< Mathayo 13 >
1 Katika siku hiyo Yesu aliondoka nyumbani na kukaa kando ya bahari.
In (now *k*) the day that having gone forth Jesus (from *k*) [from] the house was sitting by the sea.
2 Umati mkubwa ulikusanyika kwa kumzunguka, aliingia ndani ya mtumbwi na kukaa ndani yake. Umati wote walisimama kando ya bahari.
And were gathered together to Him crowds great so that He into (*k*) a boat having climbed into to sit down, and all the crowd on the shore had stood.
3 Kisha Yesu alisema maneno mengi kwa mifano, Alisema, “Tazama, mpanzi alienda kupanda.
And He spoke to them many things in parables saying; Behold went out the [one] sowing to sow.
4 Alipokuwa akipanda baadhi ya mbegu zilianguka kando ya njia na ndege walikuja wakazidonoa.
And in the sowing of him some indeed fell along the road, and (having come *N(k)(o)*) the birds (and *ko*) devoured them.
5 Mbegu zingine zilianguka juu ya mwamba, ambapo hazikupata udongo wa kutosha. Ghafla zilichipuka kwa sababu udongo haukuwa na kina.
Other now fell upon the rocky places where not it was having soil much, and immediately it sprang up through not having depth of soil.
6 Lakini jua lilipo chomoza zilichomwa kwa sababu hazikuwa na mizizi, na zilikauka.
when [the] sun now having risen they were scorched, and through the not having root were dried up.
7 Mbengu zingine zilianguka kati ya miti yenye miiba. Miti yenye miiba ilirefuka juu ikaisonga.
Other now fell upon the thorns, and grew up the thorns and (choked *N(k)O*) them.
8 Mbegu zingine zilianguka kwenye udongo mzuri na kuzaa mbegu, zingine mara mia moja zaidi, zingine sitini na zingine thelathini
Other now fell upon the soil good and were yielding fruit, some indeed a hundredfold, some however sixty, some however thirty.
9 Aliye na masikio na asikie.
The [one] having ears (to hear *ko*) he should hear.
10 Wanafunzi walikuja na kumwambia Yesu, “Kwa nini unazungumza na makutano kwa mifano?”
And having come the disciples said to Him; Because of why in parables speak You to them?
11 Yesu alijibu kuwaambia, “Mmepewa upendeleo wa kufahamu siri za ufalme wa mbinguni, bali kwao hawajapewa.
And answering He said to them; Because to you it has been granted to know the mysteries of the kingdom of the heavens, to them however not it has been granted.
12 Lakini yeyote aliyenacho, kwake yeye ataongezewa zaidi, na atapata faida kubwa. Ilasiye nacho hata kile alichonacho atanyang'anywa.
Whoever for has, will be given to him and will be abundant [to him] whoever now not has, even what he has will be taken away from him.
13 Hivyo naongea nao kwa mifano kwa sababu ingawa wanaona, wasione kweli. Na ingawa wanasikia wasisikie wala kufahamu.
Because of this in parables to them I speak Because seeing not do they see and hearing not do they hear nor do they understand.
14 Unabii wa Isaya umetimia kwao, ule usemao, “Msikiapo msikie, lakini kwa namna yoyote hamtaelewa; wakati mwonapo muweze kuona, lakini kwa namna yeyote ile msijue.
And is fulfilled (concerning *k*) them the prophecy of Isaiah who is saying: In hearing you will hear and certainly not may understand, and looking you will look and certainly not may perceive.
15 Na mioyo ya watu hawa imekuwa giza, ni vigumu kusikia, na wamefumba macho yao, ili wasiweze kuona kwa macho yao, au kusikia kwa masikio yao, au kufahamu kwa mioyo yao, hivyo wangenigeukia tena, na ningewaponya.'
Has grown dull for the heart of the people this, and with the ears barely they have heard, and the eyes of them they have closed; otherwise otherwise they may see with the eyes and with the ears they may hear and with the heart they may understand and may return and (I will heal *N(k)O*) them.’
