< Mathayo 21 >
1 Yesu na wanafunzi wake wakafika karibu na Jerusalemu na wakaenda mpaka Bethfage, katika mlima mizeituni, kisha Yesu akawatuma wanafunzi wawili,
And when they drew near to Jerusalem, and came to Bethphage at the Mount of Olives, Jesus sent two disciples,
2 akiwaambia, “Nendeni katika kijiji kinachofuata, na mara moja mtamkuta punda amefungwa pale, na mwanapunda pamoja naye. wafungueni na kuwaleta kwangu.
saying to them, Go m the village over against you, and immediately ye will find an ass tied, and a colt with her; loose and bring them to me.
3 Ikiwa mtu yeyote akiwaambia chochote kuhusu hilo, mtasema, `Bwana anawahitaji, ` na mtu huyo mara moja atawaruhusu mje pamoja nao”
And if any one say aught to you, ye shall say, The Lord hath need of them; and he will immediately send them.
4 Jambo hili lilitokea ni lile lililosemwa kupitia kwa nabii lazima litimizwe. Akawaambia,
Now this took place, that it might be fulfilled which was spoken through the prophet, saying,
5 Waambie binti Sayuni, tazama, mfalme wako anakuja kwenu, mnyenyekevu na akiwa amempanda punda, na mwana punda mme, mwana punda mchanga.
“Say to the daughter of Zion, Behold, thy king cometh to thee, meek, and riding on an ass, and on a colt the foal of a beast of burden.”
6 Kisha wanafunzi waliondoka na kufanya kama Yesu alivyowaagiza.
And the disciples o went, and did as Jesus bade them,
7 Wakamleta punda na mwanapunda, na kuweka nguo zao juu yao, naye Yesu akakaa pale.
and brought the ass and the colt, and put on them their garments, and he sat on them.
8 Wengi katika mkusanyiko walitandaza nguo zao njiani, na wengine walikata matawi kutoka kwenye miti na kutandaza barabarani.
And very many of the multitude spread their garments in the road; others cut down branches from the trees, and strewed them in the road.
9 Umati uliomtangulia Yesu na wale waliomfuata walipaza sauti, wakisema,”Hosana kwa mwana wa Daudi! Ni mbarikiwa ajaye kwa jina la Bwana. Hosana juu zaidi!”
And the multitudes that went before him, and that followed, were crying out, saying, Hosanna to the Son of David! Blessed is he that cometh in the name of the Lord! Hosanna in the highest heavens!
10 Yesu alipofika Yerusalemu, mji mzima ulishtuka na kusema, “Huyu ni nani?
And when he came into Jerusalem, the whole city was in commotion, saying, Who is this?
11 “Umati ulijibu, “Huyu ni Yesu Nabii, kutoka Nazareti ya Galilaya.”
And the multitudes said, This is the prophet Jesus, from Nazareth of Galilee.
12 Kisha Yesu akaingia katika hekalu la Mungu. akawafukuza nje wote waliokuwa wakinunua na kuuza hekaluni. Pia alipindua meza za wabadilishaji wa fedha na viti vya wauza njiwa.
And Jesus went into the temple of God, and cast out all those who sold and bought in the temple, and overturned the tables of the money-changers, and the seats of those who sold the doves;
13 Akawaambia, “Imeandikwa, `'Nyumba yangu itaitwa nyumba ya maombi, `lakini ninyi mmeifanya pango la wanyang`anyi.”
and said to them, It is written, “My house shall be called a house of prayer; but ye make it a den of robbers.”
14 kisha vipofu na vilema wakamjia hekaluni, naye akawaponya.
And the blind and lame came to him in the temple, and he cured them.
15 Lakini wakati wakuu wa makuhani na waandishi walipoona maajabu aliyoyatenda, na waliposikia watoto wakipiga kelele hekaluni na kusema, “Hosana kwa Mwana wa Daudi,” walishikwa na hasira.
But the chief priests and the scribes, when they saw the wonderful things which he did, and the children that were crying out in the temple, and saying, Hosanna to the Son of David, were much displeased;
16 Wakamwambia, “Umesikia kile kinachosemwa na hawa watu?” Yesu akawaambia, “Ndiyo! Lakini hamjawahi kusoma, 'Kutoka kwa midomo ya watoto na watoto wachanga wanyonyao mna sifa kamili?''
and said to him, Dost thou hear what these say? But Jesus saith to them, Yea; did ye never read, “From the mouth of babes and sucklings thou didst prepare praise”?
