< Mathayo 27 >
1 Muda wa asubuhi ulipofika, wakuu wote wa makuhani na wazee wa watu walikula njama dhidi ya Yesu wapate kumuua.
!- Quand le matin fut venu, tous les principaux sacrificateurs et les anciens du peuple tinrent conseil contre Jésus, pour le faire mourir.
2 Walimfunga, walimwongoza, na kumfikisha kwa Liwali Pilato.
Et après l'avoir enchaîné, ils l'emmenèrent et le livrèrent à Pilate, le gouverneur.
3 Kisha wakati Yuda, ambaye alikuwa amemsaliti, aliona kwamba Yesu amekwisha kuhukumiwa, alijuta na kurudisha vipande thelathini vya fedha kwa mkuu wa makuhani na wazee,
Alors Judas, qui l'avait trahi, voyant que Jésus était condamné, fut pris de remords et rapporta les trente pièces d'argent aux principaux sacrificateurs et aux anciens,
4 na akasema, “Nimefanya dhambi kwa kuisaliti damu isiyo na hatia.” Lakini wakajibu, “Inatuhusu nini sisi? Yaangalie hayo mwenyewe.”
en disant: J'ai péché, en livrant le sang innocent. Mais ils répondirent: Que nous importe? Cela te regarde!
5 Kisha alivirusha chini vile vipande vya fedha katika hekalu, na kuondoka zake na kujinyonga mwenyewe.
Jetant alors les pièces d'argent dans le temple, il se retira, et il alla se pendre.
6 Mkuu wa makuhani alivichukua vile vipande vya fedha na kusema, “Si halali kuiweka fedha hii katika hazina, kwa sababu ni gharama ya damu.”
Mais les principaux sacrificateurs prirent les pièces d'argent, et ils dirent: Il n'est pas permis de les mettre dans le trésor sacré, puisque c'est le prix du sang.
7 Walijadiliana kwa pamoja na fedha ikatumika kununulia shamba la mfinyazi la kuzika wageni.
Après en avoir délibéré, ils achetèrent avec cet argent le Champ du Potier, pour la sépulture des étrangers.
8 Kwa sababu hii shamba hilo limekuwa likiitwa, “Shamba la damu” hadi leo hii.
C'est pourquoi ce champ-là est appelé, encore aujourd'hui, «le Champ du sang».
9 Kisha lile neno lililokuwa limenenwa na nabii Yeremia lilitimia, kusema, “Walitwaa vipande thelathini vya fedha, gharama iliyopangwa na watu wa Israel kwa ajili yake,
Alors fut accompli ce qui avait été dit par Jérémie, le prophète: «Ils ont reçu les trente pièces d'argent, le prix de celui qui a été évalué, oui, évalué par les enfants d'Israël;
10 na waliitumia kwa shamba la mfinyanzi, kama Bwana alivyokuwa amenielekeza.”
et il les ont données pour le champ du potier, comme le Seigneur me l'avait commandé.»
11 Sasa Yesu alisimama mbele ya liwali, na liwali akamwuliza, “Je! Wewe ni mfalme wa Wayahudi?” Yesu alimjibu, “Wewe wasema hivyo.”
Jésus comparut devant le gouverneur, et le gouverneur l'interrogea, en disant: C'est toi qui es le roi des Juifs? Jésus répondit: Tu le dis.
12 Lakini wakati aliposhitakiwa na wakuu wa makuhani na wazee, hakujibu chochote.
Et pendant que les principaux sacrificateurs et les anciens l'accusaient, il ne répondait rien.
13 Kisha Pilato alimwambia, “Hujayasikia mashitaka yote dhidi yako?”
Alors Pilate lui dit: N'entends-tu pas tous les témoignages qu'ils déposent contre toi?
14 Lakini hakumjibu hata neno moja, hivyo liwali alijawa na mshangao.
Mais il ne répondit rien sur aucun point, de sorte que le gouverneur était fort étonné.
15 Sasa katika sikukuu ilikuwa desturi ya liwali kumfungua mfungwa mmoja anayechaguliwa na umati.
A chaque fête de Pâque, le gouverneur avait coutume de relâcher un prisonnier, celui que le peuple désignait.
16 Wakati huo walikuwa na mfungwa sugu jina lake Baraba.
Or, il y avait, à ce moment-là, un prisonnier fameux, nommé Barabbas.
17 Hivyo wakati walipokuwa wamekusanyika pamoja, Pilato aliwauliza, “Ni nani mnataka tumfungue kwa ajili yenu?” Baraba au Yesu anayeitwa Kristo?”
Pilate dit donc au peuple rassemblé: Lequel voulez-vous que je vous relâche: Barabbas, ou Jésus, celui qu'on appelle Christ?
