< Mathayo 11 >

1 Ikawa baada ya Yesu kumaliza kuwaelekeza wanafunzi wake kumi na wawili aliondoka plae kwenda kufundisha na kuhubiri katika miji yao,
And it happened that when Jesus had finished instructing his twelve disciples, he departed from there to teach and preach in their cities.
2 na Yohana akiwa gereszani aliposikia akiwa juu ya matendo ya Kristo, alituma ujumbe kupitia wanafunzi wake,
Now when John heard in prison the works of the Christ, he sent his disciples
3 na wakamuuliza, “Wewe ni yule ajaye, au kuna mwingine tunapaswa kumtazamia?”
and said to him, "Are you the one who is to come, or should we look for another?"
4 Yesu akajibu na kusema kwao “Nendeni mkamtaarifu Yohana yale mnayoyaona na yale mnayoyasikia.
And Jesus answered them, "Go and tell John the things which you hear and see:
5 Watu wasioona wanapata kuona, viwete wanatembea, wakoma wanatakaswa, watu wasiosikia wanasikia tena, watu waliokufa wanafufuliwa kupata uhai, na watu wahitaji wanahubiriwa habari njema.
the blind receive their sight, the lame walk, the lepers are cleansed, the deaf hear, the dead are raised up, and the poor have good news preached to them.
6 Na amebarikiwa yule asiyeona shaka juu yangu.
And blessed is he who is not offended by me."
7 Pindi watu hawa walipoondoka, Yesu alianza kusema na umati juu ya Yohana, “Ni nini mlikwenda kuona katika jangwa tete likitikiswa na upepo?
And as these went their way, Jesus began to say to the crowds concerning John, "What did you go out into the wilderness to see? A reed shaken by the wind?
8 Lakini nini mlikwenda kuona mtu aliyevaa mavazi mololo? Hakika, wale wavaao mavazi mololo hukaa katika nyumba za wafalme.
But what did you go out to see? A man in soft clothing? Look, those who wear soft things are in kings' houses.
9 Lakini mliondoka kuona nini-Nabii? Ndiyo, nawaambia, na zaidi ya Nabii.
But what did you go out to see? A prophet? Yes, I tell you, and much more than a prophet.
10 Huyu ndiye aliyeandikiwa, 'Tazama, namtuma mjumbe wangu mbele ya uso wako, ambaye ataandaa njia yako mbele yako.
This is the one of whom it is written, 'Look, I send my messenger ahead of you, who will prepare your way before you.'
11 Mimi nawaambia kweli, kati ya waliozaliwa na wanawake hakuna aliye mkuu kuliko Yohana Mbatizaji. Lakini aliye mdogo katika ufalme wa mbinguni ni mkubwa kuliko yeye.
Truly I tell you, among those who are born of women there has not arisen anyone greater than John the Baptist; yet he who is least in the kingdom of heaven is greater than he.
12 Toka siku za Yohana Mbatizaji mpaka sasa, ufalme wa Mbinguni ni wa nguvu, na watu wenye nguvu, huuchukua kwa nguvu.
And from the days of John the Baptist until now, the kingdom of heaven has suffered violence, and the violent are taking it by force.
13 Kwa kuwa manabii na sheria, ikamelcuwa wakitabiri mpaka kwa Yohana.
For all the prophets and the law prophesied until John.
14 Na kamamko tayari kukubali, huyu ni Eliya, yule ajaye.
And if you are willing to receive it, this is Elijah, who is to come.
15 Aliye na masikio ya kusikia na asikie.
He who has ears to hear, let him hear.
16 Nikilinganishe na nini kizazi hiki? Ni mfano wa watoto wanaocheza maeneo ya sokoni, wanaokaa na kuitana
"But to what should I compare this generation? It is like children sitting in the marketplaces, who call to their companions
17 na kusema, 'Tuliwapigia zomari na hamkucheza. Tuliomboleza, na hamukulia.'
and say, 'We played the flute for you, and you did not dance. We wailed in mourning, and you did not mourn.'