16 Bali macho yenu yamebarikiwa, kwa kuwa yanaona, na masikio yenu kwa kuwa yanasikia.
Of you however blessed [are] the eyes because they see and the ears of you because (they hear. *N(k)O*)
17 Hakika nawaambia manabii wengi na watu wenye haki walikuwa na hamu ya kuyaona mambo yale myaonayo, na hawakuweza kuyaona. Walitamani kusikia mambo yale mnayosikia, hawakuyasikia.
Amen for I say to you that many prophets and righteous [men] longed to see what you see, and not saw, and to hear what you hear, and not heard.
18 . Sasa sikilizeni mfano wa mpanzi.
You yourselves therefore do hear the parable of the [one] (having sown: *N(k)O*)
19 Wakati yeyote asikiapo neno la ufalme na asilifahamu, ndipo mwovu huja na kukinyakua kilichokwisha kupandwa ndani ya moyo wake. Hii ni mbegu ile iliyopandwa kando ya njia.
Everyone hearing the word of the kingdom and not understanding comes the evil one and snatches away that having been sown in the heart of him; This is the [one] on the path having been sown.
20 Yeye aliyepandwa katika miamba ni yule asikiaye neno na kulipokea haraka kwa furaha.
That which now upon the rocky places having been sown, this is the [one] the word hearing and immediately with joy receiving it.
21 Bado hana mizizi ndani yake, ila huvumilia kwa kitambo kifupi. Wakati matatizo au mateso yanapotokea kwa sababu ya neno hujikwaa ghafla.
no he has now root in himself but temporary is. when is coming however tribulation or persecution on account of the word immediately he falls away.
22 Aliyepandwa kati ya miti ya miiba, huyu ni yule alisikiaye neno lakini masumbuko ya ulimwengu na udaganyifu wa utajiri hulisonga lile neno lisije likazaa matunda. (aiōn )
That which now among the thorns having been sown, this is the [one] the word hearing, and the care of the age (this *ko*) and the deceit of riches choke the word, and unfruitful it becomes. (aiōn )
23 Aliyepandwa kwenye udongo mzuri, huyu ni yule asikiaye neno na kulifahamu. Huyu ni yule azaaye matunda na kuendelea kuzaa moja zaidi ya mara mia, nyingine sitini, nyingine thelathini.''
That however on the good (*k*) soil having been sown, this is the [one] the word hearing and understanding, who indeed brings forth fruit and produces — some indeed a hundredfold, some however sixty, some however thirty.
24 Yesu aliwapa mfano mwingine. Akisema, “Ufalme wa mbinguni unafananishwa na mtu aliye panda mbengu nzuri katika shamba lake
Another parable put He before them saying; Has become like the kingdom of the heavens a man (having sown *N(k)O*) good seed in the field of him.
25 Lakini watu waliposinzia, adui wake akaja pia akapanda magugu katikati ya ngano kisha akaenda zake.
In now the [time] to sleep the men came his enemy and (over-sowed *N(k)O*) weeds in [the] midst of the wheat and went away.
26 Baadaye ngano ilipoota na kutoa mazao yake, ndipo magugu yalitokea pia.
When now sprouted the plants and fruit produced, then appeared also the weeds.
27 Na watumishi wa mwenye shamba walikuja wakamwambia, 'Bwana, hukupanda mbengu nzuri katika shamba lako? Imekuwaje sasa lina magugu?
Having come to [him] now the servants of the master of the house said to him; Sir, surely good seed did you sow in your field? How then has it (the *k*) weeds?
28 Akawaambia, Adui ametenda hili.' Watumishi walimwambia, “Kwa hiyo unataka twende tukayang'oe?”
He then was saying to them; An enemy a man this did. And the servants (they say *N(k)O*) to him: Do you desire then [that] having gone forth (we shall gather *NK(o)*) them?
29 Mwenye shamba akisema, 'Hapana, wakati mnayang'oa magugu mtang'oa pamoja na ngano.
And (he says; *N(k)O*) No, lest when lest when gathering the weeds you may uproot together [with] them the wheat.
