< Mathayo 20 >

1 Kwa maana ufalme wa mbinguni unafanana na mmliki wa shamba, aliyeamka asubuhi na mapema ili kuajiri wafanyakazi katika shamba lake la mizabibu.
For the kingdom of heaven is like a householder, who went out early in the morning to hire laborers for his vineyard.
2 Baada ya kuwa amekubaliana na wafanyakazi dinari moja kwa kutwa, aliwatuma kwenda katika shamba lake la mizabibu.
And having agreed with the laborers for a denary a day, he sent them into his vineyard.
3 Alienda tena baada ya masaa matatu hivi na aliona wafanyakazi wengine wakiwa wamesimama bila kazi katika eneo la soko.
And going out about the third hour, he saw others standing idle in the market-place;
4 Akawaambia, 'Ninyi pia, nendeni katika shamba la mizabibu, na chochote kilicho halali nitawapa.' Hivyo wakaenda kufanya kazi.
and said to them, Go ye also into the vineyard; and whatever is right, I will give you. And they went.
5 Akaenda tena baada ya masaa sita na tena katika saa ya tisa, na alifanya hivyo hivyo.
Again going out about the sixth and the ninth hour, he did likewise.
6 Mara nyingine tena mnamo saa kumi na moja, alienda na kuwakuta watu wengine wamesimama bila kazi. Aliwaambia, 'kwanini mmesimama hapa bila kazi yoyote kwa siku nzima?
And going out about the eleventh hour, he found others standing, and saith to them, Why stand ye here all the day idle?
7 Wakamwambia, kwasababu hakuna mtu yeyote aliyetuajiri. Akawaambia, 'Nanyi ninyi pia nendeni katika shamba la mizabibu.'
They say to him, Because no one hath hired us. He saith to them, Go ye also into the vineyard.
8 Wakati wa jioni ulipofika, mwenye shamba la mizabibu alimwambia msimamizi wake, 'Waite wafanyakazi na uwalipe mishahara, kwa kuanza na wa mwisho hadi wa kwanza.'
And when evening came, the lord of the vineyard saith to his steward, Call the laborers, and give them their pay, beginning with the last, and going on to the first.
9 Walipokuja wale walioajiriwa saa kumi na moja, kila mmoja wao alipokea dinari.
And they who were hired about the eleventh hour came, and received each a denary.
10 Walipokuja wafanyakazi wa kwanza, walifikiri kuwa watapokea zaidi, lakini walipokea pia kila mmoja dinari moja kila mtu.
But when the first came, they supposed that they should receive more; and they too received each a denary.
11 Baada ya kupokea malipo yao, walimlalamikia mmiliki wa shamba.
And when they had received it, they murmured against the householder,
12 Wakasema, 'Hawa wafanyakazi wa mwisho wametumia saa moja tu katika kufanya kazi, lakini umewalinganisha na sisi, sisi tumebeba mzigo kwa siku nzima na kuungua na joto.'
saying, These last have worked but one hour, and thou hast made them equal to us, who have borne the burden and heat of the day.
13 Lakini mwenye shamba akajibu na kusema kwa mmoja wao, 'Rafiki, sikutenda jambo baya. Je! hatukukubaliana na mimi kwa dinari moja?
But he answering said to one of them, Friend, I do thee no wrong; didst not thou agree with me for a denary?
14 Pokea kile kilicho halali yako na uende zako. Ni furaha yangu kuwapa hawa wafanyakazi walioajiriwa mwisho sawa sawa na wewe.
Take thy due, and go. But I will give to this last even as to thee.
15 Je! Si haki kwangu kufanya kile ninachotaka na mali zangu? Au jicho lako ni ovu kwa sababu mimi ni mwema?
Am I not free to do what I will with my own? Is thine eye evil, because I am good?
16 Hivyo wa mwisho atakuwa kwanza na wa kwanza wa mwisho''
Thus the last will be first, and the first, last. And as
17 Yesu alipokuwa akipanda kwenda Yerusalem, aliwachukuwa wanafunzi wake kumi na mbili pembeni, na njiani akawaambia,
Jesus was going up to Jerusalem, he took the twelve apart, and on the way said to them,
18 ''Tazama tunaelekea Yerusalemu, na Mwana wa Adamu atatiwa katika mikono ya wakuu wa makuhani na waandishi. Watamhukumu kifo
Lo! we are going up to Jerusalem, and the Son of man will be delivered up to the chief priests and scribes; and they will condemn him to death,
19 na watamtoa kwa watu wa mataifa ili kumdhihaki, kumchapa na kumsulibisha. Lakini katika siku ya tatu atafufuka.''
and will deliver him up to the gentiles to mock, and scourge, and crucify; and on the third day he will rise again.
