< Mathayo 18 >
1 Muda huo huo wanafunzi wakaja kwa Yesu na kumwambia, “Ni nani aliye mkubwa katika ufalme wa mbinguni?”
At the same time came the disciples unto Jesus, saying, Who is the greatest in the kingdom of heaven?
2 Yesu akamwita mtoto mdogo, akamweka katikati yao,
And Jesus called a little child unto him, and set him in the midst of them,
3 na kusema, “Kweli nawaambieni, msipotubu na kuwa kama watoto wadogo hamtaweza kuingia katika ufalme wa Mungu.
And said, Verily I say unto you, Except all of you be converted, and become as little children, all of you shall not enter into the kingdom of heaven.
4 Hivyo yeyote ajishushaye kama mtoto mdogo, mtu kama huyo ni mkuu katika ufalme wa mbinguni.
Whosoever therefore shall humble himself as this little child, the same is greatest in the kingdom of heaven.
5 Na yeyote ampokeaye mtoto mdogo kwa jina langu anipokea mimi.
And whoso shall receive one such little child in my name receives me.
6 Lakini yeyote asababishaye mmoja kati ya wadogo hawa wanaoniamini kuasi, itakuwa vizuri kwa mtu huyo jiwe kuu la kusagia likafungwa shingoni mwake, na kuzamishwa kilindini mwa bahari.
But whoso shall offend one of these little ones which believe in me, it were better for him that a millstone were hanged about his neck, and that he were drowned in the depth of the sea.
7 Ole kwa dunia kwa sababu ya wakati wa kukwazwa! kwa kuwa haina budi kwa nyakati hizo kuja, lakini ole kwake kwa mtu yule nyakati hizo zitakuja kwa ajili yake!
Woe unto the world because of offences! for it must essentially be that offences come; but woe to that man by whom the offence comes!
8 kama mkono wako au mguu wako ukikusababishia kukwazika, ukate na uutupe mbali na wewe. Ni vizuri zaidi kwako wewe kuingia kwenye uzima ukiwa bila mkono au kilema, kuliko kutupwa kwenye moto wa milele ukiwa na mikono yote au miguu yote. (aiōnios )
Wherefore if your hand or your foot offend you, cut them off, and cast them from you: it is better for you to enter into life halt or physically disabled, rather than having two hands or two feet to be cast into everlasting fire. (aiōnios )
9 Kama jicho lako likikukwaza, uling`oe na ulitupe mbali na wewe. Ni vizuri zaidi kwako wewe uingie kwenye uzima na jicho moja, kuliko kutupwa kwenye moto wa milele ukiwa na macho yote. (Geenna )
And if your eye offend you, pluck it out, and cast it from you: it is better for you to enter into life with one eye, rather than having two eyes to be cast into hell fire. (Geenna )
10 Tazameni kwamba msije mkamdharau mmoja wa wadogo hawa. Kwa maana nawambieni kuwa mbinguni kuna malaika wao siku zote wakiutazama uso wa Baba yangu aliye mbinguni.
Take heed that all of you despise not one of these little ones; for I say unto you, That in heaven their angels do always behold the face of my Father which is in heaven.
11 (Zingatia: Maneno yanayoonekana kama ya msitari wa 11, “Kwa kuwa Mwana wa Adamu alikuja kuokoa kile kilichokuwa kimepotea” hayakuonekana katika nakala bora za kale).
For the Son of man has come to save that which was lost.
12 Mnafikiri nini? Ikiwa mtu ana kondoo mia moja, na mmoja wao akapotea, je hatawaacha tisini na tisa ya mlimani na kwenda kumtafuta mmoja aliyepotea?
How think all of you? if a man have an hundred sheep, and one of them be gone astray, does he not leave the ninety and nine, and goes into the mountains, and seeks that which is gone astray?
13 Na akiisha kumpata, kweli nawaambieni, anamfurahia kuliko wale tisini na tisa wasiopotea.
And if so be that he find it, verily I say unto you, he rejoices more of that sheep, than of the ninety and nine which went not astray.
14 Vivyo hivyo, siyo mapenzi ya Baba yenu wa mbinguni kuwa mmoja wa wadogo hawa aangamie.
Even so it is not the will of your Father which is in heaven, that one of these little ones should perish.
15 Kama ndugu yako akikukosea, nenda, kamwonyeshe dosari iliyopo kati yako na yeye akiwa pekee yake. Kama akikusikiliza, utakuwa umemrejesha ndugu yako.
Moreover if your brother shall trespass against you, go and tell him his fault between you and him alone: if he shall hear you, you have gained your brother.
16 Lakini kama hatakusikiliza, mchukue ndugu mmoja au wawili zaidi pamoja nawe, kwa kuwa kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu kila neno linaweza kuthibitishwa.
But if he will not hear you, then take with you one or two more, that in the mouth of two or three witnesses every word (rhema) may be established.
17 Na kama akipuuza kuwasikiliza, liambie kanisa jambo hilo, kama akipuuza vilevile kulisikiliza kanisa, basi na awe kama mtu wa mataifa na mtoza ushuru.
