< Mathayo 26 >

1 Wakati Yesu alipomaliza kusema maneno yote hayo, aliwaambia wanafunzi wake,
And it came to pass, when Jesus finished all these words, he said to his disciples,
2 “Mnajua kwamba baada ya siku mbili kutakuwa na sikukuu ya pasaka, na mwana wa Adamu atatolewa ili asulibiwe.”
'Ye have known that after two days the passover cometh, and the Son of Man is delivered up to be crucified.'
3 Baadaye wakuu wa makuhani na wazee wa watu walikutana pamoja katika makao ya Kuhani Mkuu, aliye kuwa anaitwa Kayafa.
Then were gathered together the chief priests, and the scribes, and the elders of the people, to the court of the chief priest who was called Caiaphas;
4 Kwa pamoja walipanga njama ya kumkamata Yesu kwa siri na kumuua.
and they consulted together that they might take Jesus by guile, and kill [him],
5 Kwa kuwa walisema, “Isifanyike wakati wa sikukuu, kusudi isije ikazuka ghasia miongoni mwa watu.”
and they said, 'Not in the feast, that there may not be a tumult among the people.'
6 Wakati Yesu alipokuwa Bethania katika nyumba ya Simoni mkoma,
And Jesus having been in Bethany, in the house of Simon the leper,
7 alipokuwa amejinyoosha mezani, mwanamke mmoja alikuja kwake akiwa amebeba mkebe wa alabasta iliyokuwa na mafuta yenye thamani kubwa, na aliyamimina juu ya kichwa chake.
there came to him a woman having an alabaster box of ointment, very precious, and she poured on his head as he is reclining (at meat).
8 Lakini wanafunzi wake walipoona jambo hilo, walichukia na kusema, “Nini sababu ya hasara hii?
And having seen [it], his disciples were much displeased, saying, 'To what purpose [is] this waste?
9 Haya yangeweza kuuzwa kwa kiasi kikubwa na kupewa maskini.”
for this ointment could have been sold for much, and given to the poor.'
10 Lakini Yesu, akiwa anajua hili, aliwaambia, “Kwa nini mnamsumbua mwanamke huyu? Kwa kuwa amefanya kitu kizuri kwangu.
And Jesus having known, said to them, 'Why do ye give trouble to the woman? for a good work she wrought for me;
11 Masikini mnao siku zote, lakini hamtakuwa pamoja nami daima.
for the poor always ye have with you, and me ye have not always;
12 Kwa sababu alipomimina mafuta haya juu ya mwili wangu, alifanya hivyo kwa ajili ya maziko yangu.
for she having put this ointment on my body — for my burial she did [it].
13 Kweli nawaambieni, popote Injili hii itakapohubiriwa katika ulimwengu mzima, kitendo alichofanya huyu mwanamke, pia kitakuwa kinasemwa kwa ajili ya kumkumbuka.”
Verily I say to you, Wherever this good news may be proclaimed in the whole world, what this [one] did shall also be spoken of — for a memorial of her.'
14 Ndipo mmoja wa wale Kumi na wawili, aliyeitwa Yuda Iskariote, alienda kwa wakuu wa makuhani
Then one of the twelve, who is called Judas Iscariot, having gone unto the chief priests, said,
15 na kusema, “Mtanipatia nini nikimsaliti?” Wakampimia Yuda vipande thelathini vya fedha.
'What are ye willing to give me, and I will deliver him up to you?' and they weighed out to him thirty silverlings,
16 Tangu muda huo alitafuta nafasi ya kumsaliti.
and from that time he was seeking a convenient season to deliver him up.
17 Hata siku ya kwanza ya mikate isiyotiwa chachu, wanafunzi walimwendea Yesu na kusema, “Wapi unataka tukuandalie ule chakula cha Pasaka?”
And on the first [day] of the unleavened food came the disciples near to Jesus, saying to him, 'Where wilt thou [that] we may prepare for thee to eat the passover?'
