< Mathayo 27 >

1 Muda wa asubuhi ulipofika, wakuu wote wa makuhani na wazee wa watu walikula njama dhidi ya Yesu wapate kumuua.
А кад би ујутру, учинише веће сви главари свештенички и старешине народне за Исуса да Га погубе.
2 Walimfunga, walimwongoza, na kumfikisha kwa Liwali Pilato.
И свезавши Га одведоше, и предаше Га Понтију Пилату, судији.
3 Kisha wakati Yuda, ambaye alikuwa amemsaliti, aliona kwamba Yesu amekwisha kuhukumiwa, alijuta na kurudisha vipande thelathini vya fedha kwa mkuu wa makuhani na wazee,
Тада видевши Јуда издајник Његов да Га осудише раскаја се, и врати тридесет сребрника главарима свештеничким и старешинама
4 na akasema, “Nimefanya dhambi kwa kuisaliti damu isiyo na hatia.” Lakini wakajibu, “Inatuhusu nini sisi? Yaangalie hayo mwenyewe.”
Говорећи: Ја сагреших што издадох крв праву. А они рекоше: Шта ми маримо за то? Ти ћеш видети.
5 Kisha alivirusha chini vile vipande vya fedha katika hekalu, na kuondoka zake na kujinyonga mwenyewe.
И бацивши сребрнике у цркви изиђе, и отиде те се обеси.
6 Mkuu wa makuhani alivichukua vile vipande vya fedha na kusema, “Si halali kuiweka fedha hii katika hazina, kwa sababu ni gharama ya damu.”
А главари свештенички узевши сребрнике рекоше: Не ваља их метнути у црквену хазну, јер је узето за крв.
7 Walijadiliana kwa pamoja na fedha ikatumika kununulia shamba la mfinyazi la kuzika wageni.
Него се договорише те купише за њих лончареву њиву за гробље гостима.
8 Kwa sababu hii shamba hilo limekuwa likiitwa, “Shamba la damu” hadi leo hii.
Од тога се и прозва она њива крвна њива и до данас.
9 Kisha lile neno lililokuwa limenenwa na nabii Yeremia lilitimia, kusema, “Walitwaa vipande thelathini vya fedha, gharama iliyopangwa na watu wa Israel kwa ajili yake,
Тада се изврши шта је казао пророк Јеремија говорећи: И узеше тридесет сребрника, цену цењенога кога су ценили синови Израиљеви;
10 na waliitumia kwa shamba la mfinyanzi, kama Bwana alivyokuwa amenielekeza.”
И дадоше их за њиву лончареву, као што ми каза Господ.
11 Sasa Yesu alisimama mbele ya liwali, na liwali akamwuliza, “Je! Wewe ni mfalme wa Wayahudi?” Yesu alimjibu, “Wewe wasema hivyo.”
А Исус стаде пред судијом, и запита Га судија говорећи: Ти ли си цар јудејски? А Исус рече му: Ти кажеш.
12 Lakini wakati aliposhitakiwa na wakuu wa makuhani na wazee, hakujibu chochote.
И кад Га тужаху главари свештенички и старешине, ништа не одговори.
13 Kisha Pilato alimwambia, “Hujayasikia mashitaka yote dhidi yako?”
Тада рече ми Пилат: Чујеш ли шта на тебе сведоче?
14 Lakini hakumjibu hata neno moja, hivyo liwali alijawa na mshangao.
И не одговори му ни једну реч тако да се судија дивљаше врло.
15 Sasa katika sikukuu ilikuwa desturi ya liwali kumfungua mfungwa mmoja anayechaguliwa na umati.
А о сваком празнику пасхе беше обичај у судије да пусти народу по једног сужња кога они хоће.
16 Wakati huo walikuwa na mfungwa sugu jina lake Baraba.
А тада имаху знатног сужња по имену Варава.
17 Hivyo wakati walipokuwa wamekusanyika pamoja, Pilato aliwauliza, “Ni nani mnataka tumfungue kwa ajili yenu?” Baraba au Yesu anayeitwa Kristo?”
И кад се сабраше, рече им Пилат: Кога хоћете да вам пустим? Вараву или Исуса прозваног Христа?
