< Mathayo 27 >
1 Muda wa asubuhi ulipofika, wakuu wote wa makuhani na wazee wa watu walikula njama dhidi ya Yesu wapate kumuua.
And when the morning came, all the chief priests and the elders of the people took counsel against Jesus, how they might put him to death.
2 Walimfunga, walimwongoza, na kumfikisha kwa Liwali Pilato.
After they had bound him, they led him away, and handed him over to Pilate, the Roman Governor.
3 Kisha wakati Yuda, ambaye alikuwa amemsaliti, aliona kwamba Yesu amekwisha kuhukumiwa, alijuta na kurudisha vipande thelathini vya fedha kwa mkuu wa makuhani na wazee,
Then when Judas, his betrayer, saw that he was condemned, he repented and brought back the thirty pieces of silver to the chief priests and elders.
4 na akasema, “Nimefanya dhambi kwa kuisaliti damu isiyo na hatia.” Lakini wakajibu, “Inatuhusu nini sisi? Yaangalie hayo mwenyewe.”
"I have sinned," he said, "in betraying innocent blood!" "What is that to us?" they answered; "you must see to that."
5 Kisha alivirusha chini vile vipande vya fedha katika hekalu, na kuondoka zake na kujinyonga mwenyewe.
And flinging down the silver into the Sanctuary, he rushed out, and went and hanged himself.
6 Mkuu wa makuhani alivichukua vile vipande vya fedha na kusema, “Si halali kuiweka fedha hii katika hazina, kwa sababu ni gharama ya damu.”
The chief priests took the money, and said, "It would be wrong to put it into the temple-treasury, because it is the price of blood."
7 Walijadiliana kwa pamoja na fedha ikatumika kununulia shamba la mfinyazi la kuzika wageni.
So after the consultation they bought the Potter’s Field with it, for a burial-place for strangers.
8 Kwa sababu hii shamba hilo limekuwa likiitwa, “Shamba la damu” hadi leo hii.
That is the reason why, to this day, the field is called "The Field of Blood."
9 Kisha lile neno lililokuwa limenenwa na nabii Yeremia lilitimia, kusema, “Walitwaa vipande thelathini vya fedha, gharama iliyopangwa na watu wa Israel kwa ajili yake,
Then was fulfilled the word spoken by the prophet Jeremiah. And I took the thirty pieces of silver, the price of him who had been priced, whom certain of the Children of Israel had priced;
10 na waliitumia kwa shamba la mfinyanzi, kama Bwana alivyokuwa amenielekeza.”
and gave them for the Potter’s Field, as the Lord had appointed me.
11 Sasa Yesu alisimama mbele ya liwali, na liwali akamwuliza, “Je! Wewe ni mfalme wa Wayahudi?” Yesu alimjibu, “Wewe wasema hivyo.”
Now Jesus stood before the Governor, and the Governor questioned him. "Are you the King of the Jews?" he asked.
12 Lakini wakati aliposhitakiwa na wakuu wa makuhani na wazee, hakujibu chochote.
"it is as you say," answered Jesus; but while he was being accused by the chief priests and elders, he answered nothing.
13 Kisha Pilato alimwambia, “Hujayasikia mashitaka yote dhidi yako?”
Then Pilate said to him, "Do you not hear what they are testifying against you?"
14 Lakini hakumjibu hata neno moja, hivyo liwali alijawa na mshangao.
But he made no answer, not even to one charge; insomuch that the Governor was greatly astonished.
15 Sasa katika sikukuu ilikuwa desturi ya liwali kumfungua mfungwa mmoja anayechaguliwa na umati.
Now it was the Governor’s custom, during the Passover, to release to the people any one prisoner whom they selected.
16 Wakati huo walikuwa na mfungwa sugu jina lake Baraba.
At that time they had a notorious prisoner named Barabbas.
17 Hivyo wakati walipokuwa wamekusanyika pamoja, Pilato aliwauliza, “Ni nani mnataka tumfungue kwa ajili yenu?” Baraba au Yesu anayeitwa Kristo?”
