< Mathayo 3 >

1 Katika siku zile Yohana Mbatizaji alikuja akihubiri katika nyika ya Yuda akisema,
In those days came John the Immerser, preaching in the wilderness of Judea,
2 “Tubuni kwa maana ufalme wa mbinguni u karibu.”
and saying: Repent, for the kingdom of heaven is at hand.
3 Kwa maana huyu ndiye aliyenenwa na nabii Isaya akisema, “sauti ya mtu aitaye kutoka jangwani; 'wekeni tayari njia ya Bwana, yanyoosheni mapito yake.”'
For this is he that was spoken of by Isaiah the prophet, saying: The voice of one crying in the wilderness, Prepare the way of the Lord, make his paths straight.
4 Sasa Yohana alivaa manyoya ya ngamia na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwituni.
But the same John had his clothing of camel’s hair, and a girdle of leather around his loins, and his food was locusts and wild honey.
5 Kisha Yerusalemu, Yuda yote, na eneo lote linalozunguka mto Yorodani wakaenda kwake.
Then went out to him Jerusalem, and all Judea, and all the region round about the Jordan,
6 Walikuwa wakibatizwa naye katika mto Yorodani huku wakitubu dhambi zao.
and were immersed by him in the Jordan, confessing their sins.
7 Lakini alipowaona wengi wa mafarisayo na masadukayo wakija kwake kubatizwa, akawaambia, ''Enyi uzao wa nyoka wenye sumu nani aliye waonya kuikimbia ghadhabu inayokuja?
But when he saw many of the Pharisees and Sadducees coming to his immersion, he said to them: Generation of vipers, who has warned you to flee from the coining wrath?
8 Zaeni matunda yaipasayo toba.
Bring forth, therefore, fruit worthy of repentance:
9 Na msifikiri na kusemezana miongoni mwenu, 'Tunaye Ibrahimu kama baba yetu.' Kwa kuwa nawaambieni Mungu anaweza kumwinulia Ibrahimu watoto hata kutoka katika mawe haya.
and think not to say within yourselves, We have Abraham for our father; for I say to you that God is able from these stones to raise up children to Abraham.
10 Tayari shoka limekwisha kuwekwa kwenye mzizi wa miti. Kwahiyo kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa kwenye moto.
Even now the ax is lying at the root of the trees: therefore, every tree that does not bring forth good fruit is cut down and thrown into the fire.
11 Ninawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba. Lakini yeye ajaye baada yangu ni mkuu kuliko mimi nami sistahili hata kubeba viatu vyake. Yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
I immerse you in water, in order to repentance; but he that comes after me is mightier than I, whose sandals I am not worthy to carry. He will immerse you in the Holy Spirit and in fire:
12 Na pepeto lake li mkononi mwake kusafisha kabisa uwanda wake na kuikusanya ngano yake ghalani. Lakini atayachoma makapi kwa moto ambao hauwezi kuzimika.
whose winnowing-shovel is in his hand, and he will thoroughly cleanse his thrashing-floor, and gather his grain into his granary; but the chaff he will burn with unquenchable fire.
13 Kisha Yesu akaja kutoka Galilaya mpaka mto Yorodani kubatizwa na Yohana.
Then came Jesus from Galilee to the Jordan to John, to be immersed by him.
14 Lakini Yohana alitaka kumzuia akisema, “Mimi nahitaji kubatizwa na wewe, nawe waja kwangu?''
But John forbade him, saying: I have need to be immersed by thee, and comest thou to me?
15 Yesu akajibu akasema, ''Ruhusu iwe hivi sasa, kwa kuwa ndivyo itupasavyo kuitimiza haki yote.'' Kisha Yohana akamruhusu.
But Jesus answering said to him: Permit it now; for thus it becomes us to perform fully every righteous act. Then he permitted him.
16 Baada ya kuwa amebatizwa, mara Yesu alitoka kwenye maji, na tazama, Mbingu zikafunguka kwake. Na alimuona Roho wa Mungu akishuka kwa mfano wa njiwa na kutulia juu yake.
And after Jesus was immersed, he came up immediately from the water; and lo, the heavens were opened to him, and he saw the Spirit of God descending like a dove, and coming upon him.
17 Tazama, sauti ilitoka mbinguni ikisema, “Huyu ni mwanangu mpendwa. Ninaye pendezwa sana naye.''
And lo, a voice from heaven, saying: This is my beloved Son, in whom I delight.

< Mathayo 3 >