< Mathayo 13 >

1 Katika siku hiyo Yesu aliondoka nyumbani na kukaa kando ya bahari.
That same day Jesus had left the house and was sitting on the shore of the Lake,
2 Umati mkubwa ulikusanyika kwa kumzunguka, aliingia ndani ya mtumbwi na kukaa ndani yake. Umati wote walisimama kando ya bahari.
when a vast multitude of people crowded round Him. He therefore went on board a boat and sat there, while all the people stood on the shore.
3 Kisha Yesu alisema maneno mengi kwa mifano, Alisema, “Tazama, mpanzi alienda kupanda.
He then spoke many things to them in figurative language. "The sower goes out," He said, "to sow.
4 Alipokuwa akipanda baadhi ya mbegu zilianguka kando ya njia na ndege walikuja wakazidonoa.
As he sows, some of the seed falls by the way-side, and the birds come and peck it up.
5 Mbegu zingine zilianguka juu ya mwamba, ambapo hazikupata udongo wa kutosha. Ghafla zilichipuka kwa sababu udongo haukuwa na kina.
Some falls on rocky ground, where it has but scanty soil. It quickly shows itself above ground, because it has no depth of earth;
6 Lakini jua lilipo chomoza zilichomwa kwa sababu hazikuwa na mizizi, na zilikauka.
but when the sun is risen, it is scorched by the heat, and through having no root it withers up.
7 Mbengu zingine zilianguka kati ya miti yenye miiba. Miti yenye miiba ilirefuka juu ikaisonga.
Some falls among the thorns; but the thorns spring up and stifle it.
8 Mbegu zingine zilianguka kwenye udongo mzuri na kuzaa mbegu, zingine mara mia moja zaidi, zingine sitini na zingine thelathini
But a portion falls upon good ground, and gives a return, some a hundred for one, some sixty, some thirty.
9 Aliye na masikio na asikie.
Listen, every one who has ears!"
10 Wanafunzi walikuja na kumwambia Yesu, “Kwa nini unazungumza na makutano kwa mifano?”
(And His disciples came and asked Him, "Why do you speak to them in figurative language?"
11 Yesu alijibu kuwaambia, “Mmepewa upendeleo wa kufahamu siri za ufalme wa mbinguni, bali kwao hawajapewa.
"Because," He replied, "while to you it is granted to know the secrets of the Kingdom of the Heavens, to them it is not.
12 Lakini yeyote aliyenacho, kwake yeye ataongezewa zaidi, na atapata faida kubwa. Ilasiye nacho hata kile alichonacho atanyang'anywa.
For whoever has, to him more shall be given, and he shall have abundance; but whoever has not, from him even what he has shall be taken away.
13 Hivyo naongea nao kwa mifano kwa sababu ingawa wanaona, wasione kweli. Na ingawa wanasikia wasisikie wala kufahamu.
I speak to them in figurative language for this reason, that while looking they do not see, and while hearing they neither hear nor understand.
14 Unabii wa Isaya umetimia kwao, ule usemao, “Msikiapo msikie, lakini kwa namna yoyote hamtaelewa; wakati mwonapo muweze kuona, lakini kwa namna yeyote ile msijue.
And in regard to them the prophecy of Isaiah is receiving signal fulfilment: "'You will hear and hear and by no means understand, and you will look and look and by no means see.
15 Na mioyo ya watu hawa imekuwa giza, ni vigumu kusikia, na wamefumba macho yao, ili wasiweze kuona kwa macho yao, au kusikia kwa masikio yao, au kufahamu kwa mioyo yao, hivyo wangenigeukia tena, na ningewaponya.'
For this people's mind is stupefied, their hearing has become dull, and their eyes they have closed; to prevent their ever seeing with their eyes, or hearing with their ears, or understanding with their minds, and turning back, so that I might heal them.'