So when they had assembled, Pilate said to them, "Whom do you want me to release to you, Barabbas, or Jesus who is called Christ?"
18 Kwa sababu alijua kwamba wamekwisha kumkamata kwa sababu ya chuki.
He knew well that it was because of enmity that they had brought Jesus before him.
19 Wakati alipokuwa akiketi kwenye kiti chake cha hukumu, mke wake alimtumia neno na kusema, “Usitende jambo lolote kwa mtu huyo asiye na hatia. Kwani nimeteswa mno hata leo katika ndoto kwa sababu yake.”
And while he was seated upon the judgment-seat, his wife had sent to him, saying, "Have nothing to do with that innocent man, for I have suffered many things today, in a dream, because of him."
20 Ndipo wakuu wa makuhani na wazee waliwashawishi makutano wamwombe Baraba, na Yesu auawe.
But the chief priests and the elders urged the crowds to ask for Barabbas, and to destroy Jesus.
21 Liwali aliwauliza, “Ni yupi kati ya wawili mnataka mimi nimwachie kwenu?” Walisema, “Baraba.”
So when Pilate said to them, "Which of the two do you want me to release unto you?" they said, "Barabbas."
22 Pilato akawaambia, “Nimtendee nini Yesu anayeitwa Kristo?” Wote wakajibu, “Msulibishe”
And Pilate asked, "What then shall I do with Jesus, who is called Christ?" What one voice they shouted, "Let him be crucified!"
23 Naye akasema, “Kwa nini, ni kosa gani ametenda?” Lakini walizidi kupaza sauti hata juu mno, “Msulibishe.”
But Pilate said, "Why, what evil has he done?" But they kept shouting the more fiercely, "Let him be crucified!"
24 Hivyo wakati Pilato alipoona hawezi kufanya lolote, lakini badala yake vurugu zilikuwa zimeanza, alitwaa maji akanawa mikono yake mbele ya umati, na kusema, “Mimi sina hatia juu ya damu ya mtu huyu asiye na hatia. Yaangalieni haya wenyewe.”
So when Pilate saw that he was accomplishing nothing, but that on the contrary a riot was threatening, he took water and washed his hands in the presence of the crowd, saying. "I am innocent of the blood of this man; you must answer for it."
25 Watu wote wakasema, “Damu yake iwe juu yetu na watoto wetu.”
All the people answered, "His blood be upon us and upon our children."
26 Kisha akamfungulia Baraba kwao, lakini alimpiga mijeredi Yesu na kumkabidhi kwao kwenda kusulibiwa.
Then he released Barabbas to them, but Jesus he scourged, and delivered to be crucified.
27 Kisha askari wa liwali wakamchukua Yesu mpaka Praitorio na kundi kubwa la maaskari wote wakamkusanyika.
Then the soldiers of the Governor took Jesus into the Praetorium, and gathered all the battalion together.
28 Wakamvua nguo zake na kumvika kanzu ya rangi nyekundu.
They stripped him and put on him a scarlet robe.
29 Kisha wakatengeneza taji ya miiba na kuiweka juu ya kichwa chake, na walimwekea mwanzi katika mkono wake wa kuume. Walipiga magoti mbele yake na kumkejeri, wakisema, “Salamu, Mfalme wa Wayahudi?”
And they twisted a thorny crown for him, and put it on his head, and placed a reed in his right hand. Then they knelt before him, in mockery, crying, "Hail, King of the Jews!"
30 Na walimtemea mate, na walitwaa mwanzi na kumpiga kichwani.
And they spit upon him, and took the reed and struck him on the head, again and again.
31 Wakati walipokuwa wakimkejeri, walimvua ile kanzu na kumvika nguo zake, na kumwongoza kwenda kumsulibisha.
At last, when they had finished their mocking, they took the robe off, and put his own garments on him, and led him away to crucify him.
32 Walipotoka nje, walimwona mtu kutoka Krene jina lake Simeoni, ambaye walimlazimisha kwenda nao ili apate kuubeba msalaba wake.
And as they went out they found a man of Cyrene, Simon by name, whom they compelled to go with them to carry his cross.
