< Mathayo 14 >

1 Kwa wakati huo, Herode alisikia habari juu ya Yesu.
In illo tempore audivit Herodes tetrarcha famam Iesu:
2 Akawaambia watumishi wake, “Huyu ni Yohana Mbatizaji amefufuka kutoka katika wafu. Kwa hiyo nguvu hizi zipo juu yake.”
et ait pueris suis: Hic est Ioannes Baptista: ipse surrexit a mortuis, et ideo virtutes operantur in eo.
3 Kwa kuwa Herode alikuwa amemkamata Yohana akamfunga na kumtupa gerezani kwa sababu ya Herodia, mke wa Filipo kaka yake.
Herodes enim tenuit Ioannem, et alligavit eum: et posuit in carcerem propter Herodiadem uxorem fratris sui.
4 Kwa kuwa Yohana alimwambia, “Si halali kumchukua yeye kuwa mke wake.”
Dicebat enim illi Ioannes: Non licet tibi habere eam.
5 Herode angemwua lakini aliwaogopa watu kwa sababu walimwona Yohana kuwa nabii.
Et volens illum occidere, timuit populum: quia sicut prophetam eum habebant.
6 Lakini wakati siku ya kuzaliwa Herode ilipofika binti wa Herodia alicheza katikati ya watu na kumpendeza Herode.
Die autem natalis Herodis saltavit filia Herodiadis in medio, et placuit Herodi.
7 Katika kujibu kili aliahidi kwa kiapo kwamba atampa chochote atakachoomba.
Unde cum iuramento pollicitus est ei dare quodcumque postulasset ab eo.
8 Baada ya kushauriwa na mama yake, alisema, “Nipe mimi hapa katika kombe kichwa cha Yohana Mbatizaji.”
At illa praemonita a matre sua, Da mihi, inquit, hic in disco caput Ioannis Baptistae.
9 Mfalme alikuwa na sikitiko kwa maombi ya binti, lakini kwa ajili ya kiapo chake, kwa sababu ya wote waliokuwa chakulani pamoja naye aliamuru kwamba inapaswa ifanyike.
Et contristatus est rex: propter iusiurandum autem, et eos, qui pariter recumbebant, iussit dari.
10 Alituma Yohana aletwe kutoka gerezani
Misitque et decollavit Ioannem in carcere.
11 ili akatwe kichwa chake na kikaletwa juu ya sinia na akapewa binti na akakipeleka kwa mama yake.
Et allatum est caput eius in disco, et datum est puellae, et attulit matri suae.
12 Kisha wanafunzi wake wakaja kuuchukua ule mwili na kuuzika, baada ya hili walienda kumwambia Yesu.
Et accedentes discipuli eius, tulerunt corpus eius, et sepelierunt illud: et venientes nunciaverunt Iesu.
13 Naye Yesu aliposika haya, akijatenga kutoka mahali pale akapanda ndani ya mashuka akaenda sehemu iliyotengwa. Wakati umati ulipo fahamu alikokuwa, walimfuata kwa miguu kutoka mijini.
Quod cum audisset Iesus, secessit inde in naviculam, in locum desertum seorsum: et cum audissent turbae, secutae sunt eum pedestres de civitatibus.
14 Kisha Yesu alikuja mbele yao akauona umati mkubwa. Akawaonea huruma na kuponya magonjwa yao.
Et exiens vidit turbam multam, et misertus est eis, et curavit languidos eorum.
15 Jioni ilipotimia, wanafunzi wakaja kwake na kusema, “Hii ni sehemu ya jangwa, na siku tayari imepita. Watawanyishe makutano ili waende vijijini wakanunue chakula kwa ajili yao.
Vespere autem facto, accesserunt ad eum discipuli eius, dicentes: Desertus est locus, et hora iam praeteriit: dimitte turbas, ut euntes in castella, emant sibi escas.
16 Lakini Yesu akawaambia, ''Hawana haja ya kwenda zao. Wapeni ninyi chakula”
Iesus autem dixit eis: Non habent necesse ire: date illis vos manducare.
17 Wakamwambia, ''Hapa tunayo mikate mitano na samaki wawili tu.”''
Responderunt ei: Non habemus hic nisi quinque panes, et duos pisces.
18 Yesu akasema, “Ileteni kwangu.”
Qui ait eis: Afferte mihi illos huc.
19 Kisha Yesu akauamuru umati kukaa chini ya nyasi. Akachukuwa mikate mitano na samaki wawili. Akatazama juu mbinguni, akabariki na kumega mikate akawapa wanafunzi. Wanafunzi wakaupatia umati.