16 Bali macho yenu yamebarikiwa, kwa kuwa yanaona, na masikio yenu kwa kuwa yanasikia.
"But as for you, blessed are your eyes, for they see, and your ears, for they hear.
17 Hakika nawaambia manabii wengi na watu wenye haki walikuwa na hamu ya kuyaona mambo yale myaonayo, na hawakuweza kuyaona. Walitamani kusikia mambo yale mnayosikia, hawakuyasikia.
For I solemnly tell you that many Prophets and holy men have longed to see the sights you see, and have not seen them, and to hear the words you hear, and have not heard them.
18 . Sasa sikilizeni mfano wa mpanzi.
"To you then I will explain the parable of the Sower.
19 Wakati yeyote asikiapo neno la ufalme na asilifahamu, ndipo mwovu huja na kukinyakua kilichokwisha kupandwa ndani ya moyo wake. Hii ni mbegu ile iliyopandwa kando ya njia.
When a man hears the Message concerning the Kingdom and does not understand it, the Evil one comes and catches away what has been sown in his heart. This is he who has received the seed by the road-side.
20 Yeye aliyepandwa katika miamba ni yule asikiaye neno na kulipokea haraka kwa furaha.
He who has received the seed on the rocky ground is the man who hears the Message and immediately receives it with joy.
21 Bado hana mizizi ndani yake, ila huvumilia kwa kitambo kifupi. Wakati matatizo au mateso yanapotokea kwa sababu ya neno hujikwaa ghafla.
It has struck no root, however, within him. He continues for a time, but when suffering comes, or persecution, because of the Message, he at once stumbles and falls.
22 Aliyepandwa kati ya miti ya miiba, huyu ni yule alisikiaye neno lakini masumbuko ya ulimwengu na udaganyifu wa utajiri hulisonga lile neno lisije likazaa matunda. (aiōn g165)
He who has received the seed among the thorns is the man who hears the Message, but the cares of the present age and the delusions of riches quite stifle the Message, and it becomes unfruitful. (aiōn g165)
23 Aliyepandwa kwenye udongo mzuri, huyu ni yule asikiaye neno na kulifahamu. Huyu ni yule azaaye matunda na kuendelea kuzaa moja zaidi ya mara mia, nyingine sitini, nyingine thelathini.''
But he who has received the seed on good ground is he who hears and understands. Such hearers give a return, and yield one a hundred for one, another sixty, another thirty.")
24 Yesu aliwapa mfano mwingine. Akisema, “Ufalme wa mbinguni unafananishwa na mtu aliye panda mbengu nzuri katika shamba lake
Another parable He put before them. "The Kingdom of the Heavens," He said, "may be compared to a man who has sown good seed in his field,
25 Lakini watu waliposinzia, adui wake akaja pia akapanda magugu katikati ya ngano kisha akaenda zake.
but during the night his enemy comes, and over the first seed he sows darnel among the wheat, and goes away.
26 Baadaye ngano ilipoota na kutoa mazao yake, ndipo magugu yalitokea pia.
But when the blade shoots up and the grain is formed, then appears the darnel also.
27 Na watumishi wa mwenye shamba walikuja wakamwambia, 'Bwana, hukupanda mbengu nzuri katika shamba lako? Imekuwaje sasa lina magugu?
"So the farmer's men come and ask him, "'Sir, was it not good seed that you sowed on your land? Where then does the darnel come from?'
28 Akawaambia, Adui ametenda hili.' Watumishi walimwambia, “Kwa hiyo unataka twende tukayang'oe?”
"'Some enemy has done this,' he said. "'Shall we go, and collect it?' the men inquire.
29 Mwenye shamba akisema, 'Hapana, wakati mnayang'oa magugu mtang'oa pamoja na ngano.
"'No,' he replied, 'for fear that while collecting the darnel you should at the same time root up the wheat with it.
30 Yaacheni yakue pamoja mpaka wakati wa mavuno. Wakati wa mavuno nitasema kwa wavunaji, 'Kwanza yang'oeri magugu na yafungeni matita matita na kuyachoma, lakini kusanyeni ngano katika ghala langu.''''
