< Mathayo 13 >

1 Katika siku hiyo Yesu aliondoka nyumbani na kukaa kando ya bahari.
The same day Jesus went out of the house, and sat by the shore of the lake;
2 Umati mkubwa ulikusanyika kwa kumzunguka, aliingia ndani ya mtumbwi na kukaa ndani yake. Umati wote walisimama kando ya bahari.
and great multitudes were gathered together to him, so that he went into a boat, and sat down; and all the multitude stood on the beach.
3 Kisha Yesu alisema maneno mengi kwa mifano, Alisema, “Tazama, mpanzi alienda kupanda.
And he spoke many things to them in parables, saying, Behold, a sower went forth to sow.
4 Alipokuwa akipanda baadhi ya mbegu zilianguka kando ya njia na ndege walikuja wakazidonoa.
And as he sowed, some seeds fell by the wayside; and the birds came and devoured them.
5 Mbegu zingine zilianguka juu ya mwamba, ambapo hazikupata udongo wa kutosha. Ghafla zilichipuka kwa sababu udongo haukuwa na kina.
And others fell upon rocky places, where they had not much earth; and they sprung up immediately, because they had no depth of earth.
6 Lakini jua lilipo chomoza zilichomwa kwa sababu hazikuwa na mizizi, na zilikauka.
But when the sun was up, they were scorched; and because they had no root, they withered away.
7 Mbengu zingine zilianguka kati ya miti yenye miiba. Miti yenye miiba ilirefuka juu ikaisonga.
And others fell among thorns; and the thorns grew up, and choked them.
8 Mbegu zingine zilianguka kwenye udongo mzuri na kuzaa mbegu, zingine mara mia moja zaidi, zingine sitini na zingine thelathini
And others fell upon good ground; and yielded fruit, some a hundred fold, some Sixty, some thirty fold.
9 Aliye na masikio na asikie.
He that hath ears, let him hear.
10 Wanafunzi walikuja na kumwambia Yesu, “Kwa nini unazungumza na makutano kwa mifano?”
And the disciples came and said to him, Why dost thou speak to them in parables?
11 Yesu alijibu kuwaambia, “Mmepewa upendeleo wa kufahamu siri za ufalme wa mbinguni, bali kwao hawajapewa.
He answered and said, Because to you it hath been given to know the mysteries of the kingdom of heaven; but to them it hath not been given.
12 Lakini yeyote aliyenacho, kwake yeye ataongezewa zaidi, na atapata faida kubwa. Ilasiye nacho hata kile alichonacho atanyang'anywa.
For whoever hath, to him will be given, and he will have abundance; but whoever hath not, from him will be taken away even what he hath.
13 Hivyo naongea nao kwa mifano kwa sababu ingawa wanaona, wasione kweli. Na ingawa wanasikia wasisikie wala kufahamu.
Therefore I speak to them in parables, because seeing they see not, and hearing they hear not, nor understand.
14 Unabii wa Isaya umetimia kwao, ule usemao, “Msikiapo msikie, lakini kwa namna yoyote hamtaelewa; wakati mwonapo muweze kuona, lakini kwa namna yeyote ile msijue.
And in them is fulfilled the prophecy of Isaiah, which saith, “Ye will hear indeed, and not understand; and ye will see indeed, and not perceive.
15 Na mioyo ya watu hawa imekuwa giza, ni vigumu kusikia, na wamefumba macho yao, ili wasiweze kuona kwa macho yao, au kusikia kwa masikio yao, au kufahamu kwa mioyo yao, hivyo wangenigeukia tena, na ningewaponya.'
For this people's heart hath become gross, and their ears are dull of hearing, and their eyes they have closed, lest they should see with their eyes, and hear with their ears, and understand with their heart, and turn from their ways, and I should heal them.”
16 Bali macho yenu yamebarikiwa, kwa kuwa yanaona, na masikio yenu kwa kuwa yanasikia.
But blessed are your eyes, for they see; and your ears, for they hear.
17 Hakika nawaambia manabii wengi na watu wenye haki walikuwa na hamu ya kuyaona mambo yale myaonayo, na hawakuweza kuyaona. Walitamani kusikia mambo yale mnayosikia, hawakuyasikia.
Truly do I say to you, that many prophets and righteous men desired to see the things which ye see, and did not see them; and to hear the things which ye hear, and did not hear them.
18 . Sasa sikilizeni mfano wa mpanzi.
Hear ye therefore the parable of the sower.
19 Wakati yeyote asikiapo neno la ufalme na asilifahamu, ndipo mwovu huja na kukinyakua kilichokwisha kupandwa ndani ya moyo wake. Hii ni mbegu ile iliyopandwa kando ya njia.
When any one heareth the word of the kingdom, and understandeth it not, the Evil One cometh, and snatcheth away that which was sown in his heart; this man is what was sown by the wayside.
20 Yeye aliyepandwa katika miamba ni yule asikiaye neno na kulipokea haraka kwa furaha.
And what was sown on the rocky places, this is he that heareth the word, and immediately receiveth it with joy,
21 Bado hana mizizi ndani yake, ila huvumilia kwa kitambo kifupi. Wakati matatizo au mateso yanapotokea kwa sababu ya neno hujikwaa ghafla.
but, having no root within him, endureth only for a time; and when tribulation or persecution ariseth on account of the word, he immediately falleth away.
