< Mathayo 15 >
1 Ndipo Mafarisayo na waadishi walikuja kwa Yesu kutoka Yerusalemu. Na kusema,
Then some Pharisees and religious teachers from Jerusalem came to Jesus and asked him,
2 “Kwa nini wanafunzi wanayahalifu mapokeo ya wazee? Kwa kuwa hawanawi mikono yao wanapokuwa wanakula chakula.''
“Why do your disciples break the tradition of our forefathers by not washing their hands before they eat a meal?”
3 Yesu akawajibu na kuwaambia, “Nanyi kwa nini mnaihalifu sheria ya Bwana kwa ajili ya mapokeo yenu?
“Why do you break God's commandment because of your tradition?” Jesus replied.
4 Kwa kuwa Mungu alisema, 'Mheshimu baba yako na mama yako; na 'Asemaye uovu kwa baba yake na mama yake, hakika atakufa.'
“For God said, ‘Honor your father and mother,’ and ‘Those who curse their father or mother should be put to death.’
5 Lakini ninyi husema, 'Kila amwambiaye baba yake na mama yake, '“Kila msaada ambao angepata kutoka kwangu sasa ni zawadi kutoka kwa Mungu,'''
But you say that if someone tells their father or mother, ‘Whatever you might have expected to get from me is now a gift to God,’ then
6 “Mtu huyo hana haja ya kumuheshimu baba yake. Katika namna hii mmelitangua neno la Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu.
they don't have to honor their father. In this way you've annulled God's word for the sake of your tradition.
7 Enyi wanafiki, ni vema kama Isaya alivyo tabiri juu yenu aliposema,
You hypocrites! How well Isaiah described you when he prophesied:
8 'Watu hawa wananiheshimu mimi kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali nami.
‘These people say they honor me but in their minds they don't care about me.
9 Wananiabudu bure, kwa sababu wanafundisha mafundisho yaliyo maagizo ya wanadamu.”'
Their worship of me is pointless. What they teach are just man-made requirements.’”
10 Ndipo akawaita makutano na kuwaambia,” Sikilizeni na mfahamu
He called the crowd over and told them, “Listen, and understand this:
11 Hakuna kitu kiingiacho mdomoni mwa mtu na kumfanya najisi. Bali, kile kitokacho kinywani, hiki ndicho kimfanyacho mtu kuwa najisi.''
it's not what goes into you through your mouth that defiles you. It's what comes out of your mouth that defiles you.”
12 Ndipo wanafunzi wakamwendea na kusema na Yesu, “Je!, Unafahamu Mafarisayo walipolisikia lile neno walikwazika?”
Then Jesus' disciples came to him and said, “You do realize that the Pharisees were offended by what you said.”
13 Yesu aliwajibu na kusema, “Kila mmea ambao Baba yangu wa mbinguni hajaupanda utang'olewa.
“Every plant my heavenly Father didn't plant will be uprooted,” Jesus replied.
14 Waacheni pekee, wao ni viongozi vipofu. Kama mtu kipofu atamuongoza kipofu mwenzake, wote wawili wataanguka shimoni.”
“Forget about them—they are blind guides. If a blind man leads another blind man, then they'll both fall into a ditch.”
15 Petro akajibu na kumwambia Yesu,” Tuelezee mfano huu kwetu,
Then Peter asked, “Please tell us what you mean by this illustration.”
16 Yesu akajibu, ''Nanyi pia bado hamuelewi?
“Haven't you understood this yet?” replied Jesus.
17 Ninyi hamuoni kuwa kila kiendacho mdomoni hupitia tumboni na kwenda chooni?
“Don't you see that whatever goes in through the mouth then passes through the stomach, and then leaves the body as waste?
18 Lakini vitu vyote vitokavyo mdomoni hutoka ndani ya moyo. Ndivyo vitu vimtiavyo mtu unajisi.
But what comes out through the mouth comes from the mind, and that's what defiles you.
19 Kwa kuwa katika moyo hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati, wizi, ushuhuda wa uongo, na matusi.
For what comes from the mind are evil thoughts, murder, adultery, sexual immorality, theft, false witness, and blasphemy
20 Haya ndiyo mambo yamtiayo mtu unajisi. Lakini kula bila kunawa mikono hakumfanyi mtu kuwa najisi.”
and those are what defile you. Eating with unwashed hands doesn't defile you.”
21 Ndipo Yesu akatoka mahali pale na akajitenga kuelekea pande za miji ya Tiro na Sidoni.
Jesus left and went to the region of Tyre and Sidon.