18 Akawaambia, “Nendeni mjini kwa mtu fulani na mwambieni, Mwalimu anasema, “Muda wangu umekaribia. Nitaitimiza Pasaka pamoja na wanafunzi wangu katika nyumba yako.””
and he said, 'Go away to the city, unto such a one, and say to him, The Teacher saith, My time is nigh; near thee I keep the passover, with my disciples;'
19 Wanafunzi walifanya kama Yesu alivyowaagiza, na waliandaa chakula cha Pasaka.
and the disciples did as Jesus appointed them, and prepared the passover.
20 Ilipofika jioni, aliketi kula chakula pamoja na wale wanafunzi Kumi na Wawili.
And evening having come, he was reclining (at meat) with the twelve,
21 Walipokuwa wanakula chakula, alisema, “Kweli nawaambia kwamba mmoja wenu atanisaliti.”
and while they are eating, he said, 'Verily I say to you, that one of you shall deliver me up.'
22 Walihuzunika sana, na kila mmoja alianza kumuuliza, “Je, hakika siyo mimi, Bwana?”
And being grieved exceedingly, they began to say to him, each of them, 'Is it I, Sir?'
23 Akawajibu, “Yule ambaye anachovya mkono wake pamoja nami katika bakuli ndiye atakaye nisaliti.
And he answering said, 'He who did dip with me the hand in the dish, he will deliver me up;
24 Mwana wa Adamu ataondoka, kama alivyoandikiwa. Lakini ole wake mtu ambaye atamsaliti Mwana wa Adamu! Ingekuwa vizuri kwa mtu huyo kama asingezaliwa.”
the Son of Man doth indeed go, as it hath been written concerning him, but woe to that man through whom the Son of Man is delivered up! good it were for him if that man had not been born.'
25 Yuda, ambaye angemsaliti alisema, “Je!, Ni mimi Rabi?” Yesu akamwambia, “Umesema jambo hilo wewe mwenyewe.”
And Judas — he who delivered him up — answering said, 'Is it I, Rabbi?' He saith to him, 'Thou hast said.'
26 Walipokuwa wakila chakula, Yesu aliutwaa mkate, akaubariki, na kuumega. Akawapa wanafunzi wake akisema, “Chukueni, mle. Huu ni mwili wangu.”
And while they were eating, Jesus having taken the bread, and having blessed, did brake, and was giving to the disciples, and said, 'Take, eat, this is my body;'
27 Akatwaa kikombe na kushukuru, akawapa na kusema, “Kunyweni wote katika hiki.
and having taken the cup, and having given thanks, he gave to them, saying, 'Drink ye of it — all;
28 Kwa kuwa hii ni damu ya agano langu, inayomwagwa kwa ajili ya wengi kwa msamaha wa dhambi.
for this is my blood of the new covenant, that for many is being poured out — to remission of sins;
29 Lakini nawaambieni, sitakunywa tena matunda ya mzabibu huu, hadi siku ile nitakapokunywa mpya pamoja nanyi katika ufalme wa Baba yangu.”
and I say to you, that I may not drink henceforth on this produce of the vine, till that day when I may drink it with you new in the reign of my Father.'
30 Walipokuwa wamemaliza kuimba wimbo, walitoka kwenda Mlima wa Mizeituni.
And having sung a hymn, they went forth to the mount of the Olives;
31 Kisha Yesu aliwaambia, “Usiku huu ninyi nyote mtajikwaa kwa sababu yangu, kwa kuwa imeandikwa, Nitampiga mchungaji na kondoo wa kundi watatawanyika.
then saith Jesus to them, 'All ye shall be stumbled at me this night; for it hath been written, I will smite the shepherd, and the sheep of the flock shall be scattered abroad;
32 Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia kwenda Galilaya.”
but, after my having risen, I will go before you to Galilee.'
