< Mathayo 17 >

1 Siku sita baadaye Yesu aliwachukua pamoja naye Petro, na Yakobo, na Yohana nduguye, na akawachukua mpaka juu ya mlima mrefu wao wenyewe.
Now after six days Jesus takes Peter, James and his brother John and leads them up on a high mountain, in private.
2 Alibadilishwa mbele yao. Uso wake ukang'aa kama jua, na nguo zake zilionekana zenye kung'aa kama nuru.
And He was transfigured before them and his face shone like the sun, while His clothes became as white as the light.
3 Tazama, pale walitokea Musa na Eliya wakiongea naye.
When wow, Moses and Elijah appeared to them, conversing with Him.
4 Petro akajibu na kumwambia Yesu, “Bwana, ni vema kwetu sisi kuwepo mahali hapa. Kama ukitamani, nitajenga hapa vibanda vitatu - kimoja chako, na kimoja kwa ajili ya Musa, na kimoja kwa ajili ya Eliya.”
Then Peter reacted and said to Jesus, “Lord, it is good for us to be here; if you wish, let us make three booths: one for you, one for Moses and one for Elijah.”
5 Wakati anaongea, tazama wingu jeupe likawatia kivuli, na tazama, ikatokea sauti toka kwenye wingu, ikisema, “Huyu ni Mwanangu mpendwa ninayependezwa naye. Msikilizeni yeye.”
While he was still speaking a brilliant cloud overshadowed them, and then, a Voice came out of the cloud saying: “This is my beloved Son in whom I am always well pleased. Hear Him!”
6 Wanafunzi waliposikia hayo, wakaanguka kifudifudi na wakaogopa sana.
As the disciples heard it they fell on their faces and were greatly afraid.
7 Kisha Yesu akaja akawagusa na kusema, “Inukeni wala msiogope.”
Then Jesus came and touched them and said, “Get up, don't be afraid.”
8 Nao wakainua nyuso zao juu lakini hawakumwona mtu isipokuwa Yesu pekee.
So lifting up their eyes they saw no one but Jesus only.
9 Na walipokuwa wakishuka mlimani, Yesu akawaagiza, akasema, “Msitoe habari ya maono hayo mpaka Mwana wa Adamu atakapofufuka kutoka katika wafu.”
As they were coming down from the mountain, Jesus commanded them saying, “Tell no one the vision until the Son of the Man is risen from the dead.”
10 Wanafunzi wake wakamwuliza, wakisema, “Ni kwanini waandishi wanasema kuwa Eliya atakuja kwanza?
So His disciples questioned Him saying, “Why then do the scribes say that Elijah must come first?”
11 Yesu akawajibu na kusema, “Eliya atakuja kweli na atarudisha mambo yote.
In answer Jesus said to them: “Elijah is indeed coming first, and he will restore all things.
12 Lakini naawaambieni ninyi, Eliya amekwisha kuja, lakini hawakumtambua. Badala yake, walimfanyia mambo watakayo wao. Na hivyo ndivyo Mwana wa Adamu atakavyoteswa katika mikono yao.”
But I say to you that ‘Elijah’ has come already, and they did not recognize him, but did to him whatever they wished. Thus also the Son of the Man is about to suffer at their hands.”
13 Ndipo wanafunzi wakatambua kuwa alikuwa akiongea habari za Yohana Mbatizaji.
Then the disciples understood that He spoke to them of John the Baptizer.
14 Walipofika katika umati wa watu, mtu mmoja alimwendea, akapiga magoti mbele zake, na kumwambia,
As they came to the crowd a man approached Him and kneeling to Him said:
15 “Bwana, umhurumie mwanangu, maana amekuwa na kifafa na kuteseka sana. Kwa kuwa mara nyingi huanguka motoni au kwenye maji.
“Lord, have mercy on my son, because he is moonstruck and suffers badly! For he often falls into the fire and often into the water.
16 Nilimleta kwa wanafunzi wako, lakini hawakuweza kumponya.
So I brought him to your disciples, but they could not cure him.”
17 Yesu akajibu akisema, “Enyi Kizazi kisichoamini na kilichoharibika, nitakaa pamoja nanyi mpaka lini? Nitavumiliana nanyi hata lini? Mlete hapa kwangu.”
Then in answer Jesus said: “O faithless and perverse generation, how long must I be with you? How long must I put up with you? Bring him here to me.”
18 Yesu alimkemea, na pepo akamtoka. Kijana aliponywa tangu saa ile.
And Jesus rebuked the demon and it came out of him, and the boy was healed from that very hour.
19 Kisha wanafunzi wakamjia Yesu kwa siri na kumwuliza, “Kwanini hatukuweza kumfukuza?”
Then the disciples came to Jesus privately and said, “Why were we not able to cast it out?”
20 Yesu akawaambia, “Kwa sababu ya imani yenu ndogo. Kweli nawaambieni, kama mtakuwa na imani hata ndogo kama punje ya mbegu ya haradali, mtaweza kuuambia mlima huu, hama kutoka hapa uende kule, nao utahama na hakutakuwa na kitu chochote cha kushindikana kwenu.
So Jesus said to them: “Because of your unbelief; for assuredly I say to you, if you have faith like a mustard seed has, you (ye) will say to this mountain, ‘Move from here to there,’ and it will move; and nothing will be impossible for you.
21 (Zingatia: Maneno ya msitari wa 21 “Lakini, aina hii ya pepo haiwezekani kutoka, ila kwa maombi na Kufunga” hayaonekani katika nakala bora za kale).
However, this class does not go out except by prayer and fasting.”
22 Wakati wakiwa bado Galilaya, Yesu akawaambia Wanafunzi wake, “Mwana wa Adamu atatiwa mikononi mwa watu.
While they were staying in Galilee Jesus said to them, “The Son of the Man is about to be betrayed into the hands of men,
23 Na watamwua, na siku ya tatu atafufuka.” Wanafunzi walihuzunika sana.
and they will kill Him, and on the third day He will be raised.” And they were seriously grieved.
24 Nao walipofika Kapenaumu, watu wakusanyao kodi ya nusu shekeli wakamwendea Petro na kusema, “Je mwalimu wenu hulipa kodi ya nusu shekeli?”
When they entered Capernaum those who collected the temple tax approached Peter and said, “Does your Teacher not pay the temple tax?”
25 Akasema, “Ndiyo” Lakini Petro alipoingia ndani ya nyumba, Yesu akaongea na Petro kwanza na kusema, “Unafikiria nini Simon? Wafalme wa dunia, hupokea kodi au ushuru kutoka nani? Kwa wale wanaowatawa kutoka kwa wageni?
He says, “Yes.” So when they entered the house Jesus anticipated him saying: “Simon, what do you think? From whom do the kings of the earth take customs or poll tax, from their sons or from strangers?”
26 Na wakati Petro aliposema, “Kutoka kwa wageni” Yesu akamwambia, hivyo watawaliwa wameondolewa katika ulipaji.
Peter says to Him, “From the strangers.” Jesus said to him: “Well then, the sons are free.
27 Lakini tusije tukawafanya watoza ushuru wakatenda dhambi, nenda baharini, tupa ndoano, na umtwae yule samaki ajaye kwanza. Baada ya kuufungua mdomo wake, utakuta mle shekeli moja. Ichukue na uwape watoza ushuru kwa ajili yangu na wewe.
But, lest we offend them, go to the sea, cast in a hook, and take the fish that comes up first. And opening its mouth you will find a ‘stater’ [a coin]; take that and give it to them for me and you.”

< Mathayo 17 >