< Mathayo 14 >
1 Kwa wakati huo, Herode alisikia habari juu ya Yesu.
At that time Herod the tetrarch heard the reports about Jesus
2 Akawaambia watumishi wake, “Huyu ni Yohana Mbatizaji amefufuka kutoka katika wafu. Kwa hiyo nguvu hizi zipo juu yake.”
and said to his servants, “This is John the Baptist; he has risen from the dead! That is why miraculous powers are at work in him.”
3 Kwa kuwa Herode alikuwa amemkamata Yohana akamfunga na kumtupa gerezani kwa sababu ya Herodia, mke wa Filipo kaka yake.
Now Herod had arrested John and bound him and put him in prison on account of Herodias, his brother Philip’s wife,
4 Kwa kuwa Yohana alimwambia, “Si halali kumchukua yeye kuwa mke wake.”
because John had been telling him, “It is not lawful for you to have her.”
5 Herode angemwua lakini aliwaogopa watu kwa sababu walimwona Yohana kuwa nabii.
Although Herod wanted to kill John, he was afraid of the people, because they regarded John as a prophet.
6 Lakini wakati siku ya kuzaliwa Herode ilipofika binti wa Herodia alicheza katikati ya watu na kumpendeza Herode.
On Herod’s birthday, however, the daughter of Herodias danced before them and pleased Herod
7 Katika kujibu kili aliahidi kwa kiapo kwamba atampa chochote atakachoomba.
so much that he promised with an oath to give to her whatever she asked.
8 Baada ya kushauriwa na mama yake, alisema, “Nipe mimi hapa katika kombe kichwa cha Yohana Mbatizaji.”
Prompted by her mother, she said, “Give me here on a platter the head of John the Baptist.”
9 Mfalme alikuwa na sikitiko kwa maombi ya binti, lakini kwa ajili ya kiapo chake, kwa sababu ya wote waliokuwa chakulani pamoja naye aliamuru kwamba inapaswa ifanyike.
The king was grieved, but because of his oaths and his guests, he ordered that her wish be granted
10 Alituma Yohana aletwe kutoka gerezani
and sent to have John beheaded in the prison.
11 ili akatwe kichwa chake na kikaletwa juu ya sinia na akapewa binti na akakipeleka kwa mama yake.
John’s head was brought in on a platter and presented to the girl, who carried it to her mother.
12 Kisha wanafunzi wake wakaja kuuchukua ule mwili na kuuzika, baada ya hili walienda kumwambia Yesu.
Then John’s disciples came and took his body and buried it. And they went and informed Jesus.
13 Naye Yesu aliposika haya, akijatenga kutoka mahali pale akapanda ndani ya mashuka akaenda sehemu iliyotengwa. Wakati umati ulipo fahamu alikokuwa, walimfuata kwa miguu kutoka mijini.
When Jesus heard about John, He withdrew by boat privately to a solitary place. But the crowds found out about it and followed Him on foot from the towns.
14 Kisha Yesu alikuja mbele yao akauona umati mkubwa. Akawaonea huruma na kuponya magonjwa yao.
When He stepped ashore and saw a large crowd, He had compassion on them and healed their sick.
15 Jioni ilipotimia, wanafunzi wakaja kwake na kusema, “Hii ni sehemu ya jangwa, na siku tayari imepita. Watawanyishe makutano ili waende vijijini wakanunue chakula kwa ajili yao.
When evening came, the disciples came to Him and said, “This is a desolate place, and the hour is already late. Dismiss the crowds so they can go to the villages and buy themselves some food.”
16 Lakini Yesu akawaambia, ''Hawana haja ya kwenda zao. Wapeni ninyi chakula”
“They do not need to go away,” Jesus replied. “You give them something to eat.”
17 Wakamwambia, ''Hapa tunayo mikate mitano na samaki wawili tu.”''
“We have here only five loaves of bread and two fish,” they answered.
18 Yesu akasema, “Ileteni kwangu.”
“Bring them here to Me,” Jesus said.