18 Kwa sababu alijua kwamba wamekwisha kumkamata kwa sababu ya chuki.
Car il savait bien que c'était par jalousie qu'ils avaient livré Jésus.
19 Wakati alipokuwa akiketi kwenye kiti chake cha hukumu, mke wake alimtumia neno na kusema, “Usitende jambo lolote kwa mtu huyo asiye na hatia. Kwani nimeteswa mno hata leo katika ndoto kwa sababu yake.”
Pendant qu'il siégeait à son tribunal, sa femme lui envoya dire: N'aie rien à faire avec ce Juste; car j'ai beaucoup souffert, aujourd'hui, en songe, à cause de lui.
20 Ndipo wakuu wa makuhani na wazee waliwashawishi makutano wamwombe Baraba, na Yesu auawe.
— Mais les principaux sacrificateurs et les anciens persuadèrent au peuple de demander Barabbas, et de faire périr Jésus.
21 Liwali aliwauliza, “Ni yupi kati ya wawili mnataka mimi nimwachie kwenu?” Walisema, “Baraba.”
Le gouverneur, prenant la parole, leur dit: Lequel des deux voulez-vous que je vous relâche? Ils répondirent: Barabbas!
22 Pilato akawaambia, “Nimtendee nini Yesu anayeitwa Kristo?” Wote wakajibu, “Msulibishe”
Pilate leur dit: Que ferai-je donc de Jésus, celui qu'on appelle Christ? Tous répondirent: Qu'il soit crucifié!
23 Naye akasema, “Kwa nini, ni kosa gani ametenda?” Lakini walizidi kupaza sauti hata juu mno, “Msulibishe.”
Le gouverneur dit: Mais quel mal a-t-il fait? Ils criaient encore plus fort: Qu'il soit crucifié!
24 Hivyo wakati Pilato alipoona hawezi kufanya lolote, lakini badala yake vurugu zilikuwa zimeanza, alitwaa maji akanawa mikono yake mbele ya umati, na kusema, “Mimi sina hatia juu ya damu ya mtu huyu asiye na hatia. Yaangalieni haya wenyewe.”
Pilate, voyant qu'il ne gagnait rien, mais que le tumulte augmentait, prit de l'eau et se lava les mains devant le peuple en disant: Je suis innocent du sang de cet homme; cela vous regarde.
25 Watu wote wakasema, “Damu yake iwe juu yetu na watoto wetu.”
Et tout le peuple répondit: Que son sang retombe sur nous et sur nos enfants!
26 Kisha akamfungulia Baraba kwao, lakini alimpiga mijeredi Yesu na kumkabidhi kwao kwenda kusulibiwa.
Alors il leur relâcha Barabbas. Quant à Jésus, après l'avoir fait battre de verges, il le leur livra pour qu'il fût crucifié.
27 Kisha askari wa liwali wakamchukua Yesu mpaka Praitorio na kundi kubwa la maaskari wote wakamkusanyika.
Les soldats du gouverneur emmenèrent Jésus dans le prétoire, et ils rassemblèrent autour de lui toute la cohorte.
28 Wakamvua nguo zake na kumvika kanzu ya rangi nyekundu.
Ils lui ôtèrent ses vêtements et le revêtirent d'un manteau d'écarlate.
29 Kisha wakatengeneza taji ya miiba na kuiweka juu ya kichwa chake, na walimwekea mwanzi katika mkono wake wa kuume. Walipiga magoti mbele yake na kumkejeri, wakisema, “Salamu, Mfalme wa Wayahudi?”
Puis, ils tressèrent une couronne d'épines, ils la lui mirent sur la tête, avec un roseau dans la main droite; et, fléchissant le genou devant lui, ils se moquaient de lui, en disant: Salut, roi des Juifs!
30 Na walimtemea mate, na walitwaa mwanzi na kumpiga kichwani.
Ils crachaient sur lui, et, prenant le roseau, ils lui en donnaient des coups sur la tête.
31 Wakati walipokuwa wakimkejeri, walimvua ile kanzu na kumvika nguo zake, na kumwongoza kwenda kumsulibisha.
Après s'être moqués de lui, ils lui ôtèrent le manteau et lui remirent ses vêtements; puis, ils l'emmenèrent pour le crucifier.
32 Walipotoka nje, walimwona mtu kutoka Krene jina lake Simeoni, ambaye walimlazimisha kwenda nao ili apate kuubeba msalaba wake.
Comme ils sortaient, ils trouvèrent un homme de Cyrène, nommé Simon, et ils le contraignirent à porter la croix de Jésus.