17 Kisha Yesu akawaacha na kwenda nje ya mji katika Bethania na kulala huko.
And he left them, and went out of the city to Bethany, and lodged there.
18 Asubuhi alipokuwa anarudi mjini, alikuwa na njaa.
And in the morning, as he was returning to the city, he was hungry.
19 Aliona mtini kandokando ya barabara. Akauendea, lakini hakupata kitu juu yake isipokuwa majani. Aliuambia, “Kusiwe na matunda kwako daima tena.” Na mara hiyo mtini ule ukanyauka. (aiōn )
And seeing one fig-tree by the road-side, he went up to it, and found nothing on it, but leaves only; and he saith to it, Let there be no fruit from thee hencefoward for ever. And immediately the fig-tree withered. (aiōn )
20 Wanafunzi walipoona, wakastaajabu na kusema, “Imekuwaje mtini umenyauka mara moja?”
And the disciples seeing it, marveled, saying, How suddenly did the fig-tree wither!
21 Yesu akajibu na kuwaambia, “Kweli nawaambieni, kama mkiwa na imani na bila wasiwasi, hamtafanya kile kilichofanyika kwa huo mtini tu, lakini mtauambia hata huo mlima, ` uchukuliwe na ukatupwe baharini, `na itafanyika.
Jesus answering said to them, Truly do I say to you, If ye have faith, and do not doubt, not only shall ye do what hath been done to the fig-tree, but should ye even say to this mountain, Be thou taken up and cast into the sea, it would be done.
22 Chochote mtakachoomba kwa sala, huku mkiamini, mtapokea.”
And all things whatever ye shall ask in prayer, believing, ye will receive.
23 Yesu alipofika hekaluni, wakuu wa makuhani na wazee wa watu wakamjia wakati alipokuwa akifundisha na kumwuliza, “Ni kwa mamlaka gani unafanya mambo haya? Na ni nani aliyekupa mamlaka haya?”
And when he had come into the temple, the chief priests and the elders of the people came to him as he was teaching, and said, By what authority doest thou these things? And who gave thee this authority?
24 Yesu akajibu na kuwaambia, “Nami tena nitawauliza swali moja. kama mkiniambia, nami vilevile nitawaambia ni kwa mamlaka gani ninafanya mambo haya.
And Jesus answering said to them, I also will ask you one question; which if ye answer me, I too will tell you by what authority I do these things.
25 Ubatizo wa Yohana- ulitoka wapi, mbinguni au kwa wanadamu?” Wakahojiana wenyewe, wakisema, tukisema, ulitoka mbinguni, `atatuambia, kwa nini hamkumwamini? `
The baptism of John, whence was it? From heaven, or from men? And they reasoned among themselves, saying, If we say, From heaven, he will say to us, Why then did ye not believe him?
26 Lakini tukisema, `ulitoka kwa wanadamu, `tunawaogopa makutano, kwa sababu wote wanamwona Yohana kama nabii.”
But if we say, From men, we fear the multitude; for all regard John as a prophet.
27 Kisha wakamjibu Yesu na kusema, “Hatujui” Akawaambia pia, “Wala mimi sitawaambia ni kwa mamlaka gani nafanya mambo haya.
And they answered Jesus and said, We do not know. And he said to them, Neither do I tell you by what authority I do these things.
28 Lakini mnafikiri nini? Mtu mwenye wana wawili. Akaenda kwa moja na kumwambia, `Mwanangu, nenda ukafanye kazi katika shamba la mizabibu
But what think ye? A man had two sons: he came to the first, and said, Son, go, work today in the vineyard.
29 leo. `Mwana akajibu na kusema, `sitakwenda, ' Lakini baadaye akabadilisha mawazo yake na akaenda.
And he answered and said, I will not. Afterward he repented, and went.
30 Na Mtu yule akaenda kwa mwana wa pili na kusema kitu kilekile. Mwana huyu akajibu na kusema, `nitakwenda, bwana', lakini hakwenda.
And he came to the other and said the same. And he answered and said, I will, sir; and went not.
31 Yupi kati ya wana wawili aliyefanya matakwa ya baba yake? Wakasema, “Mwana wa kwanza.” Yesu akawaambia, “Kweli nawaambieni, wakusanya ushuru na makahaba wataingia kwenye ufalme wa Mungu kabla yenu kuingia.