33 Walipofika mahali paitwapo Galigotha, maana yake, “Eneo la fuvu la Kichwa.”
And when they came to a place called Golgotha (the word means "Place of a Skull"),
34 Walimpa siki iliyochanganywa na nyongo anywe. Lakini alipoionja, hakuweza kuinywa.
they gave Jesus wine to drink, mingled with gall. But after tasting it he refused to drink it.
35 Wakati walipokuwa wamemsulibisha, waligawana mavazi yake kwa kupiga kura.
After crucifying him, they parted his garments among them by casting lots.
36 Na waliketi na kumwangalia.
Then they sat and watched him there.
37 Juu ya kichwa chake waliweka mashitaka dhidi yake yakisomeka, “Huyu ni Yesu, mfalme wa Wayahudi.”
They also placed above his head his accusation written, This is Jesus The King of the Jews
38 Wanyang'anyi wawili walisulibiwa pamoja naye, mmoja upande wa kulia wake na mwingine wa kushoto.
At that time two robbers, also, were crucified with him; one on his right hand, the other on his left.
39 Wale waliokuwa wakipita walimdhihaki, wakitikisa vichwa vyao
Those who passed by reviled him, wagging their heads saying.
40 na kusema, “Wewe uliyekuwa unataka kuliharibu hekalu na kulijenga katika siku tatu, jiokoe mwenyewe! Kama ni Mwana wa Mungu, shuka chini utoke msalabani!”
"You who were going to destroy the Temple and build it in three days, save yourself! If you are the Son of God, come down from the cross!"
41 Katika hali ile ile wakuu wa makuhani walikuwa wakimkashifu, pamoja na waandishi na wazee, na kusema,
In like manner the chief priests, too, with the Scribes and elders, kept taunting him.
42 “Aliokoa wengine, lakini hawezi kujiokoa mwenyewe. Yeye ni Mfalme wa Wayahudi. Na ashuke chini toka msalabani, ndipo tutakapomwamini.
"He saved other," they said, "himself he cannot save. He, the King of Israel! Let him now come down from the cross, and we will believe on him!
43 Alimtumaini Mungu. Acha Mungu amwokoe sasa kama anataka, kwa sababu alisema, 'Mimi ni Mwana wa Mungu.'”
He put his trust in God. let Him deliver him now, if He cares for him. For he said, ‘I am the Son of God!’"
44 Na wale wanyang'anyi waliokuwa wamesulibiwa pamoja naye pia walisema maneno ya kumdhihaki.
In the same way the robbers also who were being crucified with him, dept reviling him.
45 Sasa kutoka saa sita kulikuwa na giza katika nchi yote hadi saa tisa.
Now from noon darkness fell upon the whole land, until three o’clock in the afternoon.
46 Ilipofika saa tisa, Yesu akalia kwa sauti kuu, “Eloi, Eloi, lama thabakithan?” akimaanisha, “Mungu wangu, Mungu wangu, kwa nini umeniacha?”
But at three o’clock Jesus cried out in loud voice, "Eli, Eli, Lama Sabachthani?" (That is to say, "My God, my God, why hast thou forsaken me?")
47 Wakati huo baadhi yao waliokuwa wamesimama pale walisikia, wakasema, “Anamwita Eliya.”
When they heard this, some of the bystanders said "He is calling for Elijah!"
48 Mara moja mmoja wao alikimbia kuchukua sifongo na kuijaza kinywaji kichungu, akaiweka juu ya mti na kumpa apate kunywa.
At once, one of them ran, and took a sponge, and filling it with vinegar, put it on a reed, and gave him to drink.
49 Nao waliosalia wakasema, “Mwacheni peke yake, acheni tuone kama Eliya atakuja kumwokoa.”
But the rest said. "Let be! Let us see whether Elijah is coming to save him!"
50 Kisha Yesu akalia tena kwa sauti kuu na akaitoa roho yake.
And Jesus cried again with a loud voice, and yielded up his spirit.
51 Tazama, Pazia la hekalu lilipasuka sehemu mbili kutokea juu hadi chini. Na ardhi ikatetemeka na miamba ikapasuka vipande.