33 Walipofika mahali paitwapo Galigotha, maana yake, “Eneo la fuvu la Kichwa.”
Arrivés au lieu appelé Golgotha, — ce qui signifie «le lieu du Crâne, » —
34 Walimpa siki iliyochanganywa na nyongo anywe. Lakini alipoionja, hakuweza kuinywa.
ils lui donnèrent à boire du vin mêlé de fiel; mais, quand il en eut goûté, il n'en voulut point boire.
35 Wakati walipokuwa wamemsulibisha, waligawana mavazi yake kwa kupiga kura.
Après l'avoir crucifié, ils se partagèrent ses vêtements en les tirant au sort.
36 Na waliketi na kumwangalia.
Et, s'étant assis, ils restaient là à le garder.
37 Juu ya kichwa chake waliweka mashitaka dhidi yake yakisomeka, “Huyu ni Yesu, mfalme wa Wayahudi.”
Au-dessus de sa tête, ils avaient placé un écriteau portant le motif de sa condamnation: Voici Jésus, le Roi des Juifs.
38 Wanyang'anyi wawili walisulibiwa pamoja naye, mmoja upande wa kulia wake na mwingine wa kushoto.
En même temps, on crucifia avec lui deux brigands, l'un à sa droite et l'autre à sa gauche.
39 Wale waliokuwa wakipita walimdhihaki, wakitikisa vichwa vyao
Ceux qui passaient par là l'outrageaient, hochant la tête
40 na kusema, “Wewe uliyekuwa unataka kuliharibu hekalu na kulijenga katika siku tatu, jiokoe mwenyewe! Kama ni Mwana wa Mungu, shuka chini utoke msalabani!”
et disant: Toi qui détruis le temple et qui le rebâtis en trois jours, sauve-toi toi-même, si tu es le Fils de Dieu, et descends de la croix!
41 Katika hali ile ile wakuu wa makuhani walikuwa wakimkashifu, pamoja na waandishi na wazee, na kusema,
De même aussi, les principaux sacrificateurs, avec les scribes et les anciens, disaient en se moquant:
42 “Aliokoa wengine, lakini hawezi kujiokoa mwenyewe. Yeye ni Mfalme wa Wayahudi. Na ashuke chini toka msalabani, ndipo tutakapomwamini.
Il en a sauvé d'autres; il ne peut se sauver lui-même! S'il est le roi d'Israël, qu'il descende maintenant de la croix, et nous croirons en lui.
43 Alimtumaini Mungu. Acha Mungu amwokoe sasa kama anataka, kwa sababu alisema, 'Mimi ni Mwana wa Mungu.'”
Il se confie en Dieu; que Dieu le délivre maintenant, s'il l'aime; car il a dit: Je suis le Fils de Dieu.
44 Na wale wanyang'anyi waliokuwa wamesulibiwa pamoja naye pia walisema maneno ya kumdhihaki.
Et les brigands, crucifiés avec lui, lui adressaient les mêmes outrages.
45 Sasa kutoka saa sita kulikuwa na giza katika nchi yote hadi saa tisa.
Depuis la sixième heure jusqu'à la neuvième, il y eut des ténèbres sur tout le pays.
46 Ilipofika saa tisa, Yesu akalia kwa sauti kuu, “Eloi, Eloi, lama thabakithan?” akimaanisha, “Mungu wangu, Mungu wangu, kwa nini umeniacha?”
Vers la neuvième heure, Jésus cria d'une voix forte: Éli, Éli, lamma sabachtani. c'est-à-dire: «Mon Dieu, mon Dieu, pourquoi m'as-tu abandonné?»
47 Wakati huo baadhi yao waliokuwa wamesimama pale walisikia, wakasema, “Anamwita Eliya.”
Quelques-uns de ceux qui étaient présents, l'ayant entendu, disaient: Il appelle Élie.
48 Mara moja mmoja wao alikimbia kuchukua sifongo na kuijaza kinywaji kichungu, akaiweka juu ya mti na kumpa apate kunywa.
Aussitôt l'un d'eux courut prendre une éponge, et, l'ayant remplie de vinaigre, il la mit au bout d'un roseau et lui donna à boire.
49 Nao waliosalia wakasema, “Mwacheni peke yake, acheni tuone kama Eliya atakuja kumwokoa.”
Mais les autres disaient: Laisse! Voyons si Élie viendra le délivrer.
50 Kisha Yesu akalia tena kwa sauti kuu na akaitoa roho yake.
Et Jésus, ayant de nouveau jeté un grand cri, rendit l'esprit.
51 Tazama, Pazia la hekalu lilipasuka sehemu mbili kutokea juu hadi chini. Na ardhi ikatetemeka na miamba ikapasuka vipande.