Et cum iussisset turbam discumbere super foenum, acceptis quinque panibus, et duobus piscibus, aspiciens in caelum benedixit, et fregit, et dedit discipulis panes, discipuli autem dederunt turbis.
20 Wakala wote na kushiba. Kisha wakavikusanya vipande vyote vya chakula na kujaza vikapu kumi na mbili.
Et manducaverunt omnes, et saturati sunt. Et tulerunt reliquias, duodecim cophinos fragmentorum plenos.
21 Wale waliokula walikadiriwa kuwa wanaume elfu tano bila ya kusehabu wanawake na watoto.
Manducantium autem fuit numerus, quinque millia virorum, exceptis mulieribus, et parvulis.
22 Mara moja aliwaamuru wanafunzi waingie ndani ya mashua, wakati huo yeye akawaaga umati waende zao.
Et statim compulit Iesus discipulos ascendere in naviculam, et praecedere eum trans fretum, donec dimitteret turbas.
23 Baada ya kuwaaga umati kwenda zao, akapanda juu mlimani kuomba pekee yake. Wakati ilipokuwa jioni alikuwa huko pekee yake.
Et dimissa turba, ascendit in montem solus orare. Vespere autem facto solus erat ibi.
24 Lakini sasa mashua ilipokuwa katikati ya bahari ukiyumbayumba kwa sababu ya mawimbi, kwani upepo ulikuwa wa mpisho.
navicula autem in medio mari iactabatur fluctibus: erat enim contrarius ventus.
25 Katika usiku wa zamu ya nne Yesu aliwakaribia, akitembea juu ya maji.
Quarta enim vigilia noctis, venit ad eos ambulans supra mare.
26 Wakati wanafunzi wake walipomwona akiitembea juu ya bahari, walihofu na kusema, “Ni mzuka,'' na kupaaza sauti katika hali ya uoga.
Et videntes eum supra mare ambulantem, turbati sunt, dicentes: Quia phantasma est. Et prae timore clamaverunt.
27 Yesu akawaambia mara moja, akisema, “Jipeni moyo! ni mimi! msiogope.”
Statimque Iesus locutus est eis, dicens: Habete fiduciam: ego sum, nolite timere.
28 Petro alimjibu kwa kusema, “Bwana, kama ni wewe, niamuru nije kwako juu ya maji.''
Respondens autem Petrus dixit: Domine, si tu es, iube me ad te venire super aquas.
29 Yesu akasema, “Njoo.'' Hivyo Petro akatoka ndani ya mashua na akatembea juu ya maji kwenda kwa Yesu.
At ipse ait: veni. Et descendens Petrus de navicula, ambulabat super aquam ut veniret ad Iesum.
30 Lakini Petro alipoona mawimbi, aliogopa, na kuanza kuzama, chini, akaita sauti na kusema, “Bwana, niokoe!''
Videns vero ventum validum, timuit: et cum coepisset mergi, clamavit dicens: Domine, salvum me fac.
31 Haraka Yesu akanyoosha mkono wake akamnyanyua Petro, na kumwambia, “Wewe mwenye imani ndogo, kwa nini ulikuwa na mashaka?”
Et continuo Iesus extendens manum, apprehendit eum: et ait illi: Modicae fidei, quare dubitasti?
32 Ndipo Yesu na Petro walipoingia katika mashua, upepo ulikoma kuvuma.
Et cum ascendisset in naviculam, cessavit ventus.
33 Wanafunzi mashuani wakamwabudu Yesu na kusema, “Kweli wewe ni Mwana wa Mungu.”
Qui autem in navicula erant, venerunt, et adoraverunt eum, dicentes: Vere filius Dei es.
34 Na walipokwisha kuvuka, walifika katika nchi ya Genesareti.
Et cum transfretassent, venerunt in terram Genesar.
35 Na watu katika eneo lile walipomtambua Yesu, walituma ujumbe kila sehemu za kando, na kuleta kila aliyekuwa mgonjwa.
Et cum cognovissent eum viri loci illius, miserunt in universam regionem illam, et obtulerunt ei omnes male habentes:
36 Walimsihi kwamba waweze kugusha pindo la vazi lake, na wengi walioligusa waliponywa.
et rogabant eum ut vel fimbriam vestimenti eius tangerent. Et quicumque tetigerunt, salvi facti sunt.

< Mathayo 14 >