< Mathayo 23 >

1 Baadaye aliongea na umati wa watu na wanafunzi wake. Akasema,
AYO nae si Jesus, jacuentuse y linajyan taotao, yan y disipuluña sija,
2 “Waandishi na Mafarisayo wanakalia kiti cha Musa.
Ylegña: Y escriba yan y Fariseo sija manmatatachong gui tachong Moises;
3 Kwa hiyo chochote wanacho waamuru kufanya, fanyeni huku mkiwachunguza. Lakini msije mkaiga matendo yao, kwa sababu wao hutamka mambo wasiyoyafanya.
Todo y mansinangane jamyo na inadaje, fatinas yan adaje; lao chamiyo fumatitinas taegüije y finatinasñiñija, sa sija jasasangan, lao ti jafatitinas.
4 Kweli, wao hufunga mizigo mizito ambayo ni vigumu kuibeba, na kisha huwabebesha watu mabegani mwao. Lakini wao wenyewe hawasogezi hata kidole kuibeba.
Sa manmangogode catga sija na manmacat ya mapot machule, ya japolo gui jilo y apagan y taotao sija; lao sija ni y calalotñija ti manmalago janacalamten.
5 Matendo yao yote, huyafanya ili watazamwe na watu. Kwa sababu wao hupanua masanduku yao na huongeza ukubwa wa mapindo ya mavazi yao.
Lao todo y chechoñija, jafatinas para umalie ni y taotao sija sa janaancho y filacteriañija, ya jajujuto y madoblan y magagonñija.
6 Wao hupendelea kukaa maeneo ya kifahari katika sherehe na katika viti vya heshima ndani ya masinagogi,
Ya yañija y finenana na saga gui guipot, yan y finenana na tachong gui sinagoga;
7 na kusalimiwa kwa heshima maeneo ya sokoni, na kuitwa “Walimu” na watu.
Yan y manmasaluda gui plasa, yan ufanmafanaan ni y taotao sija, Rabi.
8 Lakini ninyi hampaswi kuitwa “Walimu,” Kwa kuwa mnaye Mwalimu mmoja, na ninyi wote ni ndugu.
Lao jamyo chamiyo fanmalalago manmafanaan. Rabi; sa unoja Maestronmiyo, ya todo jamyo mañelo.
9 Msimuite mtu yeyote hapa duniani kuwa baba yenu, kwa kuwa mnaye Baba mmoja tu, naye yuko mbinguni.
Chamiyo fanmamananaan ni uno tatanmiyo gui tano; sa unoja Tatanmiyo, na gaegue gui langet.
10 Wala msije kuitwa 'walimu,' kwa kuwa mnaye Mwalimu mmoja tu, yaani Kristo.
Ni infanmamanaan uno amunmiyo; sa unoja amunmiyo, si Cristo.
11 Bali aliye mkubwa miongoni mwenu atakuwa mtumishi wenu.
Lao y mas dangculo guiya jamyo, güiya utentagonmiyo.
12 Yeyote ajiinuae atashushwa. Na yeyote anaye jishusha atainuliwa.
Sa jayeja y munadangculon namae sagüe, umumitde; ya jayeja y munaumitden namaesagüe, güiya udangculo.
13 Lakini ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Mnawafungia watu ufalme wa mbinguni. Nanyi hamwezi kuuingia, na hamwaruhusu wanaoingia kufanya hivyo.
Lao ay ay para jamyo escriba yan Fariseo sija, hipocrita! sa injichom y raenon langet gui menan y taotao sija; ya ni jamyo ti manjalom, ni y para ufanjalom ti inpelo na ufanjalom.
14 (Zingatia: Msitari wa 14 hauonekani katika nakala bora za kale. Baadhi ya nakala huongeza msitari huu baada ya msitari wa 12. Msitari wa 14 “Ole wenu wandishi na Mafarisayo wanafiki! Kwa kuwa mnawameza wajane”).
(Ay ay para jamyo, escriba yan Fariseo sija, hipocrita! sa inticho y guima y biuda sija yan inagó y tinaetae; pot este inresibe dangculo na sentensia.)
