< Mathayo 19 >

1 Ilitokea wakati Yesu alipomaliza maneno hayo, akaondoka Galilaya, na akaenda mpakani mwa Yudea mbele ya mto Jordani.
And it came to pass when Jesus had finished these discourses, that he departed from Galilee, and came into the borders of Judea, beyond the Jordan.
2 Umati mkubwa ukamfuata, na akawaponya huko.
And many multitudes followed him; and he cured them there.
3 Mafarisayo wakamjia, wakamjaribu, wakamwambia, “Je ni halali kwa mtu kumwacha mke wake kwa sababu yoyote?”
And the Pharisees came to him to tempt him, and said to him: Is it lawful for a man to put away his wife for every cause?
4 Yesu akajibu na kusema, “Hamkusoma, kwamba yeye aliyewaumba mwanzo aliwaumba mume na mke?
He answered and said to them: Have you not read that the Creator, at the beginning, created them male and female,
5 Na tena akasema, 'Kwa sababu hiyo mwanaume atamwacha baba yake na mama yake na kuungana na mke wake, nao wawili watakuwa mwili mmoja?'
and said, For this cause shall a man leave his father and his mother, and shall cleave to his wife, and the two shall be one flesh?
6 Hivyo siyo wawili tena, bali mwili mmoja. Basi, kile alichokiunganisha Mungu, mtu yeyote asikitenganishe.”
So then, they are no longer two, but one flesh. Therefore, what God has joined together, let not man put asunder.
7 Wakamwambia, “Sasa kwa nini Musa alituamuru kutoa hati ya talaka na kumwacha?”
They said to him: Why, then, did Moses command us to give a bill of divorce and put her away?
8 Akawaambia, “Kwa ugumu wenu wa mioyo Musa aliwaruhusu kuwaacha wake zenu, lakini tangu mwanzo haikuwa hivyo.
He said to them: Moses, on account of the hardness of your hearts, permitted you to put away your wives; but from the beginning it was not so.
9 Nawaambieni, kwamba yeyote atayemwacha mke wake, isipokuwa kwa sababu ya uzinzi, na akamwoa mwingine, amezini. Na mwanaume atakayemwoa mke aliyeachwa amezini.”
But I say to you, That whoever puts away his wife, unless for lewdness, and marries another, commits adultery; and he that marries her that is put away, commits adultery.
10 Wanafunzi wakamwambia Yesu, “Kama ndivyo ilivyo kwa mume na mkewe, siyo vizuri kuoa.”
His disciples said to him: If the relation of man and wife be such, it is not good to marry.
11 Lakini Yesu akawaambia, “Si kila mtu anaweza kupokea mafundisho haya, bali ni kwa wale tu walioruhusiwa kupokea.
But he said to them: All can not accept this saying; only those to whom it is given.
12 Kwa vile wapo matowashi waliozaliwa tokea tumboni mwa mama zao. Na vilevile kuna matowashi waliofanywa na watu. Na kuna matowashi waliojifanya matowashi kwa ajili ya ufalme wa mbinguni. Awezaye kupokea mafundisho haya na ayapokee.”
For there are eunuchs that were born such from their mother’s womb; and there are eunuchs that have been made eunuchs by men; and there are eunuchs that have made themselves eunuchs for the sake of the kingdom of heaven. Let him accept it that is able to accept it.
13 Kisha akaletewa baadhi ya watoto wadogo ili awawekee mikono juu yao na kuomba, lakini wanafunzi wake wakawakemea.
Then little children were brought to him, that he might lay his hands on them and pray. And the disciples rebuked them.
14 Bali Yesu akasema, “Waruhusuni watoto wadogo, wala msiwakataze kuja kwangu, kwa maana ufalme wa mbinguni ni wa watu kama wao.
But Jesus said: Let the little children come to me, and forbid them not: for of such is the kingdom of heaven.
15 Naye akaweka mikono yake juu yao, na kisha akaondoka pale.
And he laid his hands on them, and departed from that place.
