< Mathayo 20 >

1 Kwa maana ufalme wa mbinguni unafanana na mmliki wa shamba, aliyeamka asubuhi na mapema ili kuajiri wafanyakazi katika shamba lake la mizabibu.
“For the kingdom of heaven is like a landowner who went out early in the morning to hire workers for his vineyard.
2 Baada ya kuwa amekubaliana na wafanyakazi dinari moja kwa kutwa, aliwatuma kwenda katika shamba lake la mizabibu.
He agreed to pay them a denarius for the day and sent them into his vineyard.
3 Alienda tena baada ya masaa matatu hivi na aliona wafanyakazi wengine wakiwa wamesimama bila kazi katika eneo la soko.
About the third hour he went out and saw others standing in the marketplace doing nothing.
4 Akawaambia, 'Ninyi pia, nendeni katika shamba la mizabibu, na chochote kilicho halali nitawapa.' Hivyo wakaenda kufanya kazi.
‘You also go into my vineyard,’ he said, ‘and I will pay you whatever is right.’
5 Akaenda tena baada ya masaa sita na tena katika saa ya tisa, na alifanya hivyo hivyo.
So they went. He went out again about the sixth hour and the ninth hour and did the same thing.
6 Mara nyingine tena mnamo saa kumi na moja, alienda na kuwakuta watu wengine wamesimama bila kazi. Aliwaambia, 'kwanini mmesimama hapa bila kazi yoyote kwa siku nzima?
About the eleventh hour he went out and found still others standing around. ‘Why have you been standing here all day long doing nothing?’ he asked.
7 Wakamwambia, kwasababu hakuna mtu yeyote aliyetuajiri. Akawaambia, 'Nanyi ninyi pia nendeni katika shamba la mizabibu.'
‘Because no one has hired us,’ they answered. So he told them, ‘You also go into my vineyard.’
8 Wakati wa jioni ulipofika, mwenye shamba la mizabibu alimwambia msimamizi wake, 'Waite wafanyakazi na uwalipe mishahara, kwa kuanza na wa mwisho hadi wa kwanza.'
When evening came, the owner of the vineyard said to his foreman, ‘Call the workers and pay them their wages, starting with the last ones hired and moving on to the first.’
9 Walipokuja wale walioajiriwa saa kumi na moja, kila mmoja wao alipokea dinari.
The workers who were hired about the eleventh hour came and each received a denarius.
10 Walipokuja wafanyakazi wa kwanza, walifikiri kuwa watapokea zaidi, lakini walipokea pia kila mmoja dinari moja kila mtu.
So when the original workers came, they assumed they would receive more. But each of them also received a denarius.
11 Baada ya kupokea malipo yao, walimlalamikia mmiliki wa shamba.
On receiving their pay, they began to grumble against the landowner.
12 Wakasema, 'Hawa wafanyakazi wa mwisho wametumia saa moja tu katika kufanya kazi, lakini umewalinganisha na sisi, sisi tumebeba mzigo kwa siku nzima na kuungua na joto.'
‘These men who were hired last worked only one hour,’ they said, ‘and you have made them equal to us who have borne the burden and the scorching heat of the day.’
13 Lakini mwenye shamba akajibu na kusema kwa mmoja wao, 'Rafiki, sikutenda jambo baya. Je! hatukukubaliana na mimi kwa dinari moja?
But he answered one of them, ‘Friend, I am not being unfair to you. Did you not agree with me on one denarius?
14 Pokea kile kilicho halali yako na uende zako. Ni furaha yangu kuwapa hawa wafanyakazi walioajiriwa mwisho sawa sawa na wewe.
Take your pay and go. I want to give this last man the same as I gave you.
15 Je! Si haki kwangu kufanya kile ninachotaka na mali zangu? Au jicho lako ni ovu kwa sababu mimi ni mwema?
Do I not have the right to do as I please with what is mine? Or are you envious because I am generous?’
16 Hivyo wa mwisho atakuwa kwanza na wa kwanza wa mwisho''
So the last will be first, and the first will be last.”