Which of the two did the will of his father? They say, The first. Jesus saith to them, Truly do I say to you, that the publicans and the harlots go into the kingdom of God before you.
32 Kwa maana Yohana alikuja kwenu kwa njia iliyo nyoofu, lakini hamkumwamini, wakati wakusanya ushuru na makahaba walimwamini. Na ninyi, mlipoona hilo likitendeka, hamkuweza kutubu ili baadaye mumwamini.
For John came to you as a preacher of righteousness, and ye did not believe him; but the publicans and the harlots believed him; and ye, when ye had seen it, did not afterward repent, that ye might believe him.
33 Sikilizeni mfano mwingine. Kulikuwa na mtu, mtu mwenye eneo kubwa la ardh. Alipanda mizabibu, akaiwekea uzio, akatengeneza na chombo cha kukamlia divai, akajenga na mnara wa walinzi, na akalikodisha kwa watunza zabibu. Kisha akaenda katika nchi nyingine.
Hear another parable. There was a householder, who planted a vineyard, and set a hedge about it, and dug in it a wine-press, and built a tower, and let it out to husbandmen, and went abroad.
34 Wakati wa mavuno ya mizabibu ulipokaribia, aliwatuma baadhi ya watumishi kwa wakulima wa mizabibu kuchukua mizabibu yake.
And when the season of the fruits drew near, he sent his servants to the husbandmen, that they might receive his fruits.
35 Lakini wakulima wa zabibu wakawachukua watumishi wake, wakampiga mmoja, wakamwua mwingine, na wakampiga mmoja kwa mawe.
And the husbandmen took his servants, and beat one, and killed another, and stoned another.
36 Kwa mara nyingine, Mmiliki aliwatuma watumishi wengine, wengi zaidi ya wale wa kwanza, lakini wakulima wa mizabibu waliwatendea vilevile.
Again he sent other servants more than the first; and they dealt with them in the same manner.
37 Baada ya hapo bwana yule akamtuma kwao mwana wake, akisema, `'Watamheshimu mwanangu.'`
And afterward he sent to them his son, saying, They will respect my son.
38 Lakini wakulima wa mizabibu walipomwona kijana yule, wakaambizana, `'Huyu ni mrithi, Njooni, tumuue na tumiliki urithi.'
But the husbandmen, when they saw the son, said among themselves, This is the heir; come, let us kill him, and get his inheritance.
39 `Hivyo wakamchukua, wakamtupa nje ya shamba la mizabibu na kumwua.
And they took him, and cast him out of the vineyard, and killed him.
40 Je mmliki wa shamba la mizabibu atakapokuja, atawafanya nini wakulima wa mizabibu?”
When therefore the lord of the vineyard cometh, what will he do to those husbandmen?
41 Wakamwambia, “Atawaharibu hao watu waovu katika njia ya ukali zaidi, na kisha atalikodisha shamba la mizabibu kwa wakulima wengine wa mizabibu, watu ambao watalipa kwa ajili ya mizabibu itakapoiva.”
They say to him, He will bring those wicked men to a miserable end, and will let out his vineyard to other husbandmen, who will render him the fruits in their season.
42 Yesu akawaambia, “Hamkusoma katika maandiko, 'Jiwe walilolikataa waashi limekuwa jiwe kuu la msingi. Hili lilitoka kwa Bwana, na inashangaza machoni petu?'
Jesus saith to them, Did ye never read in the Scriptures, “The stone which the builders rejected, the same hath become the corner-stone; from the Lord did this come, and it is marvelous in our eyes?”
43 Hivyo nawaambieni, Ufalme wa Mungu utatwaliwa kutoka kwenu na kupewa taifa linalojali matunda yake.
Therefore I say to you, that the kingdom of God will be taken away from you, and given to a nation yielding the fruits thereof.
44 Yeyote atakayeanguka juu ya jiwe hilo atavunjwa vipandevipande. Lakini kwa yeyote litakayemwangukia, litamsaga.”
45 Wakuu wa makuhani na mafarisayo waliposikia mifano yake, wakaona kuwa anawazungumzia wao.
And the chief priests and the Pharisees when they heard his parables, knew that he was speaking of them.
46 Lakini kila walipotaka kunyosha mikono juu yake, waliogopa makutano, kwa sababu watu walimtazama kama nabii.
And they sought to seize him, but feared the multitudes, because they regarded him as a prophet.