16 Tazama mtu mmoja akaja kwa Yesu na kusema, “Mwalimu, ni kitu gani kizuri ninachotakiwa kufanya ili nipate kuwa na uzima wa milele?” (aiōnios g166)
And behold, one came and said to him: Good teacher, what good thing must I do that I may have eternal life? He said to him: (aiōnios g166)
17 Yesu akamwambia, “Kwa nini unaniuliza ni kitu gani kizuri? Kuna mmoja tu aliye mwema, lakini kama ukitaka kupata uzima, shika sheria za Mungu.”
Why do you call me good? There is none good but one, that is God. But if you desire to enter into life, keep the commandments.
18 Yule mtu akamwuliza, “Ni sheria zipi?” Yesu akasema, “Usiue, usizini, usiibe, usishuhudie uongo,
He said to him: Which? Jesus replied: You shall not kill; You shall not commit adultery; You shall not steal; You shall not give false testimony;
19 waheshimu baba yako na mama yako, na mpende jirani yako kama nafsi yako.”
Honor your father and your mother; and, You shall love your neighbor as yourself.
20 Mtu yule akamwambia, “Mambo yote hayo nimeyatii. Bado ninahitaji nini?
The young man said to him: All these have I kept from my youth, what do I lack?
21 “Yesu akamwambia, “Kama ukitaka kuwa mkamilifu, nenda, ukauze ulivyo navyo, na uwape maskini, na utakuwa na hazina mbinguni. Kisha njoo unifuate.”
Jesus said to him: If you would be perfect, go, sell your possessions, and give to the poor, and you shall have treasure in heaven; and come, follow me.
22 Lakini kijana yule aliposikia yale Yesu aliyomwambia, akaondoka kwa huzuni, kwa sababu alikuwa na amemiliki mali nyingi.
When the young man heard that saying, he went away grieved; for he had great possessions.
23 Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kweli nawaambieni, ni vigumu kwa mtu tajiri kuingia katika ufalme wa mbinguni.
Jesus said to his disciples: Verily I say to you, A rich man will with difficulty enter into the kingdom of heaven.
24 Tena nawaambieni, ni rahisi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano, kuliko kwa mtu tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.”
And again I say to you: It is easier for a camel to go through the eye of a needle, than for a rich man to enter into the kingdom of God.
25 Wanafunzi waliposikia hivyo, wakashangaa sana na kusema, “Ni yupi basi atakayeokoka?”
When the disciples heard it, they were greatly amazed, and said: Who, then, can be saved?
26 Yesu akawatazama na kusema, “Kwa wanadamu hilo haliwezekani, lakini kwa Mungu yote yanawezekana.”
But Jesus looked on them, and said to them: With men, this is impossible; but with God, all things are possible.
27 Kisha Petro akamjibu na kumwambia, “Tazama, tumeacha vyote na kukufuata wewe. Ni kitu gani tutakachopata?”
Then Peter answered and said to him: Behold, we have left all and followed thee; what, then, shall we have?
28 Yesu akawaambia, “Kweli nawaambieni, yeye aliyenifuata mimi, katika uzao mpya wakati Mwana wa Adam atakapoketi katika kiti cha enzi cha utukufu wake, ninyi pia mtaketi juu ya viti kumi na viwili vya enzi, kuwahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.
Jesus said to them: Verily I say to you, That, in the restoration, when the Son of man shall sit on his glorious throne, you also who have followed me shall sit on twelve thrones, judging the twelve tribes of Israel.
29 Kila mmoja wenu aliyeacha nyumba, kaka, dada, baba, mama, watoto, au shamba kwa ajili ya jina langu, atapokea mara mia na kuurithi uzima wa milele. (aiōnios g166)
And every one that has left houses, or brothers, or sisters, or father, or mother, or wife, or children, or lands, for my name’s sake, shall receive a hundred-fold, and shall inherit eternal life. (aiōnios g166)
30 Lakini wengi walio wa kwanza sasa, watakuwa wa mwisho, na walio wa mwisho watakuwa wa kwanza.
But many that are first shall be last; and the last first.

< Mathayo 19 >