22 Aliyepandwa kati ya miti ya miiba, huyu ni yule alisikiaye neno lakini masumbuko ya ulimwengu na udaganyifu wa utajiri hulisonga lile neno lisije likazaa matunda. (aiōn g165)
And what was sown among the thorns, this is he that heareth the word, but the cares of the world and the deceitfulness of riches choke the word, and he becometh unfruitful. (aiōn g165)
23 Aliyepandwa kwenye udongo mzuri, huyu ni yule asikiaye neno na kulifahamu. Huyu ni yule azaaye matunda na kuendelea kuzaa moja zaidi ya mara mia, nyingine sitini, nyingine thelathini.''
And what was sown on the good ground, this is he that heareth the word, and understandeth it; who also beareth fruit, and yieldeth, one a hundred fold, another sixty, another thirty fold.
24 Yesu aliwapa mfano mwingine. Akisema, “Ufalme wa mbinguni unafananishwa na mtu aliye panda mbengu nzuri katika shamba lake
Another parable he put forth to them, saying, The kingdom of heaven is like a man who sowed good seed in his field.
25 Lakini watu waliposinzia, adui wake akaja pia akapanda magugu katikati ya ngano kisha akaenda zake.
But while men slept, his enemy came, and sowed tares among the wheat; and went away.
26 Baadaye ngano ilipoota na kutoa mazao yake, ndipo magugu yalitokea pia.
But when the blade grew up, and put forth fruit, then appeared the tares also.
27 Na watumishi wa mwenye shamba walikuja wakamwambia, 'Bwana, hukupanda mbengu nzuri katika shamba lako? Imekuwaje sasa lina magugu?
So the servants of the householder came and said to him, Sir, didst not thou sow good seed in thy field? Whence then hath it tares?
28 Akawaambia, Adui ametenda hili.' Watumishi walimwambia, “Kwa hiyo unataka twende tukayang'oe?”
He said to them, An enemy did this. The servants say to him, Dost thou wish then that we go and gather them up?
29 Mwenye shamba akisema, 'Hapana, wakati mnayang'oa magugu mtang'oa pamoja na ngano.
But he said, Nay; lest, while ye gather up the tares, ye root up the wheat with them.
30 Yaacheni yakue pamoja mpaka wakati wa mavuno. Wakati wa mavuno nitasema kwa wavunaji, 'Kwanza yang'oeri magugu na yafungeni matita matita na kuyachoma, lakini kusanyeni ngano katika ghala langu.''''
Let both grow together until the harvest; and in the time of harvest I will say to the reapers, Gather up first the tares, and bind them in bundles, to burn them; but gather the wheat into my barn.
31 Kisha Yesu aliwatolea mfano mwingine. Akasema, “Ufalme wa mbinguni unafanana na mbegu ya haradali ambayo mtu aliichukua na kuipanda katika shamba lake.
Another parable he put forth to them, saying, The kingdom of heaven is like a grain of mustard, which a man took and sowed in his field.
32 Mbegu hii kwa hakika ni ndogo kuliko mbegu zingine zote. Lakini imeapo huwa kubwa kuliko mimea yote ya bustani, huwa mti, kiasi kwamba ndege wa angani huja na kujenga viota katika matawi yake.”
Which is the least indeed of all seeds; but when it is grown, it is greater than the herbs, and becometh a tree, so that the birds of the air come and lodge in its branches.
33 Akawaambia mfano mwingine tena.”Ufalme wa mbinguni ni kama chachu ile iliyo twaliwa na mwanamke na kuichanganya kwa vipimo vitatu kwa unga mpaka viumuke.
Another parable he spoke to them: The kingdom of heaven is like leaven, which a woman took and hid in three measures of meal, till the whole was leavened.
34 Hayo yote Yesu aliyasema kwenye umati kwa mifano. Na pasipo mifano hakusema chochote kwao.
All these things Jesus spoke to the multitudes in parables, and without a parable he spoke nothing to them;
35 Hii ilikuwa kwamba kile kilichokwisha semwa kupitia kwa nabii kiweze kutimia, pale aliposema, “Nitafumbua kinywa changu katika mifano. Nitasema mambo yale yaliyokuwa yamefichwa tangu misingi ya ulimwengu”.
that it might be fulfilled which was spoken through the prophet Isaiah, saying, “I will open my mouth in parables; I will utter things hidden from the foundation [[of the world]].”
36 Kisha Yesu aliwaacha makutano na kwenda nyumbani. Wanafunzi wake walimwendea na kusema, “Tufafanulie mfano wa magugu ya shambani.''
Then he sent the multitudes away, and went into the house. And his disciples came to him, saying, Explain to us the parable of the tares of the field.
37 Yesu alijibu na kusema, “Apandae mbegu nzuri ni Mwana wa Adamu.
He answered and said, He that soweth the good seed is the Son of man.
