< Mathayo 22 >

1 Yesu alisema nao tena katika mifano, akisema,
Once again, Jesus spoke to them in parables:
2 “Ufalme wa mbinguni unafanana na mfalme aliyeandaa sherehe ya harusi ya mwanawe.
“The kingdom of heaven is like a king who prepared a wedding banquet for his son.
3 Akawatuma watumishi wake kuwakaribisha waliokuwa wamealikwa kuja katika sherehe ya harusi, lakini hawakufika.
He sent his servants to call those he had invited to the banquet, but they refused to come.
4 Mfalme aliwatuma tena watumishi wengine, akisema. “Waambieni wote walioalikwa, Angalieni, nimeandaa chakula. Fahali na ndama wangu wanono wamechinjwa, na mambo yote yako tayari, Njoni katika sherehe ya harusi.”
Again, he sent other servants and said, ‘Tell those who have been invited that I have prepared my dinner. My oxen and fattened cattle have been killed, and everything is ready. Come to the wedding banquet.’
5 Lakini watu hao hawakuzingatia kwa dhati mwaliko wake. Baadhi walirejea katika mashamba yao, na wengine walirudi katika sehemu zao za biashara.
But they paid no attention and went away, one to his field, another to his business.
6 Wengine waliwainukia watumishi wa mfalme na kuwadharirisha na kuwaua.
The rest seized his servants, mistreated them, and killed them.
7 Lakini mfalme alikasirika. Alituma jeshi lake, akawaua wale wauaji na kuuteketeza mji wao kwa moto.
The king was enraged, and he sent his troops to destroy those murderers and burn their city.
8 Kisha aliwaambia watumishi wake, “Harusi iko tayari, lakini walioalikwa hawakustahili.
Then he said to his servants, ‘The wedding banquet is ready, but those I invited were not worthy.
9 Kwa hiyo nendeni kwenye makutano ya njia kuu, waalikeni watu wengi kadri iwezekanavyo waje kwenye sherehe ya harusi.”
Go therefore to the crossroads and invite to the banquet as many as you can find.’
10 Watumishi walienda njia kuu na kuwakaribisha watu wowote waliowaona, wema na wabaya. Hivyo ukumbi wa harusi ulijaa wageni.
So the servants went out into the streets and gathered everyone they could find, both evil and good, and the wedding hall was filled with guests.
11 Lakini mfalme alipoingia kuwatazama wageni, alimuona mtu mmoja ambaye hakuvaa vazi rasmi la harusi!
But when the king came in to see the guests, he spotted a man who was not dressed in wedding clothes.
12 Mfalme alimwuliza, 'Rafiki, ulipataje kufika hapa ndani bila vazi la harusi?' Na mtu huyo hakujibu chochote.
‘Friend,’ he asked, ‘how did you get in here without wedding clothes?’ But the man was speechless.
13 Ndipo mfalme alipowaambia watumishi wake, “Mfungeni mtu huyu mikono na miguu na mtupeni nje katika giza, huko ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.
Then the king told the servants, ‘Tie him hand and foot, and throw him into the outer darkness, where there will be weeping and gnashing of teeth.’
14 Kwa kuwa watu wengi wanaitwa, lakini wateule ni wachache.”
For many are called, but few are chosen.”
15 Ndipo Mafarisayo waliondoka na kupanga jinsi ya kumkamata Yesu katika maneno yake mwenyewe.
Then the Pharisees went out and conspired to trap Jesus in His words.
16 Ndipo walipowatuma wanafunzi wao pamoja na Maherode. Na walimwambia Yesu, “Mwalimu, tunajua kuwa wewe ni mtu wa kweli, na kwamba unafundisha matakwa ya Mungu katika ukweli. Haujali maoni ya mtu mwingine na hauoneshi upendeleo kwa watu.
They sent their disciples to Him along with the Herodians. “Teacher,” they said, “we know that You are honest and that You teach the way of God in accordance with the truth. You seek favor from no one, because You pay no attention to external appearance.
17 Kwa hiyo tuambie, unafikiri nini? Je, ni sahihi kisheria kulipa kodi kwa Kaisari au hapana?”
So tell us what You think: Is it lawful to pay taxes to Caesar or not?”
18 Yesu alifahamu uovu wao na akasema, “Kwa nini mnanijaribu, enyi wanafiki?
But Jesus knew their evil intent and said, “You hypocrites, why are you testing Me?
19 Nionesheni pesa itumikayo kulipia kodi.” Ndipo wakamletea dinari.
Show Me the coin used for the tax.” And they brought Him a denarius.
20 Yesu akawauliza, “Sura na jina hili ni vya nani?”
“Whose image is this,” He asked, “and whose inscription?”
21 Wakamjibu, “Vya Kaisari.” Ndipo Yesu akawaambia, “Mpeni Kaisari vitu vilivyo vyake na vya Mungu mpeni Mungu.”
“Caesar’s,” they answered. So Jesus told them, “Give to Caesar what is Caesar’s, and to God what is God’s.”