And if he shall neglect to hear them, tell it unto the church: but if he neglect to hear the church, let him be unto you as an heathen man and a publican.
18 Kweli nawaambieni, chochote kile mtakachokifunga duniani na mbinguni kitafungwa. na chochote mtakachokifungua duniani na mbinguni kitafunguliwa.
Verily I say unto you, Whatsoever all of you shall bind on earth shall be bound in heaven: and whatsoever all of you shall loose on earth shall be loosed in heaven.
19 Tena nawaambieni kwamba kama watu wawili kati yenu wakikubaliana juu ya jambo lolote duniani waliombalo, hilo Baba yangu wa mbinguni atalifanya.
Again I say unto you, That if two of you shall agree on earth as concerning any thing that they shall ask, it shall be done for them of my Father which is in heaven.
20 Kwa kuwa wawili au watatu wakikusanyika pamoja kwa jina langu, Mimi niko katikati yao.
For where two or three are gathered together in my name, there am I in the midst of them.
21 Tena Petro akaja na kumwambia Yesu, “Bwana, ni mara ngapi ndugu yangu akinikosea nami nimsamehe? Hata mara saba?”
Then came Peter to him, and said, Lord, how often shall my brother sin against me, and I forgive him? till seven times?
22 Yesu akamwambia, “Sikuambii mara saba, lakini hata sabini mara saba.
Jesus says unto him, I say not unto you, Until seven times: but, Until seventy times seven.
23 Kwa sababu hiyo ufalme wa mbinguni ni sawa na mfalme fulani aliyetaka kusahihisha hesabu kutoka kwa watumwa wake.
Therefore is the kingdom of heaven likened unto a certain king, which would take account (logos) of his servants.
24 Alipoanza kusahihisha hesabu, mtumwa moja akaletwa kwake ambaye alikuwa anamdai talanta elfu kumi.
And when he had begun to reckon, one was brought unto him, which owed him ten thousand talents.
25 Kwa kuwa hakuwa na njia ya kulipa, bwana wake aliagiza auzwe, mke wake pamoja na watoto wake na kila kitu alichokuwa nacho, na malipo yafanyike.
But forasmuch as he had not to pay, his lord commanded him to be sold, and his wife, and children, and all that he had, and payment to be made.
26 Hivyo mtumwa alianguka, akapiga magoti mbele yake, akisema, 'Bwana, uwe na uvumilivu pamoja nami, na nitakulipa kila kitu.'
The servant therefore fell down, and worshipped him, saying, Lord, have patience with me, and I will pay you all.
27 Hivyo bwana wa yule mtumwa, kwa kuwa alisukumwa sana na huruma, alimwachilia na kumsamehe deni hilo
Then the lord of that servant was moved with compassion, and loosed him, and forgave him the debt.
28 Lakini mtumwa yule alitoka na kumpata mmoja kati ya watumwa wenzake, aliyekuwa anamdai denari mia. Alimvuta, akamkaba kooni, na kumwambia, 'Nilipe kile ninachokudai.'
But the same servant went out, and found one of his fellow servants, which owed him an hundred pence: and he laid hands on him, and took him by the throat, saying, Pay me that you owe.
29 Lakini yule mtumwa mwenzake alianguka na kumsihi sana, akisema, 'Uwe na uvumilivu nami, na nitakulipa.'
And his fellow servant fell down at his feet, and besought him, saying, Have patience with me, and I will pay you all.
30 Lakini mtumwa yule wa kwanza alikataa. Badala yake, alienda na kumtupa gerezani, mpaka atakapo mlipa kile anachomdai.
And he would not: but went and cast him into prison, till he should pay the debt.
31 Na walipoona watumwa wenzake kile kilichotokea. Walisikitishwa sana. Walikuja na kumwambia bwana wao kila kitu kilichotokea.
So when his fellow servants saw what was done, they were very sorry, and came and told unto their lord all that was done.
32 Ndipo yule bwana wa mtumwa yule alimwita, na kumwambia, 'Ewe mtumwa mwovu, nilikusamehe wewe deni langu lote kwa sababu ulinisihi sana.
Then his lord, after that he had called him, said unto him, O you wicked servant, I forgave you all that debt, because you desired me:
33 Je! Haukutakiwa kuwa na huruma kwa mtumwa mwenzio, kama mimi nilivyokuhurumia wewe?
Should not you also have had compassion on your fellow servant, even as I had pity on you?
34 Bwana wake alikasirika na kumkabidhi kwa wale watesaji mpaka atakapolipa kiasi chote alichokuwa anadaiwa.
And his lord was angry, and delivered him to the tormentors, till he should pay all that was due unto him.
35 Hivyo ndivyo Baba yangu wa Mbinguni atakavyowafanyia, kama kila mmoja wenu hatamsamehe ndugu yake kutoka moyoni mwenu.”
So likewise shall my heavenly Father do also unto you, if all of you from your hearts forgive not every one his brother their trespasses.