20 Kisha mama wa wana wa Zebedayo alikuja kwa Yesu na wana wake. Alipiga magoti mbele yake na kumwomba kitu kutoka kwake.
Then came to him the mother of the sons of Zebedee with her sons, falling down before him, and asking a certain thing of him.
21 Yesu akamwambia, “Unataka nini?” Akamwambia, ''Amuru kuwa hawa wanangu wawili wakae, mmoja mkono wako wa kulia na mmoja mkono wako wa kushoto katika ufalme wako.''
And he said to her, What is thy wish? She saith to him, Grant that these my two sons may sit, one on thy right hand, and one on thy left, in thy kingdom.
22 Lakini Yesu akajibu na kusema, “Haujui kile unachoomba. Je! Unaweza kukinywea kikombe ambacho nitakinywea?” wakamwambia, “Tunaweza.”
But Jesus answering said, Ye know not what ye ask. Can ye drink the cup which I am to drink? They say to him, We can.
23 Akawaambia, “Kikombe changu hakika mtakinywea. Lakini kukaa mkono wangu wa kulia na mkono wangu wa kushoto si jukumu langu kuwapa, lakini ni kwa wale ambao wamekwisha kuandaliwa na Baba yangu.”
He saith to them, Ye will indeed drink my cup; but to sit on my right hand and on my left is not mine to give, but it will be given to those for whom it hath been prepared by my Father.
24 Wanafunzi wengine kumi waliposikia hivyo, wakahuzunishwa sana na wale ndugu wawili.
And when the ten heard this, they were much displeased with the two brothers.
25 Lakini Yesu aliwaita mwenyewe na kuwaambia, “Mnafahamu ya kuwa watawala wa mataifa huwatiisha, na wakuu wao hutekeleza mamlaka juu yao.
But Jesus called them to him, and said, Ye know that the rulers of the nations lord it over them, and their great men exercise a strict authority over them.
26 Lakini isiwe hivyo kwenu. Badala yake, yeyote atakayetaka kuwa mkubwa miongoni mwenu lazima awe mtumishi wenu.
Not so shall it be among you; but whoever desireth to become great among you, will be your minister;
27 Na atakaye kuwa wa kwanza miongoni mwenu lazima awe mtumishi wenu.
and whoever desireth to be first among you, will be your servant;
28 Kama vile Mwana wa Adamu hakuja kutumikiwa, bali kutumika, na kutoa uhai wake kuwa ukombozi kwa wengi.”
even as the Son of man came not to be served, but to serve, and to give his life a ransom for many.
29 Wakati wakitoka Yeriko, umati mkubwa ulimfuata.
And as they were going out of Jericho, a great multitude followed him.
30 Na waliwaona vipofu wawili wameketi kando ya barabara. Waliposikia kuwa Yesu alikuwa anapita, walipaza sauti na kusema, “Bwana, Mwana wa Daudi, utuhurumie.”
And lo! two blind men, who were sitting by the way-side, when they heard that Jesus was passing by, cried out, saying, Have pity on us, Son of David!
31 Lakini umati ukawakemea, na kuwaambia nyamazeni. Hata hivyo, wao wakapaza sauti zaidi na kusema, “Bwana, Mwana wa Daudi, utuhurumie.”
And the multitude sharply bade them be silent. But they cried out the more, saying, Lord, have pity on us, Son of David!
32 Kisha Yesu alisimama na aliwaita na kuwauliza, “Mnataka niwafanyie nini?”
And Jesus stopped, and called them, and said, What would ye have me do for you?
33 Wakamwambia, “Bwana kwamba macho yetu yafumbuliwe.”
They say to him, Lord, to open our eyes.
34 Basi Yesu, akiwa amevutwa na huruma, akayagusa macho yao, mara hiyo, wakapokea uwezo wa kuona na wakamfuata.
Then Jesus, moved with compassion, touched their eyes; and they immediately received sight, and followed him.

< Mathayo 20 >