< Mathayo 27 >

1 Muda wa asubuhi ulipofika, wakuu wote wa makuhani na wazee wa watu walikula njama dhidi ya Yesu wapate kumuua.
When morning came, all the chief priests and elders of the people conspired against Jesus to put Him to death.
2 Walimfunga, walimwongoza, na kumfikisha kwa Liwali Pilato.
They bound Him, led Him away, and handed Him over to Pilate the governor.
3 Kisha wakati Yuda, ambaye alikuwa amemsaliti, aliona kwamba Yesu amekwisha kuhukumiwa, alijuta na kurudisha vipande thelathini vya fedha kwa mkuu wa makuhani na wazee,
When Judas, who had betrayed Him, saw that Jesus was condemned, he was filled with remorse and returned the thirty pieces of silver to the chief priests and elders.
4 na akasema, “Nimefanya dhambi kwa kuisaliti damu isiyo na hatia.” Lakini wakajibu, “Inatuhusu nini sisi? Yaangalie hayo mwenyewe.”
“I have sinned by betraying innocent blood,” he said. “What is that to us?” they replied. “You bear the responsibility.”
5 Kisha alivirusha chini vile vipande vya fedha katika hekalu, na kuondoka zake na kujinyonga mwenyewe.
So Judas threw the silver into the temple and left. Then he went away and hanged himself.
6 Mkuu wa makuhani alivichukua vile vipande vya fedha na kusema, “Si halali kuiweka fedha hii katika hazina, kwa sababu ni gharama ya damu.”
The chief priests picked up the pieces of silver and said, “It is unlawful to put this into the treasury, since it is blood money.”
7 Walijadiliana kwa pamoja na fedha ikatumika kununulia shamba la mfinyazi la kuzika wageni.
After conferring together, they used the money to buy the potter’s field as a burial place for foreigners.
8 Kwa sababu hii shamba hilo limekuwa likiitwa, “Shamba la damu” hadi leo hii.
That is why it has been called the Field of Blood to this day.
9 Kisha lile neno lililokuwa limenenwa na nabii Yeremia lilitimia, kusema, “Walitwaa vipande thelathini vya fedha, gharama iliyopangwa na watu wa Israel kwa ajili yake,
Then what was spoken through Jeremiah the prophet was fulfilled: “They took the thirty pieces of silver, the price set on Him by the people of Israel,
10 na waliitumia kwa shamba la mfinyanzi, kama Bwana alivyokuwa amenielekeza.”
and they gave them for the potter’s field, as the Lord had commanded me.”
11 Sasa Yesu alisimama mbele ya liwali, na liwali akamwuliza, “Je! Wewe ni mfalme wa Wayahudi?” Yesu alimjibu, “Wewe wasema hivyo.”
Meanwhile Jesus stood before the governor, who questioned Him: “Are You the King of the Jews?” “You have said so,” Jesus replied.
12 Lakini wakati aliposhitakiwa na wakuu wa makuhani na wazee, hakujibu chochote.
And when He was accused by the chief priests and elders, He gave no answer.
13 Kisha Pilato alimwambia, “Hujayasikia mashitaka yote dhidi yako?”
Then Pilate asked Him, “Do You not hear how many charges they are bringing against You?”
14 Lakini hakumjibu hata neno moja, hivyo liwali alijawa na mshangao.
But Jesus gave no answer, not even to a single charge, much to the governor’s amazement.
15 Sasa katika sikukuu ilikuwa desturi ya liwali kumfungua mfungwa mmoja anayechaguliwa na umati.
Now it was the governor’s custom at the feast to release to the crowd a prisoner of their choosing.
16 Wakati huo walikuwa na mfungwa sugu jina lake Baraba.
At that time they were holding a notorious prisoner named Barabbas.
17 Hivyo wakati walipokuwa wamekusanyika pamoja, Pilato aliwauliza, “Ni nani mnataka tumfungue kwa ajili yenu?” Baraba au Yesu anayeitwa Kristo?”
So when the crowd had assembled, Pilate asked them, “Which one do you want me to release to you: Barabbas, or Jesus who is called Christ?”