30 Yaacheni yakue pamoja mpaka wakati wa mavuno. Wakati wa mavuno nitasema kwa wavunaji, 'Kwanza yang'oeri magugu na yafungeni matita matita na kuyachoma, lakini kusanyeni ngano katika ghala langu.''''
do allow to grow together both (until *N(k)O*) the harvest; and in (the *k*) time of the harvest I will say to the harvesters; do gather first the weeds and do bind them into bundles in order to burn them; and the wheat (do gather together *NK(o)*) into the barn of mine.’
31 Kisha Yesu aliwatolea mfano mwingine. Akasema, “Ufalme wa mbinguni unafanana na mbegu ya haradali ambayo mtu aliichukua na kuipanda katika shamba lake.
Another parable put He before them saying; Like is the kingdom of the heavens to a grain of mustard, which having taken a man sowed in the field of him;
32 Mbegu hii kwa hakika ni ndogo kuliko mbegu zingine zote. Lakini imeapo huwa kubwa kuliko mimea yote ya bustani, huwa mti, kiasi kwamba ndege wa angani huja na kujenga viota katika matawi yake.”
which smallest indeed is of all the seeds, when however it may be grown, greater than the garden plants it is and becomes a tree so that to come the birds of the air and perching in the branches of it.
33 Akawaambia mfano mwingine tena.”Ufalme wa mbinguni ni kama chachu ile iliyo twaliwa na mwanamke na kuichanganya kwa vipimo vitatu kwa unga mpaka viumuke.
Another parable spoke He to them: Like is the kingdom of the heavens to leaven, which having taken a woman (hid *NK(o)*) in of flour measures three until of it was leavened all.
34 Hayo yote Yesu aliyasema kwenye umati kwa mifano. Na pasipo mifano hakusema chochote kwao.
These things all spoke Jesus in parables to the crowds and without a parable (no [thing] *N(k)O*) He was speaking to them,
35 Hii ilikuwa kwamba kile kilichokwisha semwa kupitia kwa nabii kiweze kutimia, pale aliposema, “Nitafumbua kinywa changu katika mifano. Nitasema mambo yale yaliyokuwa yamefichwa tangu misingi ya ulimwengu”.
so that may be fulfilled that having been spoken through the prophet saying; I will open in parables the mouth of Mine, I will utter [things] hidden from [the] foundation [of the] world.
36 Kisha Yesu aliwaacha makutano na kwenda nyumbani. Wanafunzi wake walimwendea na kusema, “Tufafanulie mfano wa magugu ya shambani.''
Then having dismissed the crowds He went into the house (Jesus. *k*) And came to Him the disciples of Him saying; (do explain *N(k)O*) to us the parable of the weeds of the field.
37 Yesu alijibu na kusema, “Apandae mbegu nzuri ni Mwana wa Adamu.
And answering He said (to them: *k*) The [One] sowing the good seed is the Son of Man;
38 Shamba ni ulimwengu; na mbegu nzuri, hawa ni wana wa ufalme. Magugu ni wana wa yule mwovu, na adui aliye zipanda ni ibilisi.
and the field is the world; and [the] good seed, these are the sons of the kingdom; and the weeds are the sons of the evil [one];
39 Na mavuno ni mwisho wa ulimwengu, na wavunaji ni malaika. (aiōn )
and the enemy which having sown them is the devil; and the harvest [the] consummation (of the *k*) age is; and the harvesters angels are. (aiōn )
40 Kama vile magugu yanavyo kusanywa na kuchomwa moto, hivyo ndivyo itakavyo kuwa mwisho wa ulimwengu. (aiōn )
As therefore is gathered the weeds and in fire (is burned up, *NK(o)*) thus it will be in the consummation of the age (this. *k*) (aiōn )
41 Mwana wa Adamu atatuma malaika wake, na kukusanya kutoka katika ufalme wake mambo yote yaliyosababisha dhambi na wale watendao maasi.
Will send forth the Son of Man the angels of Him, and they will gather out of the kingdom of Him all the causes of sin and those practicing lawlessness
42 Watawatupa wote katika tanuru la moto, ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.
and they will cast them into the furnace of the fire; there will be the weeping and the gnashing of teeth.
43 Ndipo watu wenye haki watakapong'aa kama jua katika Ufalme wa Baba yao. Yeye aliye na masikio na sikie.
Then the righteous will shine forth as the sun in the kingdom of the Father of them. The [one] having ears (to hear *ko*) he should hear.
