< Mathayo 14 >

1 Kwa wakati huo, Herode alisikia habari juu ya Yesu.
And at that time Herod the tetrarch heard the fame of Jesus,
2 Akawaambia watumishi wake, “Huyu ni Yohana Mbatizaji amefufuka kutoka katika wafu. Kwa hiyo nguvu hizi zipo juu yake.”
and he said to his servants, This is John the Baptist; he is risen from the dead; and therefore miracles are wrought in him.
3 Kwa kuwa Herode alikuwa amemkamata Yohana akamfunga na kumtupa gerezani kwa sababu ya Herodia, mke wa Filipo kaka yake.
For Herod having arrested John, bound him, and put him in prison, on account of Herodias the wife of his brother Philip.
4 Kwa kuwa Yohana alimwambia, “Si halali kumchukua yeye kuwa mke wake.”
For John said to him, It is not lawful for thee to have her.
5 Herode angemwua lakini aliwaogopa watu kwa sababu walimwona Yohana kuwa nabii.
And wishing to kill him, he feared the multitude, because they esteemed him as a prophet.
6 Lakini wakati siku ya kuzaliwa Herode ilipofika binti wa Herodia alicheza katikati ya watu na kumpendeza Herode.
Herod's birthday being celebrated, the daughter of Herodias danced in the midst, and pleased Herod;
7 Katika kujibu kili aliahidi kwa kiapo kwamba atampa chochote atakachoomba.
consequently with an oath he promised to give to her whatsoever she might ask.
8 Baada ya kushauriwa na mama yake, alisema, “Nipe mimi hapa katika kombe kichwa cha Yohana Mbatizaji.”
And being instigated by her mother, she says, Give me the head of John the Baptist here in a charger.
9 Mfalme alikuwa na sikitiko kwa maombi ya binti, lakini kwa ajili ya kiapo chake, kwa sababu ya wote waliokuwa chakulani pamoja naye aliamuru kwamba inapaswa ifanyike.
And the king was grieved; nevertheless on account of his oaths, and those who were sitting with him, he commanded it to be given.
10 Alituma Yohana aletwe kutoka gerezani
And sending, he beheaded John in prison;
11 ili akatwe kichwa chake na kikaletwa juu ya sinia na akapewa binti na akakipeleka kwa mama yake.
and his head was brought in a charger, and given to the damsel: and she brought it to her mother.
12 Kisha wanafunzi wake wakaja kuuchukua ule mwili na kuuzika, baada ya hili walienda kumwambia Yesu.
And His disciples, having come, took the body, and buried it; and having come they proclaimed it to Jesus.
13 Naye Yesu aliposika haya, akijatenga kutoka mahali pale akapanda ndani ya mashuka akaenda sehemu iliyotengwa. Wakati umati ulipo fahamu alikokuwa, walimfuata kwa miguu kutoka mijini.
And Jesus hearing, departed thence in a ship privately into a desert place. And the multitudes hearing, followed Him on foot from the cities.
14 Kisha Yesu alikuja mbele yao akauona umati mkubwa. Akawaonea huruma na kuponya magonjwa yao.
And Jesus having come out saw a great multitude; and was moved with compassion in their behalf, and healed their sick.
15 Jioni ilipotimia, wanafunzi wakaja kwake na kusema, “Hii ni sehemu ya jangwa, na siku tayari imepita. Watawanyishe makutano ili waende vijijini wakanunue chakula kwa ajili yao.
And it being evening, His disciples came to Him saying, It is a desert place, and the hour is already advanced; therefore send away the multitudes, that they having gone into the villages, may purchase for themselves victuals.
16 Lakini Yesu akawaambia, ''Hawana haja ya kwenda zao. Wapeni ninyi chakula”
And Jesus said to them, They have no need to go away; you give them to eat.
17 Wakamwambia, ''Hapa tunayo mikate mitano na samaki wawili tu.”''
And they say to Him, We have nothing here except five loaves and two fishes.
18 Yesu akasema, “Ileteni kwangu.”
And He said, Bring them hither to me.