18 Kwa sababu alijua kwamba wamekwisha kumkamata kwa sababu ya chuki.
For he knew it was out of envy that they had handed Jesus over to him.
19 Wakati alipokuwa akiketi kwenye kiti chake cha hukumu, mke wake alimtumia neno na kusema, “Usitende jambo lolote kwa mtu huyo asiye na hatia. Kwani nimeteswa mno hata leo katika ndoto kwa sababu yake.”
While Pilate was sitting on the judgment seat, his wife sent him this message: “Have nothing to do with that innocent man, for I have suffered terribly in a dream today because of Him.”
20 Ndipo wakuu wa makuhani na wazee waliwashawishi makutano wamwombe Baraba, na Yesu auawe.
But the chief priests and elders persuaded the crowds to ask for Barabbas and to have Jesus put to death.
21 Liwali aliwauliza, “Ni yupi kati ya wawili mnataka mimi nimwachie kwenu?” Walisema, “Baraba.”
“Which of the two do you want me to release to you?” asked the governor. “Barabbas,” they replied.
22 Pilato akawaambia, “Nimtendee nini Yesu anayeitwa Kristo?” Wote wakajibu, “Msulibishe”
“What then should I do with Jesus who is called Christ?” Pilate asked. They all answered, “Crucify Him!”
23 Naye akasema, “Kwa nini, ni kosa gani ametenda?” Lakini walizidi kupaza sauti hata juu mno, “Msulibishe.”
“Why?” asked Pilate. “What evil has He done?” But they shouted all the louder, “Crucify Him!”
24 Hivyo wakati Pilato alipoona hawezi kufanya lolote, lakini badala yake vurugu zilikuwa zimeanza, alitwaa maji akanawa mikono yake mbele ya umati, na kusema, “Mimi sina hatia juu ya damu ya mtu huyu asiye na hatia. Yaangalieni haya wenyewe.”
When Pilate saw that he was accomplishing nothing, but that instead a riot was breaking out, he took water and washed his hands before the crowd. “I am innocent of this man’s blood,” he said. “You bear the responsibility.”
25 Watu wote wakasema, “Damu yake iwe juu yetu na watoto wetu.”
All the people answered, “His blood be on us and on our children!”
26 Kisha akamfungulia Baraba kwao, lakini alimpiga mijeredi Yesu na kumkabidhi kwao kwenda kusulibiwa.
So Pilate released Barabbas to them. But he had Jesus flogged, and handed Him over to be crucified.
27 Kisha askari wa liwali wakamchukua Yesu mpaka Praitorio na kundi kubwa la maaskari wote wakamkusanyika.
Then the governor’s soldiers took Jesus into the Praetorium and gathered the whole company around Him.
28 Wakamvua nguo zake na kumvika kanzu ya rangi nyekundu.
They stripped Him and put a scarlet robe on Him.
29 Kisha wakatengeneza taji ya miiba na kuiweka juu ya kichwa chake, na walimwekea mwanzi katika mkono wake wa kuume. Walipiga magoti mbele yake na kumkejeri, wakisema, “Salamu, Mfalme wa Wayahudi?”
And they twisted together a crown of thorns and set it on His head. They put a staff in His right hand and knelt down before Him to mock Him, saying, “Hail, King of the Jews!”
30 Na walimtemea mate, na walitwaa mwanzi na kumpiga kichwani.
Then they spit on Him and took the staff and struck Him on the head repeatedly.
31 Wakati walipokuwa wakimkejeri, walimvua ile kanzu na kumvika nguo zake, na kumwongoza kwenda kumsulibisha.
After they had mocked Him, they removed the robe and put His own clothes back on Him. Then they led Him away to crucify Him.
32 Walipotoka nje, walimwona mtu kutoka Krene jina lake Simeoni, ambaye walimlazimisha kwenda nao ili apate kuubeba msalaba wake.
Along the way they found a man from Cyrene, named Simon, and they forced him to carry the cross of Jesus.