17 Yesu alipokuwa akipanda kwenda Yerusalem, aliwachukuwa wanafunzi wake kumi na mbili pembeni, na njiani akawaambia,
As Jesus was going up to Jerusalem, He took the twelve disciples aside and said,
18 ''Tazama tunaelekea Yerusalemu, na Mwana wa Adamu atatiwa katika mikono ya wakuu wa makuhani na waandishi. Watamhukumu kifo
“Look, we are going up to Jerusalem, and the Son of Man will be delivered over to the chief priests and scribes. They will condemn Him to death
19 na watamtoa kwa watu wa mataifa ili kumdhihaki, kumchapa na kumsulibisha. Lakini katika siku ya tatu atafufuka.''
and will deliver Him over to the Gentiles to be mocked and flogged and crucified. And on the third day He will be raised to life.”
20 Kisha mama wa wana wa Zebedayo alikuja kwa Yesu na wana wake. Alipiga magoti mbele yake na kumwomba kitu kutoka kwake.
Then the mother of Zebedee’s sons came to Jesus with her sons and knelt down to make a request of Him.
21 Yesu akamwambia, “Unataka nini?” Akamwambia, ''Amuru kuwa hawa wanangu wawili wakae, mmoja mkono wako wa kulia na mmoja mkono wako wa kushoto katika ufalme wako.''
“What do you want?” He inquired. She answered, “Declare that in Your kingdom one of these two sons of mine may sit at Your right hand, and the other at Your left.”
22 Lakini Yesu akajibu na kusema, “Haujui kile unachoomba. Je! Unaweza kukinywea kikombe ambacho nitakinywea?” wakamwambia, “Tunaweza.”
“You do not know what you are asking,” Jesus replied. “Can you drink the cup I am going to drink?” “We can,” the brothers answered.
23 Akawaambia, “Kikombe changu hakika mtakinywea. Lakini kukaa mkono wangu wa kulia na mkono wangu wa kushoto si jukumu langu kuwapa, lakini ni kwa wale ambao wamekwisha kuandaliwa na Baba yangu.”
“You will indeed drink My cup,” Jesus said. “But to sit at My right or left is not Mine to grant. These seats belong to those for whom My Father has prepared them.”
24 Wanafunzi wengine kumi waliposikia hivyo, wakahuzunishwa sana na wale ndugu wawili.
When the ten heard about this, they were indignant with the two brothers.
25 Lakini Yesu aliwaita mwenyewe na kuwaambia, “Mnafahamu ya kuwa watawala wa mataifa huwatiisha, na wakuu wao hutekeleza mamlaka juu yao.
But Jesus called them aside and said, “You know that the rulers of the Gentiles lord it over them, and their superiors exercise authority over them.
26 Lakini isiwe hivyo kwenu. Badala yake, yeyote atakayetaka kuwa mkubwa miongoni mwenu lazima awe mtumishi wenu.
It shall not be this way among you. Instead, whoever wants to become great among you must be your servant,
27 Na atakaye kuwa wa kwanza miongoni mwenu lazima awe mtumishi wenu.
and whoever wants to be first among you must be your slave—
28 Kama vile Mwana wa Adamu hakuja kutumikiwa, bali kutumika, na kutoa uhai wake kuwa ukombozi kwa wengi.”
just as the Son of Man did not come to be served, but to serve, and to give His life as a ransom for many.”
29 Wakati wakitoka Yeriko, umati mkubwa ulimfuata.
As they were leaving Jericho, a large crowd followed Him.
30 Na waliwaona vipofu wawili wameketi kando ya barabara. Waliposikia kuwa Yesu alikuwa anapita, walipaza sauti na kusema, “Bwana, Mwana wa Daudi, utuhurumie.”
And there were two blind men sitting beside the road. When they heard that Jesus was passing by, they cried out, “Lord, Son of David, have mercy on us!”
31 Lakini umati ukawakemea, na kuwaambia nyamazeni. Hata hivyo, wao wakapaza sauti zaidi na kusema, “Bwana, Mwana wa Daudi, utuhurumie.”
The crowd admonished them to be silent, but they cried out all the louder, “Lord, Son of David, have mercy on us!”
32 Kisha Yesu alisimama na aliwaita na kuwauliza, “Mnataka niwafanyie nini?”
Jesus stopped and called them. “What do you want Me to do for you?” He asked.
33 Wakamwambia, “Bwana kwamba macho yetu yafumbuliwe.”
“Lord,” they answered, “let our eyes be opened.”
34 Basi Yesu, akiwa amevutwa na huruma, akayagusa macho yao, mara hiyo, wakapokea uwezo wa kuona na wakamfuata.
Moved with compassion, Jesus touched their eyes, and at once they received their sight and followed Him.

< Mathayo 20 >