15 Ole wenu Waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Mnavuka ngambo ya bahari na kufika kumfanya mtu mmoja aamini yale mnayoyafundisha, na anapokuwa kama ninyi, mnamfanya mara mbili mwana wa jehanamu kama ninyi wenyewe mlivyo. (Geenna g1067)
Ay ay para jamyo, escriba yan Fariseo sija, hipocrita! sa inlilicue y tase yan y tano para infatinas un prosélito, ya anae esta infatinas, infatitinas güe lalajin sasalaguan dosbiaje mas qui jamyo. (Geenna g1067)
16 Ole wenu viongozi vipofu, ninyi msemao, Yeyote aapaye kwa hekalu, si kitu. Lakini anayeapa kwa dhahabu ya hekalu, amefungwa na kiapo chake.
Ay ay para jamyo, bachet na guia sija ni y ilegmiyo: Jayeja y manjula pot templo, taya este; lao jayeja y manjula pot y oron y templo, gaeisao güe.
17 Enyi vipofu wapumbavu, kipi ni kikubwa kuliko kingine, dhahabu au hekalu ambalo limeweka wakfu dhahabu kwa Mungu?
Manbababa yan manbachet! Jafa mas dangculo, y oro pat y templo, ni y munasantos y oro?
18 Na, yeyote aapaye kwa madhabahu, si kitu. Bali anayeapa kwa sadaka iliyo juu yake, amefungwa na kiapo chake.
Ya jayeja y manjula pot y attat, taya este; lao jayeja y manjula pot y ninae ni gaegue gui jiloña, gaeisao güe.
19 Enyi watu vipofu, kipi ni kikubwa kuliko kingine, sadaka au madhabahu ambayo huweka wakfu sadaka zinazotolewa kwa Mungu?
Manbachet jamyo! Jafa mas dangculo, y ninae pat y attat ni munasantos y ninae?
20 Kwa hiyo, yeye aapaye kwa madhabahu huapa kwa hiyo na kwa vitu vyote vilivyo juu yake.
Enao mina y manjula pot y attat, manjula pot ayo yan todo y guaja gui jiloña.
21 Naye aapaye kwa hekalu, huapa kwa hilo na kwa yeye akaaye ndani yake.
Ya y manjula pot y templo, manjula pot ayo yan pot güiya y sumaga gui jinalomña.
22 Na yeye aapaye kwa mbingu, huapa kwa kiti cha enzi cha Mungu na kwa yeye aketie juu yake.
Ya y manjula pot y langet, manjula pot y trono Yuus, yan pot güiya ni gaegue na matatachong gui jiloña.
23 Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnalipa zaka kwa bizali, mnaanaa na mchicha, lakini mnaacha mambo mazito ya sheria- haki, rehema, na imani. Lakini haya mnapaswa kuwa mmeyafanya, na siyo kuacha mengine bila kuyatekeleza.
Ay ay para jamyo, escriba yan Fariseo sija, hipocrita! sa manmanapase jamyo diesmo y yetba buena, yan anis yan comino, ya inpelo y mas dangculo gui lay; y juisio, y minaase, yan y jinenggue. Este nesesita umafatinas, ya munga mapolo na ti infatinas y otro sija.
24 Enyi viongozi vipofu, ninyi ambao mnachuja mdudu mdogo lakini mnameza ngamia!
Bachet jamyo na guia sija! sa inguicula y ñamo, ya inpapañot y cameyo.
25 Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnasafisha nje ya vikombe na nje ya sahani, lakini ndani pamejaa dhuluma na kutokuwa na kiasi.
Ay ay para jamyo, escriba yan Fariseo sija, hipocrita! sa infagagase y sumanjiyeng y posuelo yan y plato; lao y sumanjalom bula inamot yan minampos.
26 Enyi Mafarisayo vipofu, safisheni kwanza ndani ya kikombe na ndani ya sahani, ili upande wa nje nao pia uwe safi.
Fariseo bachet jao! fagase finena y sumanjalom gui posuelo yan y plato, ya despues y sumanjiyong ugasgas locue.
27 Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnafanana na makaburi yaliyopakwa chokaa, ambayo kwa nje huonekana mazuri, lakini kwa ndani yamejaa mifupa ya wafu na kila kitu kilicho kichafu.