19 Kisha Yesu akauamuru umati kukaa chini ya nyasi. Akachukuwa mikate mitano na samaki wawili. Akatazama juu mbinguni, akabariki na kumega mikate akawapa wanafunzi. Wanafunzi wakaupatia umati.
And He directed the crowds to sit down on the grass. Taking the five loaves and the two fish and looking up to heaven, He spoke a blessing. Then He broke the loaves and gave them to the disciples, and the disciples gave them to the people.
20 Wakala wote na kushiba. Kisha wakavikusanya vipande vyote vya chakula na kujaza vikapu kumi na mbili.
They all ate and were satisfied, and the disciples picked up twelve basketfuls of broken pieces that were left over.
21 Wale waliokula walikadiriwa kuwa wanaume elfu tano bila ya kusehabu wanawake na watoto.
About five thousand men were fed, in addition to women and children.
22 Mara moja aliwaamuru wanafunzi waingie ndani ya mashua, wakati huo yeye akawaaga umati waende zao.
Immediately Jesus made the disciples get into the boat and go on ahead of Him to the other side, while He dismissed the crowds.
23 Baada ya kuwaaga umati kwenda zao, akapanda juu mlimani kuomba pekee yake. Wakati ilipokuwa jioni alikuwa huko pekee yake.
After He had sent them away, He went up on the mountain by Himself to pray. When evening came, He was there alone,
24 Lakini sasa mashua ilipokuwa katikati ya bahari ukiyumbayumba kwa sababu ya mawimbi, kwani upepo ulikuwa wa mpisho.
but the boat was already far from land, buffeted by the waves because the wind was against it.
25 Katika usiku wa zamu ya nne Yesu aliwakaribia, akitembea juu ya maji.
During the fourth watch of the night, Jesus went out to them, walking on the sea.
26 Wakati wanafunzi wake walipomwona akiitembea juu ya bahari, walihofu na kusema, “Ni mzuka,'' na kupaaza sauti katika hali ya uoga.
When the disciples saw Him walking on the sea, they were terrified. “It’s a ghost!” they said, and cried out in fear.
27 Yesu akawaambia mara moja, akisema, “Jipeni moyo! ni mimi! msiogope.”
But Jesus spoke up at once: “Take courage! It is I. Do not be afraid.”
28 Petro alimjibu kwa kusema, “Bwana, kama ni wewe, niamuru nije kwako juu ya maji.''
“Lord, if it is You,” Peter replied, “command me to come to You on the water.”
29 Yesu akasema, “Njoo.'' Hivyo Petro akatoka ndani ya mashua na akatembea juu ya maji kwenda kwa Yesu.
“Come,” said Jesus. Then Peter got down out of the boat, walked on the water, and came toward Jesus.
30 Lakini Petro alipoona mawimbi, aliogopa, na kuanza kuzama, chini, akaita sauti na kusema, “Bwana, niokoe!''
But when he saw the strength of the wind, he was afraid, and beginning to sink, cried out, “Lord, save me!”
31 Haraka Yesu akanyoosha mkono wake akamnyanyua Petro, na kumwambia, “Wewe mwenye imani ndogo, kwa nini ulikuwa na mashaka?”
Immediately Jesus reached out His hand and took hold of Peter. “You of little faith,” He said, “why did you doubt?”
32 Ndipo Yesu na Petro walipoingia katika mashua, upepo ulikoma kuvuma.
And when they had climbed back into the boat, the wind died down.
33 Wanafunzi mashuani wakamwabudu Yesu na kusema, “Kweli wewe ni Mwana wa Mungu.”
Then those who were in the boat worshiped Him, saying, “Truly You are the Son of God!”
34 Na walipokwisha kuvuka, walifika katika nchi ya Genesareti.
When they had crossed over, they landed at Gennesaret.
35 Na watu katika eneo lile walipomtambua Yesu, walituma ujumbe kila sehemu za kando, na kuleta kila aliyekuwa mgonjwa.
And when the men of that place recognized Jesus, they sent word to all the surrounding region. People brought all the sick to Him
36 Walimsihi kwamba waweze kugusha pindo la vazi lake, na wengi walioligusa waliponywa.
and begged Him just to let them touch the fringe of His cloak. And all who touched Him were healed.