Leave both to grow together until the harvest, and at harvest-time I will direct the reapers, Collect the darnel first, and make it up into bundles to burn it, but bring all the wheat into my barn.'"
31 Kisha Yesu aliwatolea mfano mwingine. Akasema, “Ufalme wa mbinguni unafanana na mbegu ya haradali ambayo mtu aliichukua na kuipanda katika shamba lake.
Another parable He put before them. "The Kingdom of the Heavens," He said, "is like a mustard-seed, which a man takes and sows in his ground.
32 Mbegu hii kwa hakika ni ndogo kuliko mbegu zingine zote. Lakini imeapo huwa kubwa kuliko mimea yote ya bustani, huwa mti, kiasi kwamba ndege wa angani huja na kujenga viota katika matawi yake.”
It is the smallest of all seeds, and yet when full-grown it is larger than any herb and forms a tree, so that the birds come and build in its branches."
33 Akawaambia mfano mwingine tena.”Ufalme wa mbinguni ni kama chachu ile iliyo twaliwa na mwanamke na kuichanganya kwa vipimo vitatu kwa unga mpaka viumuke.
Another parable He spoke to them. "The Kingdom of the Heavens," He said, "is like yeast which a woman takes and buries in a bushel of flour, for it to work there till the whole mass has risen."
34 Hayo yote Yesu aliyasema kwenye umati kwa mifano. Na pasipo mifano hakusema chochote kwao.
All this Jesus spoke to the people in figurative language, and except in figurative language He spoke nothing to them,
35 Hii ilikuwa kwamba kile kilichokwisha semwa kupitia kwa nabii kiweze kutimia, pale aliposema, “Nitafumbua kinywa changu katika mifano. Nitasema mambo yale yaliyokuwa yamefichwa tangu misingi ya ulimwengu”.
in fulfilment of the saying of the Prophet, "I will open my mouth in figurative language, I will utter things kept hidden since the creation of all things."
36 Kisha Yesu aliwaacha makutano na kwenda nyumbani. Wanafunzi wake walimwendea na kusema, “Tufafanulie mfano wa magugu ya shambani.''
When He had dismissed the people and had returned to the house, His disciples came to Him with the request, "Explain to us the parable of the darnel sown in the field."
37 Yesu alijibu na kusema, “Apandae mbegu nzuri ni Mwana wa Adamu.
"The sower of the good seed," He replied, "is the Son of Man;
38 Shamba ni ulimwengu; na mbegu nzuri, hawa ni wana wa ufalme. Magugu ni wana wa yule mwovu, na adui aliye zipanda ni ibilisi.
the field is the world; the good seed--these are the sons of the Kingdom; the darnel, the sons of the Evil one.
39 Na mavuno ni mwisho wa ulimwengu, na wavunaji ni malaika. (aiōn g165)
The enemy who sows the darnel is the Devil; the harvest is the Close of the Age; the reapers are the angels. (aiōn g165)
40 Kama vile magugu yanavyo kusanywa na kuchomwa moto, hivyo ndivyo itakavyo kuwa mwisho wa ulimwengu. (aiōn g165)
As then the darnel is collected together and burnt up with fire, so will it be at the Close of the Age. (aiōn g165)
41 Mwana wa Adamu atatuma malaika wake, na kukusanya kutoka katika ufalme wake mambo yote yaliyosababisha dhambi na wale watendao maasi.
The Son of Man will commission His angels, and they will gather out of His Kingdom all causes of sin and all who violate His laws;
42 Watawatupa wote katika tanuru la moto, ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.
and these they will throw into the fiery furnace. There will be the weeping aloud and the gnashing of teeth.
43 Ndipo watu wenye haki watakapong'aa kama jua katika Ufalme wa Baba yao. Yeye aliye na masikio na sikie.
Then will the righteous shine out like the sun in their Father's Kingdom. Listen, every one who has ears!