Ay ay para jamyo, escriba yan Fariseo sija, hipocrita! sa manparejo jamyo yan y manmablanquea na naftan na y sanjiyongña magajet na mauleg malie: lao y sumanjalomña bula tolang manmatae, yan todo y ináplacha.
28 Vivyo hivyo, nanyi kwa nje mwaonekana wenye haki mbele ya watu, lakini kwa ndani mmejaa unafiki na udhalimu.
Taegüenao locue jamyo y sumanjiyong magajet na manunas malie jamyo ni taotao sija; lao y sumanjalom bula hipocresia yan inechong.
29 Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mwajenga makaburi ya manabii na kuyapamba makaburi ya wenye haki.
Ay ay para jamyo escriba yan Fariseo sija, hipocrita! sa infatinas naftan y profeta sija, ya inadotna y naftan y manunas,
30 Ninyi mwasema, kama tungeishi siku za baba zetu, tusingekuwa tumeshiriki pamoja nao kumwaga damu za manabii.
Ya ilegmiyo: Yaguin mangaeguejam gui jaanin y tatanmame sija, ti infangachong yan sija gui jâgâ y profeta sija.
31 Kwa hiyo mwajishuhudia wenyewe kwamba ninyi ni watoto wa hao waliowaua manabii.
Ayo mina jamyo mismo innae testimonio contra jamyo, na jamyo famaguon ayo sija y pumuno y profeta sija.
32 Pia ninyi mnakamilisha kujaza sehemu inayostahili dhambi ya baba zenu.
Jamyo locue innabula y medidan y tatanmiyo.
33 Enyi nyoka, wana wa vipiribao, kwa namna gani mtaikwepa hukumu ya jehanamu? (Geenna g1067)
Colebla sija, rasan colebla sija! Jaf taemano jamyo insujaye gui sentensian sasalaguan? (Geenna g1067)
34 Kwahiyo, tazama, nawatuma kwenu manabii, watu wenye hekima, na waandishi. Baadhi yao mtawaua na kuwasulibisha. Na baadhi yao mtawachapa ndani ya masinagogi yenu na kuwafukuza kutoka mji mmoja hadi mwingine.
Enaomina estagüeyo na junae jamyo profeta sija, yan manmalate yan escribasija; ya palo guiya sija inpino ya inatane gui quiluus; ya y palo guiya sija, inpanag gui sinagoganmiyo, ya inpetsigue sija guinin siuda asta siuda;
35 Matokeo ni kwamba juu yenu patatokea damu zote za wenye haki zilizomwagwa duniani, kuanzia damu ya Habili mwenye haki hadi kwa damu ya Zakaria mwana wa Barakia, mliye muua kati ya patakatifu na madhabahu.
Para ufato gui jilomiyo todo y tunas na jâgâ ni y machuda gui jilo y tano, desde y jâgân Abel y tinas, asta y jâgâ Sacharias, lajin Barachias, ni inpino gui entalo templo yan y attat.
36 Kweli, nawaambieni, mambo haya yote yatakipata kizazi hiki.
Magajet jusagane jamyo, na todo estesija ufanmato gui jilo este na generasion.
37 Yerusalemu, Yerusalemu, wewe unayewaua manabii na kuwapiga mawe wale ambao wanatumwa kwako! mara ngapi nimewakusanya watoto wako pamoja kama vile kuku awakusanyavyo vifaranga wake chini ya mbawa zake, lakini haukukubali!
Jerusalem! Jerusalem! ni y pumuno y profeta sija, ni infagas ni acho todo y manmatago para jago, cuanto biaje malagoyo na jurecoje y famaguonmo, calang y ponedera yan jarecoje y poyitasña sija gui papa papaña, lao ti manmalago jamyo!
38 Tazama, nyumba yako imebaki ukiwa.
Estagüe na madingo guiya jamyo y guimanmiyo na ti mataotagüe.
39 Nami nakuambia, Kuanzia sasa na kuendelea hautaniona, hadi utakaposema, 'Amebarikiwa yeye ajaye kwa jina la Bwana.”'
Sa guajo jamyo sumangane, na desde pago, ti inliiyo, asta qui ilegmiyo: Dichoso güe y mato. pot y naan y Señot.

< Mathayo 23 >