33 Lakini Petro alimwambia, “Hata kama wote watakukataa kwa sababu ya mambo yatakayokupata, mimi sitakukataa.”
And Peter answering said to him, 'Even if all shall be stumbled at thee, I will never be stumbled.'
34 Yesu akamjibu, “kweli nakuambia, usiku huu kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
Jesus said to him, 'Verily I say to thee, that, this night, before cock-crowing, thrice thou wilt deny me.'
35 Petro akamwambia, “hata kama ingenipasa kufa na wewe, sitakukana.” Na wanafunzi wengine wote wakasema vivyo hivyo.
Peter saith to him, 'Even if it may be necessary for me to die with thee, I will not deny thee;' in like manner also said all the disciples.
36 Baadaye Yesu alienda nao mahali panapoitwa Gethsemane na aliwaambia wanafunzi wake, “Kaeni hapa wakati nikienda huko na kuomba.”
Then come with them doth Jesus to a place called Gethsemane, and he saith to the disciples, 'Sit ye here, till having gone away, I shall pray yonder.'
37 Akamchukua Petro na wana wawili wa Zebedayo na akaanza kuhuzunika na kusononeka.
And having taken Peter, and the two sons of Zebedee, he began to be sorrowful, and to be very heavy;
38 Kisha aliwaambia, “Roho yangu ina huzuni kubwa sana, hata kiasi cha kufa. Bakini hapa na mkeshe pamoja nami.”
then saith he to them, 'Exceedingly sorrowful is my soul — unto death; abide ye here, and watch with me.'
39 Akenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, na kuomba. Akasema, “Baba yangu, kama inawezekana, kikombe hiki kiniepuke. Isiwe kama ninavyotaka mimi, bali kama utakavyo wewe.”
And having gone forward a little, he fell on his face, praying, and saying, 'My Father, if it be possible, let this cup pass from me; nevertheless, not as I will, but as Thou.'
40 Akawaendea wanafunzi na akawakuta wamelala usingizi, na akamwambia Petro, “Kwa nini hamkuweza kukesha nami kwa saa moja?
And he cometh unto the disciples, and findeth them sleeping, and he saith to Peter, 'So! ye were not able one hour to watch with me!
41 Kesheni na kuomba kusudi msiingie majaribuni. Roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu.”
watch, and pray, that ye may not enter into temptation: the spirit indeed is forward, but the flesh weak.'
42 Akaenda zake mara ya pili na kuomba, akasema, “Baba yangu, kama jambo hili haliwezi kuepukika na ni lazima nikinywee kikombe hiki, mapenzi yako yatimizwe.”
Again, a second time, having gone away, he prayed, saying, 'My Father, if this cup cannot pass away from me except I drink it, Thy will be done;'
43 Akarudi tena na kuwakuta wamelala usingizi, kwa kuwa macho yao yalikuwa mazito.
and having come, he findeth them again sleeping, for their eyes were heavy.
44 Kisha akawaacha tena akaenda zake. Akaomba mara ya tatu akisema maneno yaleyale.
And having left them, having gone away again, he prayed a third time, saying the same word;
45 Baadaye Yesu aliwaendea wanafunzi wake na kuwaambia, “Bado mmelala tu na kujipumzisha? Tazameni, saa imekaribia, na Mwana wa Adamu anasalitiwa mikononi mwa wenye dhambi.
then cometh he unto his disciples, and saith to them, 'Sleep on henceforth, and rest! lo, the hour hath come nigh, and the Son of Man is delivered up to the hands of sinners.
46 Amkeni, tuondoke. Tazama, yule anaye nisaliti amekaribia.”
Rise, let us go; lo, he hath come nigh who is delivering me up.'
47 Wakati alipokuwa bado anaongea, Yuda mmoja wa wale Kumi na Wawili, akafika. Kundi kubwa lilifika pamoja naye likitokea kwa wakuu wa makuhani na wazee wa watu. Walikuja na mapanga na marungu.