18 Kwa sababu alijua kwamba wamekwisha kumkamata kwa sababu ya chuki.
Јер знаше да су Га из зависти предали.
19 Wakati alipokuwa akiketi kwenye kiti chake cha hukumu, mke wake alimtumia neno na kusema, “Usitende jambo lolote kwa mtu huyo asiye na hatia. Kwani nimeteswa mno hata leo katika ndoto kwa sababu yake.”
А кад сеђаше у суду, поручи му жена његова говорећи: Немој се ти ништа мешати у суд тог праведника, јер сам данас у сну много пострадала њега ради.
20 Ndipo wakuu wa makuhani na wazee waliwashawishi makutano wamwombe Baraba, na Yesu auawe.
А главари свештенички и старешине наговорише народ да ишту Вараву, а Исуса да погубе.
21 Liwali aliwauliza, “Ni yupi kati ya wawili mnataka mimi nimwachie kwenu?” Walisema, “Baraba.”
А судија одговарајући рече им: Кога хоћете од ове двојице да вам пустим? А они рекоше: Вараву.
22 Pilato akawaambia, “Nimtendee nini Yesu anayeitwa Kristo?” Wote wakajibu, “Msulibishe”
Рече им Пилат: А шта ћу чинити с Исусом прозваним Христом? Рекоше му сви: Да се разапне.
23 Naye akasema, “Kwa nini, ni kosa gani ametenda?” Lakini walizidi kupaza sauti hata juu mno, “Msulibishe.”
Судија пак рече: А какво је зло учинио? А они гласно повикаше говорећи: Да се разапне.
24 Hivyo wakati Pilato alipoona hawezi kufanya lolote, lakini badala yake vurugu zilikuwa zimeanza, alitwaa maji akanawa mikono yake mbele ya umati, na kusema, “Mimi sina hatia juu ya damu ya mtu huyu asiye na hatia. Yaangalieni haya wenyewe.”
А кад виде Пилат да ништа не помаже него још већа буна бива, узе воду те уми руке пред народом говорећи: Ја нисам крив у крви овог праведника: ви ћете видети.
25 Watu wote wakasema, “Damu yake iwe juu yetu na watoto wetu.”
И одговарајући сав народ рече: Крв његова на нас и на децу нашу.
26 Kisha akamfungulia Baraba kwao, lakini alimpiga mijeredi Yesu na kumkabidhi kwao kwenda kusulibiwa.
Тада пусти им Вараву, а Исуса шибавши предаде да се разапне.
27 Kisha askari wa liwali wakamchukua Yesu mpaka Praitorio na kundi kubwa la maaskari wote wakamkusanyika.
Тада војници судијини узеше Исуса у судницу и скупише на Њ сву чету војника.
28 Wakamvua nguo zake na kumvika kanzu ya rangi nyekundu.
И свукавши Га обукоше Му скерлетну кабаницу.
29 Kisha wakatengeneza taji ya miiba na kuiweka juu ya kichwa chake, na walimwekea mwanzi katika mkono wake wa kuume. Walipiga magoti mbele yake na kumkejeri, wakisema, “Salamu, Mfalme wa Wayahudi?”
И оплетавши венац од трња метнуше Му на главу, и дадоше Му трску у десницу; и клекнувши на колена пред Њим ругаху Му се говорећи: Здраво, царе јудејски!
30 Na walimtemea mate, na walitwaa mwanzi na kumpiga kichwani.
И пљунувши на Њ узеше трску и бише Га по глави.
31 Wakati walipokuwa wakimkejeri, walimvua ile kanzu na kumvika nguo zake, na kumwongoza kwenda kumsulibisha.
И кад Му се наругаше, свукоше с Њега кабаницу, и обукоше Га у хаљине Његове, и поведоше Га да Га разапну.
32 Walipotoka nje, walimwona mtu kutoka Krene jina lake Simeoni, ambaye walimlazimisha kwenda nao ili apate kuubeba msalaba wake.
И излазећи нађоше човека из Кирине по имену Симона и натераше га да Му понесе крст.