19 Kisha Yesu akauamuru umati kukaa chini ya nyasi. Akachukuwa mikate mitano na samaki wawili. Akatazama juu mbinguni, akabariki na kumega mikate akawapa wanafunzi. Wanafunzi wakaupatia umati.
And commanding the multitudes to sit down on the grass; and taking the five loaves and the two fishes, looking up to heaven, He blessed them; and breaking, gave the bread to the disciples, and the disciples to the multitudes.
20 Wakala wote na kushiba. Kisha wakavikusanya vipande vyote vya chakula na kujaza vikapu kumi na mbili.
And all ate, and were filled: and they took up the remainder of the fragments twelve baskets full.
21 Wale waliokula walikadiriwa kuwa wanaume elfu tano bila ya kusehabu wanawake na watoto.
And the men eating were about five thousand, besides women and children.
22 Mara moja aliwaamuru wanafunzi waingie ndani ya mashua, wakati huo yeye akawaaga umati waende zao.
And Jesus immediately constrained His disciples to embark into the ship and go before Him to the other side, until he can send away the multitudes.
23 Baada ya kuwaaga umati kwenda zao, akapanda juu mlimani kuomba pekee yake. Wakati ilipokuwa jioni alikuwa huko pekee yake.
And having dismissed the multitudes He went up into the mountain alone, to pray. And it being evening He was there alone.
24 Lakini sasa mashua ilipokuwa katikati ya bahari ukiyumbayumba kwa sababu ya mawimbi, kwani upepo ulikuwa wa mpisho.
And the ship was already midsea, laboring by the waves; for the wind was contrary.
25 Katika usiku wa zamu ya nne Yesu aliwakaribia, akitembea juu ya maji.
And at the fourth watch of the night, He came to them, walking on the sea.
26 Wakati wanafunzi wake walipomwona akiitembea juu ya bahari, walihofu na kusema, “Ni mzuka,'' na kupaaza sauti katika hali ya uoga.
And the disciples seeing Him walking on the sea, were afrighted, saying, It is a specter; and they cried out from fear.
27 Yesu akawaambia mara moja, akisema, “Jipeni moyo! ni mimi! msiogope.”
And immediately Jesus spoke to them, saying, Be of good cheer; I am here; fear not.
28 Petro alimjibu kwa kusema, “Bwana, kama ni wewe, niamuru nije kwako juu ya maji.''
And Peter responding said, Lord, if thou art there, command me to come to thee on the waters.
29 Yesu akasema, “Njoo.'' Hivyo Petro akatoka ndani ya mashua na akatembea juu ya maji kwenda kwa Yesu.
And He said, Come. And Peter having come down from the ship, walked on the waters, and came toward Jesus.
30 Lakini Petro alipoona mawimbi, aliogopa, na kuanza kuzama, chini, akaita sauti na kusema, “Bwana, niokoe!''
And seeing the wind strong, became alarmed; and beginning to sink, he cried out, saying, Lord, save me.
31 Haraka Yesu akanyoosha mkono wake akamnyanyua Petro, na kumwambia, “Wewe mwenye imani ndogo, kwa nini ulikuwa na mashaka?”
And Jesus immediately reaching out His hand, received him, and says to him, O thou of little faith, wherefore didst thou doubt?
32 Ndipo Yesu na Petro walipoingia katika mashua, upepo ulikoma kuvuma.
And they having come into the ship, the wind ceased.
33 Wanafunzi mashuani wakamwabudu Yesu na kusema, “Kweli wewe ni Mwana wa Mungu.”
And those in the ship having come worshiped Him, saying, Truly thou art the Son of God.
34 Na walipokwisha kuvuka, walifika katika nchi ya Genesareti.
And crossing over, they came into the land of Gennesaret.
35 Na watu katika eneo lile walipomtambua Yesu, walituma ujumbe kila sehemu za kando, na kuleta kila aliyekuwa mgonjwa.
And the men of that place recognizing Him, sent into all the surrounding country and brought to Him all the sick;
36 Walimsihi kwamba waweze kugusha pindo la vazi lake, na wengi walioligusa waliponywa.
and they continued to intreat Him that they should only touch the hem of His garment: and so many as touched were thoroughly saved.

< Mathayo 14 >