33 Walipofika mahali paitwapo Galigotha, maana yake, “Eneo la fuvu la Kichwa.”
And when they came to a place called Golgotha, which means The Place of the Skull,
34 Walimpa siki iliyochanganywa na nyongo anywe. Lakini alipoionja, hakuweza kuinywa.
they offered Him wine to drink, mixed with gall; but after tasting it, He refused to drink it.
35 Wakati walipokuwa wamemsulibisha, waligawana mavazi yake kwa kupiga kura.
When they had crucified Him, they divided up His garments by casting lots.
36 Na waliketi na kumwangalia.
And sitting down, they kept watch over Him there.
37 Juu ya kichwa chake waliweka mashitaka dhidi yake yakisomeka, “Huyu ni Yesu, mfalme wa Wayahudi.”
Above His head they posted the written charge against Him: THIS IS JESUS, THE KING OF THE JEWS.
38 Wanyang'anyi wawili walisulibiwa pamoja naye, mmoja upande wa kulia wake na mwingine wa kushoto.
Two robbers were crucified with Him, one on His right hand and the other on His left.
39 Wale waliokuwa wakipita walimdhihaki, wakitikisa vichwa vyao
And those who passed by heaped abuse on Him, shaking their heads
40 na kusema, “Wewe uliyekuwa unataka kuliharibu hekalu na kulijenga katika siku tatu, jiokoe mwenyewe! Kama ni Mwana wa Mungu, shuka chini utoke msalabani!”
and saying, “You who are going to destroy the temple and rebuild it in three days, save Yourself! If You are the Son of God, come down from the cross!”
41 Katika hali ile ile wakuu wa makuhani walikuwa wakimkashifu, pamoja na waandishi na wazee, na kusema,
In the same way, the chief priests, scribes, and elders mocked Him, saying,
42 “Aliokoa wengine, lakini hawezi kujiokoa mwenyewe. Yeye ni Mfalme wa Wayahudi. Na ashuke chini toka msalabani, ndipo tutakapomwamini.
“He saved others, but He cannot save Himself. He is the King of Israel! Let Him come down now from the cross, and we will believe in Him.
43 Alimtumaini Mungu. Acha Mungu amwokoe sasa kama anataka, kwa sababu alisema, 'Mimi ni Mwana wa Mungu.'”
He trusts in God. Let God deliver Him now if He wants Him. For He said, ‘I am the Son of God.’”
44 Na wale wanyang'anyi waliokuwa wamesulibiwa pamoja naye pia walisema maneno ya kumdhihaki.
In the same way, even the robbers who were crucified with Him berated Him.
45 Sasa kutoka saa sita kulikuwa na giza katika nchi yote hadi saa tisa.
From the sixth hour until the ninth hour darkness came over all the land.
46 Ilipofika saa tisa, Yesu akalia kwa sauti kuu, “Eloi, Eloi, lama thabakithan?” akimaanisha, “Mungu wangu, Mungu wangu, kwa nini umeniacha?”
About the ninth hour Jesus cried out in a loud voice, “Eli, Eli, lema sabachthani?” which means, “My God, My God, why have You forsaken Me?”
47 Wakati huo baadhi yao waliokuwa wamesimama pale walisikia, wakasema, “Anamwita Eliya.”
When some of those standing there heard this, they said, “He is calling Elijah.”
48 Mara moja mmoja wao alikimbia kuchukua sifongo na kuijaza kinywaji kichungu, akaiweka juu ya mti na kumpa apate kunywa.
One of them quickly ran and brought a sponge. He filled it with sour wine, put it on a reed, and held it up for Jesus to drink.
49 Nao waliosalia wakasema, “Mwacheni peke yake, acheni tuone kama Eliya atakuja kumwokoa.”
But the others said, “Leave Him alone. Let us see if Elijah comes to save Him.”
50 Kisha Yesu akalia tena kwa sauti kuu na akaitoa roho yake.
When Jesus had cried out again in a loud voice, He yielded up His spirit.
51 Tazama, Pazia la hekalu lilipasuka sehemu mbili kutokea juu hadi chini. Na ardhi ikatetemeka na miamba ikapasuka vipande.
