< Mathayo 17 >
1 Siku sita baadaye Yesu aliwachukua pamoja naye Petro, na Yakobo, na Yohana nduguye, na akawachukua mpaka juu ya mlima mrefu wao wenyewe.
And after six days Jesus takes Peter, and James, and John his brother, and carries them up into an exceedingly high mountain privately.
2 Alibadilishwa mbele yao. Uso wake ukang'aa kama jua, na nguo zake zilionekana zenye kung'aa kama nuru.
And was transfigured before them, and His face shone like the sun, and His garments became white as the light.
3 Tazama, pale walitokea Musa na Eliya wakiongea naye.
And behold, Moses and Elijah appeared unto them, talking with Him.
4 Petro akajibu na kumwambia Yesu, “Bwana, ni vema kwetu sisi kuwepo mahali hapa. Kama ukitamani, nitajenga hapa vibanda vitatu - kimoja chako, na kimoja kwa ajili ya Musa, na kimoja kwa ajili ya Eliya.”
And Peter responding, said to Jesus, Lord, it is good for us to be here: it you will, let us make here three tabernacles; one for thee, and one for Moses, and one for Elijah.
5 Wakati anaongea, tazama wingu jeupe likawatia kivuli, na tazama, ikatokea sauti toka kwenye wingu, ikisema, “Huyu ni Mwanangu mpendwa ninayependezwa naye. Msikilizeni yeye.”
He still speaking, behold, a white cloud overshadowed them: and behold a voice out of the cloud, saying, This is my beloved Son, in whom I am delighted; hear ye Him.
6 Wanafunzi waliposikia hayo, wakaanguka kifudifudi na wakaogopa sana.
And the disciples, hearing, fell on their face, and feared exceedingly.
7 Kisha Yesu akaja akawagusa na kusema, “Inukeni wala msiogope.”
And Jesus came to them and touching them said, Arise, and fear not.
8 Nao wakainua nyuso zao juu lakini hawakumwona mtu isipokuwa Yesu pekee.
And lifting up their eyes, they saw no one, except Jesus only.
9 Na walipokuwa wakishuka mlimani, Yesu akawaagiza, akasema, “Msitoe habari ya maono hayo mpaka Mwana wa Adamu atakapofufuka kutoka katika wafu.”
And they coming down from the mountain, Jesus charged them, saying, Tell the vision to no one, until the Son of man may rise from the dead.
10 Wanafunzi wake wakamwuliza, wakisema, “Ni kwanini waandishi wanasema kuwa Eliya atakuja kwanza?
And His disciples asked Him, saying, Why then do the scribes say that it behooves Elijah to come first?
11 Yesu akawajibu na kusema, “Eliya atakuja kweli na atarudisha mambo yote.
And Jesus responding said to them, Elijah indeed comes, and will restore all things:
12 Lakini naawaambieni ninyi, Eliya amekwisha kuja, lakini hawakumtambua. Badala yake, walimfanyia mambo watakayo wao. Na hivyo ndivyo Mwana wa Adamu atakavyoteswa katika mikono yao.”
but I say unto you, that Elijah has already come, and they recognized Him not, but did unto Him so many things as they wished; thus the Son of man is also about to suffer by them.
13 Ndipo wanafunzi wakatambua kuwa alikuwa akiongea habari za Yohana Mbatizaji.
Then the disciples understood that He spoke to them concerning John the Baptist.
14 Walipofika katika umati wa watu, mtu mmoja alimwendea, akapiga magoti mbele zake, na kumwambia,
And they having come to the multitude, the man came to Him, worshiping Him on his knees,
15 “Bwana, umhurumie mwanangu, maana amekuwa na kifafa na kuteseka sana. Kwa kuwa mara nyingi huanguka motoni au kwenye maji.
and saying, Lord, have mercy on my son, because he is a lunatic and suffers terribly: for frequently he falls into the fire, and frequently into the water.
16 Nilimleta kwa wanafunzi wako, lakini hawakuweza kumponya.
And I brought him to thy disciples, and they were not able to heal him.
17 Yesu akajibu akisema, “Enyi Kizazi kisichoamini na kilichoharibika, nitakaa pamoja nanyi mpaka lini? Nitavumiliana nanyi hata lini? Mlete hapa kwangu.”
And Jesus responding said: O, faithless and perverse generation, how long shall I be with you? bring him hither to me.
18 Yesu alimkemea, na pepo akamtoka. Kijana aliponywa tangu saa ile.
And Jesus rebuked him, and the demon came out from him, and the child was healed from that hour.
19 Kisha wanafunzi wakamjia Yesu kwa siri na kumwuliza, “Kwanini hatukuweza kumfukuza?”
Then the disciples coming to Jesus privately, said, Wherefore were we not able to cast him out?
20 Yesu akawaambia, “Kwa sababu ya imani yenu ndogo. Kweli nawaambieni, kama mtakuwa na imani hata ndogo kama punje ya mbegu ya haradali, mtaweza kuuambia mlima huu, hama kutoka hapa uende kule, nao utahama na hakutakuwa na kitu chochote cha kushindikana kwenu.
and Jesus says to them, On account of your unbelief. For truly I say unto you, If you have faith as a grain of mustard seed, you will say to this mountain, Remove hence to yonder place; and it shall remove; and nothing shall be impossible to you.
21 (Zingatia: Maneno ya msitari wa 21 “Lakini, aina hii ya pepo haiwezekani kutoka, ila kwa maombi na Kufunga” hayaonekani katika nakala bora za kale).
22 Wakati wakiwa bado Galilaya, Yesu akawaambia Wanafunzi wake, “Mwana wa Adamu atatiwa mikononi mwa watu.
And they sojourning in Galilee, Jesus said to them, The Son of man is about to be betrayed into the hands of men.
23 Na watamwua, na siku ya tatu atafufuka.” Wanafunzi walihuzunika sana.
And they will kill Him; and He will rise the third day. And they were grieved exceedingly.
24 Nao walipofika Kapenaumu, watu wakusanyao kodi ya nusu shekeli wakamwendea Petro na kusema, “Je mwalimu wenu hulipa kodi ya nusu shekeli?”
And they having come into Capernaum, those receiving the double drachma came to Peter, and said, Does your teacher pay the double drachma?
25 Akasema, “Ndiyo” Lakini Petro alipoingia ndani ya nyumba, Yesu akaongea na Petro kwanza na kusema, “Unafikiria nini Simon? Wafalme wa dunia, hupokea kodi au ushuru kutoka nani? Kwa wale wanaowatawa kutoka kwa wageni?
He says, Yes. And when he came into the house, Jesus anticipated him, saying, What seems to you, Simon? from whom do the kings of the earth receive toll or tribute? from their own sons or aliens?
26 Na wakati Petro aliposema, “Kutoka kwa wageni” Yesu akamwambia, hivyo watawaliwa wameondolewa katika ulipaji.
And he saying from aliens, Jesus said to him, Then the sons are free.
27 Lakini tusije tukawafanya watoza ushuru wakatenda dhambi, nenda baharini, tupa ndoano, na umtwae yule samaki ajaye kwanza. Baada ya kuufungua mdomo wake, utakuta mle shekeli moja. Ichukue na uwape watoza ushuru kwa ajili yangu na wewe.
But in order that we may not offend them, going to the sea, cast in a hook, and take the first fish coming up; and opening its mouth, you will find a stater: having received it, give it to them for me and thee.