And while he is yet speaking, lo, Judas, one of the twelve did come, and with him a great multitude, with swords and sticks, from the chief priests and elders of the people.
48 Tena mtu aliyekusudia kumsaliti Yesu alikuwa amewapa ishara, akisema, “Yule nitakayembusu, ndiye yeye. Mkamateni.”
And he who did deliver him up did give them a sign, saying, 'Whomsoever I will kiss, it is he: lay hold on him;'
49 Mara hiyo alikuja kwa Yesu na kusema, “Salamu, Mwalimu!” Na akambusu.
and immediately, having come to Jesus, he said, 'Hail, Rabbi,' and kissed him;
50 Yesu akamwambia, “Rafiki, lifanye lile ambalo limekuleta.” Ndipo wakaja, na kumnyooshea mikono Yesu, na kumkamata.
and Jesus said to him, 'Comrade, for what art thou present?' Then having come near, they laid hands on Jesus, and took hold on him.
51 Tazama, mtu mmoja aliyekuwa pamoja na Yesu, alinyosha mkono wake, akachomoa upanga wake, na akampiga mtumishi wa kuhani mkuu, na kumkata sikio lake.
And lo, one of those with Jesus, having stretched forth the hand, drew his sword, and having struck the servant of the chief priest, he took off his ear.
52 Ndipo Yesu akamwambia, rudisha upanga wako pale ulipoutoa, kwa kuwa wote watumiao upanga wataangamizwa kwa upanga.
Then saith Jesus to him, 'Turn back thy sword to its place; for all who did take the sword, by the sword shall perish;
53 Mnadhani kuwa siwezi kumwita Baba yangu, naye akanitumia majeshi zaidi ya kumi na mawili ya malaika?
dost thou think that I am not able now to call upon my Father, and He will place beside me more than twelve legions of messengers?
54 Lakini basi jinsi gani maandiko yangeweza kutimizwa, hivi ndivyo inapasa kutokea?”
how then may the Writings be fulfilled, that thus it behoveth to happen?'
55 Wakati huo Yesu akauambia umati, “Je! Mmekuja na mapanga na marungu kunikamata kama mnyang'anyi? Kila siku nilikaa hekaluni nikifundisha, na hamkunishika!
In that hour said Jesus to the multitudes, 'As against a robber ye did come forth, with swords and sticks, to take me! daily with you I was sitting teaching in the temple, and ye did not lay hold on me;
56 Lakini yote haya yametendeka ili Maandiko ya manabii yatimie.” Ndipo wanafunzi wake wakamwacha na kukimbia.
but all this hath come to pass, that the Writings of the prophets may be fulfilled;' then all the disciples, having left him, fled.
57 Wale waliomkamata Yesu alimpeleka kwa Kayafa, Kuhani Mkuu, mahali ambapo waandishi na wazee walikuwa wamekusanyika pamoja.
And those laying hold on Jesus led [him] away unto Caiaphas the chief priest, where the scribes and the elders were gathered together,
58 Lakini Petro alimfuata nyuma kwa mbali hadi katika ukumbi wa Kuhani Mkuu. Aliingia ndani na kukaa pamoja na walinzi aone kitakachotokea.
and Peter was following him afar off, unto the court of the chief priest, and having gone in within, he was sitting with the officers, to see the end.
59 Basi wakuu wa makuhani na Baraza lote walikuwa wakitafuta ushahidi wa uongo dhidi ya Yesu, kusudi wapate kumuua.
And the chief priests, and the elders, and all the council, were seeking false witness against Jesus, that they might put him to death,
60 Ingawa walijitokeza mashahidi wengi, Lakini hawakupata sababu yoyote. Lakini baadaye mashahidi wawili walijitokeza mbele
and they did not find; and many false witnesses having come near, they did not find; and at last two false witnesses having come near,
61 na kusema, “Mtu huyu alisema, ''Naweza kulivunja hekalu la Mungu na kulijenga tena kwa siku tatu.”'
said, 'This one said, I am able to throw down the sanctuary of God, and after three days to build it.'