38 Shamba ni ulimwengu; na mbegu nzuri, hawa ni wana wa ufalme. Magugu ni wana wa yule mwovu, na adui aliye zipanda ni ibilisi.
The field is the world; the good seed is the sons of the kingdom; but the tares are the sons of the Evil One;
39 Na mavuno ni mwisho wa ulimwengu, na wavunaji ni malaika. (aiōn g165)
the enemy that sowed them is the Devil; the harvest is the end of the world; and the reapers are angels. (aiōn g165)
40 Kama vile magugu yanavyo kusanywa na kuchomwa moto, hivyo ndivyo itakavyo kuwa mwisho wa ulimwengu. (aiōn g165)
As therefore the tares are gathered up and burned with fire, so will it be at the end of the world. (aiōn g165)
41 Mwana wa Adamu atatuma malaika wake, na kukusanya kutoka katika ufalme wake mambo yote yaliyosababisha dhambi na wale watendao maasi.
The Son of man will send forth his angels, and they will gather out of his kingdom all the stumbling-blocks, and those who do iniquity,
42 Watawatupa wote katika tanuru la moto, ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.
and will cast them into the furnace of fire; there will be wailing and gnashing of teeth.
43 Ndipo watu wenye haki watakapong'aa kama jua katika Ufalme wa Baba yao. Yeye aliye na masikio na sikie.
Then will the righteous shine forth as the sun, in the kingdom of their Father. He that hath ears, let him hear.
44 Ufalme wa mbinguni ni kama hazina iliyofichwa shambani. Mtu akaiona na kuificha. Katika furaha yake akaenda kuuza vyote alivyokuwa navyo, na kulinunua shamba.
The kingdom of heaven is like a treasure hid in a field, which a man found and hid; and for joy thereof he goeth and selleth all that he hath, and buyeth that field.
45 Tena, ufalme wa mbinguni ni kama mtu anayefanya biashara atafutaye lulu yenye thamani.
Again, the kingdom of heaven is like a merchant seeking goodly pearls.
46 Wakati alipoiona ile yenye thamani, alienda akauza kila kitu alichokuwa nacho na akainunua.
And having found one pearl of great price, he went and sold all that he had, and bought it.
47 Ufalme wa mbinguni ni kama nyavu iliyo ndani ya bahari, na kwamba hukusanya viumbe vya kila aina.
Again, the kingdom of heaven is like a net, cast into the sea, and bringing together fish of every kind;
48 Ulipojaa wavuvi waliuvuta ufukweni. Kisha wakakaa chini wakakusanya vitu vyema ndani ya vyombo, lakini visivyo na thamani vilitupwa mbali.
which, when it was full, they drew upon the beach, and sat down and gathered the good into vessels, but threw the bad away.
49 Itakuwa namna hii katika mwisho wa dunia. Malaika watakuja na kuwatenga watu waovu kutoka miongoni mwa wenye haki. (aiōn g165)
So will it be at the end of the world. The angels will come forth, and separate the wicked from among the righteous, (aiōn g165)
50 Na kuwatupa ndani ya tanuru ya moto, ambako kutakuwa na maombolezo na kusaga meno.
and will cast them into the furnace of fire; there will be wailing and gnashing of teeth.
51 Mmefahamu mambo yote haya? Wanafunzi walimjibu, ''Ndiyo.''
Did ye understand all these things? They say to him, Yea.
52 Kisha Yesu akawambia, ''Kila mwandishi ambaye amekuwa mwanafunzi wa ufalme anafanana na mwenye nyumba atoaye katika hazina yake vitu vipya na vya kale.''
And he said to them, Thus then every scribe, instructed for the kingdom of heaven, is like a householder, who bringeth out from his storehouse things new and old.
53 IkawaYesu alipomaliza mifano yote hiyo, akaondoka katika sehemu hiyo.
And it came to pass, when Jesus had ended these parables, that he departed thence.
54 Kisha Yesu akafika katika mkoa wake na akawafundisha watu katika sinagogi. Matokeo yake ni kuwa walishangaa na kusema, “Ni wapi mtu huyu alipopata hekima hii na miujiza hii?
And having come into his own country, he taught them in their synagogue, so that they were astonished, and said, Whence hath this man this wisdom, and the miracles?
55 Mtu huyu siyo mwana wa seremala? Mariamu siyo mamaye? Na ndugu zake siyo Yakobo, Yusuph, Simoni na Yuda?
Is not this the carpenter's son? Is not his mother called Mary, and his brothers, James, and Joseph, and Simon, and Judas?
56 Na dada zake tunao hapa petu? Basi mtu huyu ameyapata wapi haya yote?”.
And his sisters, are they not all with us? Whence then hath this man all these things?
57 Aliwachukiza. Lakini Yesu aliwambia, “Nabii hakosi kuwa na heshima isipokuwa kwao na katika nchi yao.
And they took offence at him. But Jesus said to them, A prophet is not without honor, except in his own country, and in his own house.
58 Na hakuweza kufanya miujiza mingi kwa sababu hawakuwa na imani naye.
And he did not work many miracles there, because of their unbelief.

< Mathayo 13 >