44 Ufalme wa mbinguni ni kama hazina iliyofichwa shambani. Mtu akaiona na kuificha. Katika furaha yake akaenda kuuza vyote alivyokuwa navyo, na kulinunua shamba.
(again *k*) Like is the kingdom of the heavens to treasure hidden in the field, which having found a man hid. and for the joy of it goes and he sells all as much as he has and buys the field that.
45 Tena, ufalme wa mbinguni ni kama mtu anayefanya biashara atafutaye lulu yenye thamani.
Again like is the kingdom of the heavens to a man a merchant seeking fine pearls.
46 Wakati alipoiona ile yenye thamani, alienda akauza kila kitu alichokuwa nacho na akainunua.
(who *k*) having found (now *no*) one very precious pearl, having gone away he has sold all things as much as he was having and he bought it.
47 Ufalme wa mbinguni ni kama nyavu iliyo ndani ya bahari, na kwamba hukusanya viumbe vya kila aina.
Again like is the kingdom of the heavens to a dragnet having been cast into the sea and of every kind having gathered together,
48 Ulipojaa wavuvi waliuvuta ufukweni. Kisha wakakaa chini wakakusanya vitu vyema ndani ya vyombo, lakini visivyo na thamani vilitupwa mbali.
which when it was filled having drawn up on the shore and having sat down they collected the good into (vessels, *N(k)O*) the and bad out they cast.
49 Itakuwa namna hii katika mwisho wa dunia. Malaika watakuja na kuwatenga watu waovu kutoka miongoni mwa wenye haki. (aiōn )
Thus will it be in the consummation of the age; will go out the angels and will separate the evil from [the] midst of the righteous (aiōn )
50 Na kuwatupa ndani ya tanuru ya moto, ambako kutakuwa na maombolezo na kusaga meno.
and will cast them into the furnace of the fire; There will be the weeping and the gnashing of the teeth.
51 Mmefahamu mambo yote haya? Wanafunzi walimjibu, ''Ndiyo.''
(says to them Jesus *k*) Did you understand these things all? They say to Him; Yes (Lord. *k*)
52 Kisha Yesu akawambia, ''Kila mwandishi ambaye amekuwa mwanafunzi wa ufalme anafanana na mwenye nyumba atoaye katika hazina yake vitu vipya na vya kale.''
He then said to them; Because of this every scribe having been discipled (into *k*) ([in] the kingdom *N(k)O*) of the heavens like is to a man a master of a house who puts forth out of the treasure of him [things] new and old.
53 IkawaYesu alipomaliza mifano yote hiyo, akaondoka katika sehemu hiyo.
And it came to pass when finished Jesus parables these, He withdrew from there;
54 Kisha Yesu akafika katika mkoa wake na akawafundisha watu katika sinagogi. Matokeo yake ni kuwa walishangaa na kusema, “Ni wapi mtu huyu alipopata hekima hii na miujiza hii?
And having come into the region of Him He was teaching them in the synagogue of them so that to be astonished they and to say: From where [came] to this [man] wisdom this and the miraculous powers?
55 Mtu huyu siyo mwana wa seremala? Mariamu siyo mamaye? Na ndugu zake siyo Yakobo, Yusuph, Simoni na Yuda?
Surely this is the of the carpenter Son? (Surely *N(k)O*) the mother of Him is named Mary? And the brothers of Him James and (Joseph *N(k)O*) and Simon and Judas?
56 Na dada zake tunao hapa petu? Basi mtu huyu ameyapata wapi haya yote?”.
And the sisters of Him surely all with us are? From where then to this [man] these things all?
57 Aliwachukiza. Lakini Yesu aliwambia, “Nabii hakosi kuwa na heshima isipokuwa kwao na katika nchi yao.
And they were offended at Him. But Jesus said to them; Not is a prophet without Honor only except in the hometown (of him *k*) and in the household of him.
58 Na hakuweza kufanya miujiza mingi kwa sababu hawakuwa na imani naye.
And not He did there miracles many because of the unbelief of them.