18 Kwa kuwa Yohana alikuja bila kula mkate au kunywa mvinyo, na wakawa wanasema, 'Ana pepo.'
For John came neither eating nor drinking, and they say, 'He has a demon.'
19 Mwana wa Adamu alikuja akila na kunywa na wakasema 'Angalia, ni mtu mlaji na mlevi, rafiki wa watoza ushuru na wenye dhambi!' Lakini hekima inadhihirishwa kwa matendo yake.''
The Son of Man came eating and drinking, and they say, 'Look, a gluttonous man and a drunkard, a friend of tax collectors and sinners.' But wisdom is justified by her children."
20 Yesu alianza kuikemea miji ambamo baadhi ya matendo yake ya ajabu yalitendeka, kwa sababu walikuwa hawajatubu,
Then he began to denounce the cities in which most of his mighty works had been done, because they did not repent.
21 Ole wako, Kolazini, Ole wako Bethsaida! Kama matendo makuu yangetendeka Tiro na Sidoni yale yaliyotendeka hapa, wangekuwa wametubu zamani kwa kuvaa magunia na kujipaka majivu.
"Woe to you, Chorazin. Woe to you, Bethsaida. For if the mighty works had been done in Tyre and Sidon which were done in you, they would have repented long ago in sackcloth and ashes.
22 Lakini itakuwa uvumilivu kwa Tiro na Sidoni siku ya hukumu kuliko kwako.
But I tell you, it will be more tolerable for Tyre and Sidon on the day of judgment than for you.
23 Wewe, Kapernaum, unadhani utainuliwa hadi mbinguni? Hapana utashushwa hadi chini kuzimu. Kama kwa Sodoma kungefanyika matendo makuu, kama yalifanyika kwako, ingekuwepo hadi leo. (Hadēs g86)
And you, Capernaum, who are exalted to heaven, you will be brought down to hell. For if the mighty works had been done in Sodom which were done in you, it would have remained until this day. (Hadēs g86)
24 Bali nasema kwako kwamba itakuwa rahisi kwa nchi ya Sodoma kusimama siku ya hukumu kuliko wewe.
But I tell you that it will be more tolerable for the land of Sodom, on the day of judgment, than for you."
25 Katika muda huo Yesu alisema, “Nakusifu wewe, Baba, Bwana wa Mbingu na Nchi, kwa sababu uliwaficha mambo haya wenye hekima na ufahamu, na kuyafunua kwa wasio na elimu, kama watoto wadogo.
At that time, Jesus answered, "I thank you, Father, Lord of heaven and earth, that you hid these things from the wise and intelligent, and revealed them to little children.
26 Baba kwa kuwa ilikupendeza hivyo machoni pako.
Yes, Father, for so it was well-pleasing in your sight.
27 Mambo yote yamekabidhiwa kwangu kutoka kwa Baba. Na hakuna amjuaye Mwana isipokuwa Baba, na hakuna amjuaye Baba isipokuwa Mwana, na yeyote ambaye Mwana ana hamu ya kumfunulia.
All things have been delivered to me by my Father. No one knows the Son, except the Father; neither does anyone know the Father, except the Son, and he to whom the Son desires to reveal him.
28 Njoni kwangu, nyinyi nyote mnaosumbuka na mnaolemewa na mzigo mzito, nami nitawapumzisha.
"Come to me, all you who labor and are heavily burdened, and I will give you rest.
29 Jitieni nira yangu na mjifunze kutoka kwangu, kwa kuwa mimi ni mnyenyekevu na mpole wa moyo na mtapata pumziko la nafsi zenu.
Take my yoke upon you, and learn from me, for I am gentle and humble in heart; and you will find rest for your souls.
30 Kwa kuwa nira yangu ni laini na mzigo wangu ni mwepesi.
For my yoke is easy, and my burden is light."

< Mathayo 11 >