22 Tazama akaja mwanamke Mkanani kutoka pande hizo. Akapaza sauti akisema, ''Nihurumie, Bwana, Mwana wa Daudi; binti yangu anateswa sana na pepo.''
A Canaanite woman from that area came, shouting out, “Lord, son of David! Please have mercy on me, because my daughter is suffering badly because she's possessed by a demon!”
23 Lakini Yesu hakumjibu neno. Wanafunzi wake wakaja wakimsihi, wakisema, ''Muondoe aende zake, maana anatupigia kelele.''
But Jesus didn't reply at all. His disciples came to him and told him, “Tell her to stop following us. All her shouting is really annoying!”
24 Yesu aliwajibu na kusema, Sikutumwa kwa mtu yeyoye isipokuwa kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.''
“I was sent only to the lost sheep of the house of Israel,” Jesus said to the woman.
25 Lakini alikuja na kuinama mbele yake, akisema, ''Bwana nisaidie.''
But the woman came and kneeled before him, and said, “Lord, please help me!”
26 Alimjibu na kusema, “Siyo vema kuchukua chakula cha watoto na kuwatupia mbwa,”
“It's not right to take the children's food and throw it to the dogs,” Jesus told her.
27 Akasema, “Ndiyo, Bwana, hata hivyo mbwa wadogo hula chakula kiagukacho mezani mwa Bwana wao.”
“Yes, Lord, but even dogs are allowed to eat crumbs that fall from their master's table,” she replied.
28 Ndipo Yesu akajibu na akisema “Mwanamke, imani yako ni kubwa. Na ifanyike kwako kama utakavyo.” Na binti yake alikuwa ameponywa katika wakati huo.
“You have great trust in me,” Jesus answered. “Your wish is granted!” And her daughter was healed immediately.
29 Yesu aliondoka mahali pale na kwenda karibu na bahari ya Galilaya. Kisha alienda juu ya mlima na kuketi huko.
Jesus returned, passing by the Sea of Galilee. He went into the mountains nearby where he sat down.
30 Kundi kubwa likaja kwake. Na kumletea viwete, vipofu, bubu, vilema na wengine wengi, waliokuwa wagonjwa. Waliwaweka katika miguu ya Yesu na akawaponya.
Huge crowds came to him, bringing those who were lame, blind, crippled, dumb, and many others who were sick. They laid them on the ground at his feet, and he healed them.
31 Nao umati wakashangaa walipoona mabubu wakiongea, na vilema wakifanywa wazima, viwete wakitembea, na vipofu wakiona. Walimsifu Mungu wa Israeli.
The crowd was astounded at what they saw happen: the deaf could speak, the crippled were healed, the lame could walk, and the blind could see. They praised the God of Israel.
32 Yesu akawaita wanafunzi wake na kusema, “Nimewaonea huruma umati, kwa sababu wamekuwa nami kwa siku tatu bila kula kitu chochote. Sitawaaga waende kwao bila kula, wasije wakazimia njiani.”
Jesus called his disciples over and told them, “I feel really sorry for all these people, because they've been with me now for three days, and they have nothing to eat. I don't want to send them away hungry, in case they faint on their way home.”
33 Wanafunzi wake wakamwambia, “Ni wapi tunaweza kupata mikate ya kutosha hapa nyikani kushibisha umati mkuwbwa hivi?”
“Where could we find enough bread here in this desert to feed such a huge crowd?” the disciples responded.
34 Yesu akawaambia, “Mna mikate mingapi?” Wakasema, “Saba, na samaki wadogo wachache.”
“How many loaves of bread do you have?” Jesus asked. “Seven, and a few small fish,” they replied.
35 Yesu akawaamuru umati uketi chini.
Jesus told the crowd to sit down on the ground.
36 Aliitwaa ile mikate saba na samaki, na baada ya kushukuru, akaimega na kuwapa wanafunzi. Wanafunzi wakawapa umati.
He took the seven loaves and the fish, and after blessing the food he broke it into pieces and gave it to the disciples, and the disciples gave it to the crowds.
37 Watu wote wakala na kutosheka. Na wakakusanya mabaki ya vipande vya chakula vilivyosalia vipande vipande, vilijaa vikapu saba.
Everybody ate until they were full, and then they collected the leftovers, filling seven baskets.
38 Wote waliokula walikuwa wanaume elfu nne bila wanawake na watoto.
Four thousand men ate the food, not counting women and children.
39 Kisha Yesu akauaga umati waende zao na akaingia ndani ya mashua na kwenda sehemu za Magadani.
Then he sent the crowds away, got into a boat, and went to the Magadan region.