62 Kuhani Mkuu alisimama na kumwuliza, “Hauwezi kujibu? Hawa wanakushuhudia nini dhidi yako?”
And the chief priest having stood up, said to him, 'Nothing thou dost answer! what do these witness against thee?
63 Lakini Yesu alikaa kimya. Kuhani Mkuu akamwambia, “Kama Mungu aishivyo, nakuamuru utwambie, kama wewe ni Kristo, Mwana wa Mungu.”
and Jesus was silent. And the chief priest answering said to him, 'I adjure thee, by the living God, that thou mayest say to us, if thou art the Christ — the Son of God.'
64 Yesu akamjibu, “Wewe mwenyewe umesema jambo hilo. Lakini nakuambia, toka sasa na kuendelea utamwona Mwana wa Adamu ameketi mkono wa kulia wenye Nguvu, na akija katika mawingu ya mbinguni.”
Jesus saith to him, 'Thou hast said; nevertheless I say to you, hereafter ye shall see the Son of Man sitting on the right hand of the power, and coming upon the clouds, of the heaven.'
65 Ndipo Kuhani Mkuu alirarua mavazi yake na kusema, “Amekufuru! Je, twahitaji tena ushahidi wa nini? Angalia, tayari mmesikia akikufuru.
Then the chief priest rent his garments, saying, — 'He hath spoken evil; what need have we yet of witnesses? lo, now ye heard his evil speaking;
66 Je! Mnawaza nini? Wakajibu na kusema, “Anastahili kifo.”
what think ye?' and they answering said, 'He is worthy of death.'
67 Kisha walimtemea mate usoni na kumpiga ngumi, na kumchapa makofi kwa mikono yao,
Then did they spit in his face and buffet him, and others did slap,
68 na kusema, “Tutabirie, wewe Kristo. Ni nani amekuchapa?”
saying, 'Declare to us, O Christ, who he is that struck thee?'
69 Wakati huo Petro alikuwa amekaa nje katika ukumbi, na mtumishi wa kike alimwendea na kusema, “Wewe pia ulikuwa pamoja na Yesu wa Galilaya.”
And Peter without was sitting in the court, and there came near to him a certain maid, saying, 'And thou wast with Jesus of Galilee!'
70 Lakini alikana mbele yao wote, akisema, Sijui kitu unachosema.”
And he denied before all, saying, 'I have not known what thou sayest.'
71 Alipoenda nje ya lango, mtumishi mwingine wa kike alimwona na kuwaambia waliokuwepo hapo, “Mtu huyu pia alikuwa pamoja na Yesu wa Nazareti.”
And he having gone forth to the porch, another female saw him, and saith to those there, 'And this one was with Jesus of Nazareth;'
72 Akakana tena kwa kiapo, “Mimi simjui mtu huyu.”
and again did he deny with an oath — 'I have not known the man.'
73 Muda mfupi baadaye, wale waliokuwa wamesimama karibu, walimwendea na kusema na Petro, “Kwa hakika wewe pia ni mmoja wao, kwa kuwa hata lafudhi yako inaonesha.”
And after a little those standing near having come, said to Peter, 'Truly thou also art of them, for even thy speech doth make thee manifest.'
74 Ndipo alianza kulaani na kuapa, “Mimi simfahamu mtu huyu,” na mara hiyo jogoo akawika.
Then began he to anathematise, and to swear — 'I have not known the man;' and immediately did a cock crow,
75 Petro alikumbuka maneno aliyoambiwa na Yesu, “Kabla jogoo hajawika utanikana mara tatu.”
and Peter remembered the saying of Jesus, he having said to him — 'Before cock-crowing, thrice thou wilt deny me;' and having gone without, he did weep bitterly.

< Mathayo 26 >