44 Ufalme wa mbinguni ni kama hazina iliyofichwa shambani. Mtu akaiona na kuificha. Katika furaha yake akaenda kuuza vyote alivyokuwa navyo, na kulinunua shamba.
"The Kingdom of the Heavens is like treasure buried in the open country, which a man finds, but buries again, and, in his joy about it, goes and sells all he has and buys that piece of ground.
45 Tena, ufalme wa mbinguni ni kama mtu anayefanya biashara atafutaye lulu yenye thamani.
"Again the Kingdom of the Heavens is like a jewel merchant who is in quest of choice pearls.
46 Wakati alipoiona ile yenye thamani, alienda akauza kila kitu alichokuwa nacho na akainunua.
He finds one most costly pearl; he goes away; and though it costs all he has, he buys it.
47 Ufalme wa mbinguni ni kama nyavu iliyo ndani ya bahari, na kwamba hukusanya viumbe vya kila aina.
"Again the Kingdom of the Heavens is like a draw-net let down into the sea, which encloses fish of all sorts.
48 Ulipojaa wavuvi waliuvuta ufukweni. Kisha wakakaa chini wakakusanya vitu vyema ndani ya vyombo, lakini visivyo na thamani vilitupwa mbali.
When full, they haul it up on the beach, and sit down and collect the good fish in baskets, while the worthless they throw away.
49 Itakuwa namna hii katika mwisho wa dunia. Malaika watakuja na kuwatenga watu waovu kutoka miongoni mwa wenye haki. (aiōn g165)
So will it be at the Close of the Age. The angels will go forth and separate the wicked from among the righteous, (aiōn g165)
50 Na kuwatupa ndani ya tanuru ya moto, ambako kutakuwa na maombolezo na kusaga meno.
and will throw them into the fiery furnace. There will be the weeping aloud and the gnashing of teeth."
51 Mmefahamu mambo yote haya? Wanafunzi walimjibu, ''Ndiyo.''
"Have you understood all this?" He asked. "Yes," they said.
52 Kisha Yesu akawambia, ''Kila mwandishi ambaye amekuwa mwanafunzi wa ufalme anafanana na mwenye nyumba atoaye katika hazina yake vitu vipya na vya kale.''
"Therefore," He said, "remember that every Scribe well trained for the Kingdom of the Heavens is like a householder who brings out of his storehouse new things and old."
53 IkawaYesu alipomaliza mifano yote hiyo, akaondoka katika sehemu hiyo.
Jesus concluded this series of parables and then departed.
54 Kisha Yesu akafika katika mkoa wake na akawafundisha watu katika sinagogi. Matokeo yake ni kuwa walishangaa na kusema, “Ni wapi mtu huyu alipopata hekima hii na miujiza hii?
And He came into His own country and proceeded to teach in their synagogue, so that they were filled with astonishment and exclaimed, "Where did he obtain such wisdom, and these wondrous powers?
55 Mtu huyu siyo mwana wa seremala? Mariamu siyo mamaye? Na ndugu zake siyo Yakobo, Yusuph, Simoni na Yuda?
Is not this the carpenter's son? Is not his mother called Mary? And are not his brothers, James, Joseph, Simon and Judah?
56 Na dada zake tunao hapa petu? Basi mtu huyu ameyapata wapi haya yote?”.
And his sisters--are they not all living here among us? Where then did he get all this?"
57 Aliwachukiza. Lakini Yesu aliwambia, “Nabii hakosi kuwa na heshima isipokuwa kwao na katika nchi yao.
So they turned angrily away from Him. But Jesus said to them, "There is no prophet left without honour except in his own country and among his own family."
58 Na hakuweza kufanya miujiza mingi kwa sababu hawakuwa na imani naye.
And He performed but few mighty deeds there because of their want of faith.

< Mathayo 13 >