33 Walipofika mahali paitwapo Galigotha, maana yake, “Eneo la fuvu la Kichwa.”
И дошавши на место које се зове Голгота, то јест костурница,
34 Walimpa siki iliyochanganywa na nyongo anywe. Lakini alipoionja, hakuweza kuinywa.
Дадоше Му да пије сирће помешано са жучи, и окусивши не хте да пије.
35 Wakati walipokuwa wamemsulibisha, waligawana mavazi yake kwa kupiga kura.
А кад Га разапеше, разделише хаљине Његове бацивши коцке;
36 Na waliketi na kumwangalia.
И сеђаху онде те Га чуваху.
37 Juu ya kichwa chake waliweka mashitaka dhidi yake yakisomeka, “Huyu ni Yesu, mfalme wa Wayahudi.”
И метнуше Му више главе кривицу Његову написану: Ово је Исус цар јудејски.
38 Wanyang'anyi wawili walisulibiwa pamoja naye, mmoja upande wa kulia wake na mwingine wa kushoto.
Тада распеше с Њиме два хајдука, једног с десне а једног с леве стране.
39 Wale waliokuwa wakipita walimdhihaki, wakitikisa vichwa vyao
А који пролажаху хуљаху на Њ машући главама својим.
40 na kusema, “Wewe uliyekuwa unataka kuliharibu hekalu na kulijenga katika siku tatu, jiokoe mwenyewe! Kama ni Mwana wa Mungu, shuka chini utoke msalabani!”
И говорећи: Ти који цркву разваљујеш и за три дана начињаш помози сам себи; ако си син Божји, сиђи с крста.
41 Katika hali ile ile wakuu wa makuhani walikuwa wakimkashifu, pamoja na waandishi na wazee, na kusema,
А тако и главари свештенички с књижевницима и старешинама подсмевајући се говораху:
42 “Aliokoa wengine, lakini hawezi kujiokoa mwenyewe. Yeye ni Mfalme wa Wayahudi. Na ashuke chini toka msalabani, ndipo tutakapomwamini.
Другима поможе, а себи не може помоћи. Ако је цар Израиљев, нека сиђе сад с крста па ћемо га веровати.
43 Alimtumaini Mungu. Acha Mungu amwokoe sasa kama anataka, kwa sababu alisema, 'Mimi ni Mwana wa Mungu.'”
Он се уздао у Бога: нека му помогне сад, ако му је по вољи, јер говораше: Ја сам син Божји.
44 Na wale wanyang'anyi waliokuwa wamesulibiwa pamoja naye pia walisema maneno ya kumdhihaki.
Тако исто и хајдуци разапети с Њим ругаху Му се.
45 Sasa kutoka saa sita kulikuwa na giza katika nchi yote hadi saa tisa.
А од шестог сата би тама по свој земљи до сата деветог.
46 Ilipofika saa tisa, Yesu akalia kwa sauti kuu, “Eloi, Eloi, lama thabakithan?” akimaanisha, “Mungu wangu, Mungu wangu, kwa nini umeniacha?”
А око деветог сата повика Исус гласно говорећи: Или! Или! Лама савахтани? То јест: Боже мој! Боже мој! Зашто си ме оставио?
47 Wakati huo baadhi yao waliokuwa wamesimama pale walisikia, wakasema, “Anamwita Eliya.”
А неки од оних што стајаху онде чувши то говораху: Овај зове Илију.
48 Mara moja mmoja wao alikimbia kuchukua sifongo na kuijaza kinywaji kichungu, akaiweka juu ya mti na kumpa apate kunywa.
И одмах отрча један од њих те узе сунђер, и напуни оцта, па натаче на трску, те Га појаше.
49 Nao waliosalia wakasema, “Mwacheni peke yake, acheni tuone kama Eliya atakuja kumwokoa.”
А остали говораху: Стани да видимо хоће ли доћи Илија да му помогне.
50 Kisha Yesu akalia tena kwa sauti kuu na akaitoa roho yake.
А Исус опет повика гласно и испусти душу.
51 Tazama, Pazia la hekalu lilipasuka sehemu mbili kutokea juu hadi chini. Na ardhi ikatetemeka na miamba ikapasuka vipande.