Alors, voici que le voile du temple se déchira en deux, depuis le haut jusqu'en bas. La terre trembla, les rochers se fendirent,
52 Makaburi yalifunguka, na miili ya watakatifu wengi waliokuwa wamelala usingizi walifufuliwa.
les tombeaux s'ouvrirent, et les corps de plusieurs saints qui étaient morts ressuscitèrent:
53 Walitoka kwenye makaburi baada ya ufufuo wake, waliingia mji mtakatifu, na wakaonekana na wengi.
étant sortis de leurs tombeaux, ils entrèrent dans la ville sainte après sa résurrection, et ils apparurent à plusieurs personnes.
54 Basi yule akida na wale ambao walikuwa wakimtazama Yesu waliona tetemeko na mambo yaliyokuwa yakitokea, walijawa na woga sana na kusema, “Kweli huyu alikuwa Mwana wa Mungu.”
Le centenier et ceux qui, avec lui, gardaient Jésus, ayant vu le tremblement de terre et tout ce qui était arrivé, furent fort effrayés, et ils dirent: Véritablement, celui-ci était le Fils de Dieu!
55 Wanawake wengi waliokuwa wakimfuata Yesu kutoka Galilaya ili kumhudumia walikuwa pale wakitazama kutoka kwa mbali.
Or, il y avait là plusieurs femmes qui regardaient de loin: c'étaient celles qui avaient suivi Jésus depuis la Galilée, pour le servir.
56 Miongini mwao walikuwa Mariamu Magdarena, Mariamu mama yake Yakobo na Joseph, na mama wa watoto wa Zebedayo
De ce nombre étaient Marie-Madeleine et Marie, mère de Jacques et de Joses, et la mère des fils de Zébédée.
57 Ilipofika jioni, alikuja mtu tajiri kutoka Arimathayo, aliyeitwa Yusufu, ambaye pia alikuwa mwanafunzi wa Yesu.
Le soir étant venu, un homme riche, d'Arimathée, nommé Joseph, qui lui-même était disciple de Jésus,
58 Alimwendea Pilato na kuuomba mwili wa Yesu. Kisha Pilato aliagiza apate kupewa.
alla trouver Pilate et lui demanda le corps de Jésus; alors Pilate ordonna qu'on le lui remît.
59 Yusufu aliuchukua mwili akaufunga na nguo ya sufi safi,
Joseph prit le corps, l'enveloppa dans un linceul blanc,
60 na akaulaza katika kaburi jipya lake alilokuwa amelichonga mwambani. Kisha akavingirisha jiwe kubwa likafunika mlango wa kaburi na akaenda zake.
et il le déposa dans un sépulcre neuf qu'il avait fait tailler dans le roc pour lui-même; puis, il roula une grande pierre à l'entrée du sépulcre et il s'en alla.
61 Mariamu Magdalena na Mariamu mwingine walikuwa pale, wamekaa kuelekea kaburi.
Or, Marie-Madeleine et l'autre Marie étaient là, assises en face du tombeau.
62 Siku iliyofuata ambayo ilikuwa siku baada ya maandalio, wakuu wa makuhani na Mafarisayo walikusanyika pamoja kwa Pilato.
Le lendemain, — qui était le jour après la préparation —, les principaux sacrificateurs et les pharisiens se rendirent ensemble chez Pilate,
63 Wakamwambia, “Bwana, tunakumbuka kuwa wakati yule mdanganyifu alipokuwa hai, alisema, 'Baada ya siku tatu atafufuka tena.'
et ils lui dirent: Seigneur, nous nous sommes souvenus que cet imposteur, quand il vivait encore, disait: Après trois jours, je ressusciterai.
64 Kwahiyo, agiza kwamba kaburi lilindwe salama mpaka siku ya tatu. Vinginevyo, wanafunzi wake wanaweza kuja kumwiba na kusema kwa watu, 'Amefufuka kutoka wafu.' Na udanganyifu wa mwisho utakuwa mbaya kuliko ule wa kwanza.”
Ordonne donc que le tombeau soit gardé sûrement jusqu'au troisième jour, de peur que ses disciples ne viennent l'enlever et qu'ils ne disent au peuple: Il est ressuscité des morts. Cette dernière imposture serait pire que la première.
65 Pilato akawaambia, “Chukueni walinzi. Nendeni mkafanye hali ya usalama kama muwezavyo.”
Pilate leur dit: Vous avez une garde; allez, et gardez-le comme vous l'entendrez.
66 Hivyo walikwenda na kufanya kaburi kuwa salama, jiwe liligongwa mhuri na kuweka walinzi.
Ils s'en allèrent donc, et ils s'assurèrent du tombeau, en scellant la pierre et en y plaçant la garde.