22 Waliposikia hivyo walishangaa. Kisha walimwacha na kwenda zao.
And when they heard this, they were amazed. So they left Him and went away.
23 Siku hiyo baadhi ya Masadukayo walikuja kwa Yesu, wale wasemao kuwa hakuna ufufuo wa wafu. Wakamwuliza,
That same day the Sadducees, who say there is no resurrection, came to Jesus and questioned Him.
24 wakisema, “Mwalimu, Musa alisema, Ikiwa mtu amefariki bila kuzaa watoto, ndugu yake na amrithi huyo mwanamke na ampatie mtoto kwa ajili ya ndugu yake.
“Teacher,” they said, “Moses declared that if a man dies without having children, his brother is to marry the widow and raise up offspring for him.
25 Walikuwapo ndugu saba. Wa kwanza alioa na kisha akafariki bila kuzaa watoto. Akamwachia mke nduguye.
Now there were seven brothers among us. The first one married and died without having children. So he left his wife to his brother.
26 Kisha ndugu yake wa pili naye akafanya vivyo hivyo, kisha yule wa tatu, ikawa hivyo hadi kwa yule wa saba.
The same thing happened to the second and third brothers, down to the seventh.
27 Baada ya kufanya hivyo wote, yule mwanamke naye alifariki.
And last of all, the woman died.
28 Sasa katika ufufuo huyo mwanamke atakuwa mke wa nani katika ndugu hao saba? Kwa sababu wote walimuoa.”
In the resurrection, then, whose wife will she be of the seven? For all of them were married to her.”
29 Lakina Yesu aliwajibu na kuwaambia, “Mnakosea, kwa sababu hamjui Maandiko wala nguvu za Mungu.
Jesus answered, “You are mistaken because you do not know the Scriptures or the power of God.
30 Kwa kuwa katika ufufuo, watu hawaoi wala kuolewa. Badala yake watu huwa kama malaika huko mbinguni.
In the resurrection, people will neither marry nor be given in marriage. Instead, they will be like the angels in heaven.
31 Lakini kuhusu ufufuo wa wafu, hamjawahi kusoma kile ambacho Mungu alikisema kwenu, akisema,
But concerning the resurrection of the dead, have you not read what God said to you:
32 Mimi ni Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo? Mungu si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa walio hai.”
‘I am the God of Abraham, the God of Isaac, and the God of Jacob’? He is not the God of the dead, but of the living.”
33 Wakati kusanyiko waliposikia hili, waliyashangaa mafundisho yake.
When the crowds heard this, they were astonished at His teaching.
34 Lakini Mafarisayo waliposikia kuwa Yesu amewanyamazisha Masadukayo, walijikusanya wao wenyewe kwa pamoja.
And when the Pharisees heard that Jesus had silenced the Sadducees, they themselves gathered together.
35 Mmoja wao, akiwa mwana sheria, alimwuliza swali kwa kumjaribu.
One of them, an expert in the law, tested Him with a question:
36 “Mwalimu, ni amri ipi iliyo kuu kuliko zote katika sheria?”
“Teacher, which commandment is the greatest in the Law?”
37 Yesu akamjibu, “Lazima umpende Bwana kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote.
Jesus declared, “‘Love the Lord your God with all your heart and with all your soul and with all your mind.’
38 Hii ndiyo amri iliyo kuu na ya kwanza.
This is the first and greatest commandment.
39 Na ya pili inafanana na hiyo- Ni lazima kumpenda jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.
And the second is like it: ‘Love your neighbor as yourself.’
40 Sheria zote na Manabii hutegemea amri hizi mbili.”
All the Law and the Prophets hang on these two commandments.”
41 Na Mafarisayo walipokuwa bado wamejikusanya pamoja, Yesu aliwauliza swali.
While the Pharisees were assembled, Jesus questioned them:
42 Akisema, “J! e, Mwafikiri nini juu ya Kristo? Yeye ni Mwana wa nani?” Nao wakamjibu, “Ni mwana wa Daudi.”
“What do you think about the Christ? Whose son is He?” “David’s,” they answered.
43 Yesu akawajibu, “Ni kwa namna gani Daudi katika Roho anamwita Bwana, akisema,
Jesus said to them, “How then does David in the Spirit call Him ‘Lord’? For he says:
44 'Bwana alimwambia Bwana wangu, “Kaa mkono wangu wa kuume, hadi nitakapowafanya maadui zako wawekwe chini ya miguu yako.”'?”
‘The Lord said to my Lord, “Sit at My right hand until I put Your enemies under Your feet.”’
45 Kama Daudi anamwita Kristo “Bwana,” jinsi gani atakuwa mtoto wake?”
So if David calls Him ‘Lord,’ how can He be David’s son?”
46 Hakuna aliyeweza kumjibu neno tena, na hakuna aliyethubutu tena kumwuliza maswali zaidi tangu siku hiyo na kuendelea.
No one was able to answer a word, and from that day on no one dared to question Him any further.

< Mathayo 22 >