即使是所罗门最荣耀时刻的穿着,也比不上任何一朵野花。
30 Ikiwa Mungu anayavalisha majani katika mashamba, ambayo yadumu siku moja na kesho yanatupwa katika moto, je ni kwa kiasi gani atawavalisha ninyi, ninyi wenye imani ndogo?
田野的草今天还在,明天就会被扔进炉火中,如果上帝这样装扮田野,你们这些缺乏信任的人,上帝又怎会为你们做更多?
31 Kwa hiyo msiwe na wasiwasi nakusema, 'Je tutakula nini?' au “Je tutakunywa nini?” au “Je tutavaa nguo gani?”
所以不要忧虑,不要想着:‘我们该吃什么?喝什么?穿什么?’
32 Kwa kuwa mataifa wanatafuta mambo haya, na Baba yenu wa mbinguni anajua kuwa mnahitaji hayo.
这些只是异教徒的追求,你们的天父知道你们需要的一切。
33 Lakini kwanza tafuteni ufalme wake na haki yake na haya yote yatakabidhiwa kwako.
你们要先寻求天国,寻求他的生命正道,寻求他将给予你的一切。
34 Kwa hiyo, usione shaka kwa ajili ya kesho, kwa kuwa kesho itajishughulikia yenyewe. Kila siku inatosha kuwa na tatizo lake yenyewe.
所以不要为明天忧虑,因为明天自有明天的担忧。每天邪恶的事情已经够多了。”