At that moment the veil of the temple was torn in two from top to bottom. The earth quaked and the rocks were split.
52 Makaburi yalifunguka, na miili ya watakatifu wengi waliokuwa wamelala usingizi walifufuliwa.
The tombs broke open, and the bodies of many saints who had fallen asleep were raised.
53 Walitoka kwenye makaburi baada ya ufufuo wake, waliingia mji mtakatifu, na wakaonekana na wengi.
After Jesus’ resurrection, when they had come out of the tombs, they entered the holy city and appeared to many people.
54 Basi yule akida na wale ambao walikuwa wakimtazama Yesu waliona tetemeko na mambo yaliyokuwa yakitokea, walijawa na woga sana na kusema, “Kweli huyu alikuwa Mwana wa Mungu.”
When the centurion and those with him who were guarding Jesus saw the earthquake and all that had happened, they were terrified and said, “Truly this was the Son of God.”
55 Wanawake wengi waliokuwa wakimfuata Yesu kutoka Galilaya ili kumhudumia walikuwa pale wakitazama kutoka kwa mbali.
And many women were there, watching from a distance. They had followed Jesus from Galilee to minister to Him.
56 Miongini mwao walikuwa Mariamu Magdarena, Mariamu mama yake Yakobo na Joseph, na mama wa watoto wa Zebedayo
Among them were Mary Magdalene, Mary the mother of James and Joseph, and the mother of Zebedee’s sons.
57 Ilipofika jioni, alikuja mtu tajiri kutoka Arimathayo, aliyeitwa Yusufu, ambaye pia alikuwa mwanafunzi wa Yesu.
When it was evening, there came a rich man from Arimathea named Joseph, who himself was a disciple of Jesus.
58 Alimwendea Pilato na kuuomba mwili wa Yesu. Kisha Pilato aliagiza apate kupewa.
He went to Pilate to ask for the body of Jesus, and Pilate ordered that it be given to him.
59 Yusufu aliuchukua mwili akaufunga na nguo ya sufi safi,
So Joseph took the body, wrapped it in a clean linen cloth,
60 na akaulaza katika kaburi jipya lake alilokuwa amelichonga mwambani. Kisha akavingirisha jiwe kubwa likafunika mlango wa kaburi na akaenda zake.
and placed it in his own new tomb that he had cut into the rock. Then he rolled a great stone across the entrance to the tomb and went away.
61 Mariamu Magdalena na Mariamu mwingine walikuwa pale, wamekaa kuelekea kaburi.
Mary Magdalene and the other Mary were sitting there opposite the tomb.
62 Siku iliyofuata ambayo ilikuwa siku baada ya maandalio, wakuu wa makuhani na Mafarisayo walikusanyika pamoja kwa Pilato.
The next day, the one after Preparation Day, the chief priests and Pharisees assembled before Pilate.
63 Wakamwambia, “Bwana, tunakumbuka kuwa wakati yule mdanganyifu alipokuwa hai, alisema, 'Baada ya siku tatu atafufuka tena.'
“Sir,” they said, “we remember that while He was alive that deceiver said, ‘After three days I will rise again.’
64 Kwahiyo, agiza kwamba kaburi lilindwe salama mpaka siku ya tatu. Vinginevyo, wanafunzi wake wanaweza kuja kumwiba na kusema kwa watu, 'Amefufuka kutoka wafu.' Na udanganyifu wa mwisho utakuwa mbaya kuliko ule wa kwanza.”
So give the order that the tomb be secured until the third day. Otherwise, His disciples may come and steal Him away and tell the people He has risen from the dead. And this last deception would be worse than the first.”
65 Pilato akawaambia, “Chukueni walinzi. Nendeni mkafanye hali ya usalama kama muwezavyo.”
“You have a guard,” Pilate said. “Go, make the tomb as secure as you know how.”
66 Hivyo walikwenda na kufanya kaburi kuwa salama, jiwe liligongwa mhuri na kuweka walinzi.
So they went and secured the tomb by sealing the stone and posting the guard.

< Mathayo 27 >