И гле, завеса црквена раздре се надвоје од горњег краја до доњег; и земља се потресе, и камење се распаде;
52 Makaburi yalifunguka, na miili ya watakatifu wengi waliokuwa wamelala usingizi walifufuliwa.
И гробови се отворише, и усташе многа тела светих који су помрли;
53 Walitoka kwenye makaburi baada ya ufufuo wake, waliingia mji mtakatifu, na wakaonekana na wengi.
И изашавши из гробова, по васкрсењу Његовом, уђоше у свети град и показаше се многима.
54 Basi yule akida na wale ambao walikuwa wakimtazama Yesu waliona tetemeko na mambo yaliyokuwa yakitokea, walijawa na woga sana na kusema, “Kweli huyu alikuwa Mwana wa Mungu.”
А капетан и који с њим чуваху Исуса видевши да се земља тресе и шта би, поплашише се врло говорећи: Заиста овај беше Син Божји.
55 Wanawake wengi waliokuwa wakimfuata Yesu kutoka Galilaya ili kumhudumia walikuwa pale wakitazama kutoka kwa mbali.
И онде беху и гледаху издалека многе жене које су ишле за Исусом из Галилеје и служиле Му.
56 Miongini mwao walikuwa Mariamu Magdarena, Mariamu mama yake Yakobo na Joseph, na mama wa watoto wa Zebedayo
Међу којима беше Марија Магдалина и Марија мати Јаковљева и Јосијина и мати синова Зеведејевих.
57 Ilipofika jioni, alikuja mtu tajiri kutoka Arimathayo, aliyeitwa Yusufu, ambaye pia alikuwa mwanafunzi wa Yesu.
А кад би увече, дође човек богат из Ариматеје, по имену Јосиф, који је такође био ученик Исусов.
58 Alimwendea Pilato na kuuomba mwili wa Yesu. Kisha Pilato aliagiza apate kupewa.
Овај приступивши к Пилату замоли га за тело Исусово. Тада Пилат заповеди да му даду тело.
59 Yusufu aliuchukua mwili akaufunga na nguo ya sufi safi,
И узевши Јосиф тело зави Га у платно чисто;
60 na akaulaza katika kaburi jipya lake alilokuwa amelichonga mwambani. Kisha akavingirisha jiwe kubwa likafunika mlango wa kaburi na akaenda zake.
И метну Га у нови свој гроб што је био исекао у камену; и наваливши велики камен на врата од гроба отиде.
61 Mariamu Magdalena na Mariamu mwingine walikuwa pale, wamekaa kuelekea kaburi.
А онде беше Марија Магдалина и друга Марија, и сеђаху према гробу.
62 Siku iliyofuata ambayo ilikuwa siku baada ya maandalio, wakuu wa makuhani na Mafarisayo walikusanyika pamoja kwa Pilato.
Сутрадан пак по петку сабраше се главари свештенички и фарисеји код Пилата,
63 Wakamwambia, “Bwana, tunakumbuka kuwa wakati yule mdanganyifu alipokuwa hai, alisema, 'Baada ya siku tatu atafufuka tena.'
И рекоше: Господару! Ми се опоменусмо да овај лажа каза још за живота: После три дана устаћу.
64 Kwahiyo, agiza kwamba kaburi lilindwe salama mpaka siku ya tatu. Vinginevyo, wanafunzi wake wanaweza kuja kumwiba na kusema kwa watu, 'Amefufuka kutoka wafu.' Na udanganyifu wa mwisho utakuwa mbaya kuliko ule wa kwanza.”
Зато заповеди да се утврди гроб до трећег дана да не дођу како ученици његови ноћу и да га не украду и не кажу народу: Уста из мртвих; и биће последња превара гора од прве.
65 Pilato akawaambia, “Chukueni walinzi. Nendeni mkafanye hali ya usalama kama muwezavyo.”
Рече им Пилат: Ево вам страже, па идите те утврдите како знате.
66 Hivyo walikwenda na kufanya kaburi kuwa salama, jiwe liligongwa mhuri na kuweka walinzi.
А они отишавши са стражом утврдише гроб, и запечатише камен.

< Mathayo 27 >