And lo, the veil of the sanctuary was torn in two, from the top to the bottom;
52 Makaburi yalifunguka, na miili ya watakatifu wengi waliokuwa wamelala usingizi walifufuliwa.
the earth quaked; the rocks split; the tombs were opened, and many bodies of the saints who had fallen asleep were raised.
53 Walitoka kwenye makaburi baada ya ufufuo wake, waliingia mji mtakatifu, na wakaonekana na wengi.
And coming forth out of the tombs, after his resurrection, they went into the holy city and appeared to many.
54 Basi yule akida na wale ambao walikuwa wakimtazama Yesu waliona tetemeko na mambo yaliyokuwa yakitokea, walijawa na woga sana na kusema, “Kweli huyu alikuwa Mwana wa Mungu.”
When the Roman captain and the soldiers who were with him, guarding Jesus, saw the earthquake and all that happened, they were greatly terrified and said, "Certainly this man must have been God’s Son."
55 Wanawake wengi waliokuwa wakimfuata Yesu kutoka Galilaya ili kumhudumia walikuwa pale wakitazama kutoka kwa mbali.
And there were present several women who were looking on from a distance; they had followed Jesus from a Galilee, ministering to him.
56 Miongini mwao walikuwa Mariamu Magdarena, Mariamu mama yake Yakobo na Joseph, na mama wa watoto wa Zebedayo
among them being Mary Magdalene, Mary the mother of Jamesand Joses, and the mother of Zebedee’s sons.
57 Ilipofika jioni, alikuja mtu tajiri kutoka Arimathayo, aliyeitwa Yusufu, ambaye pia alikuwa mwanafunzi wa Yesu.
When it was eventide, there came a rich man of Arimathea, named Josephus, who was himself a disciple of Jesus.
58 Alimwendea Pilato na kuuomba mwili wa Yesu. Kisha Pilato aliagiza apate kupewa.
This man went to Pilate and asked for the body of Jesus.
59 Yusufu aliuchukua mwili akaufunga na nguo ya sufi safi,
Pilate then commanded that it be given over to him.
60 na akaulaza katika kaburi jipya lake alilokuwa amelichonga mwambani. Kisha akavingirisha jiwe kubwa likafunika mlango wa kaburi na akaenda zake.
So Joseph took the body, and wrapped it in a clean linen cloth, and laid it in his own new tomb, which he had cut in the rock; and after rolling a great stone against the opening of the tomb, he went away.
61 Mariamu Magdalena na Mariamu mwingine walikuwa pale, wamekaa kuelekea kaburi.
And Mary Magdalene was there, and the other Mary, sitting opposite the tomb.
62 Siku iliyofuata ambayo ilikuwa siku baada ya maandalio, wakuu wa makuhani na Mafarisayo walikusanyika pamoja kwa Pilato.
The day after - that is, the day following the Preparation - the chief priests and Pharisees went in a body to Pilate and said.
63 Wakamwambia, “Bwana, tunakumbuka kuwa wakati yule mdanganyifu alipokuwa hai, alisema, 'Baada ya siku tatu atafufuka tena.'
"We recollect, Sir, that when he was living this imposter said, ‘I will rise again after three days.’
64 Kwahiyo, agiza kwamba kaburi lilindwe salama mpaka siku ya tatu. Vinginevyo, wanafunzi wake wanaweza kuja kumwiba na kusema kwa watu, 'Amefufuka kutoka wafu.' Na udanganyifu wa mwisho utakuwa mbaya kuliko ule wa kwanza.”
Now therefore give order to have the sepulcher securely guarded until the third day, for fear his disciples may come and steal him away, and then tell the people, ‘He is risen from the dead’; and so the last error will be worse than the first."
65 Pilato akawaambia, “Chukueni walinzi. Nendeni mkafanye hali ya usalama kama muwezavyo.”
"You can have a guard," said Pilate. "Go your way, make it as secure as you can."
66 Hivyo walikwenda na kufanya kaburi kuwa salama, jiwe liligongwa mhuri na kuweka walinzi.
So they went and made the sepulcher secure, by sealing the stone in the presence of the guard.